Mheshimiwa Rais Kikwete anaipenda Tanzania?

Watanzania

JF-Expert Member
Jul 7, 2009
727
42
Ni haki kwa wananchi kujiridhisha kama rais anaipenda nchi yetu. Kuna mambo kadhaa ambayo rais anawezapimwa kama anaipenda nchi yake. Hili suala la Mh. Rais Kikwete kufanya safari nyingi nje ya nchi kwa nchi maskini kama ilivyo yetu ni mojawapo ya kigezo cha kumpima rais kama anapenda nchi . Ukimwangalia Rais Kikwete akiwa nje ya nchi utagundua kuwa anafurahia kuwa nje ya nchi kuliko Tanzania. Rais ambaye anatarajiwa kuwa na muda wa kutosha kutafakari matatizo ya nchi na kuyapatia ufumbuzi yeye anafunga safari nyingi na anafurahia kuwa nje ya nchi yake kuliko kutulia nchini na kutoa uongozi unaohitajika. Je hii si dalili ya rais kutoipenda nchi yake kwa dhati?
 
what do you expect from mtoto wa kikwere?hapo ndo kishajituma mpaka uwezo wake umefika mwisho.
 
angeipenda nnchi yake hawa kina RA, E, Lowassa, Manji, WANGEKUA NDANI WANAPIGA SOGA na LIYUMBA.
 
You are right, ni dalili ya kutokua mzalendo. Sasa nani wa kulaumiwa au tufanyeje ukizingatia tuna miaka mingine 6 ya kuwa nae.
 
Anaweza kuipenda nchi kwa maana ya geographical position na mambo ya namna hiyo lakini akawa hawapendi wananchi.je tunahitaji lipi kati ya hayo.
 
Kwa ujumla tusha liwa!!

Hiyo miaka sita ni sawa na miaka 60 ya maendeleo kwa nyuma. By the time inafika 2015 tutakuwa hata umeme wa mgao hautakuwepo isipokuwa kwa wale wenye majenereta ya mchina. Kwa ujumla jamaa kazi haiwezi, imagine kashindwa hata kumalizia barabara za Mkapa???
 
HAIPENDI NCHI YAKE.
Mf. kama baba wa familia hakai na familia which means..............................:(
 
He is from God.....hayo ni maneno yaliyokuwa yakisika baada ya kula fedha za kampen lakin sasa husikii tena ...mara hatupendi..haipendi nchi..yako wapi sasa? Tuzidi kumuomba Mungu atufungue kiakili we will be able to find a good leader.
 
anapenda urais ila haipendi tanzania................ukweli mtupu kwani kwake maneno ni bora kuliko matendo...
 
No one show question if other fellow Tanzanias kama wanaipenda nchin au vipi.Just ask you self what you have done to the country that prove you love this country more than others.

Kinachomsumbua Kikwete ni alikua na Mbinu ya kupambana kuwa President lakini hana vision on which direction he want to take the country. Thus it
 
Lingekuwepo jopo kama inavyopaswa kuwa kwa (Baraza la mawaziri) kwamba wakati anapeleka tathmini yake ya jinsi alivyo fanikiwa au kushindwa kufikia matarajio katika ziara hizo ingekuwa na maana sana kwetu. Vinginevyo inakuwa Bora ziara na sio ziara bora zenye mafanikio na mvuto kwa nchi yetu.

Ni neno kali sana kumwambia mtu amelaaniwa lakini nahisi nchi hii imelaaniwa, ukiangalia historia ya nchi hii hakuna hata siku moja wananchi wameingia mitaani na kuandamana kwa hisia kuonyesha kwamba mambo hayaendi sawa, na mwisho wa maandamano kukawa na followup ya nguvu zaidi ya siasa rojorojo tunazofanya.

Utani umezidi sana katika utawala wa nchi hii, mtu anatoka nchini kwake kuna mali ya kutosha tu kama madini, lakini anaingia mikataba isiyo na masilahi ya taifa halafu yeye huyo kwenda kutembeza bakuli badala ya kutunza alicho nacho kiifaye nchi yake.

Enzi za mwalimu ilikuwa ni sifa kwa kiongozi kuona wizara anayo iongoza ina deliver kile kinacho tazamiwa na wananchi, hivyo hivyo kwa viongozi wote. Lakini leo imekuwa sifa kiongozi kuwa mwizi, kisa pesa za kampeni nchi ambayo viongozi wake kila wakati inafikiria uchaguzi haiwezi kuwa na maendeleo yoyote ya maana kwa nchi na wananchi kwa ujumla.

Tuwe tunafikiria uchumi na maendeleo na sio uchaguzi......uchaguzi.......uchaguzi na mtaji wa uchaguzi.

Tanzania yenye viongozi wapenda nchi inawezekana.
 
saaaana kaka,
Fikiria mfano mdogo tu..... tunaarifiwa kuwa hata watoto wake hawakwenda kusoma ulaya inamaana katika maisha yake ya uwaziri hakuwa na uwezo wa kuwasomesha huko?

Kanakwamba hiyo haitoshi wakati yuko wizaraya mambo ya nje angekosa hata michongo ya sponsorship kutoka nchi za magharibi? kumbuka kuwa kipindi hiko wanawe wawili walijiunga na vyuo vikuu hapahapa. Je tunataka uzalendo upi?
 
saaaana kaka,
Fikiria mfano mdogo tu..... tunaarifiwa kuwa hata watoto wake hawakwenda kusoma ulaya inamaana katika maisha yake ya uwaziri hakuwa na uwezo wa kuwasomesha huko?

Kanakwamba hiyo haitoshi wakati yuko wizaraya mambo ya nje angekosa hata michongo ya sponsorship kutoka nchi za magharibi? kumbuka kuwa kipindi hiko wanawe wawili walijiunga na vyuo vikuu hapahapa. Je tunataka uzalendo upi?

Enzi hizo, babu zetu walikuwa wanapewa vioo na wanatoa almasi!

watoto kusoma ndani ya nchi ndio alama tosha ya uzalendo?

Clinton mtoto wake akienda kusoma England, basi hana uzalendo na USA

Watanzania woote ambao watoto wao wanasoma nje, hawana uzalendo?

kuna hoja imejificha unayo weka wazi kwa nini unampenda JK, achana na hoja za kitoto kama hizi.

wengi wanampenda JK kwa sababu ya udini, usiwe mmoja wapo!
 
watanzania ni watu wepesi sana kudanganywa, na watu kama JK wanalijua hilo.Huwezi kuamini nilikuwa natoa maoni kwenye blogi ya michuzi, kuna mtu anafurahia kupewa daftari bure wakati ya enzi za mwalimu....na kusahau kama chakula inambidi apange foleni kama mkimbizi....

Hivi ndio tulivyo watanzania, idadi kubwa watu hawajasoma na ni rahisi kuona Tanzania watu wanampenda Kikwete na kumpatia mara ya 2 aende ofisini kufanya kazi.Wakati huyu ni mtu watanzania wanatakiwa kuandamana, keshavunja katiba si zaidi ya mara 2...na watanzania kimya kama hawapo kabisa...


  • JK kwenye uongozi wake amevunja katiba kwa kujadili kero za muungano nje ya bunge....


  • Amevunja tena katiba kwa kutengeneza kamati ya mzee Mwinyi na kuadhibu wabunge....

Lakini watu watamsamehe kwasababu amezungumza na wananchi kwa njia ya Luninga!
 
Kihistoria huyu ndo Raisi aliyesafiri zaidi nje ya nchi kwa kipindi kifupi cha utawala (4yrs) wake????????
 
Back
Top Bottom