Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,348
- 6,471
Jana katika kipindi cha Jirani cha Redio Tumaini alialikwa mkurungenzi mtendaji wa ESRF ambaye ni PhD holder nafikiri kwenye maeneo ya sayansi ya jamii. Alitoa mfano mmoja mpaka mimi mwenyewe nikashangaa. Ilikuwa hivi: msikilizaji kauliza hivi ni kwa nini tunaambiwa uchumi unakua lakini bado watanzania ni masikini. Dr. akasema kuwa kipimo cha uchumi kukua kinatokana na viashiria au matokeo kama kujengwa kwa barabara na ukuaji huu wa uchumi unatusaidia bila sisi kujua mpaka kufanya tathmini.
Akatoa mfano kwamba zamani barabara ya Dodoma - Singida haikuwa na lami hivyo ilimlazimu msafiri kulala njiani kwenye hotel ambayo alilipa 15,000/-; baada ya kuwekwa lami msafiri huyo halali tena hotel ile na ku-save 15,000/- hivyo hayo ndio matunda ya kukua kwa uchumi ila mwananchi lazima ayatafiti. Mshangao wangu unakuja na swali je, yule mwenye hotel inakuwaje? Si anakuwa amepoteza 15,000/? Je, ukuaji wa uchumi unaumiza wengine? Je, poverty itaondoka kweli? Mwenye hotel atapeleka kweli watoto wake shule bila shida?
Ukiangali hata mi-professor yetu ni balaa kwa kuchanganya mambo!
Hivi kuna tofauti kati ya professor wa Tanzania na UK au USA? Kama zipo ni zipi? Na maanisha u-professor wa ku-publish na sio title ya kufundisha chuo kikuu.
Akatoa mfano kwamba zamani barabara ya Dodoma - Singida haikuwa na lami hivyo ilimlazimu msafiri kulala njiani kwenye hotel ambayo alilipa 15,000/-; baada ya kuwekwa lami msafiri huyo halali tena hotel ile na ku-save 15,000/- hivyo hayo ndio matunda ya kukua kwa uchumi ila mwananchi lazima ayatafiti. Mshangao wangu unakuja na swali je, yule mwenye hotel inakuwaje? Si anakuwa amepoteza 15,000/? Je, ukuaji wa uchumi unaumiza wengine? Je, poverty itaondoka kweli? Mwenye hotel atapeleka kweli watoto wake shule bila shida?
Ukiangali hata mi-professor yetu ni balaa kwa kuchanganya mambo!
Hivi kuna tofauti kati ya professor wa Tanzania na UK au USA? Kama zipo ni zipi? Na maanisha u-professor wa ku-publish na sio title ya kufundisha chuo kikuu.