Mheshimiwa Zitto na wana-CHADEMA.....

Nadhani ni bora spika ajibu hoja,

kwa sababu kukataa hoja ya msingi ya kupitia upya adhabu ya Mh ili kuangalia usahihi wa adhabu yenyewe kwa misingi ya kanuni wala haliisaidii Bunge kujiboresha na kuwatumikia wananchi kwa ubora zaidi.

Kwa Spika mwenye kujiamini kwamba hatua alizochukua zilikuwa ndani ya kanuni na muongozo wa Bunge, haikuwa na haja tena kuzalisha hoja ndani ya hoja, bali ni kuisolve hoja ya kwanza kwa kuonyesha kwa uwazi kabisa kanuni kadha wa kadha. basi mambo yakesha.

Sasa badala ya kujibu hoja at hand yeye analeta personal attack(adhominems) mara ooh, "namuonea huruma kijana Zitto", mara ooh" unajua Zitto bado Mtoto kisiasa".

unajua nikitafakari kauli hizi za mh Sitta ninakumbuka kisa cha Karama na Majivuno(waziri mkuu wa kusadikika} katika kitabu cha kusadikika cha Shaaban Robert, majivuno alikuwa anaamini kabisa kwamba Karama hana busara eti kwa sababu hana mvi kichwani..sasa haya mambo ya kusadikika ndo leo tunayashuhudia katika Tanzania huru.
 
Sitta is a disgrace to the parliament. And he was supposed to be the investment center head honcho (before being speaker)? no wonder we are where we are!
 
Hivi alitumia janja ipi hadi kuukwaa uspika ? Ama ndiyo cream yenyewe jamani ?Maana mtandao huu unaimaliza Tanzania .Yeye na Mkewe wamekuwa rewarded sasa .Jamani
 
ukweli zitto anapenda sifa hata kipanya kamchora na bichwa kubwa.

na kumuhadharisha mdogo wangu bichwa hilo litapasuka mwisho.

mpenda kuandikwa kwenye magazeti na kutajwa kwenye vyombo vya habari kila saa.

akiona media iko kimya hutafuta atoke vp, mkuu ukipaa sana utaanguka vibaya maalim angalia hilo
 
Swali la Mwanakijiji ni la Muhim sana kujua nani anamshauri Zitto na kwa Interest zipi.
Kimsingi nionavyo unapokuwa na position kubwa kama Ubunge lazima uwe na washauri kadhaa juu ya jambo lako. Pia sijui mtu kama Zitto aliomba USHAURI kwa seniors wowote ktk Kambi ya Upinzani b4 hajasubmit ile Barua...Kimsingi neno WEWE linaweza kuwa TUSI au LISIWE TUSI kulingana na namna Gani umelitumia. Ukiliangalia neno wewe si TUSI kwa ujumla wake, lkn litakuwa TUSI endapo umelitumia sivyo...sote ni waswahili matumizi ya lugha twayajua.
Ipo Haja Zitto kama mtu binafsi au Umma kuwa na washauri hasa ktk Kipindi cha Kuhakikisha HAKI muhim za WaTZ zinatafutwa.

Barua ya ZITTO kuja ktk JF ilikuja kwa JINA la ZITTO, wengi tumekuwa tunaamini kuwa ni yeye na hasa ukilinganisha posts za huko nyuma, au yeye kampa mtu mwingine idhini ya kutumia Jina Lake hapa JF. Nafikiri SIRI lina limitation zake.

IPO HAJA pia Kumshauri ZITTO aoe ili aweze pata LIWAZO la MOYO kutokana na MISUKOSUKO anayoipata daily. Role ya Mwanamke alie ktk NDOA ni kubwa na hasa ukilinganisha na Role ya Mbunge.
 
Swali la Mwanakijiji ni la Muhim sana kujua nani anamshauri Zitto na kwa Interest zipi.
Kimsingi nionavyo unapokuwa na position kubwa kama Ubunge lazima uwe na washauri kadhaa juu ya jambo lako. Pia sijui mtu kama Zitto aliomba USHAURI kwa seniors wowote ktk Kambi ya Upinzani b4 hajasubmit ile Barua...Kimsingi neno WEWE linaweza kuwa TUSI au LISIWE TUSI kulingana na namna Gani umelitumia. Ukiliangalia neno wewe si TUSI kwa ujumla wake, lkn litakuwa TUSI endapo umelitumia sivyo...sote ni waswahili matumizi ya lugha twayajua.
Ipo Haja Zitto kama mtu binafsi au Umma kuwa na washauri hasa ktk Kipindi cha Kuhakikisha HAKI muhim za WaTZ zinatafutwa.

Barua ya ZITTO kuja ktk JF ilikuja kwa JINA la ZITTO, wengi tumekuwa tunaamini kuwa ni yeye na hasa ukilinganisha posts za huko nyuma, au yeye kampa mtu mwingine idhini ya kutumia Jina Lake hapa JF. Nafikiri SIRI lina limitation zake.

IPO HAJA pia Kumshauri ZITTO aoe ili aweze pata LIWAZO la MOYO kutokana na MISUKOSUKO anayoipata daily. Role ya Mwanamke alie ktk NDOA ni kubwa na hasa ukilinganisha na Role ya Mbunge.


mkuu huyu kuoa si rahisi mzoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi


huyu bwana ni mtu wakujirusha na ...... nnategemea stori zake unazielewa

tumtilieni fatiha maana mwisho wake huyu kijana ni mbaya sana akishindwa nkujielewa
 
Usichoke au usikate Tamaa...ataelewa TU...ikiwa JK nae haelewi JE tuache? may be atapata fundisho kama la KIBAKI...Zitto he still young lazima tumshauri...kama hashauriki basi wasiwalaumu wazee wa CCM ambao ni conservatives
 
ukweli zitto anapenda sifa hata kipanya kamchora na bichwa kubwa.

na kumuhadharisha mdogo wangu bichwa hilo litapasuka mwisho.

mpenda kuandikwa kwenye magazeti na kutajwa kwenye vyombo vya habari kila saa.

akiona media iko kimya hutafuta atoke vp, mkuu ukipaa sana utaanguka vibaya maalim angalia hilo

mtu wa pwani......

weka link na hiyo pic hapa sote tuone,tunahofia pengine una CHUKI ZAKO BINAFSI NA Mheshimiwa Zitoo kabwe.
 
Tulipoliongelea hili suala kwa mara ya kwanza, Zitto alituma hiyo barua hapa kwetu sisi. Wakati huo huo, Spika akatamka kuwa amesikia kuhusu hiyo barua kwenye vyombo vya habari na kuwa imesambazwa kwenye Net, lakini yeye hajaiona kwa kuwa laikuwa nje ya nchi ilipopelekwa kwake.

Naungana na Mwanakijiji kuuliza je Mh. Zitto anawashauri wa kumsaidia?

Kibinafsi, pamoja na kukubaliana na nia nzuri ya Zitto kuhoji hukumu yake kama nilivyoeleza hapa http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=8383&page=9 lakini inabidi kujiuliza, je ni mapungufu gani yaliyokuwapo katika barua ya Zitto na hoja yake?

Je alipata msaada wa Wataalamu wa sheria, kanuni na taratibu za Bunge?

Je ilikuwa ni sahihi kwake kuitawanya kwenye umma kabla ya kuthibitisha kuwa Spika kaipata?

Ukiangalia sana na kwa makini, mlolongo mzima unaonyesha kuwa Zitto alitangaza hadharani nia yake na hata kutuma barua yake hapa ukumbini. Je hichi ndicho Sitta anakiita kejeli?

Ushauri wangu kwa Zitto;

Naomba upitie maneno Kitila Mkumbo na Dada Asha walikuasa kwenye ile hoja kuhusu mtafuruku kati yako na Wangwe. Jitahidi sana kufikiria na hata kupata ushauri (hata kutoka kwa maadui) kabla ya kukimbilia hadhara na vipaza sauti.

Nalisema hili kwa kuwa wewe ama unajiamini sana au hujaufahamu kwa dhati mchezo mchafu wa siasa. Pamoja na nia yako nzuri, jinsi magazeti yanavyokuandika kama kukupa tukuzo na kuonyesha umwamba ama ubabe wa "kutetea" kauli na haki zako, madhara yake ni kuendelea kuonekana kama mpenda sifa na umaarufu.

Sitta na wenzake washaling'amua hili na hata Sitta kakuwambia wazi, bila woga na katumia kwanza kejeli kujibu barua yako, pili akatumia "utaalamu' kutupilia mbali madai ya barua yako na kisha kuwataarifu Watanzania kuwa barua yako itajadiliwa si kwa maoni na maombi yako, bali ni ukosefu wa "adabu" wa barua yako.

Sasa hivi pamoja na kuwa waonekana "mkombozi" mfano wa Mtikila au Mrema, binafsi naona kuwa ukiendelea kwa kasi hii, utaishia kuwa kama wahenga wako(Mtikila na Mrema)!

Usidanganyike na ukaribu wako kwa JK au kuaminiwa naye. CCM wankutafuta kwa udi na vumba na watahakikisha kuwa unajinyonga kwa kutumia kamba yako mwenyewe kama walivyomfanyia Mtikila na Mrema!

Achana na malumbano! Ushapata jina, sasa fanya kazi wananchi waione!

La mwisho, awali ulishatamka kuwa wataka acha siasa, tukakukoromea usiache. Jee haya malumbano na Wangwe, Sitta na kuonekana kwako kuwa "hauambiliki bin haushauriki" ni njia yako ya kujiondoa katika siasa kwa kutumia kisingizio cha "kuchoshwa" na kukwamishwa?

Kama hiyo ndiyo turufu yako, basi hata 2020 utakapotaka kugombea Urais, tutayakumbuka ya 2007-2008 !
 
hivi bado huyu bwana mnajisumbua kumpa nasaha?

mjuaji muacheni mpaka yamfike ndio atajijuu
 
Back
Top Bottom