Migiro (for Presidency 2015) na Tibaijuka (Uwaziri Mkuu 2010) Wanatosha Kuitakasa CC

huyu mchambuzi startv mbona yuko hivi?huyu kocha kweli huyu?mhhh au ocha wa wachezaji wagonjwa
 
Wantanzania lini mtaacha kukutupuka kwa kuwapa uongozi watu kwa majina, sura na muonekano wao? JK mlimpa urais sababu ya tabasamu Leo migiro mshaanza kumkampenia kisa jinsia yake na ameandaliwa na JK kuwa Rais kwa kivuli cha utawala bora mtu aliye shindwa u secretary mnataka mumpe urais? Tabasamu linawanukisha shombo sasa Ivi maumivu yanakaribia kwisha unadanganyiwa nyonyo na make up! Sishangai kwani tz kwa cheap payrool kila kitu kinawezekana
 
Asha Rose Migiro anafaa kuingia ikulu kipindi kijacho kwa sababu ni safi, si fisadi, hana doa. Sababu kubwa zaidi ni kuwa akina mama hawana roho za ulafi wa mali ya umma kwani ni waoga, wanamwogopa Mungu na ni watii wa sheria. Atakuwa makini katika kuongoza nchi kama akina mama walivyo makini ktk kupanga budget za nyumbani kwao. Zaidi ya hayo ana uzoefu wa kimataifa.Vile vile hebu tumpe mwanamama sasa kwani TUNAWEZA tukipewa nafasi. Tangu tupate uhuru ni kinababa tu. Kwani marais wanawake nchi nyingine duniani wana nini ambacho wanawake wa Tz hawana? Wana JF nadhani hoja yangu imepita bila kupingwa.

Naomba kuwasilisha.

Usafi na kukosa ufisadi si sifa. Hivi ndivyo kila mtu anavyotakiwa kuwa.

Dr. Migiro amefanya kitu gani kusema apewe urais?
 
Ameshindwa nini? Kama kilaza angefika huko? Wewe umefanya nini cha maana mpaka kumwita mama wa watu kilaza, acheni dharau bana,wewe ukiambiwa mama yako ni kilaza utakubali?

kama mama yangu ni kilaza nitasema ukweli,,unataka niseme mama yangu anamasters wakati ni darasa la saba huyo ni kilaza 2
 
Getrude mongella alipewa kuwa Rais wa bunge la Africa akaishia kutia aibu nchi kwa ubadhilifu!!! Mnapigiwa chapuo ili mpate madaraka sababu yenyewe ni kwamba hao watakaowafadhili wanajua ni rahisi kumtumia mwanamke akiwa kiongozi; mfano ni Anna Makinda anavyotumiwa na jakaya Kikwete kufanikisha matakwa yake binafsi yasiyokuwa na tija kwa nchi!! Asha Rose will be worse than Makinada.
Hayo yote ni kweli kabisa. Lakini je na hao waliokuwa marais walitumiwa na nani hadi kila wakimaliza kipindi cha uongozi wanasemwa vibaya tu? Pia marais watatu mfululizo walipokuwa wakipigiwa chapuo tuliambiwa ni safi, ni wenzetu, tuwape kura za ndiyo. Sasa je kiko wapi? Mbona sasa wanaitwa mafisadi? Bado nasema Migiro anafaa kuwa rais kwa sababu naye ni binadamu si malaika and no human being is perfect.
 
Asha Rose Migiro anafaa kuingia ikulu kipindi kijacho kwa sababu ni safi, si fisadi, hana doa. Sababu kubwa zaidi ni kuwa akina mama hawana roho za ulafi wa mali ya umma kwani ni waoga, wanamwogopa Mungu na ni watii wa sheria. Atakuwa makini katika kuongoza nchi kama akina mama walivyo makini ktk kupanga budget za nyumbani kwao. *Zaidi ya hayo ana uzoefu wa kimataifa.Vile vile hebu tumpe mwanamama sasa kwani TUNAWEZA tukipewa nafasi. Tangu tupate uhuru ni kinababa tu. *Kwani marais wanawake * nchi nyingine duniani wana nini ambacho wanawake wa Tz hawana? Wana JF nadhani hoja yangu imepita bila kupingwa.*

Naomba kuwasilisha.

Mkuu mamayeyo,
Ni mawazo mazuri taifa kufikia muda kuwa na rais mwanamke hasa ukizingatia nchi hii haijawahi kupata rais mwanamke.
*Bahati mbaya mpaka sasa hivi hatuna mwanamke Tanzania anayeweza kushika nafasi ya uraisi hasa ukizingatia changamoto zinazokabili taasisi ya uraisi nchini, majukumu yanayomkabili rais wetu *ajaye na matarajio ya wananchi.

maadui wakubwa wa nchi hii baada ya uhuru-kama mara nyingi ilivyoainishwa na baba wa taifa *Mwl. Nyerere ni ujinga, umaskini na maradhi.*
Bahati mbaya kutokana na uongozi dhaifu hasa baada ya awamu ya Mwl.Nyerere, maadui hawa wamejijenga zaidi Na maadui wapya wameibuka. maadui walioongezeka ni Ufisadi, matumizi mabaya ya madaraka na sasa hivi udini! matumizi mabaya ya madaraka yametokana na katiba mbovu Na sheria ambazo haziwezi kuwajibisha viongozi.*
Udini umeletwa kwa makusudi na baadhi ya viongozi ili kujipatia umasrufu Wa kisiasa kiurahisi.

kwa hiyo mkuu, Sasa hivi nchi yetu inahitaji kiongozi atakayeweza kukabiliana Na changamoto nilizizitaja hapo juu. Tunahitaji rais atakayeweza kupambana na mfumo wa kifisadi ambao ndio kikwazo kikubwa kwa nchi hii kuweza kupata Maendeleo-huyu candidate wako hili haliwezi. tunahitaji rais atakayejenga mfumo wa viongozi kuwajibika-huyu mtu wako hili haliwezi! tunahitaji mtu atakayeondoa matumizi mabaya ya madaraka, kuondoa katiba Na sheria zinazogandamiza wananchi-huyu mwanamama hawezi. tunahitaji kiongozi atakayesimamia rasilimali za nchi yetu zitumike kwa ajili ya wananchi Na Maendeleo Na nchi-chaguo lako hawezi. Vile vile Nadhani huelewi kwamba chaguo lako alishindwa ku-deliver UN ambako taratibu za majukumu ziko clear. Je hapa ambako kila kitu si clear atafanya nini?

Mkuu Nakukumbusha kuwa rais wa nchi, kwa nchi zenye kuhitaji Maendeleo, huchaguliwa kwa kuzingatia mahitaji halisi ya nchi wakati huo. Tofauti Na hapa mnachagua rais kwa kuzingatia uchama na ushabiki Wa kisiasa badala ya mahitaji ya nchi wakati huo Na uwezo Wa candidate ku-deliver.
halafu Mkuu, uwezo Wa mtu haupimwi kwa kuangalia mhusika ameshika nafasi zipi Na ngapi za uongozi, bali akiwa katika hizo nafasi amefanya nini katika kuleta Maendeleo ya watu anaowaongoza.

Nadhani Mkuu mpaka hapo ingawa nimeeleza kwa ufupi nadhani angalau *umepata mwanga kidogo ni kiongozi gani tunayemhitaji ili aokoe Jahazi letu la Tanzania ambalo linazama kwa kasi.
 
Mada nyingine si za kuleta humu THE HOME OF GREAT THINKERS! Hamjakoma tu mliyofanya 2005, mtu kashindwa kumanage body yenye resources zote at her exposure sha mnampigia debe aje kuongoza a country like this. Tunataka mtu mwenye uwezo na great thinker wa kutatua matatizo yanayowakabili wananchi sio PhD ya darasani ambazo kila mtu ana uwezo wa kuwa nazo. Moderator tusaidieni kutuwekea thread zenye mashiko umu javini.
 
ameshindwa kupewa 2nd term kwa kuwa ni kimeo. km kweli alikuwa ni mahiri, ban ki moon angempa kipindi cha pili. kachemka. wawmawake watz wote waliokwenda kufanya kazi kimataifa walichemka eg mama mongela, bongo hapa twaona jinsi makinda anavyochemka. kwa hiyo tuna precedent nzuri sana kuwa hawawezi kuperfom vzr. lakini mleta thread km unampenda sana migiro mwalike ukanywe nae chai.
Sawa kabisa. Wanawake hawawezi kuperform vizuri. Je wanaume wanaweza? Mbona hao waliopita hawasifiwi? Kwa mantiki hiyo Migiro anafaa.
 
Mkuu mamayeyo,
Ni mawazo mazuri taifa kufikia muda kuwa na rais mwanamke hasa ukizingatia nchi hii haijawahi kupata rais mwanamke.
*Bahati mbaya mpaka sasa hivi hatuna mwanamke Tanzania anayeweza kushika nafasi ya uraisi hasa ukizingatia changamoto zinazokabili taasisi ya uraisi nchini, majukumu yanayomkabili rais wetu *ajaye na matarajio ya wananchi.

maadui wakubwa wa nchi hii baada ya uhuru-kama mara nyingi ilivyoainishwa na baba wa taifa *Mwl. Nyerere ni ujinga, umaskini na maradhi.*
Bahati mbaya kutokana na uongozi dhaifu hasa baada ya awamu ya Mwl.Nyerere, maadui hawa wamejijenga zaidi Na maadui wapya wameibuka. maadui walioongezeka ni Ufisadi, matumizi mabaya ya madaraka na sasa hivi udini! matumizi mabaya ya madaraka yametokana na katiba mbovu Na sheria ambazo haziwezi kuwajibisha viongozi.*
Udini umeletwa kwa makusudi na baadhi ya viongozi ili kujipatia umasrufu Wa kisiasa kiurahisi.

kwa hiyo mkuu, Sasa hivi nchi yetu inahitaji kiongozi atakayeweza kukabiliana Na changamoto nilizizitaja hapo juu. Tunahitaji rais atakayeweza kupambana na mfumo wa kifisadi ambao ndio kikwazo kikubwa kwa nchi hii kuweza kupata Maendeleo-huyu candidate wako hili haliwezi. tunahitaji rais atakayejenga mfumo wa viongozi kuwajibika-huyu mtu wako hili haliwezi! tunahitaji mtu atakayeondoa matumizi mabaya ya madaraka, kuondoa katiba Na sheria zinazogandamiza wananchi-huyu mwanamama hawezi. tunahitaji kiongozi atakayesimamia rasilimali za nchi yetu zitumike kwa ajili ya wananchi Na Maendeleo Na nchi-chaguo lako hawezi. Vile vile Nadhani huelewi kwamba chaguo lako alishindwa ku-deliver UN ambako taratibu za majukumu ziko clear. Je hapa ambako kila kitu si clear atafanya nini?

Mkuu Nakukumbusha kuwa rais wa nchi, kwa nchi zenye kuhitaji Maendeleo, huchaguliwa kwa kuzingatia mahitaji halisi ya nchi wakati huo. Tofauti Na hapa mnachagua rais kwa kuzingatia uchama na ushabiki Wa kisiasa badala ya mahitaji ya nchi wakati huo Na uwezo Wa candidate ku-deliver.
halafu Mkuu, uwezo Wa mtu haupimwi kwa kuangalia mhusika ameshika nafasi zipi Na ngapi za uongozi, bali akiwa katika hizo nafasi amefanya nini katika kuleta Maendeleo ya watu anaowaongoza.

Nadhani Mkuu mpaka hapo ingawa nimeeleza kwa ufupi nadhani angalau *umepata mwanga kidogo ni kiongozi gani tunayemhitaji ili aokoe Jahazi letu la Tanzania ambalo linazama kwa kasi.
Asante kwa kunielimisha. Na kwa mtazamo wako huo unafikiri ni nani anafaa kuwa rais kipindi kijacho?
 
Utafiti wako kuhusu ufisadi na wanawake haujakaa sawaswa. Hivi Blandina Nyoni ni mwaume vile? Hivi uwanamke siku hizi ni sifa ya uongozi? Spika sifa kuu mwanamke, Raisi shart awemwanamke. Huo ni ubaguzi wa kijinsia. Kazi pekee ambayo sifa yake sharti awe mwanamke ni kubeba mimba lakini kazi zingine sio lazima kupimwa kwa jinsia.
 
usawa upo lkn si kutoka magamba. Mbegu yoyote toka huko tunaikataa kwa nguvu zote! Tunataka watu wapya ni si mentality za magamba plse!
 
Mwinyi, Mkapa na Kikwete walifanya kitu gani hadi wakapewa urais?
Ndio maana safari hii unatakiwa utuambie huyo mama kafanya kitu gani hadi apewe Uraisi? Hayo makosa kama yalifanyika huko nyuma, hayatakiwi kurudiwa tena, la hasha. Safari hii tunataka kuhakikisha mtu anayekacha mdahalo kama Kikwete hapewi nafasi kabisaa na katika huo mdahalo itabidi aeleze amewahi kusimamia nini na kwa kiwango gani cha ufanisi. Hivyo wewe hapa unatakiwa kutetea hoja yako kwa kutueleza ni kitu gani amewahi kukifanya huyo mama hadi apewe Uraisi, simple!
 
We mleta mada huu upumbavu umecopy na kupaste kutoka bbc matangazo ya jioni hii palikuwa na mjadala wa kipumbavu hivi hivi.
 
Sijaona vigezo vinavyotosheleza kumfanya awe rais wa Tz. Moja ya disqualifying features kwa huyu mama ni kuwa yeye ni mwanaCCM so hawezi kuleta lolote jipya akiwa ndani ya thithimwewe kwa kuwa matatizo ya nchi hii yameletwa na mfumo huu huu wa thithimwewe. Tunahitaji akili kubwa zaidi na iliyo nje ya CCM kutatua matatizo ya nchi hii!!!!!
 
Ameshindwa nini? Kama kilaza angefika huko? Wewe umefanya nini cha maana mpaka kumwita mama wa watu kilaza, acheni dharau bana,wewe ukiambiwa mama yako ni kilaza utakubali?

Mimi nakubali mama yangu Anne Makinda ni kilaza
 
mkuu Daudi mchambuzi, please usimtusi Dr. Migiro bana kwa kumwita kilaza, unadhalilisha usomi na utendaji wake uliotukuka,zaidi unatudhalilisha hata mabinti ambao tuko inspired na huyu mama.she was ther she did her job at her best level, wako wanawake katika serikali hii ambao ukiwaita vilaza hakuna atakaye pinga hilo but si huyu mama.miongoni mwa wanawake wa shoka katika nchi hii huwezi kuacha kumweka dr. rose migiro kwenye hiyo list hilo liko wazi na halina mjadala.binafsi napenda angepata nafasi ya kugombea post ya u-president katika nchi hii lakini si kwakuwa ni zamu ya wanawake kama wengine watakavyosuggest but kwakuwa ni mtendaji mzuri na image yake inakubalika katika jamii.kwani hao tuliowapa nafasi wanamzidi nini so far(ukimtoa baba wa taifa JK Nyerere).alipata nafasi ya kutuwakilisha UN, alifanya aliyoweza kufanya kwa uwezo wake na chance aliyopewa, wengi tunamu-attack kwakuwa tuko nje hatukujuwa what is it like to be there and kind of challenges thereon, methods zilizokuwa zinatumika kutackle hizo issues and the like!
however tatizo kubwa linakuwa yuko kwenye chama cha magamba so hata akipata chance hatoweza kufanya yale watz wengi tunahitaji atokee mtu wa kuyafanya, coz atakuwa still kwenye rotten system ya magamba, may be cdm tukichukua nchi tumtumie kuijenga nchi hii, kama alivyofanya obama kwa hillary clinton aliminclude kwenye serikali yake coz anafahamu hillary ni jembe just like dr. rose migiro
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom