Lekanjobe Kubinika
JF-Expert Member
- Dec 6, 2006
- 3,020
- 577
- Thread starter
- #81
ninachosikitika ni ile hali ya watanzania ''kuamini kuwa'' JPM is working independently!yani watanzania seriously tunaamini JPM IS NOT ONE OF THEM!lol!
i am so so sorry for my country
Tanzania ya sasa ni kweli inao viongozi wazuri ambao hatuwajui kwa sababu hawajapata nafasi kuonekana. Tena basi, ni vigumu kuwaona viongozi wazuri kwa sababu sio wapayukaji ila ni watendaji wazuri. Ukibahatika kuona vitu vyao ndio unatambua. Si unajua debe tupu haliachi kutika?
Sio lazima atoke CCM, mimi sina chama tangu vyama vingi vilipoanza 1992, lakini hilo haliniweki pembeni kutafakari nani anafaa kuwa kiongozi wangu, kwani ni lazima atakuwapo kiongozi tu nitake nisitake. Kweli ubabaishaji wa viongozi wangu umenilazimisha nisuse hata shughuli za uchaguzi, kwa sababu dhahiri - anayemzidi mwenzie kwa ufisadi ndiye anachaguliwa kuwa kiongozi mara nyingi. Siku ikitokea JPM anagombea urais nakuhakikishia nitajiandikisha kupiga kura na kumpigia.
Leka