Rucho Ongiri
Member
- Dec 23, 2011
- 7
- 3
Mheshimiwa mbunge wa viti maalum mkoa wa Arusha, Joyce Mukya jana ameamua kusherehekea Sikukuu ya Christmas na Mwaka mpya kwa kutoa zawadi mbalimbali kwa vituo vitano vya kulea watoto yatima vilivyoko Manispaa ya Arusha na wilaya ya Arumeru.
Misaada iliyotolewa na mbunge huyo ambaye hii ni mara yake ya kwanza kuingia bungeni ni pamoja na kilo 250 za unga wa sembe, mchele kilo 125, sukari kilo 100, ndoo tano za mafuta ya kupikia, mbuzi watano, katoni 25 za juisi, chumvi kilo 50, dazani tano za majani ya chai na mifuko mitano ya pipi.
Vituo vya kulea yatima vilivyopatiwa misaada hiyo katika hafla fupi iliyofanyika ofisini mbunge huyo zilizoko jengo la ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Arusha ni pamoja na Faraja Orphanage children home kilichopo eneo la Shangarai wilayani Arumeru, Kibowa centre, Medical Daughters of Merry, Tuamkeni Orphans care na Mama Hadija children home, vyote vya Manispaa ya Arusha.
Mbunge huyo aliwaomba watu wenye uwezo kuacha ubinafsi kwa kujifikiria wao na familia zao, badala yake wawafikirie wengine wenye shida na uhitaji katika jamii kama watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu kwa kushirikiana nao kiasi kidogo walichojaaliwana Mwenyezi Mungu.
picha za tukio hilo baadaye...!
Misaada iliyotolewa na mbunge huyo ambaye hii ni mara yake ya kwanza kuingia bungeni ni pamoja na kilo 250 za unga wa sembe, mchele kilo 125, sukari kilo 100, ndoo tano za mafuta ya kupikia, mbuzi watano, katoni 25 za juisi, chumvi kilo 50, dazani tano za majani ya chai na mifuko mitano ya pipi.
Vituo vya kulea yatima vilivyopatiwa misaada hiyo katika hafla fupi iliyofanyika ofisini mbunge huyo zilizoko jengo la ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Arusha ni pamoja na Faraja Orphanage children home kilichopo eneo la Shangarai wilayani Arumeru, Kibowa centre, Medical Daughters of Merry, Tuamkeni Orphans care na Mama Hadija children home, vyote vya Manispaa ya Arusha.
Mbunge huyo aliwaomba watu wenye uwezo kuacha ubinafsi kwa kujifikiria wao na familia zao, badala yake wawafikirie wengine wenye shida na uhitaji katika jamii kama watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu kwa kushirikiana nao kiasi kidogo walichojaaliwana Mwenyezi Mungu.
picha za tukio hilo baadaye...!