futikamba
JF-Expert Member
- Jan 18, 2010
- 243
- 13
Habari za jioni wakuu
Kwa muda sasa nimekuwa nikipitia pitia thread katika jukwaa hili na kwa kusema ukweli, mengi yasemwayo yanaumiza saaana.
Yapata miaka 50 sasa tokea tupate uhuru. Serikali yetu inahangaika kuandaa sherehe kwa mabilioni ya pesa, kutetea posho na wao kujipendelea ktk kila sekta hali watanzania walio wengi wanaishi kwa kipato chini ya $1. Hali ni mbaya sana. Nawashangaa kweli hawa viongozi wetu.
Juzi nimeangalia taarifa ya habari hapo ITV walionyeshwa wamama na watoto wadogo wakiokota mabaki ya chakula na mkaa jalalani ili kuweza kukidhi njaa zao. Jamani!! tena ni dodoma ambako muheshimiwa waziri mkuu wetu alisema kwamba posho zinawasaidia omba omba nje ya bunge. Inauma sana asee... Huo ni moja tu ya mifano miiingi sana ambayo ukifikiria, inasikitisha sana.
Natoa wito sasa kwa watanzania kusema BAAASI. Uvumilivu na utushinde sasa, utu wa viongozi wetu umegeuka wa kinyama sana. Hata sijui hawana ile "guilty conciousness" kwenye nafsi zao??? Wakati wao wakiendelea kwa ari, nguvu na kasi zaidi kuandaa hilo lisheree lao la miaka 50 ya uhuru na umaskini na sisi tujipange kufanya maandamano ya amani nchi nzima kuwakosoa katika kila idara. YES WE CAN. Nani sasa atatuondoa katika dimbwi hili la umaskini wa kutupwa kama sio sisi wenyewe? Huu sasa si uvumilivu bali ni upumbavu (samahani kwa neno hilo, kama muelewa utaelewa tu maana yangu). Tujikomboe jamani....
FK
Kwa muda sasa nimekuwa nikipitia pitia thread katika jukwaa hili na kwa kusema ukweli, mengi yasemwayo yanaumiza saaana.
Yapata miaka 50 sasa tokea tupate uhuru. Serikali yetu inahangaika kuandaa sherehe kwa mabilioni ya pesa, kutetea posho na wao kujipendelea ktk kila sekta hali watanzania walio wengi wanaishi kwa kipato chini ya $1. Hali ni mbaya sana. Nawashangaa kweli hawa viongozi wetu.
Juzi nimeangalia taarifa ya habari hapo ITV walionyeshwa wamama na watoto wadogo wakiokota mabaki ya chakula na mkaa jalalani ili kuweza kukidhi njaa zao. Jamani!! tena ni dodoma ambako muheshimiwa waziri mkuu wetu alisema kwamba posho zinawasaidia omba omba nje ya bunge. Inauma sana asee... Huo ni moja tu ya mifano miiingi sana ambayo ukifikiria, inasikitisha sana.
Natoa wito sasa kwa watanzania kusema BAAASI. Uvumilivu na utushinde sasa, utu wa viongozi wetu umegeuka wa kinyama sana. Hata sijui hawana ile "guilty conciousness" kwenye nafsi zao??? Wakati wao wakiendelea kwa ari, nguvu na kasi zaidi kuandaa hilo lisheree lao la miaka 50 ya uhuru na umaskini na sisi tujipange kufanya maandamano ya amani nchi nzima kuwakosoa katika kila idara. YES WE CAN. Nani sasa atatuondoa katika dimbwi hili la umaskini wa kutupwa kama sio sisi wenyewe? Huu sasa si uvumilivu bali ni upumbavu (samahani kwa neno hilo, kama muelewa utaelewa tu maana yangu). Tujikomboe jamani....
FK