Miaka 50 ya Uhuru hata Supply ya Maji ya uhakika kwenye jiji lenu la dar Tumeshindwa!!

FUSO

JF-Expert Member
Nov 19, 2010
31,635
37,849
Ni aibu kubwa kuhitimisha sherehe ya miaka 50 ya uhuru bila kuwa na ugawaji (supply) maji ya uhakika. Mtaniambia Tanganyika ni kubwa sana je hata Jiji letu la Dar es salaam nalo imeshindikana?. Leo wiki ya pili watu tunahaha kutafuta maji. Hivi sisi watanganyika tumefanikiwa kwa lipi?

Yaani bomba la maji kutoka mto Ruvu hadi jijini liliwekwa miaka ya mwalimu (1960's) hadi leo tumeshindwa kuweka jingine? ndiyo maana mi sikusherehekea miaka 50 sababu sikuona chochote tulichothubutu na tunakoelekea naona ni giza totoro. hii inakatisha tamaa; kama mkipewa kazi wenzetu fanyeni kama mmeshindwa waachieni wengine wazifanye. umeme tumekubali lakini hata hili la maji jamani mtatuua - mnajua fika kwamba jiji letu lina joto kali tutaishi bila kuoga kweli achilia mbali maji safi ya kupikia. je kipindupindu kitaisha maana tunapikia maji ya mitaroni.
 
Back
Top Bottom