Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Daily News..............Stars host Kenya in a friendly............Former star Juma Mkambi dies.................

The Guardian....................Mkambi is no more...........................

the Citizen.........................Dar Stars, Zanzibar share the spoils....................

Uhuru...........ngasa aitosa Yanga na kubaki Azam...............................Juma Mkambi amefariki dunia......................

Nipashe...........Mgosi, Cannavaro washindwa kutambiana...........................

Tathmini............paulsen atimkia ligi ya daraja la kwanza..............................

Mwananchi..........................Kelvin Yondani, Kili Stars kuikabili Harambee.................

Champion...................Kochawa Argentina ambeba Abdi Kassim......................
 
Daily News....................Stars see Kenya as good test.......................Yanga, Manji set for rounds of talks...................

Uhuru Yanga yapata kiffa kipya kutoka Zambia....Mwape

Kwingineko...................Ivan, Asomoah waenguliwa yanga.........................Mamia wamzika Juma Mkambi.........Poulsen aska first eleven.................Ivory Coas na Zambia tishio kwa Stars challenge Cup.....................

Another test for Stars................Mbivu mbichi kujulikana leo kati ya Stars na Harambee.........
 
Champion..........Mfungaji bora wa Uganda atua Yanga.......................
Mseto: John Rocco; Simba letteni 400.......................

Mwanahalisi.........................Buriani jenrali Juma Mkambi.............................Mwaikimba aonyesha makali Stars............................................Aimairisha nyota ya Poulsen.....................................

Michuanoi ya Chalenji timu zaanza kuwasili................

Daily News...............................Stars cruise over Harambee.....................Zambia coach seek good CECAFA outing..................

Warithi wa Mwakalebela, Kaijage wajitokeza.............................................
 
champion..........mfungaji bora wa uganda atua yanga.......................
Mseto: John rocco; simba letteni 400.......................

Mwanahalisi.........................buriani jenrali juma mkambi.............................mwaikimba aonyesha makali stars............................................aimairisha nyota ya poulsen.....................................

Michuanoi ya chalenji timu zaanza kuwasili................

Daily news...............................stars cruise over harambee.....................zambia coach seek good cecafa outing..................

Warithi wa mwakalebela, kaijage wajitokeza.............................................

hivi jana mwaikimba alicheza dk 90?
 
Mwananchi................................Kipenga chalenji chapulizwa............................Waamuzi wanne watimuliwa...................Aahidi mabao...............Kifaa kipya cha Simba Ally Ahmed Shibori aliyetokea Duma ya Zanzibar..........................Tenisi BQ Open.....................Nigeria yaishtaki Guinea kwa kuchezesha midume...........................Majeruhi Fabregas, Eboue waitesa Arsenal....................Real Madrid yamtegema Mourihno kuiua Barca J'tatu...................................Rooney aomba radhi kwa mashabiki wa Man UTD.............................Amerika ya Kusini kuzibeba Hispania, Ureno..................Makinda England wauzwa kwa mkopo............................Mechi zote za Tusker chalenji kufanyika Uwanja wa Taifa..............................Poulsen aita mashabiki viwanjani............................Wakali Simba, Yanga kuiongoza Uganda Cranes........................."Yamtia Kiwewe Mulee"...................................Beki Z'bar Heroes atamba..........................Ratiba ya mazoezi Kili.............
 
The Saturday Standard of Kenya..................................................TOON v. BLUE ARMY...................Chelsea look for return to form at Newcastle...............................Wenger wants Mourinho punished.......................Manchester: I would have gone abroad-Rooney........................Berlin: Schaaf in last chance saloon.......................................Milan hope surging as Ibrahimovic powers on.............ENGLISH PREMIER LEAGUE FIXTURES........A.VIlla v. Arsenal.......(3.45pm).....................all others Kick off time is 6.0pm........................Bolton v. Blackpool.............................Everton v. West Brom................................Fulham v. Birmingham..............Manchester UTD v. Blackburn..................................Stoke City v. Man City...............West Ham v.Wigan............................Wolves v. Sunderland........................SUNDAY>.............................at 4.30pm...............Newcastle v. Chelsea.........................AT 7pm.........................Totenham v. Liverpool............................
 
The Saturday Standard of Kenya........................................CECAFA KICK OFF........................Somalia and Burundi first line up in Dar in such of 3.6 million prize......................Confident Uganda arrive, target hat-trick.........RIVARLY.......................Rivals Stars and the Cranes share hotel......................................CECAFA: Zanzibar to host 2011 club tourney...........................
 
Kili Stars simanzi, Bara yaanza vibaya .................Nipashe................Stars yalainika mbele ya JK

Yanga yaivutia kofia Simba.......................................

Majimaji yasaka kipa..................................Stars 0................................Zambia 1
 
The Guardian.....................Zanzibar Heroes shocks Sudan.................................

Daily News......................Gyptian thrills Dar fans.........................................Heroes win as Elephants flop.................

Majira.....................Kocha Zanzibar aipania Ivory Coast...............................

Habari Leo.............................Nyota mpya Simba aipigia Zanzibar bao 2...............................................

Nipashe...................Kocha Papic kurejea Yanga leo......................................

Zanzibar Leo................................Poulsen awatoa hofu mashabiki................Stars kufika fainali....................Simba waipamba Zanzibar haeroes......................

Shiboli apiga mbili......................

Kamati yanga kumjadili Mosha....................... kuhusiana na kujiengua.......................

Bingwa........................Papic kujitia kitanzi.................................

Champion..........................Ynaga yamwaga 40 Milioni kumnasa mganda.........................Yamtupa kipa mzungu Uganda......................
 
Bingwa......................Wapya Simba, Yanga hadharani..............................

Kili Stars kanyaga twende.............................

Mwanaspoti................................Mgosi: Straika mpya noma...........................

Uwazi.......................Jack chuzi amzimia Mnyika.............................

64 wawania mikoba ya Mwakalebela, Kaijage...............................

Muhidin Gurumo apata na nafuu.........................

Malawi, Uganda zafanya kweli...................zang'ara..............................

Stars kufufa matumaini leo....................................Jk watembelea Gurumo, Remmy Ongara Muhimbili Hospitali walikolazwa.................


Uganda trounce Ethiopia......................
 
Kilimanjaro Stars yashinda 3-0, lakini... Send to a friend Tuesday, 30 November 2010 20:32 0diggsdigg

Makoba Hassan
KILIMANJARO Stars imefufua matumaini ya kusonga mbele kwenye michuano ya Chalenji baada ya kuichapa Somalia kwa mabao 3-0 mbele ya maelfu ya mashabiki wake walioingia bure kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Kwa ushindi huo, Kili Stars wapo nyuma ya Chipolopolo ya Zambia na Intamba ya Burundi, ambazo jana zilitoka suluhu 0-0 na kufikisha pointi nne kila moja, zikiitangulia Kili Stars ambayo itamaliza ngwe hiyo kwa kazi pevu dhidi ya Burundi.

Ndugu zao, Zanzibar Heroes walioanza vizuri Jumapili kwa kuilaza Sudan 2-0, wana kibarua kingine dhidi ya Ivory Coast katika mchezo wa Kundi B.

Timu hiyo iliyoanza mchezo kwa kasi na kukosa nafasi lukuki, ilipata bao la kuongoza kwa penalti ya kipindi cha kwanza iliyofungwa na Henry Joseph ambaye kama Mrisho Ngassa, aling'ara katika mchezo huo.

Mabao mengine ya Kili Stars yalifungwa wachezaji waliotokea benchi, John Boko aliyechukua nafasi ya Thomas Ulimwengu ambaye mbio zake zilishindwa kumsaidia baada ya kukosa mabao mengi katika mchezo huo.

Naye kiungo Nurdin Bakari aliyeingia badala yaMohammed Banka aliyekuwa butu, alikamilisha ushindi kwa bao zuri baada ya krosi safi ya Ngassa, ambaye alipokea pasi ya Joseph.

Katika mchezo huo, mabeki wa Stars, Kelvin Yondani na Juma Nyosso walifanya makosa kadhaa ambayo laiti Wasomali wangekuwa makini, wangeweza kupata bao kupitia mshambuliaji wake Yassi Mohammed Idrissa.

Kocha Jan Poulsen alisema baada ya mchezo kuwa vijana wake walipata nafasi nyingi, lakini walishindwa kuzitumia, hata hivyo amefurahi kuona wameshinda.

Alisema mchezo dhidi ya Burundi utakuwa mgumu, kwani amewaona dhidi ya Zambia, wanacheza vizuri na atajipanga kuwakabili.

"Si mechi ya kubeza, Burundi nimewaona, ni wazuri, nitakutana na wachezaji wangu kuweka mkakati wa jinsi ya kuwakabili," alisema.

Naye Doris Maliyaga anaripoti kuwa Ivory Coast ambayo ilichapwa na Rwanda 2-1 imeshika mkononi tiketi ya Zanzibar Heroes kusonga mbele katika mechi ya leo.

Mchezo mwingine utakuwa baina ya Rwanda na Sudan saa 8 mchana.
Kocha wa Zanzibar Heroes, Stewart Hall amewaambia wachezaji wake wasitishike na majina huku nahodha Nadir Haroub akiwaeleza wenzake wasiwe nahofu lakini akawataka Watanzania wote kujitokeza kwa wingi ili washuhudie wimbi la ushindi.

Hata hivyo, Watanzania leo huenda wakamwona kiungo Abdi Kassim ‘Babi' akiwa na Zanzibar Heroes aliyetarajiwa kuwasili jana saa 9.00 mchana akitokea katika majaribio kwenye klabu ya Long Tang ya Vietnam, ambayo anaichezea pia Danny Mrwanda.

Kikosi hicho ambacho kinasifika kuwa na ulinzi mkali unaongozwa na nahodha wake Nadir Haroub na Aggrey Morris wakati safu ya ushambulizi ikiimarishwa na mshambuliaji mpya wa Simba, Ally Ahmed Shiboli.

Ivory Coast inaundwa na chipukizi wengi na ina kumbukumbu ya kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Wanyarwanda.
Stewart aliiambia Mwananchi kuwa Ivory Coast ni wazuri, lakini anaamini kikosi chake ni kizuri zaidi ya hao kutokana na maandalizi waliyoyafanya kabla ya michuano pamoja na jana akiisisitizia beki yake kuwa makini zaidi ili isiruhusu mabao.

''Naamini itakuwa mechi nzuri, lakini ngumu kwa sababu Ivory Coast ni wazuri pia wana kasi ya mchezo,nasi pia tumejiandaa vilivyo kuona tunakabiliana nao,''alisema kocha huyo.
 
TFF yawaombea ruksa wanafunzi waone mechi Send to a friend Tuesday, 30 November 2010 20:26 0diggsdigg

Calvin Kiwia na Sweetbert Lukonge

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limewataka viongozi wa shule mbalimbali nchini kuwaruhusu wanafunzi wao kwenda Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kushuhudia michuano ya Chalenji inyaoendelea .

Hatua hiyo imefuatia uamuzi wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) kuondoa viingilio katika michuano hiyo na kuwawezesha watu wote kuingia bure katika mechi hizo hadi kumalizika kwa hatua ya makundi.

Akizungumza na Mwananchi, Rais wa TFF, Leodegar Tenga alisema kuwa hatua hiyo itawasaidia wafunafunzi hao kujifunza mambo mengi ya soka kwa kuangalia wachezaji kutoka nchi zote zinazoshiriki michuano hiyo.

"Ningefurahi sana kuwaona watoto wa shule wakija hapa kuangalia mashindano haya ambayo kwa kweli nimefurahishwa na viwango vinavyoonyeshwa na wachezaji.

"Ningependa kuwaomba viongozi wa shule wawaruhusu watotot waje kutazama mechi kwa sababu katika kipindi hiki hakuna viingilio mpaka hapo hatua ya kwanza itakapokuwa imemalizika," alisema Tenga.

Katika hatua nyingine, Tenga amewataka wapenzi na mashabiki soka nchini kuendelea kuiunga mkono timu ya taifa ya Tanzania Bara , Kilimanjaro Stars licha ya kuanza vibaya mashindano hayo.

"Tusiache kuwapa moyo vijana wetu licha ya kuonyesha kiwango cha chini, hawa ni watoto wetu tusiwatupe.

"Jana (juzi) tulikaa nao pamoja na kocha Jan Poulsen na kwa pamoja ammegundua kosa lake na wameahidi kuhakikisha wanapigana kwa nguvu zao ili kurudisha imani kwa Watanzania.

Katika mechi ya kwanza, Kilimanjaro Stars ilipoteza kwa Chipolopolo kwa bao1-0 .

Nao wadau wa soka wamempongeza Tenga kwa kutambua umuhimu wao uwanjani na kuwaruhusu kuingia bure kwenye michuano ya Chalenji.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Mwananchi jana, jijini Dar es Salaam walisema wanamshukuru Tenga kuuthamini mchango wao pindi wawapo uwanjani na kuwataka viongozi wa soka nchini kuiga mfano wake.

"Kwa hili, Tenga ni kiongozi wa kuigwa nchini ,anajua kula na kipofu, tunamshukuru kwa kutambua mchango wetu uwanjani na tunamuahidi kujitokeza kwa wingi kuzishangilia timu zetu, Kilimanjaro Stars na Zanzibar Heroes," alisema mmoja wa mashabiki hao.

Tenga alitangaza juzi kuwa kutokana na mashabiki hao kumwomba kupunguza viingilio vya michuano hiyo, aliamua kufuta viingilio vya michezo yote ya Jumanne mpaka Ijumaa kwa lengo la kuwahamasisha mashabiki hao kuingia uwanjani kwa wingi kama inavyokuwa kwa mechi za watani wa jadi, Simba na Yanga.
 
Kocha Zambia aibashiria mema Uganda Send to a friend Tuesday, 30 November 2010 20:24 0diggsdigg

Jessca Nangawe

KOCHA wa Zambia , Dario Bonetti ameitabiria mema Uganda Cranes kuwa itafika mbali katika michuano ya Chalenji inayoendelea kwa sasa baada ya kuonyesha mchezo mzuri juzi dhidi ya Ethiopia.

Uganda ambao wapo Kundi C ndio mabingwa watetezi na juzi walianza vyema mashindano hayo baada ya kuitandika Ethiopia 2-1.

Akizungumza na Mwananchi wakati wa mchezohuo, Bonetti alisema timu hiyo imekuwa ikicheza mpira wa uzoefu hali inayoonyesha wana uzoefu mkubwa katika mashindano hayo na hivyo wana nafasi kubwa ya kutetea ubingwa wao kwa mara nyingine.

Alisema tangu mashindano hayo yaanze mwishoni mwa juma lililopita, amevutiwa na mchezo huo ambao ulikuwa na ushindani mkubwa kwa timu zote mbili na kuongeza kuwa endapo wataendelea na kasi hiyo katika michezo inayofuata wana nafasi kubwa ya kufika mbali.

Raia huyo wa Italia alisisitiza kuwa timu za ukanda huu wa Afrika Mashariki zimekuwa zikionyesha ushindani mkubwa katika michuano hiyo na kuongeza kuwa zina kila sababu ya kushiriki mashindano makubwa ya kimataifa ikiwemo kombe la dunia na fainali za Afrika.

"Nimeona uwezo mkubwa ambao umeonyeshwa na timu ya Uganda,ushindani ni mkubwa tangu mchezo wetu wa kwanza na Tanzania Bara pamoja na timu nyingine, lakini mchezo huu wa Uganda na Ethiopia umenionyesha ni jinsi gani soka la ukanda huu inavyopiga hatua,"alisema.

Uganda kesho watakutana kesho na Malawi katika mchezo mwingine wa Kundi C huku Kenya na Ethiopia, pia zikiumiza nyasi.
 
Phiri apanga mbinu za kuiua Cranes Send to a friend Tuesday, 30 November 2010 20:23 0diggsdigg

Doris Maliyaga

BEKI wa zamani wa kimataifa wa Malawi ambaye kwa sasa ni kocha, Kinnah Phiri amesema nguvu zake zote anazielekeza katika mechi ijayo tayari kuwakabili Uganda.

Malawi inajivunia mshambuliaji wake mahiri, Davis Banda aliyewafungia mabao mawili kati ya matatu waliyoshinda dhidi ya Kenya.
Akizungumza na Mwananchi, Phiri alisema kikosi chake alichokuja nacho ni kizuri na sasa anakiandaa vilivyo kuona anawafunga mabingwa hao watetezi.

''Kikosi changu ni kizuri, lakini naamini kitaimarika zaidi katika mechi ya pili mtaona mabadiliko kwa sababu nakwenda kukifanyia kazi ili kushinda mwechi yetu dhidi ya Uganda.

Malawi inajiandaa na mechi ya pili dhidi ya Uganda ambayo inashika nafasi ya pili ikiwa na pointi sawa na Mawalawi inayoongoza lakini ina idadi kubwa ya mabao.
 
Mourinho: Hatujaaibishwa na kipigo cha Barca Send to a friend Tuesday, 30 November 2010 20:22 0diggsdigg

MADRID, Hispania

KOCHA wa Real Madrid, Jose Mourinho amesema timu yake haikuaibishwa na kipigo cha mabao 5-0 dhidi ya Barcelona juzi.

Mabao ya Xavi, Pedro, mawili na David Villa na juhudi binafsi za Jeffren ziliiwezesha Barcelona kupata ushindi mnono na kukalia kiti cha uongozi Primera Liga.

Hicho ni kipigo kikubwa kwa Mourinho tangu aanze kazi hapa na kwingineko.

Katika mchezo huo, Real ilipata pigo baada ya beki wake, Sergio Ramos kutolewa kwa kadi nyekundu kwenye Uwanja wa Camp Nou.

Mourinho alisema kuwa kipigo hicho hakimnyimi usingizi na badala yake ataendelea na kazi yake kama kawaida.

"Timu moja ilicheza vizuri sana, nyingine vibaya ," alisema Mourinho . "Moja ilistahili ushindi na nyingine kipigo . Kuaibishwa ? Hapana . Ni rahisi kusahau kipigo hiki, lakini hatukuwa wazuri.

"Tuliwazawadia mabao mawili, tena kwa ujinga . Niliutazama mchezo .

"Nilijaribu kubadili mambo kadhaa wakati wa mapumziko, nikaweza, lakini muda si mrefu wakafunga tena, nami sikuwa na kitu zaidi cha kufanya, tukawa tumepoteza mchezo.

"Wiki moja iliyopita tulikuwa mbele ya Barca kwa pointi moja zaidi, leo hatuna pointi. Kama ambavyio nimesema mara zote , Barca ni timu iliyokamilika wakati Madrid bado ina safari ndefu."

Naye Pep Guardiola , ambaye aliulizwa kama kipigo kinaweza kumwondoa kibaruani Mourinho, baada ya ushindi wa 8-0 dhidi ya Almeria ambao ulimwondoa Juanma Lillo, alijibu: "Sidhani kama hili linaweza kutokea."

"Mchezo huu ni ushahidi wa tofauti baina ya timu hizi mbili. Zote ni nzuri, zilikuwa hazijafungwa, vinara wa ligi .
Leo (jana) wachezaji wangu walicheza vizuri na hiyo ndiyo tofauti.

"Kwa sasa ni rahisi kusema, sisi ni bora zaidi yao, lakini tusubiri tuone mbele ya safari. Miaka michache ijayo, tutaona . Wana kiwango kizuri, lakini tumewazidi.

"Kwa miaka miwili sasa, tumekuwa bora zaidi yao, Madrid na huu ndio ukweli. Kwa muda, tutakaa chini na kufurahia,'' alisema . Kwa siku chache zijazo tutakuwa wenye furaha."

Mshambuliaji Villa, ambaye alitumia vuziri pasi za Lionel Messi, alisema:
"Ni ushindi muhimu sana. Tumekuwa tukisaka ushindi, tumeupata. Pia, matokeo na jinsi yalivyopatika, ni vitu ambavyo vinavutia."
 
TI yataka mchakato wa uenyeji Kombe la Dunia usimame Send to a friend Tuesday, 30 November 2010 20:21 0diggsdigg

ZURICH, Uswisi

SHIRIKA la Kimataifa la Kupambana na Rushwa la Transparency International (TI) limelishauri Shirikisho la Soka la Kimataifa, Fifa kuahirisha uchaguzi wa nchi ambazo zitaandaa fainali za Kombe la Dunia ambao unafanyika Ijumaa.

TI imeshauri mchakato huo wa kupata wenyeji wa fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 na 2022 usimame kutokana na madai mapya ya rushwa.
Kamati ya utendaji ya Fifa inatarajiwa Ijumaa kupiga kura kuchagua nchi ambazo zitakuwa wenyeji wa fainali hizo kubwa za soka duniani.

"Tunashauri uchaguzi wa nchi ambazo zitaandaa fainali za 2018 na 2022, Desemba 2 usubiri kwanza madai yote ambayo yamechapishwa na vyombo vya habari yachunguzwe na kubainishwa ," ilieleza T I, tawi la Uswisi katika taarifa yake.

"Madai hayo yametia doa mpango mzima wa kupata wenyeji wa fainali zijazo za Kombe la Dunia ili kuepusha utata unaoweza kujitokeza ," iliongeza taarifa hiyo.

Gazeti la Tages-Anzeiger la hapa liliripoti kuwa Ricardo Teixeira wa Brazil, bosi wa soka wa Afrika, Issa Hayatou na mwenzake wa Amerika Kusini, Nicolas Leoz wanahusika katika ripoti ya siri ya malipo kutoka kwa mshirika wa Fifa aliyefilisika, ISMM/ISL zaidi ya miaka 10 iliyopita.

Kampuni hiyo ilifilisika mwaka 2001 kutokana na utata wa madai ya kutoa rushwa ili kupata haki za televisheni za kuonyesha mechi za kombe hilo, madai ambayo yalifikishwa mahakamani na Fifa, kisha kufutwa.

Mahakama moja ya Uswisi iliwatoza faini maofisa watatu waandamizi wa ISMM/ISL mwaka 2008 kwa matumizi mabaya ya fedha au makosa yanayohusiana na masuala ya uhasibu.

Leoz, pia alikuwa tayari ameorodheshwa kama mmoja wa watuhumiwa wa upokeaji malipo kutoka kampuni hiyo iliyokuwa ikijihusisha na masoko, kashfa ambayo iliyahusisha pia makampuni mengine kadhaa, madai ambayo yalifunguliwa katika mahakama za Uswisi mwaka 2005.

TI imeogeza kuwa hata kama madai ya sasa hayataweza kuthibitishwa, yanahitaji kuchunguzwa na tume huru ili kupat ukweli badala ya kamati ya maadili ya Fifa.

Maombi ya kupata timu wenyeji wa fainali za mwaka 2018 na 2022 ziliingia doa baada ya timu ya waandishi wa habari wa gazeti moja la Uingereza kufichua madai dhidi ya maofisa wawili wa kamati ya utendaji ya shirikisho hilo, Reynald Temarii, raia wa Tahiti na Amos Adamu kutoka Nigeria kuomba rushwa kwa lengo la kuuza kura zao.

Kumekuwa na hisia kuwa kura hiyo ya siri inaweza kuathiriwa na kukosekana kwa mwakilishi wa Shirikisho la Soka la Oceania (OFC) , ambalo limeombwa nafasi ya Temarii ijazwe kwanza na mtu mwingine.

Ingawa Fifa imesisitiza kuwa kura zitapigwa na wajumbe 22 kati ya 24 wa kamati yake ya utendaji, lakini mkuu wa timu ya maombi ya England ya fainali za 2018, Andy Anson aliwaambia waandishi wa habari kuwa anaamini wapigakura watakuwa 23.

"Ninaamini kuwa OFC watapewa nafasi ya kupiga kura ," alisema Anson .

Naye mwanasheria wa Temarii , Geraldine Lesieur, aliliambia Shirika la Habari la AFP kwamba Fifa ilimtaka aachane na mpango wake wa kukata rufaa kwa niaba ya mteja wake kupinga kufungiwa mwaka mmoja, baada ya kusafishwa dhidi ya tuhuma za hongo.

Hata hivyo , Temarii hajapokea ripoti kamili ya uamuzi wa suala hilo, hatua ambayo kisheria ina umuhimu mkubwa kumwezesha kuamua kukata rufaa au la, alieleza mwanasheria wake.

"Mteja wangu (Temarii)m ataamua baada ya kuarifiwa rasmi kupitia hukumu dhidi yake," alisema Lesieur. "Tunaendelea kusubiri."

Temarii ameiambia AFP kwamba kura yake angeitoa kwa nchi mbili ambazo zingechaguliwa na wakuu wa shirikisho la soka la Oceania.

Rais wa Fifa, Sepp Blatter ameahidi kuwa 'Fifa mpya' utateua watu makini kuandaa fainali za 2018 na 2022, akisema mabadiliko mengine yatafuata baadaye kwenye shirikisho hilo.

England, Russia, Hispania/ Ureno na Uholanzi/Ubelgiji zinaomba uenyeji wa 2018 wakati Australia, Marekani, Japan, Qatar na Korea Kusini zinaomba fainali za 2022.

Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, Mwana wa Mfalme William, Waziri Mkuu wa Russia, Vladimir Putin, warithi wa ufalme wa Qatar na Rais wa zamani wa Marekani, Bill Clinton watakuwa miongoni mwa wazito ambao watahudhuria mkutano huo wa kamati ya utendaji ya Fifa leo na kesho kuwashawishi wajumbe.
 
Kili Stars yachanua Chalenji


*Yaizabua Somali 3-0

Na Elizabeth Mayemba.

WENYEJI wa michuano ya Chalenji Tanzania Bara 'Kilimanjaro Stars' jana imechanua katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam baada ya kuifunga Somali mabao
2-0.

Kwa matokeo hayo, Kili Stars angalau imeresha matumaini kwa mashabiki wake ambao walipoteza, baada ya kufungwa bao 1-0 na Zambia katika mechi ya ufunguzi.

Mchezo huo wa jana uliweza kushuhudiwa na mashabiki wengi waliojitokeza uwanjani hapo, baada ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), inayosimamia michuano hiyo kuondoa viingilio kuanzia jana hadi Jumamosi.

Kilimanjaro Stars ililazimika kusbiri hadi dakika ya 43, kupata bao kwa mkwaju wa penalti baada ya uliowekwa kimiani na Henry Joseph. Penalti hiyo ilitolewa na mwamuzi wa mchezo huo kutokana na Shaban Nditi kuangushwa eneo la hatari.

Kabla ya bao hilo Kilimanjaro Stars ilikosa mabao dakika ya 7, 17, 25 na 37 nafasi ambazo washambuliaji wake, Salum Machaku, Thomas Ulimwengu na Mrisho Ngassa kushindwa kuzitumia.

Timu ya Bara ilipata bao lake la pili dakika ya 76 kupitia kwa John Boko ambaye alikutana mpira uliotemwa na kipa Somalia ambaye alishindwa kuudaka.

Kilimanjaro Stars ilihitimisha mabao yake dakika ya 88 kupitia kwa Nurdin Bakari aliyefungwa kwa kichwa baada ya kazi nzuri ya Ngassa, ambaye alipiga krosi nzuri iliyotua kwa mfungaji.

Katika mechi hiyo kama Stars ingekuwa makini ingeweza kuondoka na ushindi mnono kutokana na mabeki wa Somalia kujichanganya mara kwa mara kila mashambulizi yalipopelekwa golini kwao.

Mechi nyingine iliyochezwa mchana katika uwanja huo, timu za Zambia 'Chipolopolo' ma Burundi zilitoka suluhu katika mchezo mkali uliokuwa wa vuta nikuvute.

Michuano hiyo itaendelea tena leo ambapo mechi ya kwanza itazikutanisha Sudan na Rwanda na mechi ya jioni itakuwa kati ya Zanzibar na Ivory Coast.
 
Sherehe za Uhuru zaikwaza TFF


Na Mwandishi Wetu.

MECHI za awali za mashindano ya Kombe la Chalenji, zimeshindwa kupigwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kama ilivyopangwa awali kutokana na maandalizi ya
sikukuu ya Uhuru wa Tanzania.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Rais wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Leodegar Tenga alisema walipata maelekezo kutoka serikalini kwamba uwanja huo, utatumika kwenye sherehe za sikukuu ya Uhuru.

"Ni kweli tulipanga michezo ya awali ipigwe kwenye uwanja huo (Uhuru), lakini wenzetu wa serikalini wakatuambia tusiutumie kwa sasa mpaka watakapomaliza shughuli zao," alisema Tenga.

Alisema kutokana na hilo ndiyo maana wakaamua waombe michezo yote ifanyikie kwenye Uwanja wa Taifa, jijini licha ya uwanja huo kuendeshwa kwa gharama.

Akizungumzia kuhusu makato ya uwanja huo, alisema wanadhamini wameshamalizana na serikali kila kitu na endapo kama kutakuwa na madeni hakuna shaka watayabeba wao, kama wadhamini.

Akijibu kuhusu serikali kukiuka utaratibu waliojiwekea kwamba uwanja huo usitumike mara tatu kwa wiki, alisema hakukuwa na njia mbadala ndiyo maana wakaamua hivyo.

Alisema tayari mashindano hayo yalishatangazwa na timu zilishawasili, hivyo ingekuwa ngumu wasubiRi mpaka sherehe hizo za Uhuru zimalizike au kuahirisha mashindano.
 
Kozi ya ukocha wa kikapu kuanza leo


Na Amina Athumani

KOZI ya ukocha wa mpira wa kikapu, inatarajia kuanza leo katika viwanja vya Donbosco, Dar es Salaam ambayo itaendeshwa na mkufunzi kutoka Shirikisho la Kimataifa la
mchezo huo (FIBA) raia wa Kenya, Samwel Wanjohi.

Akizungumza kwa simu Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF), Alexanda Msofe alisema tayari mkufunzi huyo amewasili juzi usiku kwa ajili ya kuendesha kozi hiyo.

Alisema kozi hiyo imeandaliwa na TBF Kwa kushirikiana na FIBA Afrika na kwamba hiyo ni programu, inayoendeshwa na vyama vyote wanachama wa FIBA kwa lengo la kutaka kila mwanachama kuwa na maendeleo mazuri ya kufufua vipaji vipya vya mchezo huo.

Msofe alisema kozi hiyo itashirikisha makocha 26, kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania ambapo washiriki wake ni wale waliohitimu kozi ya awali ya ukocha ya Modulle 1, iliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

Alisema kozi hiyo itawawezesha makocha hao kutoa mafunzo ya kinadharia na vitendo katika mikoa watakayokwenda kwa ajili ya kufundisha makocha wengine wasiokuwa na elimu ya ukocha ya mchezo huo na pia itasaidia kuibua vipaji vingi zaidi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom