katika sherehe za ccm zilizofanyika katika viwanja vya ccm kirumba jijini mwanza na kuonyeshwa na star tv . watu wanaokadiriwa 100,000 walihudhuria sherehe hizo (makisio na taarifa ndani ya jf) . idadi hii ni kubwa zaidi ya uwezo wa uwanja huo wa kuchukua watu 20,000 , idadi ya watu walioingia katika uwanja huo ni mara tano zaidi ya uwezo wa uwanja halisi .hivyo basi natarajia kufungua kesi mahakamani dhidi ya jk, nape , na ccm hii ni kutokana na kuhatarisha usalama wa watu waliohudhuria sherehe hizo kwa kuzidisha idadi ya watu katika uwanja huo kupita uwezo wa kiwanja chenyewe . tabia hii ya kuzidisha idadi ya watu imeliingiza taifa katika matatizo makubwa ikiwamo ajali ya mv spice icelander huko nungwi , mv bukoba , na ile ya watoto waliofariki katita disco toto huko tabora(kama sijakosea). ambapo maafa hayo yalisababisha vifo na wahusika walichukuliwa hatua kwa njia moja au nyingine ikiwamo kufikishwa mahakamani, katika kuhakikisha sheria za nchi zinafuatwa basi ni lazima kila mmoja kuwajibika na kuwajibishwa kutokana na nafasi yake. naomba kukaribisha maoni ili kuwezesha sheria kufuata mkondo pale kesi itakapotinga mahakamani