Miaka inavyokwenda, Congo inapoteza mvuto kimuziki

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,877
2,758
Nimekaa sehem napata flash back za congo. Nawasikiliza kabasele, mabelee, boziana, defao, wenge n.k. Ni nyimbo tamu sana ambazo ziko kwenye collection. Najiuliza, zile enzi zimeenda wapi? Sasa hivi congo wanaovuma ni kofi na fally. Slowly slowly Congo is losing the battle
 
che che che... Unapenda dezo dezo. Mh! Inauma. No tshala muana, no mbilia, no replacement
 
Kwa kweli sidhani kama Congo inapoteza coz ukienda kwenye ma international awards bado wamo tu. Sema nchi zingine zimeamka na wanatoa pia kanda nzuri nzuri. KAma hapa tanzania inakua rahisi kwa watu kuelewa mimbo ya kina ray c na jay d sababu ni kiswahili na pia wanapatikana hapa kwa concerts na charity. Kule Nigeria pia Music industry imeamka, baada ya apartheid South Africa inakuja na studio kali kali etc.
Kwa wanao penda mziki wa Congo (kama mimi) tunawaona wapo tu, na soko lao limeelekea nchi zingine zaidi ya east africa, ndio maana hawaji ku-promote mziki wao huku kama ilivo kua hapo zamani...
 
Kwa kweli sidhani kama Congo inapoteza coz ukienda kwenye ma international awards bado wamo tu. Sema nchi zingine zimeamka na wanatoa pia kanda nzuri nzuri. KAma hapa tanzania inakua rahisi kwa watu kuelewa mimbo ya kina ray c na jay d sababu ni kiswahili na pia wanapatikana hapa kwa concerts na charity. Kule Nigeria pia Music industry imeamka, baada ya apartheid South Africa inakuja na studio kali kali etc.
Kwa wanao penda mziki wa Congo (kama mimi) tunawaona wapo tu, na soko lao limeelekea nchi zingine zaidi ya east africa, ndio maana hawaji ku-promote mziki wao huku kama ilivo kua hapo zamani...
Labda kwa sababu ma-DJ wengi wa bongo ni bongo flavor lakin still muziki wa congo ni superior kwa bongo flavor yetu in terms of beats na organization ya muziki wenyewe. Wa kwetu ni vululu!
 
Kwa kweli sidhani kama Congo inapoteza coz ukienda kwenye ma international awards bado wamo tu. Sema nchi zingine zimeamka na wanatoa pia kanda nzuri nzuri. KAma hapa tanzania inakua rahisi kwa watu kuelewa mimbo ya kina ray c na jay d sababu ni kiswahili na pia wanapatikana hapa kwa concerts na charity. Kule Nigeria pia Music industry imeamka, baada ya apartheid South Africa inakuja na studio kali kali etc. Kwa wanao penda mziki wa Congo (kama mimi) tunawaona wapo tu, na soko lao limeelekea nchi zingine zaidi ya east africa, ndio maana hawaji ku-promote mziki wao huku kama ilivo kua hapo zamani...
hicho kizazi nilichotaja hapo juu ndo hakina mrithi. Hivi sasa kwani anaevuma congo ni nani? Kiukweli congo inapoteza. Hata sauz nao wanapoteza. Kama si mafikizolo, malaika na minanawe, south is losing too
 
dah kaka wewe mtizamo wako km mimi sisikii tena wa Congo wakiimba kwa sauti zao tamu. kazini kwenye Computer nna collection za TPOK JAZZ yaani kwa sauti tamu ya YULUU MABIALA naweza sikiliza KAMIKAZE siku nzima! kesho yake ntasikiliza MATATA YA MWASI siku nzima nikifika home ntaweka BISALELA! dah zile sauti hakuna tena. wa Congo hiyo ndo talanta yao walopewa na mungu. hata king kiki na marquis au akiwa OSS masantula ngoma ya mpwita. HASSAN REHANI BITCHUKA huyu jamaa ni kiboko sauti yake ilikuwa stereo mbaya kaka umentonesha kidonda ntaandika hapa mpaka kesho. ukitaka nyimbo za zamani naanzia alhamis redio free africa kuanzia saa nne usiku mpaka saba alfajiri ZOMBOKO ndani ya nyumba. Ijumaa redio one stereo tatu asubuhi mpaka sita kamili mchana. Jpili tunaanza na redio magic saa tatu asubuhi mpaka saa sita mchana. redio one saa nne mpaka sita mchana. mchana redio Mlimani kuanzia saa tisa alasiri mpaka saa kumi na mbili jioni. usiku Redio magamba(radio uhuru) na mikidadi mahmoud saa tano mpaka saba alfajiri. Radio Tanzania sijasikiliza muda mrefu sana na so sijajua km kile cha jili bd kipo
 
dah kaka wewe mtizamo wako km mimi sisikii tena wa Congo wakiimba kwa sauti zao tamu. kazini kwenye Computer nna collection za TPOK JAZZ yaani kwa sauti tamu ya YULUU MABIALA naweza sikiliza KAMIKAZE siku nzima! kesho yake ntasikiliza MATATA YA MWASI siku nzima nikifika home ntaweka BISALELA! dah zile sauti hakuna tena. wa Congo hiyo ndo talanta yao walopewa na mungu. hata king kiki na marquis au akiwa OSS masantula ngoma ya mpwita. HASSAN REHANI BITCHUKA huyu jamaa ni kiboko sauti yake ilikuwa stereo mbaya kaka umentonesha kidonda ntaandika hapa mpaka kesho. ukitaka nyimbo za zamani naanzia alhamis redio free africa kuanzia saa nne usiku mpaka saba alfajiri ZOMBOKO ndani ya nyumba. Ijumaa redio one stereo tatu asubuhi mpaka sita kamili mchana. Jpili tunaanza na redio magic saa tatu asubuhi mpaka saa sita mchana. redio one saa nne mpaka sita mchana. mchana redio Mlimani kuanzia saa tisa alasiri mpaka saa kumi na mbili jioni. usiku Redio magamba(radio uhuru) na mikidadi mahmoud saa tano mpaka saba alfajiri. Radio Tanzania sijasikiliza muda mrefu sana na so sijajua km kile cha jili bd kipo
mh! Nimekutonesha mkuu. But gone are the sweetest days. Hivi kati ya bichuka na dede nani zaidi? Namkumbuka pia mbwembwe...'mmekwishazaa nyinyi sasa ni ndugu, ni lazima mtakutana kwa ajili ya mwanenu. Hizo siku hazirudi
 
Dede na Bitchuka wanaimba sauti tofauti. Bitchuka sauti yake ni nyembamba yenye kuweza kufika mpaka the highest pitch ila dede sauti yake ipo unique kwangu Bitchuka zaidi mkuu.
 
Kwangu mi naona bichuka ana sauti unique pia. Unaukumbuka wimbo ule unaoimba, 'nilipomaliza masomo nilipata kazi...' Huu wimbo uko akilini toka niko mdogo sana kisa hiyo sauti ya bichuka. Dede ndiye mwenye sauti ya stereo
 
Ni kweli kuna kushuka kwa kiasi fulanni kwa kwa wanamuziki wa Congo. Mojawapo ya sababu ni Kufanana kwa muzikiunaopigwa Congo na ule wa hapa nyumbani mathalan bendi za FM Acdemia, na Akudo, Twanga na Extra Bongo nk. Kufanana huku kunaufanya muziki wa Kongo uskose wateja kwani hauna jipya. Paia Kufariki kwa wanamuziki nguli kama kina Madilu System, Francoo nk ingawa nawashangaa kina Tshala Muana, Kanda Bongoman Nimon Tokilala nk nini kimewazimisha gafla. Something is wrong somewhere.
 
Hata mi nahofia hivyo. Something is wrong. Aidha mapromota ama nini sijui
 
Nimekaa sehem napata flash back za congo. Nawasikiliza kabasele, mabelee,
boziana, defao, wenge n.k. Ni nyimbo tamu sana ambazo ziko kwenye collection. Najiuliza, zile enzi zimeenda wapi?
Sasa hivi congo wanaovuma ni kofi na fally. Slowly slowly Congo is losing the battle

Muziki wa Kongo ulikuwa enzi zile bhana, yaani ukiusikia hata kama huijui lugha inayotumika lakini
utajikuta ukisisimkwa mwili, lakini siku hizi wamebaki hao mashalobaro wanaojichubua... Teh tehe tehe!
Thanx mkuu kwa kunikumbusha habari hii
 
Ngoja niwaambie kitu kimoja, mwalimu wa wanamuziki wa Congo alikuwa ni nani? Ni Pepe Kalle, Pepe Kalle kila akitoa album anakuja na vitu vipya, sasa ile ya kumwona Pepe Kalle na vitu ndo iliwafanya Wakongo waige tabia ya kuibua staili mpya mpya za kimuziki, Pepe Kalle kawatoka Wakongo, hakuna image nyingine kama ya Pepe Kalle pale Congo, toka Pepe Kale alipofariki, muziki wa Congo ulipotea njia!
Kwa sasa anayeharibu muziki ni Werrason, Fally Ipupa yeye anajitahidi kurudisha hadhi ya Muziki wa Congo lkn bado hajaweza kuwa Image kwa wanamuziki wa Kikongo hadi sasa, Koffi kwa vile ni Mkongwe amerudi kule kule alikopiga zamani!
 
Back
Top Bottom