Miezi 3 done! - Miaka Minne baadaye tunaremburiana!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Ulaghai wa Bernard Madoff ulijulikana tarehe 10 Disemba pale alipowaambia wanae kuwa biashara yake ilikuwa ni mradi wa ponzi. Watoto wakawaambia wanausalama siku hiyo hiyo: kilichofuata:

a: Kesho yake FBI walimkamta na kumfungulia mashtaka ya security fraud
b: Siku tano baadaye mali zake na zile za shirika zake zikazuiliwa na kupewa msimamizi maalum
c: Leo (miezi mitatu baadaye) Madoff amekubali kuwa na hatia ya mashtaka 11 ambayo jumla ya vifungo vyake akipewa adhabu ya juu kabisa ni miaka 150!


Here is the kicker:

Tanzania tuligundua wizi wa EPA lini, Meremeta lini, Mwananchi Gold, Deep Green, Rada, Minara n.k Lini?

What does that tell about our law enforcement agencies?

Najiuliza hivi kama wizi huu wa benki kuu ungekuwa umetokea kwenye nchi hizi za wenzetu hivi kweli bado kungekuwa na watu wanaendelea kutaka tununue mitumba ya Dowans? Hapa nawaza tu wala sina point yoyote!!
 
Mkuu hakuna kinachoweza kufanyika kama rais na yeye anausika kwa njia moja ama ntingine. Nakubaliana na Mh. Pinda kuwa kuwagusa mafisadi ni kuoindua nchi kwani hata kama hupo ushaidi wa kutosha watafanya makosa ya makusudi watu washinde kesi.

Inawezekana Kagoda ni mkuu mwenyewe au ilifinance uchaguzi kwahiyo kusema kagoda ni CCM maana na serikali iliyoko madarakani ni batili inabidi ijiudhuru uitishwe uchaguzi mpya.

My take:
Narudia tena kwa afya ya Taifa letu, CCM yetu na wananchi wake ni vyema Mkuu wa kaya angejiuzuru na kutisha uchaguzi upya, nina imani atashinda kwani atakuwa na mtaji wa kuwa kiongozi mkuu pekee wa tanzania kuwajibika na hii itampa credit sana na atashinda.

Kuendela kungangania kutaibua mengi ambayo 2010 yatamweka kwenye wakati mgumu sana.
 
Siku mkulu wa kaya atakapojiuzulu na kuitishwa uchaguzi.....I will instantly fly to Tanzania just to be "part of the history!"
its so unfortunate that it will never happen.Sheria/katiba butu,uongozi butu,wananchi elimu duni,huduma za afya ziiii....Hivi hasa tuna kipi cha kujivunia???
 
Well said Mkjj, Huwa nikifikiria hata ile kesi ya maziwa ya watoto China of which in 4 months it was closed na wanaendelea na mambo mengine. Mimi nadhani sisi pamoja na kuhusika kwa Mkulu lakini hatuna utamaduni wa kumaliza mambo. Tunaendekeza sana longo longo! Tungekuwa na utamaduni huo ina maana wananchi wangekuwa wanademand kuona mwisho mapema wa kila ishu kubwa kubwa. Lakni hapa tukiambiwa iko mahakamanindio basi tena.

Look at Mahalu's case how many yrs bro?????
 
Tatizo ni vimelea vya Sultani CCM,wao ndio wezi wao ndio mahakama wao ndio Katiba sasa unafikiri kesi itakwisha hapo ,itapigwa tarehe mpaka wanaosikiliza watashikwa na usingizi wasijue kilichosemwa na kuamuliwa.Yaani hata wakizinduka kwenye usingizi wanaambiwa ushahidi umetupiliwa mbali na washitakiwa wapo huru.
 
Mheshimiwa mwanakijiji, kutokana na maelezo ya kesi hiyo. Hivi hapa mjini hatuna mradi unaondeshwa na kanisa wenye sura ya Ponzi scheme. Maana inaonekana hamna wanachozalisha.

Kama kweli hamna wanachozalisha, am crossing my finger it will colapse like all ponzi scheme. Haleluya tutamuona.
 
Hivi tukijiuliza swali sisi wenyewe kwamba kwa haya yote yaliyotokea, sisi kama wadau wakubwa wa Tanzania nini tunangojea? Je, tunangojea hawa wahusika pamoja na mkulu waresign? Je, tunangojea uchaguzi wa 2010? je tunangojea vyombo vya sheria vifanye kazi yake?

Swali kubwa: Kama tunasubiria moja wapo ya vitu nilivyotaja hapo juu kutokea, Je, Tumekuwa tukingojea hayo tangu lini? Tumepiga kelele kuhusu hayo tangu lini? Hawa jamaa wameziba masikio au nafasi walizo nazo zinawafanya wawe hivyo? Tutaishi kwa matumaini haya mpaka lini? au tuishi kwa matumaini mpaka ''Yesu atakaporudi'' Kuna mtu anajua atarudi lini? au wote tusitruggle na kuwa sehemu ya ufisadi (survival for fittest)

I am getting confused here....! Tufanye nini sasa ili tuweze kufika kwenye ''mbingu'' tunayotaka?
 
Last edited:
Tutaendelea kuwa confused, mpaka tutakapo amua kuwa na akili ya wananchi wa kenya kukataa kubuluzwa.

hivi tukiamua tusipige kura kwa kigezo kwamba hatuoni mtu wote ni wezi itakuwaje? utashitaki nchi nzima, tunahitaji misimamo ya kiukweli.
 
Na kinachoumiza saaana kichwa, huyu huyu JK naye atasimama kugombea, japo najua nyimbo hazitakuwa maisha bora kwa kila mtanzania, nadhani zitakuwa tukifanya kazi kwa bidiii
 
:kwa afya ya Taifa letu, CCM yetu na wananchi wake ni vyema Mkuu wa kaya angejiuzuru na kutisha uchaguzi upya, nina imani atashinda kwani atakuwa na mtaji wa kuwa kiongozi mkuu pekee wa tanzania kuwajibika na hii itampa credit sana na atashinda.

Kuendela kungangania kutaibua mengi ambayo 2010 yatamweka kwenye wakati mgumu sana.


THIS IS PRACTICAL MR JAMCO!................bravo.

Ninayo imani kwamba,HAYA MAMBO YANA UKOMO WAKE!SIKU YAJA.

"'.........SAUTI YA WENGI NI SAUTI YA MUNGU..............''watu waliokaa kwenye giza nene sasa wameona mwanga mkuu!
 
Mahakama za Bongo ni Kangaroo Courts. Makampuni ya mawakili ndo Magenge hasa ya Matapeli, Mafisadi, Majizi, nk you name it. Therefore law enforcement ni fiction. Kwa nini sasa tujiulize kuwa mambo hayaishi? Yataishaje? Nani atayamaliza?

Kila siku linazaliwa jipya. Unajua kwa nini? Ukijaribu kushughulikia hili, wakati huna nia ya kulishughulikia, haliwezi kuisha! Na hilo litazua jingine, ambalo nalo hutaki liishe, kwanza hukutaka lijulikane, ila limejulikana kwa sababu na lile lilijulikana. Kwa hiyo ni kamchezo ka kupakana matope, siyo kushughulikia mambo!!! Mambo yakishughulikiwa yangeisha! Lakini ni nani ayashughulikie? Atayashughulikiaje?

Hivi ni vita vya Kunguru, akishamshinda mwingine, anajiona na yeye ni kunguru tuuu. To break this vicious cycle, ni kudra tuuu. Tunaweza kuelekea kokote, kwani katika huu mchezo wa kupakana matope, we may end up creating warlords. Kuna wakati hizi verbal attacks and counter attacks zitakuwa physical.

Hapa ni safari moja huanzisha nyingine!!!
 
Narudia tena kwa afya ya Taifa letu, CCM yetu na wananchi wake ni vyema Mkuu wa kaya angejiuzuru na kutisha uchaguzi upya....

Hapana, tunachohitaji ni ku-overhaul system zetu zote. marekani imewezekana kwa sababu susyem zao zinaruhusu hivyo. Pia unaweza kuona aina ya uzalendo na honesty waliyokuwa nayo... watoto wamemsemea baba yao... baba alipokamatwa hakuleta ubishi, amekiri.
hapa kwetu bado tunaendeleza mchezo wa kukataa kila kitu, hata vile ambavyo ushahidi wa wazi unaonyesha kuwa fulani anahusika kwa asilimia 100
 
Hivi tukijiuliza swali sisi wenyewe kwamba kwa haya yote yaliyotokea, sisi kama wadau wakubwa wa Tanzania nini tunangojea? Je, tunangojea hawa wahusika pamoja na mkulu waresign? Je, tunangojea uchaguzi wa 2010? je tunangojea vyombo vya sheria vifanye kazi yake?

Swali kubwa: Kama tunasubiria moja wapo ya vitu nilivyotaja hapo juu kutokea, Je, Tumekuwa tukingojea hayo tangu lini? Tumepiga kelele kuhusu hayo tangu lini? Hawa jamaa wameziba masikio au nafasi walizo nazo zinawafanya wawe hivyo? Tutaishi kwa matumaini haya mpaka lini? au tuishi kwa matumaini mpaka ''Yesu atakaporudi'' Kuna mtu anajua atarudi lini? au wote tusitruggle na kuwa sehemu ya ufisadi (survival for fittest)

I am getting confused here....! Tufanye nini sasa ili tuweze kufika kwenye ''mbingu'' tunayotaka?

Maswali mazuri sana umejiuliza mkuu,,

Ili tufikie hali waliyofikia hawa jamaa yafaa tujue walifanyaje mpaka wakawa hivyo haikuwa miujiza ni lazima kuna jambo walifanya mpaka wakafika hapo.

Siku waTanzania wataamua kumaliza kiburi cha hawa viongozi wetu ndipo tutakapokuwa tumefanikisha haya,, by the way haitakuwa muda mrefu tumekaribia tuweni imara,, ng'ambo tumekaribia.

Imebakia one move mtaona mambo yote yatakuwa sawa,, nani alijua kuwa silikali ikiamua kununua Dowani generators itapingwa na kuacha? kwa nini imeacha? inajua sasa hivi ukicheza tu wabongo wanakujia juu
 
Siku mkulu wa kaya atakapojiuzulu na kuitishwa uchaguzi.....I will instantly fly to Tanzania just to be "part of the history!"
its so unfortunate that it will never happen.Sheria/katiba butu,uongozi butu,wananchi elimu duni,huduma za afya ziiii....Hivi hasa tuna kipi cha kujivunia???

Mbona mengi tu ya kujivunia?

1. Wezi wakubwa wakubwa wa mali ya umma walioundiwa vyombo maalumu vya kuwalinda wao na wanamitandao

2. Tunajivunia nchi iliyowageuza wananchi wake kuwa kitoweo, vikongwe wanaouwawa kwa tuhuma za uchawi, alibono wanaoteketea kwa imani kama hizo. Walio nyuma ya haya yote ni hao wanye mali na walioundiwa vyombo vya kuwalinda. kama sio kweli mlalahoi gani mwenye uwezo kununua "mkono wa ndugu yako kwa milioni 30?"

3. Tunaringia nchi yenye jeshi la polisi magereza na hata la wananchi kwa sababu hizo nilizozitaja hapo juu.

4. Tunaringia nchi, ambayo yeyote mlalahoi ilimradi awe mzungu, aje ni mfuko wa rambo yenye shati lake lakini ndani ya miezi 5 anaondoka na brifcase iliyojaa mamilioni ya dola za kimarekani. Kama huamini, jiulize kina rich walianzisha kampuni ya dola 100, walipataje mradi wa mabilioni kuzalisha umeme. NDUGU YANGU WEWE HAYA MACHACHE NA MENGINE MENGI HUYAONI?

UKIONA KUELEWA MENGI YALIYOPO MUULIZE ZITO (ZZ) ANAWEZA KUKUELEWESHA ZAIDI UKAFAHAMU KIRAHISI.
 
Tutaendelea kuwa confused, mpaka tutakapo amua kuwa na akili ya wananchi wa kenya kukataa kubuluzwa.

hivi tukiamua tusipige kura kwa kigezo kwamba hatuoni mtu wote ni wezi itakuwaje? utashitaki nchi nzima, tunahitaji misimamo ya kiukweli.

Ahsnte sana Caroline Danzi........hakuna atakaeshtaki nchi nzima mie mwenyewe nitakuwa mstari wa mbele kutokupiga KURA!!!!!!!!!!!!!![/COLOR
 
Siku mkulu wa kaya atakapojiuzulu na kuitishwa uchaguzi.....I will instantly fly to Tanzania just to be "part of the history!"
its so unfortunate that it will never happen.Sheria/katiba butu,uongozi butu,wananchi elimu duni,huduma za afya ziiii....Hivi hasa tuna kipi cha kujivunia???

If JK is not part of the solution then he is part of the problem.
 
Of coz JK is part of the problem. Kama kiongozi wa nchi hatamki neno na yote yanayotokea walio chini yake wanaona kwa nini kujisumbua wanasema ilimradi liende as long as pay cheque ipo na rushwa inapatikana who cares.Solution itapatikana 2010 kama upinzani ukichukua madaraka maana itawaburuza waheshimiwa wote mahakamani.
 
sikilizeni ndugu zangu, tunae muona mtu wa maana ndio ane tumaliza, tulitegemea tuna chagua kijana mwenzetu ambaye ataiendeleza nchi na kuwamaliza wazee wa CCM AKA majambazi lakini naona tumekosea sana, Huyu raisi wetu ndio kiongozi wa wizi wote huu, je jiulize mbona mambo madogo madogo anafatilia sana na watumishi wa umma wenye nyazifa ndogo ndogo wamesimamishwa kazi bila maelezo lakini wizi wakuu wanao ifilisi nchi anawajua vizuri sana lakini hakuna anacho kifanya. Rostam ni best friend wake na je kuna mwizi mkubwa Tanzania zaidi ya Rostam??? Inamaana Kiwete Hajui? Au wako share?
 
Well said Mkjj, Huwa nikifikiria hata ile kesi ya maziwa ya watoto China of which in 4 months it was closed na wanaendelea na mambo mengine. Mimi nadhani sisi pamoja na kuhusika kwa Mkulu lakini hatuna utamaduni wa kumaliza mambo. Tunaendekeza sana longo longo! Tungekuwa na utamaduni huo ina maana wananchi wangekuwa wanademand kuona mwisho mapema wa kila ishu kubwa kubwa. Lakni hapa tukiambiwa iko mahakamanindio basi tena.

Look at Mahalu's case how many yrs bro?????

Mkuu nadhani tatizo linaanzia kwa wananchi kama wangekua wanatia msukumo na kuonyeshwa kuchoshw nadhani nao wangetia mkazo
 
Sasa jamani wakamataji, washitaki, wahukumu ndio hao hao waliopewa madaraka na watuhumiwa unategemea nini? ila kila kitu kina mwisho, tunaona wenzetu wanafanyaje tunajifunza taratibu, watalipa tu hata kama ni wajukuu wao WATALIPA KILA SENTI THAT IS A PROMISE
 
Back
Top Bottom