Migogoro ya ardhi ni vita inayoinyemelea mikoa ya kusini

Ileje

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,759
12,175
Kifo cha mkulima pale Ikwiriri kilichosababishwa na mfugaji ni dalili tosha kuwa sasa vita ya ardhi imeanza rasmi kuinyemelea mikoa ya kusini!

Itakumbukwa kuwa wafugaji wengi walihamishwa kutoka Ihefu na kupelekwa mikoa ya Lindi na Pwani. Zoezi hili lilifanyika bila kuweka miundombinu muhimu kwa ajili ya mifugo kama majosho, maeneo ya malisho, maji kwa ajili ya mifugo na matumizi ya nyumbani, maeneo ya makazi ya wakulima na wafugaji nk.

Changamoto kubwa ni uhaba wa maji hasa wakati wa kiangazi ambapo madimbwi yote ya maji na mito mingi ambayo hutumika kunyweshea mifugo hukauka na hivyo wafugaji kulazimika kupeleka mifugo yao katika makorongo ya mito sehemu ambazo pia wakulima ambao ni wakazi asili wa huko wamekuwa wakitumia kupata maji kwa matumizi yao ya nyumbani. Hali hii imekuwa ikisababishwa ugomvi ukubwa baina ya jamii hizi mbili za wafugaji wenye asili ya wasukuma na wenyeji.

Hivyo wakati umefika kwa viongozi wa kisiasa, wizara zinazohusika na maswala ya jamii, halmashauri za wilaya wakakaa pamoja na wananchi kutafuta ufumbuzi wa changamoto hii vinginevyo tutegemee vifo vingi zaidi vya wananchi na mifugo yao, uharibifu wa mali na mazingira.

WAKATI NI HUU HAKUNA MUDA WA KUPOTEZA!
 
You are right ,hata Katavi Jana wameuawa watu watatu ugomvi wa ardhi na hospitali kuna majeruhi 25 or more wa mishale,nadhani hakuna waandishi huko ndio sababu hakuna matangazo,lakini ni serious zaidi ya Ikwiriri.FFU wamemwagwa toka Sumbawanga kutuliza.
 
tena rufiji ikae chonjo sana maana wana eneo kubwa sana ambalo liko wazi na lenye rutuba ila linahitaji uwekezaji wa hali ya juu. Na hapa tutashuhudia uporaji wa hali ya juu wa ardhi toka kwa wawekezaji wa nje
 
You are right ,hata Katavi Jana wameuawa watu watatu ugomvi wa ardhi na hospitali kuna majeruhi 25 or more wa mishale,nadhani hakuna waandishi huko ndio sababu hakuna matangazo,lakini ni serious zaidi ya Ikwiriri.FFU wamemwagwa toka Sumbawanga kutuliza.
Nakumbuka kulikuwa na azimio la Mtowisa miaka ya 1990 ambalo kwa kiasi kikubwa lilikuwa linatatua migogoro baina ya wafugaji wa kisukuma na wenyeji kwa kufanya mikutano ya mara kwa mara. Aidha nakumbuka ujumbe kutoka mkoa wa Morogoro ukiongozwa na mkuu wa mkoa wa enzi hizo uliwahi kufanya ziara mkoani Rukwa ili kujifunza namna ya kutatua migogoro ya aina hii. Ni vizuri azimio lile likapitiwa upya ili lliendelee kutumika katika kusuluhisha migogoro ya aina hii.
 
..migogoro yote hii bado kuna wa-Tz wanataka tukaribishe jumuiya nzima ya Afrika Mashariki kumiliki ardhi Tanzania.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom