Mheshimiwa John Mnyika: What is Plan C

<br />
<br />
Hatupaswi kuendelea kuweka makalio yetu chini na kuendelea kulalamika...Tumenung'unika sana,tumelalamika sana,sasa inatosha.Hatuna haja ya kuendelea tena kuumiza makoo yetu wala kuzidi kutia mikono mifukoni mwetu tukitafuta shilingi dhaifu (ambayo hata hivyo imekuwa adimu kwa wengi)ili eti tufanye jambo la mfano kwa watawala.Ni muda muafaka wa kutumia nguvu yetu ili kuleta mabadiliko chanya kwa ustawi wa taifa letu!

Mkuu nakuunga mkono na hili ndio tunapaswa tufanye mabadiliko sio kwa njia ya kupiga tuu kelele ambazo washirika wa upende wa pili hata haziwaumizi, wao wanaendeela kupokea ten percent zao na hali inaendelea kuwa ile ile naona sasa muda wa kufanya kile watawala hawataki umefika wa kutetea haki zetu na kupata kile ambacho tunakitaka kwa ajili ya kusaidia Tanzania ambayo inalemaa na kuendelea kudidimia
 
Mhh nadhani haujanipata Gaijin hapa mimi ninaongelea short term solution na sio kwamba iwe the way to go.., bali ni symbolic.., na kama Tanesco wanaweza kununua au kukopa vyombo vya kuzalishia pengine basi na sisi wanajamii tunaweza tukawakopa mafuta yetu (pesa zetu) na watu wataendelea kulipia according to their meters na hapo wanajamii tunaweza kuidai Tanesco in the near future au tuka-minize tulichowakopa kwenye usage yetu... (mfano I we owe you 20,000/= our bill normally is 100/= a month therefore we owe you 200 months of service)<br />
<br />
Lakini all in all in the long run huenda hii ikawa expensive solution lakini the first thing ni kuonyesha we can (as symbolic)... na hata kama kuwashauri Tanesco wapunguze feed in Tariff who is better to do... kama sio viongozi wetu..,

"...lakini the first thing ni kuonyesha we can(as symbolic)..."Mkuu hii isiwe kwa kuendelea kutoboa mifuko yetu zaidi,hawa watu wamekubuhu,hawasikii la mwazini wala la mteka maji msikitini,hawafundishiki hawa!
 
<br />
<br />
"...lakini the first thing ni kuonyesha we can(as symbolic)..."Mkuu hii isiwe kwa kuendelea kutoboa mifuko yetu zaidi,hawa watu wamekubuhu,hawasikii la mwazini wala la mteka maji msikitini,hawafundishiki hawa!

All in all if anything should be done... needs to be done now..., sababu kukaa bila kufanya kitu ni kuendelea kutoboka mifuko....,kwa kukosa umeme tunapoteza kipato chetu kikubwa na tukijitahidi kununua generator ni kwamba uzalishaji unakuwa wa gharama kuliko ambavyo ingekuwa..., na mkuu kuleta changes kwa kuingia barabarani iwe ni last option (sababu hii sometimes haina guarantee...)
 
Mnaruka ruka weee, kuweni wawazi bana kuwa mnataka kuandamana kama Misri, Tunisia na kwingine ili kuingoa serikali kwanguvu
 
&#670;ont&#633;act Sniper;2377430 said:
Tik tok tik tok.......Kuna kitu kilnalazimishwa kutokea hapa, tena bila ya serikali kujua kuwa inarutubisha mazingira ya kitu hicho kutokea.....Siongezi neno, na tusubiri.
Lakini Plac ni mbaya sana, nilkuwa naiongelea mahali fulani leo na watu fulani namna Plan c inavyotengenezwa na kuwafanya wananchi wajikute wapo barabarani bila hata ya kuitwa au kuhimizwa kufanya hivyo.....ni rahsi sana, ni kama uji kwa mwenye mapengo.....Mtakapoona hayo yanatokea mjue yametimia.
Mawazo yako unanikumbusha ile siku ya msiba wa Kawawa, mie nilifikiri ni jirani yangu tuu ndiye aliyewaza vile kumbe ni wengi.
Watu wamechoshwa kabisa na Si si Em
 
CCM imeshindwa kuongoza nchi hii na sasa wanatakiwa kwa hiari yao waseme imetosha na watupishe

Haitafika siku ambayo watakiri kwa vinywa vyao kuwa eti wameshindwa...haitatokea hiyo.Pia hatupaswi kusubiri kauli yao,ishara na dalili zinaonesha wazi kushindwa kwao!
 
Mnaruka ruka weee, kuweni wawazi bana kuwa mnataka kuandamana kama Misri, Tunisia na kwingine ili kuingoa serikali kwanguvu

Mkuu hapa nimeomba solution ya nini kifanyike hususan short term kuondokana na hii shida ya umeme...; nadhani hata wewe utakubali serikali iliyo madarakani imeshindwa kazi... sasa wewe unadhani tufanye nini.., kuwangoa huenda ikawa long term solution..,
 
Mkuu hapa nimeomba solution ya nini kifanyike hususan short term kuondokana na hii shida ya umeme...; nadhani hata wewe utakubali serikali iliyo madarakani imeshindwa kazi... sasa wewe unadhani tufanye nini.., kuwangoa huenda ikawa long term solution..,

VOR naona unazunguka zunguka tuu yaani unakwepa kutoa jibu
Sema wazi ni nini haja yako na nini unataka maana kote unazunguka hutoi solution ya nini kifanyike
Maana umekuwa na wewe mlalamishi badala ya kuwa wazi nini kifanyike
 
VOR naona unazunguka zunguka tuu yaani unakwepa kutoa jibu
Sema wazi ni nini haja yako na nini unataka maana kote unazunguka hutoi solution ya nini kifanyike
Maana umekuwa na wewe mlalamishi badala ya kuwa wazi nini kifanyike

Long Term & Best Solution ya Matatizo yote ya Tanzania

  • System kubadilika ambayo inaweza kumwajibisha kiongozi yoyote yule na kuwa na transparency ya kila kitu kinachofanyika. (Unless kila atakaeingia kwenye kiti anaweza akawa corrupt)
  • Kubadilika kwa System inabidi kuwa na fair playing field sababu wale ambao wananufaika na uozo wa sasa watajitahidi system ibaki kama ilivyo
  • Hata kama system ikiwa in place lazima kuwe na Upinzani wa nguvu ili hata kama wakipingana na kitu wawe na nguvu ya kupinga hicho kitu (na hapa ninamaanisha bungeni atleast wabunge wawe 40% to 60% yaani wapinzani wawe na meno Bungeni bila hivyo Bunge litabaki kuwa rubberstamp.
Utaona kwamba ili hayo hapo juu yafanikiwe inahitaji kitu kimoja tu (KIFO CHA CCM) na hapa sisemi sababu ya ushabiki, bali ni sababu ya upendo wa nchi yangu CCM ilivyojijengea na kujinyakulia vitega uchumi na kuweka mizizi kila mahali (wakuu wa wilaya)..., inafanya kazi ya wapinzani kuwa ngumu sana.. kwahiyo hata CCM ikuvunjika katika vyama kama vitatu vya Siasa tutakuwa tumetengeneza level playing field ya upinzani wa kweli.. Sasa swali ni kwamba ni vipi CCM itakufa...???

Kufanya Mapinduzi??.... its not a guarantee sababu wale wale watu wanaweza wakajitokeza tena na kuendelea wanayofanya CCM kwa jina lingine..., Hapa mkuu tatizo sio watu ndani ya CCM pekee bali ni CCM yenyewe na nguvu zake...

Kwahiyo mkuu je tusubiri ku-sort out tatizo la umeme wakati tunasubiri hayo hapo juu yatokee (sababu that is long term solution..) what is short term au hakuna short term?.., Solar ingekuwa cheaper, affordable na practical mimi ningeshaacha zamani kuwategemea hawa jamaa katika issue zangu
 
Kinachosikitisha na kwa serikali kuamini katika kusema uongo na kudharau wananchi kwa kiwango cha hali ya juu
Dr Mrisho Jakaya Kikwete ni raisi aiyekubuhu kwa kusema uongo asiye hata na chembe moja ya uoga,haheshimu kabisa wananchi wake,ni mjivuni na mropokaji haijapita hata miezi miwili aliposema yeye sio mvua kwa hiyo hawezi kujaza mabwawa lakini alipokua anasaini ununuzi wa IPTL miongo miwili iliyopita hakujua kwamba mabwawa hayatoshi tena bali angeweza kupanga mpango wakutengeneza mabwawa mengine ya kuvuna maji

Amemuambukiza Waziri wake MKuu Mh.Mizengo Kayanda Peter Pinda,huyu ndio hovyo na muongo sana ,anakisilani anadharau hata wabunge wanaowakilisha wananchi kwa kuwajibu majibu ya mkato yasiyojitosheleza,hakuna analofanya zaidi ya kuzungusha mikono akihitaji huruma ya wananchi karibu miaka minne yuko madarakani,amengia kukiwa na tatizo kubwa la uemem nchi ikiwa gizani hadi leo amebaki kutuambia wananchi tumuelewe utamuelewa mtu asiye adilifu,aliyelewa madaraka asiyemfikiria mwananchi

Waziri Ngeleja kafundishwa uongo mpaka amehitimu kuwa mwongo nambari one asiye na tone moja la aibu kazi kuzungusha macho akitunga uongo kugeuza watanzania mafara,mwishoni mwa mwaka jana pale ubungo alisema ikifika machi mwaka huu tatizo la umeme ingekuwa historia,hatujakaa sawa mwezi machi akasema mitambo itaingia mei na hakutakuwa na shida tena ,sasa anasema mwishoni mwa mweezi wa Agusti,aibu na haiwezekani kuwa na viongozi wasio waadilifu wanadharau wananchi,waongo,wala rushwa,ten parcent hizo ,kila mtu ajifikirie alipo jee hawa watu waongo waendelee kuwa na dhamana yetu mpaka baada ya miaka minne ijayo hilo haliwezekani
Mtanzania amka sasa hakuna wa kukuinua wewe mwenyewe amua sasa kataa hawa viongozi waongo waliokosa heshima
 
VOR hizo zote ni long term plan ambazo zinahitaji sana elimu ya siasa kuweza kufikisha ujumbe kama huo. Utashi ambao watanzania hata hivi vyama vilivyopo hawataki kufanya. Kuwaelewesha watu right zao wajue kuwa wanajitajika wafanyiwe nini na serikali yao na wao wafanye nini. kama wanalipa kodi ipaswavyo wajue kuwa wataidai serikali yao huduma za kijamii.

Wenzetu wanajua umuhimu huo na ndo maana huduma za kijamii ni must sio ombi wala ahadi za wabunge na rais ambazo hazina guarantee
Uwajibikaji uwepo kama kiongozi yoyote ameshindwa kupeform wananchi wawe na ruhusa ya kumuondoa na sio sasa mtu anaboronga an bado ana nguvu za kusema sijiuzulu. wananchi wawe na jeuri ya kumwambia wazi umeshindwa ondoka madarakani wapishe wenye kuweza
Kupunguza nguvu za mtu mmoja alitye na madaraka ya kuteua kila mtu na kumwajibisha atakavyotaka yeye na umma pia uwe na uwezo wa kusema hapa yatosha ondoka madarakani
Bunge lenye uwezo na lenye mamlaka ya kuiambia serikali basi hapa yatosha na sio kukaa mle ndani kutetea matumbo yao tuu

Haya ni long term plan
Kwa sasa na tatizo tulilo nalo nini suluhisho la haraka kutuondoa kwenye hili giza
Hapo ndio ninapokutaka VOR unipe suluhisho maana hata za kwako bado ni long term plan
 
Nashauri maandamano ya kudai umeme tanzania nzima..tuanze na mwanza kwa wenje,then arusha! bila hivyo hakuna mabadiliko.. tuandamane
 
Jamaa yupo Bungeni analeta habari zile zile za kila siku: (Waziri Malima)
  • Ukosekanaji wa mafuta (wasambazaji kugoma)
  • mvua
  • gesi
  • matengenezo
Story zile zile za kila siku..., hakuna jipya hapa.., Pia kama kawaida anaitupia lawama Tanesco kwamba haikuwaambia wananchi ni nini kilichokuwa kinaendelea..... (bure kabisa hawa watu)...

Eti matatizo mengi yametokea kwa wakati mmoja.., hivi hawa wasambazaji waligoma lini?? na huu mgao umeanza lini?
 
Mtanzania amka sasa hakuna wa kukuinua wewe mwenyewe amua sasa kataa hawa viongozi waongo waliokosa heshima
Mbona watu tumeshawakataa sana au unashauri njia ipi nyingine ya kuwakataa...

Yaani hapa nimetoka kuangalia tamko la serikali kuhusu huu mgao.., yaani hakuna jipya ni yale yale ambayo huwa wanasema kila siku, mafuta kuchelewa, maji, matengenezo n.k...., yaani hata hakuna umuhimu wa kuongea angeweka tu recorded tape (CD) sababu walichosema leo ndio walisema jana na watasema kesho
 
Back
Top Bottom