Mheshimiwa Zitto, kwa hili umekosea

Kama serikali inamiliki Tanesco kwa asilimia 100 na kuisajili kama kampuni binafsi tunaweza kweli kusema ni kampuni binafsi au ya umma? I'll argue kwamba Tanesco ni shirika la umma kwani linamilikiwa kwa asilimia 100 na wananchi wa Tanzania lakini siwezi kusema ni kampuni binafsi. Lakini pia kwa vile haina hisa ambazo zinaweza kununuliwa na "watu" binafsi zinaweza kufanya Tanesco iwe binafsi kwani maamuzi yote yanayuusiana na uendeshaji wake yanafanywa na serikali na uongozi wake huingizwa na serikali. Nadhani tuna uwezo wa kutosha tu wa kufikiria ni jinsi gani tuibadili Tanesco ili iwe tunavyoitaka na mimi naamini njia mojawapo ni kuwaweka wanasiasa pembeni na shirika liwe la kibiashara zaidi.

Mzee Wetu,

Kwanza Nonda hajambo?

Nadhani Mh.Zitto alikuwa anamaanisha kuwa kuna mashirika na taasisi za umma amabazo zimeanzishwa kwa sheria zao maalumu na kuna yale yaliyoanzishwa chini ya Cap.212 (Companies Act 2004). Ni haya ya mwisho (TANESCO) ambayo ni rahisi kuya float kuliko yale ya sheria maalum (TPA) ambayo inabidi Bunge litengue sheria zilizoyaanzisha na kuyarudisha katika Comanies Act. PSRC ilikiuka sana hili na mashirika mengi yaliuzwa kwa kuvunja sheria na iko siku itabidi lianzishwe hili jambo.
 
Kwa Hoja hii na mwazo ya wachangiaji wengi hakika inatoa mwelekeo na maana nzima ya forum na si ushabiki na matusi, wengine tulishaanza kukata tamaa na hii forum amabyo tuliiamini sana kama kielelezo cha fikara chanya za watanzania wenye mapenzi mema kwa nchi yao.
Inawezekana kabisa mawazo na mchango wa Zito ukawa na ukweli juu ya kutomuelewa vema, lakini kutomuelewa huko na hizi hoja zako bado ni mwiba na angalizo muhimu kuwa watanzania wenye mapenzi mema na Taifa hili wapo makini na hawakumbatii ushabiki na rangi za vyama.
Ukisoma comment za Mzee Mwanakijiji hapo juu utaona reflection na nyongeza ya mambo kama haya.
Kukupongeza tu haitoshi zaidi ya kusema na hili ni angalizo na mwamko mwingine kwa wachangiaji katika forum kuleta hoja kama hizi za kina kama wafanyavyo akina mpevu, mjengwa na wengine wengi
BRAVO
 
mawazo chanya kama haya ni adimu sana kuyapata ndani ya ccm.....kijina umejitahidi sana........jitihada hizi wambie hata hao ccm huko ndani .......
 
ZITTO na Wana CHADEMA wengine.

Anacholiza Mwanamagamba huyu ni kwamba, mapendekezo ya kuuza hisa za airtel na NBC
ni kwaajili ya kupata ufumbuzi wa haraka wa matatizo ya kiuchumi tuliyonayo sasa?

Sababu kinachoeleweka ni kwamba strategy ya sasa ya CHADEMA ni kuishikinikiza serikali
kutunasua kwenye hali tete tuliyonayo sasa, bei za bidhaa muhimu zimepanda sana,
serikali nayo imeishiwa pesa n.k.

Hayo ndio mategemeo yangu pia, mimi namuunga Mkono Mwanamagamba lakini katika
approach tofauti ambayo nitaiibua ndani ya siku chache zijazo.

Naomba tusilifichie hili swala kwenye mambo ya kisera, sera ndio nguzo kuu ya mijadala
ya kisiasa, lakini huu sio muda wa CHADEMA kuishinikiza serikali ya CCM kutekeleza sera zake,
sio kazi ya CHADEMA kuisaidia serikali kufanikiwa katika utendaji wake.

Uuzaji wa hisa za serikali katika Makampuni hayo utasaidia vipi kupunguza ugumu wa maisha
in a six month period. Swali halijajibiwa.

Thanks Mwanamagamba
 
Njia za muda mrefu ni kuongeza uzalishaji wa chakula na kuboresha miundombinu chakula kifike sokoni.

...Uzalishaji wa chakula unaongezwa vipi, kama tunategemea wakulima wadogo (peasants) katika kilimo na bei za mazao yao ni ndogo kiasi cha kutochochea uzalishaji zaidi, bali uzalishaji wa kuganga njaa?

...Ingekuwa vyema kama ingefahamika ni kiasi gani ununuzi wa mazao kwa kutumia hati ya malipo umeweza kuwasaidia wakulima katika bei ya mazao yao.

...Bila kipato cha mkulima kuongezeka ili aweze kurudisha uwekezaji wake katika kilimo, kukiendana na mfumo mzuri wa usambazaji na uuzaji, hakutakuwa na maendeleo yeyote kwenye kudhibiti mfumuko wa bei za mazao.
 
Bei ya mafuta hatuwezi kuincontrol mpaka tuchimbe mafuta wenyewe na tuwe na uwezo wa kuyatumia wenyewe. Njia peke tunaweza kupunguza gharama za mafuta ni kupunguza kodi, kuweka subsidies katika wauzaji wa mafuta

...Hata kama tukichimba, bei itakuwa ya soko na hivyo hakutakuwa na tofauti ya maana, waulize nigeria au indonesia.

...Labda, hilo pendekezo lako la pili, na litakuwa na maana zaidi pale tutakapokuwa tunazalisha yetu. Hata hivyo nalo si endelevu kwakuwa litaingilia nguvu za soko.
 
Nashukuru sana. Nipo Sumbawanga. Hujanielewa. Ninashauri kufanya IPO ya Airtel na NBC ili kwanza kupata mapato kwa serikali lakini pili kwa kumilikisha uchumi kwa umma. IPO ni kwa wananchi kupitia soko la hisa.

Hukunielewa vema na ninaomba unielewe. Siku zote nimekuwa mstari wa mbele kuhakikisha DSE inakuwa more liquid. Nataka tuwe na kampuni nyingi sana DSE. Hii itawezesha uwazi.


It is good that you have responded immediately.Hata mimi nilianza kutoelewa vizuri mwanzoni. Mimi nadhani ni vizuri ukafanya clarification kwenye media ili watu wengi zaidi wakuelewe vizuri maana haya mambo ya uchumi magumu kuyaelewa. CCM wasije wakaanzisha proganda kupitia hoja hii.
 
Kwanini Tanesco isiuzwe kwa wananchi na wao wakapewa hisa na hiyo ikasaidia kuipatia equity zaidi? Ukifikiria sana unaweza kuona kuwa Tanesco ndiyo inapotential kubwa ya kurudisha return nzuri kama itawekwa mikononi mwa wannachi kwa njia ya hisa huku serikali ikibakia na strategic shares (say 1 share). Tena tunaweza kufanya share za aina tatu za mtu mmoja mmoja, za taasisi na makampuni mengine na hiyo ya serikali. sema makampuni na taasisi nyingine zinapewa share asilimia 49 na Kampuni moja ikikatazwa kuwa na shares zaidi ya asilimia fulani ili kuondoa monopoly na wananchi wapewe nafasi ya kununua asilimia 50 na kuwa ni majority owners wa Tanesco huku vile vile mwananchi mmoja au familia moja ikizuiwa kiutaratibu kuwa na hisa kiasi fulani.

Tuiache NBC ilivyo au tuiboreshe lakini tubinafsishe Tanesco kimkakati bila kuhatarisha usalama na uhuru wetu wanishati.

...Wazo zuri na lenye kuweza kuleta faida kubwa kwa nchi. Ila, lazima ukumbuke au utambue kuwa huo ni mgodi wa watu, hawawezi kuuachia kiurahisi namna hiyo. Wao watavunia wapi?
 
Kama tunataka kusambaza umeme vijijini,itabidi TANESCO iwe overhauled na ioperate at a break even point to minimize costs kwa wanavijiji,sidhani kama hii ni recipe nzuri kwa private investors,otherwise tanesco ingeshakuwa na private captal kubwa tu!

...Kobello, si lazima kila mtu apate umeme iwe ni kijijini au mijini, ingawa itakuwa vigumu kuishi mjini bila umeme.

...Muhimu ni umeme kuwepo maeneo hayo ili kila anayeuhitaji na kuweza kuulipia aupate.

...Fahamu kwamba, tatizo Tanesco au sekta ya umeme nchi si ukosefu wa private investors, ni mvurugo wa kisiasa katika masuala ya kiuchumi.
 
Nashukuru sana. Nipo Sumbawanga. Hujanielewa. Ninashauri kufanya IPO ya Airtel na NBC ili kwanza kupata mapato kwa serikali lakini pili kwa kumilikisha uchumi kwa umma. IPO ni kwa wananchi kupitia soko la hisa.

Hukunielewa vema na ninaomba unielewe. Siku zote nimekuwa mstari wa mbele kuhakikisha DSE inakuwa more liquid. Nataka tuwe na kampuni nyingi sana DSE. Hii itawezesha uwazi.

Hon. Zitto, I like your effort to make sure that the DSE is more liquidated and to have more public companies in Tanzania. This will provide investors liquidity, marketability safety, etc of investment. It will provide Airtel and NBC with access to market funds, higher rating and public interests. Brokers will receive commission in lien to their services to investors. And, as far as the economy and the country is concerned, there will be a large saving, better growth which will move industries and higher income. These benefits may only be realized in proper regulated stock exchange either by the market itself or by law or by both.

However, as far as our securities system is concerned, I believe that a work still need to be done in terms of our corporate finance system, the way the DSE operates and more importantly our corporate governance system. One entrenched view of public companies is that they are widely-held funds of assets administered and run by specialist managers characterized by the separation of ownership from control. This gives rise to the concern that the directors who manage public companies may have considerable freedom to act with regard to their own self-interest.

There are also wider questions that have been the subject of extensive debate concerning the nature of corporate power and accountability in Tanzania. For whose benefit should these public companies operate? Should they only exist to serve the private interests of their investors or should the interests of other stakeholders (employees, creditors, community) be taken into account? What is the proper role of law in regulating the exercise of corporate power by the directors? Do we already already have in place a rigorous regulatory framework for initial public offerings in Tanzania? I think we need to first to address the factors hindering the development of the capital markets to develop these markets

An empirical study conducted by the some academicians at Mzumbe University, covering key informants from listed and unlisted companies, brokers, Capital and Securities Market Authority, and DSE has found that lack of good knowledge of the capital markets, high transaction costs, fear of information disclosure, lack of public awareness on the existence, benefits, risks and procedures for participating in capital markets and stringent listing requirements are the major factors, which hinder the development of the exchange in Tanzania. The lack of public awareness on the existence of the DSE has led only certain people to use the market. The study further found out that many listed companies do not even use the DSE to raise capital. So, it is likely that Airtel na NBC might follow the same suit.

At the end of the day is not about having many public companies trading at DSE but how effectively do we benefit from them. Unless you clarify, to me, it appears as if you are looking for a short term solution to the current problems. If this is the case, then I don't, this will help. I believe some effort still need to be undertaken within the DSE in terms of education and awareness creation about the usefulness of the Stock Exchange itself before floating securities on it. We also need to develop a strong regulatory framework on public companies. These will help the public in the long term. Otherwise, only certain people within the section of the society will benefit from the IPO.
 
Mchambuzi - unaonekana ni kijana mwenye uelewa wa mambo mengi sana hasa namna uchumi wa nchi hii ulikotoka na wapi viongozi wetu wanakoupeleka, binafsi napendekeza uje huku kwetu tuunganishe nguvu ili tuwatumikie hawa watanzania maskini.
 
I impressed with your analysis and suggestion to various points on what is best should Zitto do advice the government in the coming parliament budget assembly meeting.But sadly to hear your involvement membership-ccm at the same time having theses good ideas and views dedicated for our nation economy movement.I mean I don't understand your objective and need the development while you won't take the right decisions and actions.It's like you are waiting and asking someone to taste something good for you while would it be much better and meaningful in case you do by yourself.

Let me tell you the fact about the truth in relation to the development of our nation economy:
1.It is a simple action to take or what now you need to do rather than you had attempted the analysis above.

As I know if really we want to overcome development of this country economy the only and important thing to do is to start to promote and accept a big change by making first change the rilling political part which fail to get us in a right direction.And it's not easy and impossible that part to bring up development in economy by its own since all the failure and worse we have now is the results brought out of its policy so how comes you need keep on waiting something good from them while they only can do bad things.However it will take more than decades to get up clean while it was on leading rather than only one decade when it accept the failure and stand aside learning and building for the new image. Same like they do Democratic and Republican in USA.And guess what the main thing we had mistaken to adapt both democratization and the practical practice inducing a fair accept of the challenge.

2.So I advice to cooperate together to make change in political wise first in order to realize our dream to improve the national economy.

3.So what to do.We should promote and motivate any opposition political party which shows a vision and mission to rule and develop our economy except CCM.

4.By the way we are doing the right thing because we need to improve our livelihood now.In a right way because we are influencing through public education of civil right and responsibility of the government to maintain and deliver good lives .Addressing to anyone until the whole citizen understood and ready to take action in the coming election.In a right place in this country need change.In a right time ,from now until new ruling system took the office.

Thank you and put up on it.
 
Ushauri makini, kama Zitto kweli alisema hivyo apige break haraka, sio wazo zuri kwa nchi yetu na pia litamharibia image yake kisiasa.

NBC serikali haina HISA hata moja. Wameuzia Barclays na NBC mwaka huu inaunganishwa na barclays rasmi
 
Kwanini Tanesco isiuzwe kwa wananchi na wao wakapewa hisa na hiyo ikasaidia kuipatia equity zaidi? Ukifikiria sana unaweza kuona kuwa Tanesco ndiyo inapotential kubwa ya kurudisha return nzuri kama itawekwa mikononi mwa wannachi kwa njia ya hisa huku serikali ikibakia na strategic shares (say 1 share). Tena tunaweza kufanya share za aina tatu za mtu mmoja mmoja, za taasisi na makampuni mengine na hiyo ya serikali. sema makampuni na taasisi nyingine zinapewa share asilimia 49 na Kampuni moja ikikatazwa kuwa na shares zaidi ya asilimia fulani ili kuondoa monopoly na wananchi wapewe nafasi ya kununua asilimia 50 na kuwa ni majority owners wa Tanesco huku vile vile mwananchi mmoja au familia moja ikizuiwa kiutaratibu kuwa na hisa kiasi fulani.

Tuiache NBC ilivyo au tuiboreshe lakini tubinafsishe Tanesco kimkakati bila kuhatarisha usalama na uhuru wetu wanishati.

Unafikiri individual investor mwenye akili timamu atanunua shares TANESCO? Yaani hata hiyo prospectus yao sijui itasomekaje.


NBC serikali haina HISA hata moja. Wameuzia Barclays na NBC mwaka huu inaunganishwa na barclays
rasmi

NBC shareholding structure

ABSA Group Ltd. 55%
Government of the Republic of Tanzania 30%
International Finance Corporation 15%
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Nashukuru sana. Nipo Sumbawanga. Hujanielewa. Ninashauri kufanya IPO ya Airtel na NBC ili kwanza kupata mapato kwa serikali lakini pili kwa kumilikisha uchumi kwa umma. IPO ni kwa wananchi kupitia soko la hisa.

Hukunielewa vema na ninaomba unielewe. Siku zote nimekuwa mstari wa mbele kuhakikisha DSE inakuwa more liquid. Nataka tuwe na kampuni nyingi sana DSE. Hii itawezesha uwazi.

Mhe. Zitto pole na ziara ya Sumbuwanga mkuu.

Aksante kwa taarifa na kumwelewesha ndugu yetu wa CCM. Mimi nakuunga mkono 100 pc kwa mawazo yako na mtazamo wako makini kuhusu DSE. Ni kweli hata TBL(Kampuni ya Bia) na TCC(Sigara) wamefanimkiwa kutokana na Soko la Mtaji Dsm(DSE) baada ya kuuza hisa zao kwa Watanzania moja kwa moja na kwa kupitia soko hilo. Kuna Makampuni mengine yaliyofanikiwa kupitia utaratibu huu wa kuuza Hisa kwenye soko la mitaji k.m. Tanga Cement. So it's a good idea.

Serikali kweli inaweza kufanya hivyo kwa Airtel(formerly Celtel and Zain). Hawa jamaa walikuja hawana kitu waka-capitalise on TTCL(Kampuni ya Wazalendo) kwa kutumia Resources na Manpower ya TTCL kitapeli kuwa Celtel by then kuwa ni sister company ya TTCL . Baada ya kuanza kupata faida tu wakajitoa TTCL na kujiita Celtel Tanzania na baadaye Celtel International. Viongozi wa serikali ya CCM wanajua utapeli uliotumika wa Celtel kujitoa TTCL kwa kupitia mikono ya Mafisadi.

Juzi Zain kabla ya kujiita Airtel wameuza hisa kwa Kampuni ya Kihindi Bharti Airtel na kujipatia more than 10 Bilioni USD. Ajabu ni kwamba katika mauzo Serikali wala TTCL hawajapata mgawo wowote! Naamini kabisa hii siyo sawa hata kidogo. Mhe. Zitto nakumbuka juzi kwenye kikao cha Bunge lililomalizika uliuliza swali hilo kwa Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia kwanini Zain hawakutoa mgawo kwa Serikali/TTCL ambao ndiyo source ya mafanikio yao. Bila shaka unajua kilichojibiwa,ilikuwa ni ubabaishaji mpaka Mhe.Tundu Lissu akamwambia Spika kuwa swali lako halikujibiwa.

Kuhusu NBC the same applies. Lazima hisa za NBC ziende DSE ili watu wauziwe kwa utaratibu wa IPO.Tunajua NBC ilivyouzwa kwa bei ya kutupa ya Tshs.15 Bilioni kabla ya separation NMB/NBC. Baada ya separation ABSA wakatumia ujanja kwamba kulikuwa na debts and assets hazikuagawanywa sawa na matokeo yake ilikuja julikana kuwa NBC wanaidai NBM Tshs.15 Bilioni na NMB wakatakiwa wazilipe hizo pesa kwa NBC na matokeo yake ikawa ABSA wameuziwa NBC bureeeeeeeee!!!!Kazi saafi kabisa ya mafisadi key players wakiwa ANBEM(Anna na Benn Mkapa). Sina hakika Mkapa na mkewe walipata rushwa ya shilingi ngapi. Habari nilizo nazo ni kwamba Mkapa ana Bonge ya Jumba huko bondeni kwa mzee Madiba!

Namaliza kwa kusema kuwa Mhe. Zitto songa mbele na hoja yako binafsi kuiwasilisha Bungeni. Naamini itakuwa HOJA YENYE NGUVU,MAKINI NA IMETULIA.

Ubarikiwe.
 
Awali ya yote napenda kumpongeza sana mhe zitto kabwe na chadema kwa ujumla kwa kazi mnazozifanya nchini, hongereni sana. Pili nirudi katika mada, zitto yuko sawa kabisa hizo hisa ziuzwe ili zifidie hiyo tax gap'.mimi ni mwanafunzi pia ni mfuatiliaji sana wa uchumi na sera zake. katika sera za uchumi kuna sera maarufu iitwayo "supply side economics". katika sera hii ambayo ni nzuri sana kupambana na inflation na unemployment, jambo kuu na muhimu ni kwamba serikali isijihusishe na biashara,kama vile kumuliki hisa katika makampuni makubwa,nk.. kwa kuwa ikiwa serikali inamiliki makampuni ni dhahili kuwa kutatokea kile kiuchumi tunachokita "monopoly", kama ilivyo kwa tanesco hivi sasa. pili ,kutatokea na tatizo lingine ambalo wananchi tunalipigia kelele sana ,"Big government", serikali kubwa na hivyo pesa za walipa kodi zote huishia kuhudumia serikali badala ya wananchi. hivyo anacho propose zitto ni sahihi kwa kuwa hizo supply side tax cuts,ndio suluhisho pekee la kupambana na inflation katika nchi hii na serikali iache kufanya biashara badala yake isimamie uchumi kisera zaidi.......................
 
Huko ccm vijana mpo. Tatizo ninyi ni waoga wa mapambano mnakimbilia kubebwa ndo maana mnaminywa hamuwezi kuwashauri wale walio serikalini. Unaonaje huo mtindo wako wa ushauri ungeutumia pia kwa wenzako wa ccm wasioambilika kwa sababu ya kiburi na majivuno.
 
Back
Top Bottom