Miaka 50 baadaye: Je Unaiamini Serikali? Kwa nini?

Angalia Signature inajieleza sina cha kuongezea, Mimi sio tu kama sina Imani nayo bali naichukiya kwa jinsi ilivyojaa Rushwa na kulindana.
 
Yaani kila ninapofikiria serikali na kuangalia hali tuliyonayo, naskia hasira mnoo...:( Ndo maana sipendi kabisa kukatiza mitaa ya huku...naishia kukasirika tu!
 
hili jukwa huwa sipendi kuja huku maana napata hasira sana kila ninaposoma ni ufisadi, ufisadi, wizi, ukwapuaji mali ya umma na watetezi wetu wanasinzia bungeni
 
Ukiondoa majengo, viwanja vya michezo, wiwanja vya kulaza magari na mali zinginezo za CCM ambazo kimsingi ziliachwa na Mwalimu [mali ya Watanzania - baada ya hapo hazikuwahi kuongezeka bali zinapungua], binafsi sidhani kama kuna chama bali hizo mali. Watu waliozizunguka ndiyo tunawaita wanaCCM lakini ukiangalia hakuna hata mmoja anayetimiza masharti ya chama.
Kwa hiyo huwezi kuwaamini watu amabao wenyewe hawaamini misingi (katiba) ya chama chao!
Mnakiamini chama cha Mapinduzi kinachoongoza serikali hiyo?
 
Ukiondoa majengo, viwanja vya michezo, wiwanja vya kulaza magari na mali zinginezo za CCM ambazo kimsingi ziliachwa na Mwalimu [mali ya Watanzania - baada ya hapo hazikuwahi kuongezeka bali zinapungua], binafsi sidhani kama kuna chama bali hizo mali. Watu waliozizunguka ndiyo tunawaita wanaCCM lakini ukiangalia hakuna hata mmoja anayetimiza masharti ya chama.
Kwa hiyo huwezi kuwaamini watu amabao wenyewe hawaamini misingi (katiba) ya chama chao!

Hayo ndio mafanikio ya CCM kujisifia kuwa wamejenga Barabara, tumeleta hichi, tunafanya hichi utafikiri hizo pesa zimetoka mifukoni mwao kumbe ni Kodi yetu.
Mwanakijiji unataka watu wale Ban hapa, nimeweka kiporo maneno mengine
 
Hadi hivi sasa kama Mtanzania umesikia mengi kuhusu uongozi na utawala na matokeo yake katika maisha ya Watanzania. Umesikia sera mbalimbali zikifanyiwa kazi na mafanikio yakitangazwa. Kuanzia ujenzi wa barabara, mahospitali, kliniki, miundo mbinu mingine mingi na mipango kadha wa kadha ya maendeleo. Yawezekana umeweza kushuhudia juhudi mbalimbali za maendelo zinazofanywa na serikali. Utakuwa umesikia mipango na malengo mbalimbali ya serikali na pia kuna mambo umeyaona mwenyewe au kusimuliwa jinsi serikali ilivyofanya kuleta maendeleo.

Na siku za karibuni bila ya shaka umesikia hatua mbalimbali za jinsi gani serikali imechukua kuonesha uongozi. Kuanzia sakata la Ngeleja na Jairo, sakata la BP na Mafuta na sasa sakata la Maige na wanyama. Yote yamefanyika katika kuonesha kuwa serikali iko "on top" of things; Bunge liko "on top" na kuwa viongozi waliochaguliwa "wanasikiliza wananchi".

Lakini muda wote huo yawezekana umeona mengine mengi ambayo yameacha maswali. Katika kuadhimisha miaka hii hamsini unajisikiaje zaidi:


a. unaamini serikali zaidi?
b. Unaiamini lakini unataka uthibitisho?
c. Unaishuku mara zote?
d. Unashuku maamuzi yake?
e. Huamini kabisa?
f. Unaangalia watu gani wa serikali wanasema au kuamua; yaani unaamini katika watu binafsi kuliko taasisi zao?
g. Hujali lolote linalofanywa na serikali?

Kwanini?

Mzee Mwana Kijiji I saluti you!
Kabla ya kujibu maswali yako (a) - (g) naomba tufahamishane kwamba kwamba tulipata uhuru miaka 50 iliyopita sii issue na haimaanishi kwamba lazima sasa tuwe na maisha kama ahera! Uhuru na historia ya nchi yetu kwa ujumla ni vitu tuanvyo takiwa kuvienzi pamoja na mapungufu yaliyopo bado itabakia kuwa historia ya nchi yetu no matter tumefikaje hapa tulipo.

nina sababu zifuatazo kuandika hayo maandishi hapo juu kama ifuatavyo:-
  1. Ni kweli kwamba nchi yetu in raslimali nyingi zikiwemo madini na kadhalika, ila kwa maoni yangu kuwa na madini bila technology bado its a problem, na ukuachilia mbali waarabu waliotajirika kwa mafuta siifahamu nchi yoyote ambayo imetajirika kwa kuuza madini, kuchukua kwa mfano nchi kama urusi ambaya ina madini zote unazozijua (kasoro tanzanite!), lakini wao sii nchi tajiri kuliko zote duniani ukizingatia kwamba walizigundua miaka mingi iliyopita (nafikiri mzee bado unamkumbuka Mandleeve aliyetengeneza periodic table of elements). nchi za africa ni africa ya kusini tu na walianza miaka mingi sana iliyopita. nchi nyingine ziko vitani kugombea nani anakula zaidi na ndiko tunakoelekea!!.
  2. kuhusu nchi yetu na miaka 50 na bado bado huduma za jamii haziko sawa ni tatizo ila kumbuka nchi ambazo hazijawahi kuwa koloni na zina hata maandishi yake kama Ethiopia wana nini?
  3. Nafikisiri una mfahamu Christopher Amergo Columbus aliyevumbua Amerika ni Mhisipania na Hispania ilianza biashara miaka mingi ikiwemo ya utumwa lakini hadi leo wao na jamaa za Wareno wako kwenye PIGIS, zile nchi chokambaya kuliko zote europe, zaidi ya kucheza football hamna kitu
  4. so, kabla ya kujiuliza maswali (a) - (g) inabidi tuifahamu historia yetu na tujue tuna nini na ni nini hatuna, if you ask me tungejitahidi tukatumia resources za kutosha tuchague vijana wenye pass nzuri tuwalipie kwenye vyuo vizuri wasomee taaluma za sayansi za uchumi na madini halafu warudi wafanye kazi! (angalizo: wawe wazalendo si wazamiaji). Wajerumani na wajapani walifanya hivyo baada ya vitakuu ya pili ambapo nchi zote zilikuwa magofu kwa kupigwa mabomu n sasa uchumi wao uko juu.
  5. mwisho, tuuheshimu uhuru wetu kwani ni historia yetu, Ujerumani na Japan wangekaa kuanza kutoana macho kwamba nani kifikisha nchi yao kwenye vita kuu wasingeinuka!!
I am out.
 
Mnakiamini chama cha Mapinduzi kinachoongoza serikali hiyo?

Chama cha Mapinduzi kilijulikana kama chama cha wakulima na wafanyakazi, na kilianzishwa katika misingi ya udugu - African Socialism. Now, changes nyingi zimefanyika kimfumo na kimtazamo ndani ya hiki chama na vigumu kuelewa wakubwa hawa wanaposema kuwa bado zile 'founding principles' zinatekelezwa!

Sasa, swali kuwa nakiamini chama cha mapinduzi linanifanya nijuilize chama cha mapinduzi kipi? na kiko wapi? Kinaongozwa na nani?
Kwa mtazamo wangu, Tanzania hatuna chama cha mapinduzi, ila tuna watu wanaoomba kura na wengine kupata dhamana za uongozi kwa kutumia 'brand name ya chama cha Mapinduzi'. Na msingi wa jibu langu ni huu, kile chama cha wakulima na wafanyakazi kinafanana na hiki cha leo?
 
Chama cha Mapinduzi kilijulikana kama chama cha wakulima na wafanyakazi, na kilianzishwa katika misingi ya udugu - African Socialism. Now, changes nyingi zimefanyika kimfumo na kimtazamo ndani ya hiki chama na vigumu kuelewa wakubwa hawa wanaposema kuwa bado zile 'founding principles' zinatekelezwa!

Sasa, swali kuwa nakiamini chama cha mapinduzi linanifanya nijuilize chama cha mapinduzi kipi? na kiko wapi? Kinaongozwa na nani?
Kwa mtazamo wangu, Tanzania hatuna chama cha mapinduzi, ila tuna watu wanaoomba kura na wengine kupata dhamana za uongozi kwa kutumia 'brand name ya chama cha Mapinduzi'. Na msingi wa jibu langu ni huu, kile chama cha wakulima na wafanyakazi kinafanana na hiki cha leo?
you have explained well my view:
1. Nyerere's CCM is dead and burried. Nadhani inabidi hawa jamaa wakiomba kura kwa tiketi ya CCM tuombe watupe kirefu cha hiyo CCM.
2. Hatuna serikali...tuko ktk autopilot!
Shame and sad but true :A S 20:
 
Mwanakijiji you played your part, I appreciate the role you are playing, but I don't believe if every Tanzanian has played their real part faithfull as well as Mimi Mwanakijiji, ! this can be the major cause of failure believe me.

Hata hapa JF tunapiga kelele na watu watu walewale ambao wanaiba dawa zawagonjwa wakiwa Waganga huku Mwananyamala hosp, Muhimbili nk, tunapiga kelele na Ma-engineer wetu wanaojenga barabara ambazo dk5 viraka, tunapiga kelele humu humu kulailaum Serikali wakati sisi ndio hao Polisi wanapiga watu na Bunduki na kuuwa, ndio Mahakimu wanaongoza kwa rushwa na kufunga jela wezi wa kuku peke yao. Ndio sisi tunaolalamika ndio watafiti tunatengeneza report za uongo kusema fulani anaongoza kwa asilimia 99.99% nk.


Bado watanzania wote hatujafanya sehemu kiasi cha kuilaum serikali, sisi hawa hawa ndio wakati wa uchaguzi kura yetu tunaiuza kwa chumvi na khanga. Haya yote ni mambo ambayo tunapaswa kuyakataa sisi kama watanzania na kila mtu akajuwa na kutuogopa kuwa ndio sifa yetu, kama tukiendelea kuwa hivyo hata tukiletewa rais na chama kutoka mbinguni hakika kitashindwa. We fikiri Polisi waliouwa raia Nyamongo pamoja na kuaminiwa na kupewa ulinzi pale lakini wao wenyewe ndio waliokuwa majambazi namba moja kuiba mgodini kwa kushirikiana na raia wezi na hata hao waliowauwa ni watu waliozulumiana mali za wizi, yale yale ya msitu wa pande; Hii ndio tabia yetu na ndio maana watu wengi wa nje hawataki kuajiri wazawa ingawa tunajifanya hatujui sababu. sababu ni genes zetu za wizi na uongo lazima tuzibadili kwanza.
 
Back
Top Bottom