Lutala
JF-Expert Member
- Jun 17, 2010
- 848
- 103
Salam ndugu wanaJF,
Nina tambua kuwa maandalizi ya weekend yashapamba moto kwa serious issue ni vigumu kuzijadili.
Kinachonisumbua ni kuona kuwa watanzania wenzangu kukosa ule uthamini kwa taifa lao.
Mwaka huu nchi yetu inatimiza miaka 50 lakini mpaka sasa sijaona jitihada za kuhamasishana na kujitambia utaifa wetu. Najua viongozi wanaogopa kuzungumzia miaka 50 kwa kuwa mnajua hawana mpya sana sana wananchi wataanza kuwadai waonyeshe waliyoifanyia nchi kwa kipindi chote.
Ukiangalia mataifa mbalimbali kutimiza miaka 50 ni kitu kikubwa sana na kwa kawaida maandalizi yanatakiwa kuanza mapema ili kuweza kupata vitu vinavyoweza kuweka kumbukumbu kwa kizazi kijacho.
Vitu hivyo vinaweza kuwa nyimbo, majengo na hata majina ya watoto kuweza kutunza kumbukumbu hiyo. Mtakumbuka kuna majina kama "Uhuru, Madaraka, TANU, etc yalikuja kutokana na hamasa zilizokuwepo wakati huo na hasa katika kuthamini utaifa.
MOD naomba uweke thread itakayowezesha wanaJF kuchangia mawazo na busara zao kuhusiana na miaka 50 ya utaifa wetu. Ukumbuke kuwa viongozi kadhaa wanatembelea mtandao huu kila siku kwa hiyo wataweza kujifunza kitu kutoka kwa "great thinkers".
VIVA TANZANIA
Nina tambua kuwa maandalizi ya weekend yashapamba moto kwa serious issue ni vigumu kuzijadili.
Kinachonisumbua ni kuona kuwa watanzania wenzangu kukosa ule uthamini kwa taifa lao.
Mwaka huu nchi yetu inatimiza miaka 50 lakini mpaka sasa sijaona jitihada za kuhamasishana na kujitambia utaifa wetu. Najua viongozi wanaogopa kuzungumzia miaka 50 kwa kuwa mnajua hawana mpya sana sana wananchi wataanza kuwadai waonyeshe waliyoifanyia nchi kwa kipindi chote.
Ukiangalia mataifa mbalimbali kutimiza miaka 50 ni kitu kikubwa sana na kwa kawaida maandalizi yanatakiwa kuanza mapema ili kuweza kupata vitu vinavyoweza kuweka kumbukumbu kwa kizazi kijacho.
Vitu hivyo vinaweza kuwa nyimbo, majengo na hata majina ya watoto kuweza kutunza kumbukumbu hiyo. Mtakumbuka kuna majina kama "Uhuru, Madaraka, TANU, etc yalikuja kutokana na hamasa zilizokuwepo wakati huo na hasa katika kuthamini utaifa.
MOD naomba uweke thread itakayowezesha wanaJF kuchangia mawazo na busara zao kuhusiana na miaka 50 ya utaifa wetu. Ukumbuke kuwa viongozi kadhaa wanatembelea mtandao huu kila siku kwa hiyo wataweza kujifunza kitu kutoka kwa "great thinkers".
VIVA TANZANIA