Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Udhamini wa gofu kuboreshwa
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 4th December 2010 @ 20:00 Imesomwa na watu: 30

KAMPUNI ya Zantel imepanga kuimarisha udhamini wake kwenye michuano ya gofu ya kila mwezi ‘Monthly Mug' inayofanyika kwenye Klabu ya Gymkhana Dar es Salaam.

Nahodha wa gofu klabuni hapo, Joseph Tango alisema hayo jijini Desemba 3 na kuhamasisha wachezaji zaidi kujitokeza.

Tango alisema Zantel ambao kwa mara ya kwanza wamedhamini michuano ya Mug ya Novemba wameahidi kuendelea kuboresha zaidi udhamini wao na washindi kuondoka na zawadi nono.

"Napenda kuwahamasisha wachezaji kujitokeza kwa wingi kwenye michuano ya mwezi Desemba ili kuongeza msisimko.

"Tunashukuru kwamba hata wadhamini wetu Zantel wameahidi kuboresha zawadi, hivyo ni vema kuwaunga mkono," alisema.

Tango alisema mashindano ya Mug mwezi huu yamepangwa kufanyika Desemba 18 kwenye viwanja hivyo.

Katika mashindano yaliyopita Tango mwenyewe alikuwa mmoja wa washindi na kuondoka na simu aina ya Blackberry.

Mbali na Tango washindi wengine kama chipukizi Vailet Peter pia waliondoka na simu akiwa bingwa kwa upande wa wanawake kwenye mashindano hayo ya siku moja yanayoshirikisha wanaume na wanawake.

Mashindano hayo ya Desemba pia yatakuwa yanafunga msimu wa Mug mwaka 2010.
 
Tanzania iige kwa Ivory Coast, Malawi

ban_tahariri.jpg

amka2.gif
SHIRIKISHO la soka Tanzania (TFF) ndilo mama wa soka hapa nchini kwa sababu ndilo linalotazama na kuona maendeleo ya soka kuanzia vijana hadi timu ya taifa, ikiwa ni pamoja na maandalizi ya mashindano ya kimataifa. Pamoja na sifa hizo, ina mipangilio ambayo mingine haitekelezwi ama kufanyiwa kazi ipasavyo kutokana na kujisahau au wakati mwingine ni makusudi ambayo yanapoteza mwelekeo wa maendeleo tajwa.
Tanzania Daima tumeguswa na mashindano ya mwaka huu ya kuwania Kombe la Chalenji yaliyodhaminiwa na kampuni ya East Africa Breweries Limited (EABL) kupitia bia yake ya Tusker; mashindano ya mwaka huu yamekuja kwa kualika nchi ambazo maendeleo yake ya soka yako mbele zaidi ya nchi wanachama wa CECAFA.
Kiutendaji CECAFA wameona ni jambo jema kualika timu zenye maendeleo bora ya soka, kwa sababu imedhamiria kubadili mwelekeo baada ya miaka iliyopita kushiriki mashindano hayo kwa timu wanachama pekee, jambo ambalo litajenga dhamira ya kweli ya kushiriki Kombe la Matifa ya Afrika na Dunia.
Nchi waalikwa katika mashindano ya mwaka huu ni Ivory Coast, Zambia na Malawi ambazo zote zimefuzu hatua ya robo fainali baada ya kuonyesha uwezo uwanjani, ingawa awali ilikuwa mashindano hayo yashirikishe Cameroon, lakini haikujitokeza.
Kwa mfano kama huo, si vibaya kwa TFF kulichukulia hilo kama changamoto mojawapo ambayo itafikisha soka la Tanzania mbali kuliko ilipo sasa, jambo ambalo linatakiwa litekelezwe ipasavyo na sio siasa.
Nchi waalikwa katika mashindano ya CECAFA mwaka huu, zimeleta timu za vijana wakiwa na malengo ya mashindano ya Afrika yanayoshirikisha wachezaji wa ndani (CHAN) ambayo Tanzania bado tuna akili kwamba wachezaji walioko katika timu ya taifa ndio watacheza mashindano ya CHAN yajayo.
TFF kupitia Kurugenzi ya Ufundi isiwe na ‘mawazo mgando' ya kung'ang'ania kuwa na timu moja kila kukicha badala ya kutumia na vijana wa chini ya miaka 17 na 20 kama ambao wametumika na timu kama Sudan, Ivory Coast na hata Malawi ambazo ukiwauliza makocha wa timu hizo wanakueleza kwamba wanaandaa timu zao.
Inatakiwa TFF kuliangalia hilo kwa macho mawili kwa sababu, kuna timu ya vijana chini ya miaka 20 inayolelewa ambayo imeshashiriki michuano ya kimataifa ambayo inaweza kucheza mashindano kama ya Chalenji.
Ukiangalia Kilimanjaro Stars ina wachezaji ambao ni wa muda mrefu, ambao hawana miaka mitano mbele, jambo ambalo lilitakiwa ni TFF kuandaa timu ambayo itaziba nafasi ya wakongwe hapo baadaye.
Lakini mara nyingi, tumezoea hadi jambo litokee au liharibike kabisa ndipo tunashtuka, wakati ilitakiwa kujipanga mapema kuliko kusubiri.
Inatia hamu kuona wenzetu wakichezesha vijana wadogo ambapo soka la sasa linatakiwa kuchezwa zaidi nao, kuliko hapa kwetu wachezaji wakongwe ndio wanapewa kipaumbele zaidi ilhali zama zao zimepita.
Hata Somalia timu ambayo imefungwa michezo yake yote, imeundwa na vijana ambao pia ni wadogo ambao matunda yake yatakuja kuonekana muda si mrefu, sambamba na Malawi ambayo ilicheza soka la kueleweka kutokana na kuwa na vijana wadogo wenye vipaji.
 
h.sep7.gif
master.gif

Watanzania tuepuke vurugu michezoni
ban.mtazamo.jpg


Ally Daudi​

amka2.gif
NIANZE kwa kutoa pongezi za dhati kwa waandaaji wa mashindano ya Tusker Chalenji Cup 2010 yanayoandaliwa na Baraza la Vyama vya Soka Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kwani hadi sasa michuano hiyo inakwenda vizuri kama ilivyopangwa. Chalenji ni michuano ambayo inatambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) ikiundwa na nchi wanachama 11 ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Sudan, Ethiopia, Eritrea, Zanzibar, Somalia, Rwanda, Burundi na Djibouti.
Katika mtazamo wangu wa leo ningependa kulaani vitendo vya utovu wa nidhamu vilivyofanywa na mashabiki wa soka juzi wakati wa mchezo wa kusaka tiketi ya kucheza robo fainali ya michuano hiyo baina wenyeji Kilimanjaro Stars na dhidi ya Burundi ‘Indamba Murugamba'.
Katika mchezo huo na mingine mashabiki waliruhusiwa kuingia bure na CECAFA kwa lengo la kuhamasisha michuano hiyo baada ya mechi za awali kukumbwa na uchache wa mashabiki, lakini Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam likatoa angalizo kuwa idadi ya mashabiki wanaostahili kuingia itakapokuwa imetimia milango itafungwa na hakuna mtu atakayeruhusiwa kuingia ndani.
Nalipongeza Jeshi la Polisi kwa kuwa lilitoa tamko mapema kuwa kuingia ni bure lakini sheria ifuatwe na sio vinginevyo na kinyume na hapo jeshi hilo lingetumia nguvu kudhibiti hali hiyo kama ilivyotokea ambapo walilazimika kutumia mabomu ya machozi na njia nyingine za kutuliza fujo uwanjani hapo.
Ni dhahiri bila udhibiti huo wa jeshi na mashabiki kuachwa kuingia kiholela ingewezekana kutokea maafa makubwa kama yale yaliyotokea nchini Uingereza miaka ya nyuma na watu kadhaa kupoteza maisha.
Ilikuwa kauli nzito kutolewa na jeshi ambayo ilikuwa imezingatia kuepuka kutokea maafa ambayo yangesababishwa na mashabiki hao iwapo wangeachwa waingie kiholela bila kuzingatia idadi stahiki.
Katika mechi hiyo iliyomalizika kwa ‘Kilimanjaro Stars' kutinga robo fainali kwa kuichapa Burundi mabao 2-0, mashabiki ambao walikwama kuingia uwanjani baada ya uwanja kuwa umefurika walivamia baadhi ya milango ya kuingia na kuvunja jambo lililolazimu Jeshi la Polisi kuingilia kati na kutumia mabomu ya machozi ili kuwatawanya.
Idadi ya watu kuingia uwanjani inaeleweka kuwa ni watu 60,000 kamili kinyume na hapo ni uvunjaji wa sheria na uharibifu wa uwanja kama ilivyotokea jana baada ya mashabiki kung'ang'ania kuingia uwanjani na hatimaye kuvunja mlango mkubwa wa kuingilia uwanjani humo.
Ni jambo lililowazi kuwa Watanzania tunapenda michezo lakini sheria na ustaarabu ni lazima vifuatwe tunapokuwa uwanjani kwani kwa kufanya hivyo tutaepusha madhara mengi yanayoweza kujitokeza katika michezo.
Kwa mtazamo wangu wadau wote wa michezo tunapaswa kuungana kuwalaani wale wote walioshiriki katika vurugu hizo ambazo hazikuwa na sababu ya msingi wao kuzifanya ilhali uwanja ulikuwa umeshajaa.
Nasema jambo hilo si la kibusara hata kidogo kwani tusingeingia bure au tungewahi kufika uwanjani mapema haya yote yangetokea? Sasa ni wakati wa Watanzania kubadilika na kuacha kung'ang'ania vitu visivyowezekana ili kuepusha vurugu na uvunjaji wa amani tuwapo kwenye viwanja vya michezo.
Watanzania ni wakati wetu wa kujifunza ustaarabu wa kuwa watulivu pindi tunapokuwa uwanjani kutazama mechi, swali la kijiuliza: je, isingekuwa kuingia bure wote mngeenda Uwanja wa Taifa? Natumai jibu litakuwa ni hapana, basi kama ni hivyo nalipongeza Jeshi la Polisi kwa kazi nzuri lililoifanya katika kuwadhibiti wahuni hao wachache waliotaka kuchafua taswira ya michezo nchini.
Nawaomba Watanzania waepuke vurugu wakati wakiwa uwanjani na kushangilia kwa amani kwani michezo ni burudani na sio vita kama wanavyofanya wenzetu waliopiga hatua katika nyanja ya michezo.
Lakini mwisho ni kwa waandaaji ambao ni CECAFA kujipanga upya na kuuondoa utaratibu wa bure ambao unaweza kusababisha maaafa kwa mashabiki wa soka.
 
CECAFA Tusker Challenge Cup na changamoto ya maendeleo soka
ban.blank.jpg


Makuburi Ally​

amka2.gif
HATUA ya makundi ya mashindano ya kuwania Kombe la CECAFA Tusker Chalenji 2010 ilifikia tamati jana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwa Malawi na Ethiopia kuumana huku Kenya na Uganda nazo zikionyeshana ubabe katika mechi za mwisho za hatua hiyo. Mashindano hayo yaliyoanza kutimua vumbi Novemba 27 kwa Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars' kufungua dimba kwa kupambana na Zambia ‘Chipolopolo' na kukubali kipigo cha bao 1-0.
Mbali ya wenyeji Tanzania Bara, nchi nyingine ni Zanzibar, Kenya, Uganda, Somalia, Sudan, Burundi, Rwanda huku Malawi, Ivory Coast na Zambia zikiwa ni waalikwa, ambapo kulipangwa makundi matatu ya A, B na C.
Kundi A ziko Zambia, Tanzania bara, Burundi na Somalia wakati B ni Rwanda, Zanzibar, Ivory Coast na Sudan huku C kuna Malawi, Uganda, Ethiopia na Kenya.
Timu zilizofuzu hatua ya robo fainali kwa kundi A ni pamoja na Zambia na Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars', wakati kundi B ni Ivory Coast na Zanzibar huku kundi C Malawi na Uganda zikipenya.
Kilimanjaro Stars imetinga robo fainali baada ya juzi kuiadhibu Burundi kwa mabao 2-0 wakati Zambia katika mchezo wake wa mwisho dhidi ya Somalia waliibugiza mabao 6-0, Desemba 3.
Hadi sasa, Felix Sunzu wa Zambia anaongoza kwa kupachika mabao akifunga manne aliyoyapata katika mchezo dhidi ya Somalia.
Wafungaji wengine ni pamoja na Shemeles Bekele wa Ethiopia na Nurdin Bakari wa Kilimanjaro Stars wenye mabao matatu kila mmoja, wenye mabao mawili ni Fred Ajwang wa Kenya, Davi Banda na Victor Nyirenda wa Malawi, Kipre Tchetche wa Ivory Coast Emmanuel Okwi na Ahmed Ali Shiboli wa Zanzibar.
Wenye bao moja kila mmoja ni Jean Paul Habarugira na Claude Ndikumana wote wa Burundi, Kipre Bolou na Fabrice Kouallo wa Ivory Coast, John Baraza wa Kenya, Dolidy Birori na Peter Kagabo wa Rwanda.
Wengine ni John Bocco na Henry Joseph wa Kilimanjaro Stars, Henry Kisseka na Simeon Massa wa Uganda na Venecious Mapande, Kennedy Mulenda na Allan Mukuka wa Zambia.
Udhamini wa michauno hii kati ya Baraza la Vyama vya Michezo Afrika Mashariki na Kati, (CECAFA), na Kampuni ya Bia ya Afrika Mashariki (EABL), kupitia bia ya Tusker umedhamiria kufikisha mbali nchi wanachama, ikiwa ni michuano mikongwe ya kimataifa barani Afrika.
Kampuni ya EABL, imedhamini mashindano ya mwaka huu kwa dola 450,000 za Marekani.
Kabla ya EABL kudhamini michuano ya mwaka huu, mwaka jana kampuni ya mawasiliano ya Orange ilidhamini michuano hiyo kwa dola 175,000 za Marekani.
Mkurugenzi wa EABL, Seni Adetu anasema, michuano ya mwaka huu ni mpangilio waliojiwekea kwamba, mojawapo ya nchi wanachama ishiriki angalau fainali za kombe la dunia nchini Brazil mwaka 2014.
Naye Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholaus Musonye anasema, ufadhili wa mwaka huu wamejipanga kushiriki Kombe la Dunia nchini Brazil baada ya kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2012.
Michuano ya mwaka huu, imeleta changamoto kwa nchi wanachama wa CECAFA na muelekeo wa kushiriki Kombe la Afrika na Dunia umeonekana kutokana na viwango vilivyoonyeshwa na timu shiriki mwaka huu.
Tukianza na Malawi ni timu ambayo imejipanga vizuri kwa ajili ya maendeleo ya baadaye kama michuano ya Afrika inayoshirikisha wachezaji wa Ligi za Ndani (CHAN), na mingineyo.
Malawi ni timu ambayo inacheza katika mfumo wa ushindani wa hali ya juu, kila mchezaji anajua jinsi ya kutumia nafasi yake ipasavyo na hata washambuliaji wakifika katika maeneo ya ufungaji wanafanya kile kinachostahili.
Timu hiyo, mara nyingi washambuliaji wake hupiga mashuti makali katika milango ya mahasimu wao, ambayo imefanikisha kuendelea kudumu katika michuano hiyo.
Kocha wa Malawi, Kinnah Phiri anasema, amekuja katika michuano hiyo kuendeleza uzoefu kwa wachezaji wake, akiwa na lengo la kufanya makubwa zaidi katika mashindano yanayokuja mbele yake.
Tukija Ivory Coast, ni timu ambayo ina vijana wadogo unaweza kuwafananisha na wale wa chini ya miaka 20 ‘U-20' ya Tanzania, ambao kocha wao anasema kwamba, amekuja katika mashindano haya kwa sababu wamedhamiria kushiriki kombe la CHAN.
Kocha wa Ivory Coast, Kouadio Georges anasema, katika mashindano haya amekuja kuwaweka sawa wachezaji wake ili aijenge timu zaidi kwa ajili ya michuano ya CHAN.
Georges anasema, kwa sasa amekuja kuifunza soka timu yake katika michuano hii, ambapo alipopata mwaliko wa kushiriki, aliona ndio nafasi pekee ya kuiweka vizuri timu yake.
"Wachezaji wangu nimetoka nao Ivory Coast wakiwa na uzoefu finyu na stamina ndogo, lakini hivi sasa imeanza kupiga hatua kutokana na kwamba wachezaji wangu ni vijana wadogo ambao wanafundishika," anasema Georges.
Kocha wa Somalia, Yousuf Adam, anasema alipewa timu hiyo ndani ya wiki moja akitokea Qatar anakoishi, ambapo amepata taabu kuitengeneza ndani ya wiki moja.
Adam anasema, lakini timu yake ni bora, ingawa hakuifahamu mapema ambapo akiendelea kuketi nayo itakuwa ni moto wa kuotea mbali kwa sababu ina vijana wadogo.
Adam anasema, alikabidhiwa timu hiyo nchini Djibouti ilikoweka kambi, ambapo kuja Tanzania ni mara ya kwanza na wala hakutarajia kufika hapa nchini.
Wenyeji Kilimanjaro Stars wana timu ambayo ina upungufu ambao unatakiwa ufanyiwe kazi na kocha mkuu, Jan Poulsen, ambao ni sehemu ya ufungaji ambayo inaigharimu sana.
Bingwa mtetezi wa CECAFA ni Uganda, ambayo mwaka huu imejipanga pia kuendelea kulishikilia taji hilo kutokana na kuonyesha soka la ushindani.
Wenzetu waalikwa wamejipanga kupitia michuano hii kwamba iwe ni changamoto ya kushiriki mashindano ya CHAN, ingawa na sisi tumejipanga kushiriki Kombe la Mataifa ya Afrika na Dunia.
Changamoto ya mashindano haya, inatakiwa ipande zaidi ya hapa kwa kuendelea kusaka namna na jinsi ya kushiriki Kombe la Mataifa ya Afrika na Dunia kuliko baadaye kubweteka.
Michuano hii iwe changamoto na chachu ya kweli kushiriki Kombe la Matifa ya Afrika mwaka 2012 na Kombe la Dunia mwaka 2014; ni jambo la kusubiri na kuona.
 
CECAFA haikusoma alama za nyakati
ban.blank.jpg


Juma Kasesa​

amka2.gif
MASHINDANO ya Kombe la Chalenji ndiyo makongwe barani Afrika, ikiwa yanaandaliwa na Baraza la Vyama vya Soka Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati CECAFA. Ni michuano ambayo inatambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Soka (FIFA), ikiundwa na nchi wanachama ambazo ni Tanzania Bara, Kenya, Uganda, Sudan, Ethiopia, Eritrea, Zanzibar, Somalia, Rwanda, Burundi, Djibouti, Malawi, Zambia na Zimbabwe.
Lakini baadaye, Malawi, Zambia na Zimbabwe zilijitoa baada ya kuundwa kwa Shirikisho la Soka kwa nchi za Kusini mwa Afrika (COSAFA).
Michuano ya mwaka huu inafanyika jijini Dar es Salaam ikishirikisha nchi 12, huku Zambia, Malawi na Ivory Coast zikiwa zinashiriki kama waalikwa ili kutoa changamoto kwa timu wanachama wa CECAFA.
Kwa kifupi michuano hii ilitokana na Kombe la Gossage lililofanyika mwaka 1926 hadi 1966, ikifuatiwa na michuano ya Chalenji Afrika Mashariki na Kati, 1965 hadi 1971.
Katika makala hii ningependa kuizungumzia michuano ya Kombe la Tusker Chalenji 2010, ambayo inaendelea jijini Dar es Salaam huku Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars' ikiwa mwenyeji wa michuano hiyo ambayo mechi zake zote zinachezwa Uwanja wa Taifa.
Mashindano ya mwaka huu, ni tofauti kidogo na miaka iliyopita kutokana kupata udhamini mnono wa dola 450,000 za Marekani, kutoka kwa Kampuni ya Bia ya Afrika Mashariki (EABL).
Kubwa ambalo ndiyo hoja yangu ya leo ni kitendo cha CECAFA, kutangaza ofa kwa mashabiki na wapenzi wa soka kuingia uwanjani bure kwa lengo la kuipa changamoto michuano hiyo ambayo ni sehemu ya kutangaza vipaji vya wanasoka wa ukanda huu.
Baraza hilo kupitia Rais wake Leodegar Chilla Tenga na Katibu wake Nicholas Musonye, walitangaza ofa hiyo baada ya kuona idadi ndogo ya mashabiki waliokuwa wakijitokeza kushuhudia mechi za awali, hata zile ambazo wenyeji wa michuano hiyo ‘Kilimanjaro Stars' walicheza.
Naupongeza uamuzi huo, kwa kuwa ulikuwa ni wa kishujaa ingawa ndani yake kuna hasara ya wao kukosa mapato yatokanayo na viingilio vya mashabiki, lakini hoja yangu ni kwamba, kama hasara hiyo ipo itakuwa waliitaka wenyewe kutokana kushindwa kujipanga kwa kusoma alama za nyakati.
Swali la kujiuliza, ni kwa nini mashabiki waingize mgomo baridi kuja uwanjani, ilhali CECAFA ilitangaza viingilio vya chini katika mechi za makundi hadi hatua ya nusu fainali.
Kushindwa kwao kuelewa hali ya hamasa ya soka kwa kipindi hiki ambacho michuano hiyo imeandaliwa, hasa ukizingatia michuano hiyo inahusisha timu ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars' ambayo ni sehemu ya timu ya taifa ‘Taifa Stars', ambayo katika siku za hivi karibuni imekuwa katika mwendo wa kusuasua katika mashindano ya kimataifa.
Ni ukweli usiofichika kuwa kufanya vibaya kwa Stars katika mechi ya kirafiki dhidi ya Morroco na Tanzania kuendelea kuporomoka katika viwango vya ubora vya FIFA, kumechangia kuwanyong'onyeza mashabiki kujitokeza kwa wingi uwanjani kushuhudia mechi za makundi za michuano hiyo.
Japo CECAFA iliamua kuinogesha kwa kuzialika timu za Ivory Coast, Zambia na Malawi kushiriki, bado hakukuwa na msisimo kwa mashabiki kujitokeza kulipa kiingilio kushuhudia mechi za mashindano hayo hadi pale ilipotangaza dezo.
Hapa ndipo ambapo CECAFA ya Tenga na Musonye walipaswa kupatizama na kufanya upembuzi yakinifu ili kujiridhisha hali halisi ili kuepuka aibu ya mechi kuchezwa na kuonyeshwa na kituo cha Televisheni cha kimataifa cha Super Sports majukwaa yakiwa matupu.
Nasema Baraza hilo limepata hasara, kwa kuwa lengo lake halikuwa mashabiki waingie bure na kwa kuwa linaendeshwa kwa kutumia fedha ambazo hutokana na michango ya wanachama wake na viingilio vya mechi wanazoziandaa.
Ni wazi watakuwa na maumivu ya kukosa mapato, ingawa wana ahueni ya udhamini wa EABL.
Ambacho nakitazama ni kwamba walibweteka na ujio wa timu za Ivory Coast, Zambia na Malawi wakiamini ni timu kubwa katika medani ya Soka Afrika ambazo zingewasisimua mashabiki kuja uwanjani wakasahau kuwa hicho hakikuwa kipimo cha wao kujiamini kwa kupitiliza.
Lakini kwa kuepuka aibu hiyo ya kuona soka ya ukanda huu inachezwa kukiwa na mashabiki kiduchu katika uwanja wenye hadhi ya kimataifa, CECAFA walilazimika kuchukua hatua ya kuruhusu mashabiki kuingia bure katika mechi za makundi, ili kulinda hadhi ya soka yetu kimataifa.
Sababu inayonisukuma kuwalaumu CECAFA, ni kushindwa kwao kuhamasisha mashabiki na wapenzi wa soka kujitokeza kwa wingi uwanjani, kwa kutoa matangazo katika vyombo mbalimbali vya habari, hili lilikuwa ni kosa jingine kubwa kwao kuingia katika mtego wa kutoa ofa ya mashabiki kuingia bure.
Inajulikana ulimwengini kote, soka ni biashara kwa sasa na ili uweze kupata faida ni lazima ukubali kuwekeza katika namna yoyote ile ili baadaye kuvuna ulichopanda, jambo ambalo baraza hilo lilishindwa kwa kushirikiana na wadhamini.
Haya ni makosa ambayo, CECAFA wanapaswa kujifunza nyakati zote ambazo watakuwa wakiandaa mashindano kuepuka kuruhusu mashabiki kuingia bure, jambo linaloweza kusababisha maaafa na uwanja kuharibiwa na wahuni wachache wasio na nia njema na soka na kuibuka kwa vurugu ambazo zinaweza kuleta hasara kwa taifa.
Si haramu kuruhusu mashabiki kuingia bure, lakini kwa hili halikuwa na sababu iwapo wangejipanga vema kusoma upepo unavyovuma na kuweza kuwahamasisha mashabiki kujitokeza kwa wingi uwanjani.
Kwa Tanzania kama mwenyeji wa michuano hii ambayo inaandaliwa na CECAFA, ambayo Rais wake anatoka Tanzania ni aibu kuona mashabiki wanajitokeza wachache uwanjani, hali ambayo inaweza kuonekana kimataifa kuwa hatuna hamasa ya michezo wakati dunia ikiwa inatizama kupitia Super Sport.
Kwa Tanzania ni aibu kubwa, kwa sababu kutojitokeza kwa wingi uwanjani kutachangia Stars kufanya vibaya na hatimaye kushindwa kulichukua kombe hilo ambalo walilitwaa mara mwisho mwaka 1994 jijini Kampala chini ya kocha marehemu Syllersaid Mziray.
Ni wakati wa baraza hilo kusoma hali ya upepo inavyovuma, pale itakapokuwa ikiandaa mashindano hayo ili kuepuka kuingia katika mtego wa dezo ambao umeshapitwa na wakati katika zama hizi ambazo soka inaendeshwa kwa fedha.



h.sep3.gif
 
Yanga, mchelea mwana kulia atalia yeye!
ban.blank.jpg


Mwandishi wetu​

amka2.gif
WASWAHILI wana misemo mingi yenye maana, lakini kwa leo nataka kutumia miwili pekee kwanza; "Aliyetota hajui kutota,' na pili ‘Mchelea Mwana Kulia atalia yeye'. Nimeamua kutumia misemo hii miwili ili ili kuwekana sawa katika kulizungumzia hili sakata linalozuka na kufutika ndani ya Yanga kati ya uongozi na mfadhili wao Yusuf Manji.
Nianje na hili la "Aliyetota hajui kutota", kwani imekuwa desturi kwa wanachama kusimama upande wa Manji na kuwashupalia viongozi lakini nimebaini kuwa uwepo wao unakuwa kwa ajili ya maslahi binafsi na sio kwa maslahi ya Yanga.
Niliwaona wana Yanga hawa tangu enzi za uongozi uliopita chini ya Imani Madega, walimpa wakati mgumu wa kuiongoza klabu hiyo mwanzo hadi mwisho wa uongozi wake.
Ingawa Madega alikuwa akiwaambia wazi kuwa ni yake ni kutetea maslahi ya Yanga, wao hawakumuelewa, waliendelea kumpinga pomzwaokila mara Mamsemo wa tunaoweza kuusema katika haya yanayoendelea sasa katika klabu ya Yanga, ambako baadhi ya wanachama wamekuwa hawasikii wala kuona kuhusiana na mfadhili wao Yusuf Manji.
Wanchama hawa kila unapotaka kulijadili suala la Manji wanakuja juu hata kabla hawajajua nini unachotaka kukiongea au kukizungumza kuhusiana na Manji, wametota.
Ndio maana kundi la wanachama na mashabiki wake walishindwa kumuelewa na kumpinga mwenyekiti wa klabu hiyo Davis Mosha, alipohoji uhalali wa mfadhili huyo kuwataka wachezaji kuwapigia kura viongozi.
Wapo waliosema mfadhili ana haki ya kufanya chochote ndani ya klabu hiyo, wengine wakasema anafanya hivyo kwa sababu fedha zinaliwa na viongozi huku wengine wakisema vibaya kabisa kuhusu viongozi wao.
Lakini nilichobaini ni kuwa wote waliokuwa wakimzungumzia au kumtetea Manji, hawajui hata hilo walisemalo, kwa maana hiyo ukijaribu kubishana nao au kutaka kuwaelewesha utapoteza muda wako bure.
Lakini waswahili husema mchelea mwana kulia atalia yeye'.
 
Mfumo huu unatupeleka kuzimu
ban.blank.jpg


Kenny Mwaisabula​

amka2.gif
HATA uniamshe usingizini, kwangu mimi nahitaji mataji (vikombe), kwa maana moja tu ya ubingwa, gombana na serikali, gombana na FIFA, gombaneni wenyewe kwa wenyewe, gombaneni na waandishi wa habari hadi mpewe majina ya mabondia, lakini mimi furaha yangu ni ushindi tena si ushindi tu ni kunyakua mataji. Nje ya hapo mimi sielewi na akili yangu inakataa kuelewa. Inawezekana ikasemwa sasa, uongozi uko imara sana tofauti na zamani, mipango ya fedha leo inaonekana vizuri na kwa uwazi zaidi tofauti na zamani,
Viongozi hawalumbani tofauti na zamani, wana utaratibu mzuri wa kuzungumza tofauti na zamani, kwangu mimi yote hayo yanapitia sikio moja na kwenda sikio la pili, sielewi kama siyaoni mataji, akili inakataa kukubali.
Katika moja ya makala zangu za nyuma, nadhani katika gazeti hili hili niliwahi kuandika tatizo la soka letu kuwa si kocha wa kigeni na nilisisitiza hata aje Sir Alex Furgerson wa Manchester United ya pale England, kwa mfumo huu tutaendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu.
Wengi waliniunga mkono, ingawa wachache walisema ninawachukia wale jamaa wa pale mjengoni Karume yaani TFF, lakini ukweli sina chuki yoyote na watu wale, kwanza Sunday Kayuni ni kaka yangu, penye matatizo na mimi anaweza kuniita wakati wowote kama mdogo wake, lakini katika suala linalohusu soka sishindwi kuweka bayana hisia zangu kupitia kalamu.
Tenga, ni lazima nikiri kuwa hanijui vizuri, hivyo sina sababu ya kumchukia mtu ambaye hanijui, mi' naandika kwa kueleza mustakabali wa soka letu na si vinginevyo.
Ni ukweli usopingika kuwa pamoja na mazuri yote ya uongozi wa Leodegar Tenga, lakini hatujawahi kucheka, yaani kuchukua kombe lolote na mbaya zaidi hata pale tulipotegemea tungefika angalau fainali kwenye fainali za CHAN, bado tulitolewa asubuhi tu.
Maana katika CHAN kwa taarifa yako sisi ndio tuliopeleka kikosi cha kwanza, wengine wote walipeleka vikosi vya pili, ndio maana mi' nasema katika hilo kila siku nitakuwa upande wa kushoto na kuwaacha rafiki zangu wapenzi kina Samson Mfalila na Eddo Kuwembe upande wa kulia na tukishirikiana katika ‘Monde' tu, mi' nataka mataji tu na si vinginevyo.
Pamoja na matatizo yote, mfumo mzima wa soka wameuua kina Tenga na Kayuni, leo hatuoni cha maana walichokifanya baada ya kuondoa zile ligi za madaraja ya nne, tatu, ngazi ya kanda daraja la pili na kuendelea mikoani; leo soka mahali ambako tulikuwa tunapata timu ya taifa haliko.
Utapataje watu kama kina Leopard Tasso Mukebezi ambaye alicheza mpira wake wote Kagera, Mohammed Chuma timu ya taifa miaka 11 bila kuachwa akitokea Mtwara, Kasimu Manga na Hussein Ngulungu, wakitokea Morogoro yaani Mji Kasoro bahari, Omary Zimbwe, Abdallah Luo, Omari Mahadhi wote hao Tanga.
John Lyimo, Mbwana Bushiri wa Moshi, Yunge Mwanansali Tabora na wengine wengi tu, unategemea nini?
Wakati leo Tanzania ina miundombinu rahisi kufika popote kwa siku moja tu, iwe unaenda Mtwara, Mwanza, Songea, Rukwa, Musoma, Kagera na kwingineko, TFF bado mmeng'ang'ania timu 12 tu katika Ligi Kuu, kwa nini zisiwe 20 ili angalau mchezaji wa ligi akapata mechi 35. Mimi napata taabu! Labda mnaweza mkasema mimi tu nashangaa, hata Babu Poulsen alishangaa nchi yenye watu karibu milioni 40 ina timu 12 tu za ligi kubwa kabisa ndani ya nchi na mchezaji anacheza mechi zisizozidi 22 tu kwa mwaka, ambazo kamwe hazitomfanya kuwa fiti tofauti na malengo ya FIFA ya mechi 40.
Hali hii imempa mashaka makubwa Babu Poulsen na kubaini kuwa kuna matatizo katika mfumo wa soka la nchi yetu.
Aidha, Babu Poulsen amegundua kati ya timu 12, zaidi ya nusu ya hizo, yaani saba zinatoka mikoa ya jirani, yaani Dar es Salaam na Morogoro na zingine kila moja inatoka Songea, Dodoma, Mwanza, Kagera na Arusha, mikoa yote iliyobaki haina hata ligi daraja la nne, wana ligi moja tu wameipa jina Ligi ya TFF, naduwaa!!
Mikoa ya Manyara, Mtwara, Singida, Rukwa, Mara, Lindi, Tabora, Kigoma, Kilimanjaro, Tanga, Shinyanga, Mbeya na mingineyo, ndio giza totoro, soka limekufa!
Wajumbe wao wa TFF, wanasuburi uchaguzi tu wapande ndege waje Dar es Salaam na wavute ‘mpunga' wao, kwao wenyewe hiyo tosha kabisa, wanasema soka sasa ndio limekua tofauti na zamani, mi' ndio hapo nashangaa, jamani mie mtu wa bara huenda Kiswahili sijui vizuri.
Leo Kombe la Chalenji linachezwa mara tatu ndani ya ardhi yetu, tayari giza limetanda sijui itakuwaje, tulitakiwa twende fainali za mataifa ya Afrika Ghana, tumeshindwa!
Twende Angola tumeshindwa! Twende Afrika Kusini Kombe la Dunia ndio kabisa tumeshindwa! Tumebaki tunasema uongozi ahaa bwana safi, tofauti na zile enzi za Chalenji 1994 au Kakakuona 1992 au Mataifa huru 1980, sasa huu usafi gani?
Mimi urafiki wa mshumaa siuwezi unawaka huku unateketea, sitaki kabisa nitasimama kwenye ukweli, napenda nione mataji basi na sio kauli nyingine.
Mheshimiwa Emmanuel Nchimbi, waziri mwenye dhamana ya michezo nchini, binafsi nakupongeza sana kwa kuchukua nafasi hii inayogusa hisia za watu moja kwa moja bila kujali elimu zao. Mheshimiwa utapata maneno mengi kutoka kwa watu wa aina mbalimbali, yaani wenye elimu ya juu kabisa hadi wale wa Ngumbalu na wote hao watakwambia wanalijua soka.
Mkuu wa nchi amekuamini, na moja ya maneno hayo utakayoyapata, mojawapo ni kutoka kwangu: TFF wameuharibu mfumo mzuri tuliokuwa nao awali wa ligi, onyesha makucha yako kama alivyofanya Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli kwa kumbana mbavu Mkurugenzi wa Wakala wa Barabara nchini, (TANROADS) na wewe shusha rungu lako kwa wale waheshimiwa wa pale mjengoni TFF, yaani Karume.
Shirikiana na wizara husika ili kurudisha thamani ya mwalimu shuleni, ili wapate fedha za kutosha na kwa wakati, ili wasishughulike na masomo ya ziada wala kuuza visheti, ili wajikite kufundisha kwa bidii wakati wa masomo, ili jioni vijana wetu tuwaruhusu wawepo michezoni.
Shirikiana na wizara husika, kuhakikisha wananchi wanarudishiwa viwanja vya wazi ili watoto wao wapate mahali pa kuchezea, shule nyingi leo zinaanzishwa hazina hata viwanja vya michezo, ni hatari kweli kweli.
Shule leo hii, eneo la kiwanja inajengwa shule nyingine, sijui watoto wetu watacheza wapi! Ukienda pale shule ya Msingi Kigogo, leo pembeni pana Mkwawa, Jamii haina habari na uwanja, pale Magomeni Shule ya Msingi Karume, pembeni yake kuna shule inaitwa Dk. Omary Juma ni balaa.
Ukiyafanya hayo, sasa rudisha michezo shuleni kivitendo, nje ya hapo utakuwa unatwanga maji kwenye kinu, usitegemee lolote.
Hayo ni machache tu kutoka kwangu, lakini mengi utaambiwa na wadau, kazi kwako kuchambua pumba na chuya.
Kombe la Chalenji leo liko ndani ya ardhi yetu, napata taabu kwa mfumo wetu kama kweli tutaweza kulibakisha nyumbani.
Michezo leo imekimbia, imeenda kwao, tumebaki kusifiana upuuzi.
Wako wapi wataalamu wale waliotuletea sifa na heshima mwaka 1994 kina Stephen Nemes, Dhikiri Mchumila, Deo Mkuki, Mustafa Hoza, Edibily Lunyamila, Nteze John, Mwanamtwa Kiwelu; siwaoni nabaki nashangaa, lakini kwa mfumo huu jamani hatuwezi kufika popote.
 
Bado ipo haja ya mdahalo wa michezo kitaifa
ban.blank.jpg


Mwandishi wetu​

amka2.gif
KARIBUNI tena wadau wa safu hii ya Uwanja wa Kuchonga iwajiayo kila siku kama ya leo, lengo kuu likiwa ni kupeana changamoto za kimichezo. Bila shaka mu wazima wa afya na mnaendelea na majukumu yenu ya ujenzi wa Taifa, ila kwa wale ambao hali zao si shwari tunawaombea nafuu.
Kama ilivyo ada, kabla ya kuperuzi kile kilichojiri Uwanjani leo, tukumbushane jabo kiduchu tulichokijadili wiki iliyopita.
Wiki iliyopita tulikuwa na mada isemayo, ‘Karibu uwanjani Waziri Nchimbi, lakini fitina si unazijua".
Hapo tulitumia nafasi hiyo kumkaribisha Waziri Emmanuel Nchimbi ambaye Rais Jakaya Kikwete alimteua hivi karibuni kuwa kinara wa Wizara ya, Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, akiwa na Naibu wake Dk. Funella Mukangara.
Tuliwakaribisha katika uga wa michezo, tukijua wazi wana kazi kubwa ya kuleta ufanisi katika sekta hiyo inayogusa kwa kiasi kikubwa jamii, hatimaye tushuhudie bendera yetu ikipepea vema katika anga za kimataifa katika michezo mbalimbali.
Tulimdokeza Waziri Nchimbi, mambo lukuki kuhusiana na udhaifu mkubwa ulioko kwenye vyama, mashirikisho na taasisi mbalimbali zinazosimamia michezo hapa nchini.
Michezo kutumika kama vichaka vya kufichia mambo ya kihalifu kama vile, usafirishaji dawa za kulevya, usafirishaji wa watu nje ya nchi isivyo kihalali ‘Trafficking' na ubadhirifu wa fedha ni vitu vinavyochafua sekta ya michezo hapa nchini.
Siku hizi watu wamekuwa wakihaha kuwania nafasi za uongozi kwenye mashirikisho na vyama vya michezo, lakini lengo kubwa likiwa ni kuja kujinufaisha kupitia michezo kwa njia moja ama nyingine, huku michezo ikiendelea kuzorota.
Kwenye michezo hivi sasa, fitna ndio umekuwa utamaduni wa kawaida sasa, ni vyma vichache ambavyo vinajiendesha vema bila kugubikwa na mizengwe, ambayo bila kuangaliwa vema huwa inasababisha mitafaruku mikubwa na hivyo kuzorotesha maendeleo ya mchezo husika.
Hivyo tulimwambia Waziri Nchimbi, awe makini na wadau ambao atakuwa akifanya nao kazi, kwani akiwaamini binafsi kupita kiasi na kusubiri ripoti tu mezani, basi amekwisha asishangae wakimuingiza ‘mkenge' na Tanzania kuendelea kuimba ule ule wimbo wake wa kichwa mwendawazimu au mtalii.
Baada ya kupeana dondoo hizo kwa uchache, sasa turejee katika mada yetu ya leo; ‘Haja ya mdahalo wa kitaifa kuhusu michezo bado ipo'.
Kama alivyoanza uongozi wake wa miaka mitano ya kwanza ya awamu ya nne ya serikali ya Muungano wa Tanzania, Rais Jakaya Kikwete, alijipambanua wazi kuwa ana kiu ya kuona michezo inakua hapa nchini na kulitangaza vema taifa kimataifa.
Rais Kikwete, alifanikiwa kwa kiasi kikubwa kurejesha hamasa katika michezo hapa nchini hususan soka, huku vilevile akianza kutia mkono katika michezo mingine kama vile riadha, ngumi na judo, ambako ameweza kufanikisha kupatikana wataalamu wa kimataifa.
Mbali ya kuletwa kwa wataalamu hao wa kimataifa, Rais Kikwete akilihutubia bunge la Muungano mjini Dodoma wakati akimalizia malizia miaka yake mitano ya awali, alieleza kuwa, baada ya kufanikiwa kutia hamasa kwenye soka, sasa anahamishia nguvu zake kwenye michezo mingine na kwa kuanzia ataanza na riadha.
Lakini kubwa ambalo wadau wa michezo walikuwa wakilisubiri kwa hamu ni ile ahadi ya kuandaliwa mdahalo wa kitaifa juu ya michezo.
Rais Kikwete aliwaagiza wahusika walishughulikie hili haraka iwezekanavyo, ambako kwa kiasi fulani wadau mbalimbali walianza kuandaliwa katika kuelekea mdahalo huo wa kitaifa juu ya michezo.
Wakati mambo yakiataka kuanza kunoga, wahusika wizarani walitangaza kuahirishwa kwa mchakato huo, moja ya hoja kubwa ikiwa Rais Kikwete kutokuwepo nchini wakati huo, hivyo isingekuwa vema kama ungefanyika bila ya yeye kuhudhuria.
Lakini kama ulivyo ‘utamaduni' wetu wa mambo mengi kuishia hewani, basi jambo hilo toka wakati huo imekuwa kimya na hakuna muhusika hata mmoja aliyejaribu hata kukohoa juu ya hilo hadi leo.
Mpango huo toka wakati huo umekuwa kimya na haijulikani kama ndio umekufa kabisa ama vipi.
Lakini, kimsingi kutokana na mazingira yetu kimichezo yalivyo hivi sasa, mdahalo huo ni muhimu na nina uhakika utaibua mambo mengi ya msingi yatakayotoa picha halisi ya mustakabali wa maendeleo ya michezo hapa nchini.
Wadau watakapopewa nafasi hiyo, hakika serikali, wadau kwa ujumla watapata nafasi ya kuchangia mambo kadhaa ya kututoa katika janga hili la kuvurunda katika michezo.
Hivyo, waliopewa dhamana ya kusimamia michezo, hebu lisemeeni hili, lipangeni haraka iwezekanavyo kuhakikisha wadau wanapata nafasi hii ya kujadili mustakabali wa michezo na Rais wao ili kutafuta tiba ya kweli.
Lakini hivi sasa ni kimya, kila mtu anapigana kivyake kuhakikisha mchezo wake unasonga mbele, lakini mafanikio mara chache kuwa mazuri kwani huwa hakuna mipango na usimamizi wa uhakika katika maeneo mbalimbali yanayohusika na michezo.
Hivi ili kupata tiba ya kweli katika maendeleo ya michezo hapa nchini, wadau tunasisitiza kuwa, bado ipo haja ya kaundaa mdahalo wa michezo kitaifa.
Bila shaka wahusika watalisikia hili na kulifanyia kazi. Kwa leo tuishie hapa kila la heri tukutane wiki ijayo tena uwanjani.
 
Club E yaihamishia burudani Las Vegas Dar
ban.blank.jpg


Mwandishi wetu​

amka2.gif
KULIKUWA na kila aina ya madoido na mvuto usiokuwa wa kawaida pale Club E, Ijumaa ilipoandaa moja ya maonyesho makubwa zaidi mwaka huu nchini, likijulikana kama ‘Club E Vegas Night 2010'. Wengi katika hadhira ile, walipata kila walichopenda katika shoo hiyo kabambe iliyovuta wengi na kukutanisha watu wa aina tofauti katika kile kilichoitwa ‘Club E Vegas night 2010'.
Baadhi ya wageni walipata fursa ya kupiga picha na warembo, ambao walikuwa wamejipanga pembeni mwa gari la aina ya ‘Limousine' lililopamba lango la ukumbi wa mikutano wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Mbele ya hadhira ya watu zaidi ya 1,000 Mkuu wa Sakafu aliyevalia kwa mitindo ya kizamani, bila kusahau mwonekano wa Afro, aliruka jukwaani huku akiunguruma kupitia kipaza sauti chake, akieleza nini hasa ilikuwa maana ya usiku ule wa Vegas.
Ama kwa hakika, kulikuwa na uwiano mzuri pale ukumbini, watu wakikaa vyema, ‘Screen' nyingi za televisheni kumwezesha kila mmoja kuona apendavyo, mwanga angavu kutoka darini ukishajihishwa na rangi nzuri zikichanganywa na zile nyeusi na nyeupe kutani kiasi cha kuifanya hadhira ijisikie nyumbani, kwani japokuwa walikuwa ‘Out' ilikuwa furaha tupu.
Makundi matano ya muziki, ikiwamo bendi ya Malaika kutoka Afrika Kusini iliyojishindia tunzo kadhaa, zilikonga nyoyo za mashabiki katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City ambapo Ijumaa ilibadilika na kuwa mithili ya jengo la starehe na thamani kubwa la Las Vegas, ukizungukwa na utamaduni wa Casino hiyo maarufu duniani.
Kwa saa kadhaa baada ya saa 4 usiku, waliionyesha hadhira iliyokuwa bado imara kabisa nini hasa hufanya kwa dansi, wakicheza kama umeme, huku wakihamasisha kwa vionjo vya aina yake vyenye nguvu vya Kiafrika.
Maandalizi yakiwa makini, yenye uangalifu mkubwa na usalama ukiimarishwa kukidhi matakwa ya makutano yale ya kimataifa ukumbini, kulikuwa na steji tatu za bei mbaya kama zilivyo kwenye makasino, huku wadau wakionekana katika michezo kama kamari, gurudumu la bahati, ndoa chapchap, kula, kunywa na wengine wakicheza kuendana na mipigo mbalimbali iliyokuwa ikiporomoshwa.
Dakika chache kabla ya saa mbili usiku, kundi la wasichana, wakiwa wamevaa nguo nyekundu waliingia na kuonyesha ubunifu wa aina yake katika kucheza dansi kwa nyota waliojiandaa kuupamba usiku ule.
Wane Star aliingia na kundi lake la ngoma za jadi na kuburudisha kwa dakika 30 kwa miondoko ya Kiafrika.
Ili kuiweka hadhira sawa kwa ajili ya shoo kabambe ya Kibara, liliingia kundi jingine la wasichana, hawa wakiwa wamevalia nguo za rangi ya Zambarau, wakicheza kana kwamba ni zama za wasichana wa shule enzi hizo.
Bendi ya Malaika kutoka Afrika Kusini waliingia jukwaani na kibao chao cha pili, wakimudu kuwanyanyua wengi katika hadhira kwenye viti vyao kwa ajili ya kucheza. Washindi hao wa tuzo kutoka kwa Madiba, walitetemesha wengi kwa jinsi walivyotumbuiza kwa nguvu kama umeme, dansi yenye mchanganyiko wa Afro – Pop ikiwekwa vionjo vya kijadi vya Kwaito, kukiwa pia na vionjo vya Club, Soul, Mbaqanga, Pop-Rock na dansi yenyewe ya kawaida.
Ikaingia tena bendi ya Baucha, ikijumuisha vijana wanne waliovalia nguo nyeusi, wakirejesha miondoko ile ya nyota wa Pop duniani, hayati Michael Jackson na kwa hakika mapigo yao yalikuwa na mashiko kwa hadhira katika kipindi cha zaidi ya dakika 50 walichopewa.
Hatimaye usiku wa saa sita iliingia bendi ya Twanga Pepeta, kwa mtindo wa aina yake, wacheza dansi wake 16 wakivutana.
Uwapo wa bendi mbili hizo ulikuza tija na ufanisi wao kwa ujumla, hasa kwa jinsi ya kukata kiuno Kiafrika, miondoko inayopendwa na bendi za Malaika na Twanga Pepeta, walitoa burudani ya aina yake usiku huo mwingi.
Kati ya waliohudhuria, walionekana dhahiri watumiaji wa Sigara ya Embassy ambayo ni bidhaa ya Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC), ambapo ilikuwa wazi kwamba mikutano ya aina ile, mara mbili kila mwaka ilimaanisha kitu kikubwa katika kuwaleta pamoja.
"Tumekuwa tukihudhuria shoo hiyo tangu mwaka 2007, tunaishukuru TCC kwa kutuleta pamoja kila mwaka, nafurahia kuwa hapa na niko tayari kurukaruka," alisema Munene Denis, mmoja wa wateja.
Club E, yenye wanachama zaidi ya 2000, ilianza mwaka 2007 na imekuwa ikiandaa hafla sehemu mbalimbali kote nchini mwaka mzima, kilele chake kikiwa ni Dar es Salaam kila Desemba.
 
Sudan nayo yafungasha virago Chalenji
• Kili Stars vs Amavubi, Zenji na Uganda robo fainali

na Makuburi Ally


amka2.gif
TIMU ya soka ya Sudan jana ilikamilisha idadi ya timu nne kuaga michuano ya ‘CECAFA Tusker Challenge Cup' baada ya kukubali kipigo cha mabao 3-0 kutoka kwa Ivory Coast mchezo uliopigwa uwanja wa taifa, jijini Dar es Salaam. Timu hizo ambazo zote zina vijana wadogo, zilianza mchezo huo kwa kushambuliana kwa zamu ambapo katika dakika ya 14 Diou Sed Marc alipiga shuti kali langoni mwa Sudan lakini kipa Muner Elkhair alilitoa nje na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda.
Baada ya kukosa bao hilo, Ivory Coast waliendelea kulishambulia lango la Sudan, lakini mabeki walikuwa makini na kuondoa madhara yaliyojitokeza langoni mwao.
Pamoja na kuzuia huko, Sudan waliruhusu bao katika dakika ya 36, lililofungwa na Kone Zoumana aliyeunganisha pasi safi ya Kipre Tcchetche.
Baada ya bao hilo, Ivory Coast iliendelea kulishambulia lango la wapinzani wao, lakini hadi mwamuzi wa mchezo huo, Bamlak Tessema anapuliza filimbi ya mapumziko, Ivory Coast ilikuwa mbele kwa bao 1-0.
Kipindi cha pili, Ivory Coast iliendelea kushambulia lango la Sudan na kufanikiwa kufunga bao la pili dakika ya 59, mfungaji akiwa Kipre Tchetche kwa adhabu ndogo, baada Kone Assane kuchezewa rafu na beki wa Sudan Ahmed Abdallah.
Tchetche, alifunga kitabu cha mabao kwa kukandamiza la tatu katika dakika ya 77, baada ya kupokea pasi safi ya Kouame Desire Magloire.
Katika mchezo wa pili, Uganda iliendeleza ubabe kwa Kenya baada ya kuiadhibu kwa kuichapa mabao 2-0.
Mchezo huo uliochezeshwa na mwamuzi wa kimataifa, Israel Nkongo, hadi kipindi cha kwanza kinamalizika, matokeo yalikuwa ni 0-0.
Kipindi cha pili, timu hizo zilirejea uwanjani huku kila mmoja akiwa na ari ya kumfunga mwenzake, lakini mabeki wa kila timu walikuwa makini na kuondosha hatari.
Uganda ilifanikiwa kufunga bao la kwanza dakika ya 83 lililowekwa wavuni na Emmanuel Okwi, baada ya kuwalamba chenga mabeki wa Kenya na kuukwamisha mpira wavuni.
Baada ya bao hilo, Uganda waliendelea kulisakama lango la Kenya na katika dakika za nyongeza, kipa wa Kenya Boniface Oluoch alionyeshwa kadi nyekundu baada ya kumkanyaga kwa makusudi mshambuliaji Steven Bengo ambapo mwamuzi Nkongo aliamuru ipigwe penalti.
Beki Andrew Mwesigwa, alifunga penalti hiyo, huku langoni akiwa mchezaji wa ndani Mulinge Ndetto.
Hadi dakika 90 zinamalizika, mabingwa watetezi Uganda waliibuka kidedea.
Timu zilizotinga robo fainali ni mabingwa watetezi Uganda, Malawi, Zambia, Tanzania Bara, Zanzibar, Rwanda, Ivory Coast na Ethiopia huku Sudan, Somalia, Kenya na Burundi zikifungasha virago.
Katika hatua ya robo fainali, Zambia itaumana na Ethiopia, Malawi na Ivory Coast, huku Zanzibar ikikipiga na mabingwa watetezi Uganda wakati Kili Stars itaumizana na Rwanda.
 
Kumekucha Simba, Yanga


na Mwandishi wetu


amka2.gif
VIGOGO wa soka hapa nchini Simba na Yanga za jijini Dar es Salaam leo zinatarajiwa kuanza kujinoa kwa ajili ya kukabili mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara unaoanza kutimua vumbi Januari 15 mwakani. Wakizungumza kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam, maofisa habari wa klabu hizo walithibitisha timu zao kuanza programu za mazoezi leo kwa kuanzia na gym.
Ofisa Habari wa mabingwa watetezi Simba, Clifford Mario Ndimbo, alisema, mazoezi yatakayoanza leo yatakuwa chini ya kocha msaidizi Amri Said ‘Jap Stam', huku akisubiriwa kocha mkuu, Mzambia Patrick Phiri.
Kwa upande wake, Ofisa Habari wa Yanga Louis Sendeu, alisema, pia nao wataanza na gym chini ya kocha mkuu, Mserbia Kostadin Papic huku wakiwasubiri nyota wao walioko timu za taifa za bara na visiwani ambao wanashiriki michuano ya Chalenji inayoendelea jijini Dar es Salaam.
Klabu hizo zimeimarisha vikosi vyao wakati wa dirisha dogo kwa kusajili nyota wawili kila moja, ambapo Simba imemnyakua mshambuliaji Ali Ahmed Shiboli kutoka KMKM ya Zanzibar na kumrejesha kundini beki wake Meshack Abel aliyekuwa kwa mkopo African Lyon huku Yanga ikimtwaa Davies Mwape na Juma Seif Kijiko kutoka JKT Ruvu ya Pwani.



h.sep3.gif
 
Waziri kuvalia njuga 'bifu' la CHANEZA, CHANETA


na Tullo Chambo


amka2.gif
WAZIRI wa Habari, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Abdilahi Jihad, amesema atalivalia njuga tatizo la uhusiano usioridhisha kati ya vyama vya netiboli vya Zanzibar na Tanzania Bara. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu kutoka Zanzibar juzi, Waziri Jihad alisema, licha ya kuwa mgeni katika wizara hiyo, lakini atakaa na wahusika ili kulijadili na kulitafutia ufumbuzi, kwani linaleta picha mbaya.
Waziri huyo alisema, amekuwa akiusikia mgogoro huo na kubainisha kuwa lazima kuna matatizo hivyo atayavalia njuga kwa kushirikiana na wenzake ili hali irejee.
Chama cha Netiboli Zanzibar (CHANEZA), kimekuwa kikigoma kushirikiana na Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA), kwa muda mrefu hivi sasa na kusababisha timu ya taifa ‘Taifa Queens' kuundwa na upande mmoja tu wa bara, huku hata ligi ya Muungano ambayo ilitakiwa kufanyika Zanzibar nayo hadi sasa haileweki.
Madai makubwa ya CHANEZA ni kuwa inatengwa na wenzao wa bara, jambo ambalo CHANETA inalipinga na kudai kuna kiongozi huko visiwani anaendekeza ubinafsi kwa maslahi yake.
 
Sasa AFC kupata viongozi halali Januari


na Ramadhani Siwayombe, Arusha


amka2.gif
UCHAGUZI wa kupata viongozi halali wa timu ya AFC ya Arusha inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara ikiwa inaburuza mkia unatarajiwa kufanyika Januari 8 mwakani. Akizungumza mjini hapa juzi, Mwenyekiti wa Kamati ya muda ya timu hiyo, Peter Temu, alisema kuwa uchaguzi huo utafanyika chini ya usimamizi wa kamati ya uchaguzi ya timu hiyo iliyo chini ya uenyekiti wa wakili Mediamu Mwale.
Temu alisema kuwa baada ya kupitia na kuhakiki leja ya wanachama na kujiridhisha, wamekubaliana na uamuzi wa kamati ya uchaguzi kuwa uchaguzi ufanyike tarehe hiyo.
Alitoa wito kwa wanachama wote wa AFC wenye kadi halali, kufuatilia majina yao kama yapo katika leja itakayotumika katika uchaguzi huo.
Alifafanua kuwa, wameamua kutoa wito huo kutokana na kushindwa kupata leja ambayo ilikuwa imekwisha hakikiwa, hivyo kulazimika kutumia ya
zamani ambayo ilikuwa na majina baadhi ya wanachama.
Alipongeza kuwa kutokana na timu kuongozwa kwa zaidi ya miaka mitatu na kamati za muda, uchaguzi huo utakuwa ndio suluhu ya migogoro yote ndani ya timu hiyo.
 
10 zathibitisha ligi ya kikapu Dar


na Juma Kasesa


amka2.gif
TIMU 10 za mpira wa kikapu zimethibisha kushiriki ligi ya mkoa wa Dar es Salaam (RBA), inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Desemba 18 mwaka huu uwanja wa ndani wa taifa jijini.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Mpira wa Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (BD), Mbaga Mwamboma alisema, karibu timu nyingi zimethibisha kushiriki.
Alizitaja timu zilizojitokeza kuwa ni Oilers, Pazi, JKT Mgulani, JKT Stars ,PTW, Airwing, Lady Lion, Azania na Zanaki.
"Maandalizi yanaendelea vizuri, ila kwa upande mwingine yanakwamishwa na timu ambazo hadi sasa hazijajitokeza ili kuthitibisha ushiriki wao," alisema.
 
British press rages over 2018 World Cup bid ‘fix'
Friday, 03 December 2010 21:45 digg

London. Britain's media yesterday lashed out at football governing body FIFA's "fixed" decision to grant the hosting rights for the 2018 World Cup to Russia, ending "humiliated" England's dreams of staging the event.
England's 15-million pound (23.3-million euro, 17.7-million euro) bid ended in abject failure, receiving just two votes from the 22 delegates, one of which was presumably cast by its own representative, Geoff Thompson.
"Fixed!" screamed an outraged Sun in its headline.
"Russians knew result," the popular tabloid continued, claiming that Russia bid chief executive Alexey Sorokin told the England team on Wednesday that it had already secured the required number of votes. Former England manager and Sun columnist Terry Venables branded the vote a "complete and utter sham".
"Maybe we should not be that surprised Russia got the vote to stage the 2018 World Cup," Venables said. "After all, FIFA and the KGB are just about the last two secret organisations on the planet."
The former Tottenham manager echoed the common belief held by the nation's media that FIFA is ideologically opposed to England.
"The bleeding heart liberals in Zurich, like they did with South Africa 2010, opted for legacy over logistics," he said.
"It is a great shame. A shame for England. A shame for football. And shame on FIFA," Venables concluded.
Fellow tabloid Daily Mirror was equally straightforward in its assessment, and also slammed the decision to grant the 2022 World Cup to Qatar.
"Russia, a mafia state rotten to the core with corruption; Qatar a medieval kingdom with no freedom of speech; Both are swimming in oil money," it splashed across its front page.
"How on earth did they persuade the dodgy fatcats at FIFA to give them the World Cup? SOLD," the paper concluded.
"Was the World Cup a stitch-up?" asked the centre-right Daily Mail.
"Amid strong suspicions of shady backroom deals, the tournament went to Russia, branded a ‘virtual mafia state' in leaked U.S. diplomatic cables this week," the paper reported.

The Times' editorial pulled few punches: "The system of World Cup elections is abysmally corrupt," it claimed. "It is too small, making it easily manipulated, and it is too secret, protecting it from scrutiny".

The paper, owned by Rupert Murdoch's News Corporation, also criticised England's bid.

"England fluffed it," the paper bemoaned. "England has the best stadiums, the best infrastructure and a passionate footballing culture. And yet it has no World Cup."
 
Three clubs dominate 2011 Rally calendar Friday, 03 December 2010 21:46 digg


By Miguel Suleyman
The Citizen Reporter
Dar es Salaam. The Automobile Association of Tanzania (AAT) has released a calendar of events for the 2011 rally season, six full status events starting with Vaisakhi Rally of Kilimanjaro in March.
Only three clubs have confirmed to host the national rally championship, according to Satinder Birdi, the convener of Tanzania Rally Commission.
Birdi named the clubs as Kilimanjaro Motor Sports, Tanga Motor Sports and Arusha-based AMSC.
The calendar indicates that Dar es Salaam would host two rounds of the National Rally Championship (NRC) under the AAT wing.
The Kilimanjaro Motor Sports Club (KMSC) will host the opening round on March 18, before AAT hosts the second round in Dar es Salaam on April 23 and 24 .
Zig Zag Rally planned to rev off May 28 and 29 in Tanga will be the third round, according to Birdi.
Arusha will host the fourth round of the event dubbed Nane Nane rally on July 9 and 10.
On September 5 and 6, AAT will host the fifth round of the NRC in Dar es Salaam. Arusha will once again play host to Guru Nanak Rally planned for October 15 and 16.
Three regions will jointly host the East African Safari Classic Rally scheduled for November 19 to 27.
The rally will use routes in Arusha, Tanga and Kilimanjaro to cover its Tanzania stage before crossing to Kenya on November 27.
 
Monday December 06, 2010 Sports
Ivorians ‘avoid' Kili Stars
12_10_7qthjc.jpg
IVORY Coast defender Goua Mahan Marc (left) tussles for the ball with Sudan midfielder Ramadhan Agab, during their Cecafa Tusker Challenge Cup match at the National Stadium in Dar es Salaam on Sunday. Ivory Coast won 3-0. (Photo by Yusuf Badi)




By DAILY NEWS Reporter, 5th December 2010 @ 12:00, Total Comments: 0, Hits: 244

IVORY Coast thrashed Sudan 3-0 at the Cecafa Tusker Challenge Cup to avoid a quarterfinal clash against hosts Kilimanjaro Stars, as defending champions Uganda swept archrivals Kenya 2-0 in the late kickoff to set up a date with Zanzibar Heroes.

Ivory Coast had an easy ride against their Group B opponents, Sudan at the National Stadium in Dar es Salaam and claimed their victory courtesy of Kone Zoumana's first half goal and two second half strikes by Kipre Tchetche.

The victory lifted Kouadio Georges' side on top of group B after reaching six points, while Rwanda dropped to second position on five points.

The results of the final group matches means that, Kilimanjaro, who held second position in Group A, will now meet Rwanda in the last quarterfinal on Wednesday, while Ivory Coast face Malawi in second quarterfinal tomorrow.

The quarterfinal fixture shows that group A leaders, Zambia, will lock horns with Ethiopia who succeeded to reach the last eight via a best loser slot.

Zanzibar Heroes, who marched into the knock out stage as qualifying best loser one, face a daunting task against the defending champions Uganda in third quarterfinal on Wednesday.

Ivory Coast, playing in the tournament as guest team alongside Zambia and Malawi, dominated the game for large parts against Sudan and were one up at the interval.

A good spell of possession, Zoumana provided the breakthrough for Kouadio Georges' side from a rebound in the 36th minute when he met a rebound after goalkeeper Muner Musa had
parried a powerful drive by substitute Kipre.

Earlier, Ivory Coast had their first shot on target in the 14th minute when Diou Sad Marc forced a fine save from Musa, three minutes the Ivorian striker then had another decent effort deflected for abortive corner.

Sudan came on the scene on 22 minutes with a sweeping move but Khamis Martin's final delivery could not find any of the red shirts, allowing the ball to roll on the face of the goal.

Sudan waged another meaningful attack after the half hour mark. Ramadhan Agab was released on the left flank; he controlled the ball, cut inside before releasing a weak low shot from the edge of the box that was easily collected by Ivory Coast custodian Sangare Ali at the near post.

Georges made an early substitution when he brought in Tchetche in the 34th minutes to replace Kouadio Fabrice, Sudan followed suit moments later, with Khamis Martin giving way to Mohamed Abdelmonem.

Ivory Coast maintained their passing game in the second half and Tchetche did not have long to wait before extending their lead with a clinical finish after, rounding off an eye-catching move by the Elephants.

Ivory Coast carved out a good chance in the 73rd minute when Marc fired a shot narrowly over the bar from just outside the area. Tchetche put the icing on the cake with his second of the day with the third goal after a nice exchange of passes among Ivory Coast players, and he could have even given himself with a hat trick, had it not been for a stunning save from Musa in the final minute of the game.

Meanwhile Emmanuel Okwi and Andrew Mwesigwa scored a goal apiece at the National Stadium to earn reigning champions Uganda bragging rights over sworn rivals Kenya.

Uganda needed to avoid a heavy defeat against the Harambee Stars in their final Group C match to make the quarterfinals of this year's Cecafa Tusker Challenge cup. The victory against the already eliminated Kenya put them top of the group with seven points.

In another development Jacob Mulee on Sunday resigned at Kenya head coach following their poor performance in the regional championship. Kenya lost all their three group matches to finish bottom of Group C.
 
Stars performance wins fans' approval


By DAILY NEWS Reporter, 5th December 2010 @ 12:00, Total Comments: 0, Hits: 166

SOCCER fans have praised Kilimanjaro Stars' brave performance in their 2-0 win against Burundi in a Cecafa Tusker Challenge Cup match played on Saturday, saying the show won back their hearts.

However, the fans were also quick to warn players not to be carried away by their recent wins, but keep their concentration and focus to win the tournament's silverware that has eluded the Mainland side for the past 16 years.

After a slow start to this year's regional championship losing 1-0 to Zambia, Stars bounced back to beat Somalia 3-0, and confirmed their place in the quarter-final with an outright win against Burundi.

Stars dominated from start to finish at the National Stadium in Dar es Salaam and won with a Nurdin Bakari brace. The Young Africans versatile player, who was deployed as central striker against Burundi, scored in either half.

Speaking after the match, Jamhuri Kihwelo, a local football coach was full of praise for Jan Poulsen's team.

"It was marvelous performance that pleased every football fan who watched the game, had they been playing with such intensity and energy fans would never complain," said Kihwelo.

He added: "I am personally very impressed and very proud of our team; that is exactly what all Tanzanians want from them; they should keep their feet on the ground." "The players showed commitment and desire to win.

I think that was the key element that has been missing in their previous games," commented Jamal Sariko, a youth soccer coach in Kawe area. "Kilimanjaro Stars showed us that they can put on excellent performances.

They should not wait until they feel the pressure to produce best football," added Feisal Rajab, who watched the game on TV. Kilimanjaro Stars coach Jan Poulsen said he was satisfied with the way his boys reacted to qualify for the quarter finals.

"We needed a good performance and we got one on Saturday. We played well especially in the second half and I am proud of the fact that we were able to create chances and take them because we had to win on Saturday.

We were greatly buoyed by the huge crowd that stood behind us throughout. When you are playing at home the fans must put pressure on players to perform," said the Danish tactician.

Poulsen hailed Bakari for his goal exploits as he said: "Bakari has a good vision for the game. He started the first match but after resting him for the second match, he has been a man reborn. He has great awareness and is able to get into goal scoring positions as we saw today which adds to our variety when attacking," he added.

"We did not play well on Saturday and I think our boys were unable to handle the pressure of the match.

They are all still young and the crowd was too much for them and we ended up making uncharacteristic mistakes," Burundi assistant coach, Niyongabo Amars told the post match press conference.
 
Monday December 06, 2010 Sports
Club E brings Vegas to Dar es Salaam

By DAILY NEWS Reporter, 5th December 2010 @ 12:00, Total Comments: 0, Hits: 41

IT was pomp and glamour as Club E on Friday hosted one of the year's biggest entertainment star-studded events in the country-'The Club E Vegas Night 2010'.

A fancy long stretch limousine and hostesses clad in hot pink cat suits welcomed guests at the entrance of Mlimani City Hall. It was clear that the night was going to be full of surprises.

Before over 1000 guests, the Master of Ceremony dressed in old school attire was entertaining with his impersonation of Elvis Presley. He set the mood of the guests to experience what the Vegas night was all about.

Five music groups including award winning Malaika band from South Africa performed to hundreds of the excited audience at Mlimani City's Conference, which had, on Friday night turned into a world class expansive casino reminiscent of the Las Vegas culture.

For hours after 10pm, they showed the energetic audience what they do best with their electrifying dance moves and powerful African melodies. At a few minutes after 8pm, a group of girls dressed in red had a creative dance which seemed to be the curtain raiser for stars who were to grace the night.

They had a remarkable similarity to that of Vegas showgirls. Wanne Star followed with his traditional group treating the audience to 30 minutes of African melodies. Then Malaika band from South Africa came on stage with their second song taking majority off their seats.

The award-winning South African music group gave an electrifying performance in all their dance-angled blend of kwaito-infused Afro-pop that drew on elements of club, soul, mbaqanga, pop-rock and dance music.

A special treat for the audience was the Baucha band who entertained the audience with a tribute to Michael Jackson. They moved the crowd with hits such as ‘Smooth Criminal' and ‘Heal the World.'

The likeness to the legendary artiste had the audience rushing on stage to exchange hugs with the performer. At a quarter past mid night Twanga Pepeta band finally landed on stage in style – with a 16 member dancing troupe in tow.

The presence of both bands boosted their performances, especially because of their African waist gyrating moves loved by both Twanga Pepeta and Malaika band. They staged a thrilling performance after mid night.

Club E started in 2007 and has been hosting functions across the country through out the year with the climax being in Dar es Salaam every December.

With more than 2,000 members now, the event is not only a boost to the entertainment industry but also a major social convener for different consumers of their product in the country.
 
Monday December 06, 2010 Sports
Club E brings Vegas to Dar es Salaam

By DAILY NEWS Reporter, 5th December 2010 @ 12:00, Total Comments: 0, Hits: 41

IT was pomp and glamour as Club E on Friday hosted one of the year’s biggest entertainment star-studded events in the country-'The Club E Vegas Night 2010’.

A fancy long stretch limousine and hostesses clad in hot pink cat suits welcomed guests at the entrance of Mlimani City Hall. It was clear that the night was going to be full of surprises.

Before over 1000 guests, the Master of Ceremony dressed in old school attire was entertaining with his impersonation of Elvis Presley. He set the mood of the guests to experience what the Vegas night was all about.

Five music groups including award winning Malaika band from South Africa performed to hundreds of the excited audience at Mlimani City’s Conference, which had, on Friday night turned into a world class expansive casino reminiscent of the Las Vegas culture.

For hours after 10pm, they showed the energetic audience what they do best with their electrifying dance moves and powerful African melodies. At a few minutes after 8pm, a group of girls dressed in red had a creative dance which seemed to be the curtain raiser for stars who were to grace the night.

They had a remarkable similarity to that of Vegas showgirls. Wanne Star followed with his traditional group treating the audience to 30 minutes of African melodies. Then Malaika band from South Africa came on stage with their second song taking majority off their seats.

The award-winning South African music group gave an electrifying performance in all their dance-angled blend of kwaito-infused Afro-pop that drew on elements of club, soul, mbaqanga, pop-rock and dance music.

A special treat for the audience was the Baucha band who entertained the audience with a tribute to Michael Jackson. They moved the crowd with hits such as ‘Smooth Criminal' and ‘Heal the World.'

The likeness to the legendary artiste had the audience rushing on stage to exchange hugs with the performer. At a quarter past mid night Twanga Pepeta band finally landed on stage in style – with a 16 member dancing troupe in tow.

The presence of both bands boosted their performances, especially because of their African waist gyrating moves loved by both Twanga Pepeta and Malaika band. They staged a thrilling performance after mid night.

Club E started in 2007 and has been hosting functions across the country through out the year with the climax being in Dar es Salaam every December.

With more than 2,000 members now, the event is not only a boost to the entertainment industry but also a major social convener for different consumers of their product in the country.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom