Fredrick Sanga
JF-Expert Member
- Jan 27, 2011
- 3,153
- 697
Pamoja na kwamba huna mkuu, ni mtu wa staha, na ni mapema sana, lakini kwa kanzi ya kwanza nzito uliyopewa ulionyesha uzalendo wa hali ya juu. Najua kazi ile ya kamati ya umeme ilikuwa hatari sana, lakini uliifanya kwa umakini na uaminifu kwa umma. inawezekana kwa usalama mengine hayakusemwa lakin ulifanya. Unafaa kuchukua uraisi 2015.
Vigezo:
Umri unakuruhusu
Umeshapewa ujiko wa uwaziri, kunjua makucha
Kule kyela watakataa jinsi wanavyokuhitaji, anza kupiga debe
Wako wengine wenye sifa lakini umewazidi kielimu Dr.
Hata CDM wanakuogopa
Ni mcha Mungu
Huna Mkuu
Mtoto wa mkulima
Unaujua ukweli pamoja na kwamba umebanwa
Hawa wengine, bahati mbaya watakuwa wamwchoka
Dr Slaa. Six, Mwandosya, Makamba, Lowasa NK
tafadhali anza mbele kwa mbele, tena staili ya Magufuli.
Mwalimu alisema hivi, kama kiongozi amechaguliwa na watu, halafu anasimamia haki za watu waliomchagua basi ana haki ya kuwa kiongozi, lakini kama au hakuchaguliwa na wananchi au amechaguliwa halafu akaacha kusimamia haki za wale waliomchagua, basi anakuwa amepoteza haki ya kuwa kiongozi. huyu alikuwa mwana wa fdilisophia. Alimwambia mtu mmoja aliyekuwa TYL kuwa ni mchafu na hafai kuwa kiongozi, ana tamm ya mali, bado kijana mdogo lakini ana mali nyingi sana, huyu!. Mambo haya ni juu ya wana wa nchi, CCM, CUF, CDM, UDP, TLP, NCCR, NLD NK kuchambua pumba ni ipi na mchele ni upi.
Tatizo huwa ni kukubali kununuliwa. Vyama inabidi vifute kabisa dhana ya kununua wanachama. Kwani chama ni wanachama, na kinaendeshwa na wanachama. Kama kuna mtu anafikiri kwa visenti vyake atanunua wanachama wote amekwisha. asome alama za nyakati. kuna watu waligombea ubunge kwa pesa nyingi wameshindwa na watu waliokuwa wakichangiwa na wapiga kura.
Alama za nyakati, zinaonyesha Mheshimiwa Mwakyembe haitaji kuonga hata senti tano kwa mtanzania. Ila ajue kwamba asiposhughulikia swala hili hata nbinguni ataulizwa.