Mi-doctor (PhD) na mi-Professor ya Bongo siielewi!!

Mwanamayu

JF-Expert Member
May 7, 2010
11,348
6,471
Jana katika kipindi cha Jirani cha Redio Tumaini alialikwa mkurungenzi mtendaji wa ESRF ambaye ni PhD holder nafikiri kwenye maeneo ya sayansi ya jamii. Alitoa mfano mmoja mpaka mimi mwenyewe nikashangaa. Ilikuwa hivi: msikilizaji kauliza hivi ni kwa nini tunaambiwa uchumi unakua lakini bado watanzania ni masikini. Dr. akasema kuwa kipimo cha uchumi kukua kinatokana na viashiria au matokeo kama kujengwa kwa barabara na ukuaji huu wa uchumi unatusaidia bila sisi kujua mpaka kufanya tathmini.

Akatoa mfano kwamba zamani barabara ya Dodoma - Singida haikuwa na lami hivyo ilimlazimu msafiri kulala njiani kwenye hotel ambayo alilipa 15,000/-; baada ya kuwekwa lami msafiri huyo halali tena hotel ile na ku-save 15,000/- hivyo hayo ndio matunda ya kukua kwa uchumi ila mwananchi lazima ayatafiti. Mshangao wangu unakuja na swali je, yule mwenye hotel inakuwaje? Si anakuwa amepoteza 15,000/? Je, ukuaji wa uchumi unaumiza wengine? Je, poverty itaondoka kweli? Mwenye hotel atapeleka kweli watoto wake shule bila shida?

Ukiangali hata mi-professor yetu ni balaa kwa kuchanganya mambo!

Hivi kuna tofauti kati ya professor wa Tanzania na UK au USA? Kama zipo ni zipi? Na maanisha u-professor wa ku-publish na sio title ya kufundisha chuo kikuu.
 
Kwetu sisi shule ni kusoma kwa ajili ya kujibu mitihani ili tupate cheti cha kutusaidia kupata ajira!
 
Jana katika kipindi cha Jirani cha Redio Tumaini alialikwa mkurungenzi mtendaji wa ESRF ambaye ni PhD holder nafikiri kwenye maeneo ya sayansi ya jamii. Alitoa mfano mmoja mpaka mimi mwenyewe nikashangaa. Ilikuwa hivi: msikilizaji kauliza hivi ni kwa nini tunaambiwa uchumi unakua lakini bado watanzania ni masikini. Dr. akasema kuwa kipimo cha uchumi kukua kinatokana na viashiria au matokeo kama kujengwa kwa barabara na ukuaji huu wa uchumi unatusaidia bila sisi kujua mpaka kufanya tathmini.

Akatoa mfano kwamba zamani barabara ya Dodoma - Singida haikuwa na lami hivyo ilimlazimu msafiri kulala njiani kwenye hotel ambayo alilipa 15,000/-; baada ya kuwekwa lami msafiri huyo halali tena hotel ile na ku-save 15,000/- hivyo hayo ndio matunda ya kukua kwa uchumi ila mwananchi lazima ayatafiti. Mshangao wangu unakuja na swali je, yule mwenye hotel inakuwaje? Si anakuwa amepoteza 15,000/? Je, ukuaji wa uchumi unaumiza wengine? Je, poverty itaondoka kweli? Mwenye hotel atapeleka kweli watoto wake shule bila shida?

Ukiangali hata mi-professor yetu ni balaa kwa kuchanganya mambo!

Hivi kuna tofauti kati ya professor wa Tanzania na UK au USA? Kama zipo ni zipi? Na maanisha u-professor wa ku-publish na sio title ya kufundisha chuo kikuu.

-Sijaelewa, inamaana unahisi jibu la huyo mkurugenzi halikuwa sahihi na unataka kumkosoa ama?
 
Kuna prof. ana ka-grocary na kaeneo ka kuchemshia supu mtaani kwetu. Mmda mwingi prof huyu yupo hapo kazini kwake. Sasa jiulize kazi za ubunifu zenye tija kwa jamii pana na maendeleo endelevu zitatengenezwa na kina nani? Darasa saba? Wallah tulikotoka karibu, tunakokwenda ni mbali!!
.
 
-Sijaelewa, inamaana unahisi jibu la huyo mkurugenzi halikuwa sahihi na unataka kumkosoa ama?

Ndio nahisi hivyo. Na kama ndivyo economic theory inasema hivyo basi inabidi itazamwe upya. Je, wewe unaona yuko sahihi? Kama ndio usahihi wake ukoje?
 
Kuna prof. ana ka-grocary na kaeneo ka kuchemshia supu mtaani kwetu. Mmda mwingi prof huyu yupo hapo kazini kwake. Sasa jiulize kazi za ubunifu zenye tija kwa jamii pana na maendeleo endelevu zitatengenezwa na kina nani? Darasa saba? Wallah tulikotoka karibu, tunakokwenda ni mbali!!
.

LIKE! Wewe ni great thinker, unaangalia jambo tofauti na mazoea ya kawaida!
 
Back
Top Bottom