Mheshimiwa John Mnyika: What is Plan C

VoiceOfReason

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
5,194
1,355
Heshima Mbele Mkuu na Hongera kwa Kazi Nzuri....

Ni kweli kwamba nyie sio wakusanya Kodi lakini tulipofika tunahitaji msaada sababu kinachofanyika sasa hakifanyi kazi….

Plan A: Serikali, Waziri Ngereja na watu wake wameshindwa kazi kinachoendelea sasa ni usanii na watu hatupewi majibu yanayoeleweka

Plan B: Kuandamana mpaka kieleweke lakini sidhani kama hii itasaidia na je isiposaidia ni nini kitafuata…. what is Plan C:

Sababu watu waliotakiwa kufanya kazi yao wameshindwa tunaomba wewe Waziri kivuli tushauliane ni nini cha kufanya, na tuone kama sisi wananchi tunaweza kujinasua wenyewe katika hii laana ya kujitakia ambayo imepelekea uchumi kusimama...

Ni ukweli usiopingika kwamba sasa hali ni mbaya sana sehemu kama Mbeya, Arusha na Mwanza watu hawana umeme kwa takriban wiki sasa. Yaani umeme haurudi hata dakika moja watu wamebadilisha fridge kuwa kabati na kuvaa nguo ambayo haijanyoshwa imekuwa fashion.

Mwanza huwa wanapata mgao wa 42MW kutoka grid wakati sasa wanapewa 4MW… Sasa Je tatizo ni nini je ni mitambo au mafuta ndio hayapo na kama ni mafuta kwanini tunakodi mitambo ambayo itakuja kutumia mafuta hayo hayo na kama ni mvua iweje baada ya bajeti kupita ndio maji kuisha kabisa (yaani ule umeme tuliopata wakati bajeti haijapita ulitoka wapi..)

Pendekezo
Sababu Serikali imeshindwa Je sisi wananchi tunaweza kuchangia nini..?, Kama tatizo ni mafuta ni vema tukajua hayo mafuta gharama ni kiasi gani ili wananchi na wadau tuweze kujitolea (sababu ni more expensive kutumia generator ndogo ndogo kuliko generator kubwa za Tanesco ambazo ni more efficient). Mfano Nyakato Mwanza huwa kuna Generator sasa kama hizi hazijawashwa nina uhakika wafanya biashara wote watakuwa tayari kuona kwamba hizi zinawashwa hata kwa kuchangia gharama...

Kwa niaba ya wananchi wengine tunakuomba tuchangie mawazo ni kipi tunaweza kufanya ili kuondokana na huu usumbufu.., hata kwa kuonyesha mfano kwa kuondoa huu usumbufu hata kwa kusaidia mtaa mmoja au kuhakikisha inapita harambee ya kuchangia mafuta… (kama tatizo ni mafuta..) (nina uhakika hii italipa dividends come 2015)

Ninaomba mawazo yako mkuu wewe kama Waziri Kivuli na Mwana-Jamvi mwenzetu sababu hii emergency solution kama itafanikiwa December ambapo mvua zitaanza sioni kwanini ziitwe emergency kwangu mimi zinaonekana kama long term solution

Voiceofreason,

Nashukuru kwa maoni yako na ya wachangiaji wengine. Suala hili nitalitolea tamko rasmi. Hoja yako ilikuwa mwezi Agosti, wakati mpango wa dharura ndio ulikuwa kwenye hatua za awali za utekelezaji. Serikali ilihodhi usimamizi wa utekelezaji wa mpango husika na kiwango kikubwa iliachiwa Wizara ya Nishati na Madini. Nilitahadharisha kwamba kwa mfumo huo malengo yaliyotajwa bungeni hayatatimia kwa wakati. Sasa tuko mwezi Oktoba na malengo ya mwezi Septemba ya mpango wa dharura sehemu kubwa hayajafikiwa; tunapoelekea sio kuzuri kama hatutakuwa na Plan C kuanzia mwezi wa Oktoba/Novemba. Tuendelee kujadili na kuchukua hatua za haraka

JJ
 
VOR kwa kweli hali halisi iliyokuwepo ni matokeo ya muda mrefu ya kupeana posho na kupitisha bajeti zisizokuwa na mashiko nimesikia msemaji wa tanesco mwanza anasema mtakaa gizani kwa miezi 4 unless otherwise miujiza itokee.

Swali kwako, kama wizara ambayo ndo yenye mamlaka/madaraka ya kuregulate hali kama hii imetoa jibu rahisi namna hii kweli mnyika hata akitoa option yenye positive impanct kweli itafanyiwa kazi?

Miezi minne kwa mikoa kama mwanza,mbeya and arusha kukosa umeme ni janga la taifa kweli sh itaporomoka sana.

Note; Viongozi wengi hawawajibiki kwa kuwa hakuna wa kuwawajibisha......take a note
 
Sote tunajua kwamba jiji la Mwanza, Arusha na Mbeya yote yako chini ya CHADEMA, hatushangai pia kuona Serikali inatia kiwingu cha giza katika maeneo hayo, wanadhani wakifanya hivyo wakazi wa mikoa hiyo watabadili msimamo wao na kuunga mkono chama cha MAGAMBA. Wananchi sasa hivi hawadanganyiki wembe ni ule ule hadi kieleweke.
 
There is no need of Plan C

CCM na Serikali yake wanafanya vizuri kuleta umeme wa uhakika kwa watanzania

Mkuu kama bado unaota au una nia ya kuwakejeli watu bora usijibu. Kuna watu wana siku ya tatu hawajauona umeme wewe unawakejeli watu kuwa tutapata umeme wa uhakika
Wacha hasira za watu zipoe
 
VOR kwa kweli hali halisi iliyokuwepo ni matokeo ya muda mrefu
ya kupeana posho na kupitisha bajeti zisizokuwa na mashiko
nimesikia msemaji wa tanesco mwanza anasema mtakaa gizani kwa miezi 4
unless otherwise miujiza itokee.
swali kwako,
kama wizara ambayo ndo yenye mamlaka/madaraka ya kuregulate hali kama
hii imetoa jibu rahisi namna hii kweli mnyika hata akitoa option yenye positive impanct
kweli itafanyiwa kazi??

miezi minne kwa mikoa kama mwanza,mbeya and arusha kukosa umeme ni janga la taifa
kweli sh itaporomoka sana.

note;viongozi wengi hawawajibiki kwa kuwa hakuna wa kuwawajibisha......take a note

Miezi hii bw Makofia, kwa sisi wakaaji wa mikoa ya kanda ya ziwa ndo balaa kabisa.
Hii ni miezi ya mavuno kama Pamba,Tumbaku,Kahawa n,k

Sasa ili kuichambua pamba ginnery, kunahitaji umeme tena wa uhakika ili kwenda na muda, ndani ya kipindi cha miezi minne ya msimu.
Hivyo hivyo kwenye kahawa na mazao mengine. Huu mgao wa wiki nzima umeme hamna, sijui tutazalisha nini hapo?.

Zaidi ni uchumi wa nchi kuporomoka, Ajira kukosekana n.k
Baba Riz1, anatakiwa achukuwe maamuzi magumu kama yafuatavyo

1)Kufuta safari zote za viongozi nje ya nchi
2)Kufuta vikao na semina, warsha na kama ni lazima basi kwa kibali maalum
3)Kuachana na matumizi ya magari yanayotumia mafuta mengi (VX)
4)Kufuta EXEMPTION zote za mafuta ya migodini. n.k

Pesa zote zielekezwe tanesco kununua mitambo yao ya kuzalisha umeme, sio dharura.
Ni bora kuwa na dhiki ya muda mfupi, ili mje kupata faraja ya muda mrefu........

Jamani umeme umekatika .........kwa
 
VOR kwa kweli hali halisi iliyokuwepo ni matokeo ya muda mrefu ya kupeana posho na kupitisha bajeti zisizokuwa na mashiko nimesikia msemaji wa tanesco mwanza anasema mtakaa gizani kwa miezi 4 unless otherwise miujiza itokee.

Swali kwako, kama wizara ambayo ndo yenye mamlaka/madaraka ya kuregulate hali kama hii imetoa jibu rahisi namna hii kweli mnyika hata akitoa option yenye positive impanct kweli itafanyiwa kazi?

Note; Viongozi wengi hawawajibiki kwa kuwa hakuna wa kuwawajibisha......take a note

Mkuu hapa inabidi wananchi tuache kuitegemea serikali yetu sababu imekuwa ikituangusha mara nyingi sana..., kwahiyo tunachohitaji ni mtu ambae yupo juu anaeweza aka-mobilize watu na kutoa mawazo yetu, na sisi wananchi wenyewe kujifanyia kazi.., hata kwa michango ya hali na mali., kama kweli Mwanza kuna ma-generator.., na kama hayajawashwa, kwanini tusichangishe sisi wenyewe wananchi na kununua hayo mafuta kuliko kila mtu kununua mafuta yake mwenyewe ambayo mwisho wa siku ni gharama zaidi...,

Kwahiyo hapa ni kumuomba waziri kivuli wetu ili tuweze ku-brainstorm cha kufanya zababu waziri mwenyewe naona ameamua kuleta majibu mepesi kwa hoja nzito
 
In my view, Plan C ni kulazimisha Plan A ifanye kazi kwa nguvu ya umma. Hatuwezi kutafuta Plan C tuwaachie Serikali wakusanye kodi halafu wanagawana kwa mtindo wa biashara ya aina ya UDA.
Mnyika peke yake hawezi, lazima sote tushiriki. He has played his role already as you said.
 
Baba Riz1, anatakiwa achukuwe maamuzi magumu kama yafuatavyo

1)Kufuta safari zote za viongozi nje ya nchi
2)Kufuta vikao na semina, warsha na kama ni lazima basi kwa kibali maalum
3)Kuachana na matumizi ya magari yanayotumia mafuta mengi (VX)
4)Kufuta EXEMPTION zote za mafuta ya migodini. n.k

Pesa zote zielekezwe tanesco kununua mitambo yao ya kuzalisha umeme, sio dharura.
Ni bora kuwa na dhiki ya muda mfupi, ili mje kupata faraja ya muda mrefu........

Jamani umeme umekatika .........kwa

Mkuu hayo yote ingebidi afanye na hajafanya kabisa ni hio ndio kazi yake na majukumu yake ameamua kutofanya..., sasa sisi kama wanajamii tunaopata hizi shida tutafanya nini..? Je tusubili mpaka siku akiamua kuchukua uamuzi mgumu?, kumbuka hii ndio miaka yake mitano ya mwisho na wala haogopi kwamba atakuja tena kwetu kuomba kura..,

Sasa mkuu swali ni kwamba ni nini sisi kama wananchi tunaweza kufanya wenyewe bila kutegemea hawa watu wanaotuangusha..? (ofcourse na hapo ni baada ya maandamano plan B kutokufanya kazi)...

Hivi ni kweli sisi kama wananchi hatuwezi kuji-mobolize kwa hali na mali ili kuondokana na hii shida..?, kumbuka kwa kufanya hivyo itakuwa ni aibu kwa serikali kushindwa kazi yake (na labda hii itasaidia ukombozi wetu huko mbeleni kwa kungoa huu uongozi unaotuangusha)
 
Kwamba wakati wenzetu wanapanga mipango ya kunusuru uchumi wa nchi zao...ambao kwetu sisi tunauita imara.. Leo Tangagiza(Tanzania) bado hatujawa na mikakati madhubuti ya uzalishaji wa umeme japo kwa 14% ya hao watumiaji wa umeme!

Pendekezo ni langu ni kwamba kwa kuwa waliweza kupunguza mgao wa umeme kwa kiwango flani kabla bajeti yao haijapita, na sasa imepita mgao umezidi kuwa mkali zaidi..tafsiri yake ni kwamba wanaendelea kutufanya watanzania mbumbumbu, kutufanya tusioweza kudai kile tulichowaagiza watawala watekeleze nk....

Hivyo basi mi naona tuandamane nchi nzima kupinga kutokuwajibika kwa serikali hii.. Mi nasema Mungu yuko upande wetu 98% hembu tuwe na uthubutu wa kupinga udhalimu huu.
 
Hivi ni kweli maandamo ndio yatakayotuletea umeme....? (labda..) je kama yasipofanikiwa tutafanya nini..?, je ni kweli tutaandamana tena na tena na tena..?

Halafu kumbuka hawa jamaa ni wazee waku-spin mambo tukiandamana kudai maendeleo yetu wenyewe wanasema ni fujo ( na wapo watu wanaoamini uongo huo kwamba maandamano ni fujo)

Hivyo basi Je kweli hatuwezi kutumia njia nyingine ya attack japo kuonyesha kwamba tunapingana nao ila positively...?

Mfano mitambo yote iliyosimama kwa sababu ya kukosa mafuta wananchi kuchanga pesa na kuendesha mitambo hata kwa siku moja tu...!!! ili kuonyesha kwamba Tanzania bila giza inawezekana na viongozi wetu ni wasanii
 
Tik tok tik tok.......Kuna kitu kilnalazimishwa kutokea hapa, tena bila ya serikali kujua kuwa inarutubisha mazingira ya kitu hicho kutokea.....Siongezi neno, na tusubiri.
Lakini Plac ni mbaya sana, nilkuwa naiongelea mahali fulani leo na watu fulani namna Plan c inavyotengenezwa na kuwafanya wananchi wajikute wapo barabarani bila hata ya kuitwa au kuhimizwa kufanya hivyo.....ni rahsi sana, ni kama uji kwa mwenye mapengo.....Mtakapoona hayo yanatokea mjue yametimia.
 
Hivi ni kweli maandamo ndio yatakayotuletea umeme....? (labda..) je kama yasipofanikiwa tutafanya nini..?, je ni kweli tutaandamana tena na tena na tena..?

Halafu kumbuka hawa jamaa ni wazee waku-spin mambo tukiandamana kudai maendeleo yetu wenyewe wanasema ni fujo ( na wapo watu wanaoamini uongo huo kwamba maandamano ni fujo)

Hivyo basi Je kweli hatuwezi kutumia njia nyingine ya attack japo kuonyesha kwamba tunapingana nao ila positively...?

Mfano mitambo yote iliyosimama kwa sababu ya kukosa mafuta wananchi kuchanga pesa na kuendesha mitambo hata kwa siku moja tu...!!! ili kuonyesha kwamba Tanzania bila giza inawezekana na viongozi wetu ni wasanii

Mkuu kama ni kuongea watu washaongea na kulalamika sana ila inavyoelekea malalamiko yetu ni kama yanatokea sikio moja la viongozi kwenda jingine
Maana hakuna plan wanayokuja nayo ya kutuondolea tatizo au matatizo tuliyo nayo zaidi zaidi ni kuwa wanacheka cheka na kutupa matumaini ya mwaka 2012
Kutupa tumaini la mwaka 2012 wakati tuna tatizo la mwaka 2011 ni kama kutuambia kuwa tuendelee na tatizo letu hadi mwakani
Sishauri skana Plan C ila inapofikia hakuna mtu anayetupa taarifa sahihi za nini kinachoendelea na nini ufumbuzi wa hili tatizo letu hapo mkuu ni lazima tuingie kwenye Plan C
Tunazidi kubweteka wakati ufisadi ndo unazidi, rasilimali zetu zinaliwa kama hazina mwenyewe, viongozi wanatumbua raha as if sisi tushakufa hatupo na wamebaki wao kwenye hii nchi ya wadanganyika, na gharama za maisha kwa mwananchi wa hali ya chini ndo imekuwa balaa
Tunapaswa tuamke mkuu kwenye huu usingizi tuliolala ambao hauelekei kuwa na mwisho
 
ʞontɹact Sniper;2377430 said:
Tik tok tik tok.......Kuna kitu kilnalazimishwa kutokea hapa, tena bila ya serikali kujua kuwa inarutubisha mazingira ya kitu hicho kutokea.....Siongezi neno, na tusubiri.
Lakini Plac ni mbaya sana, nilkuwa naiongelea mahali fulani leo na watu fulani namna Plan c inavyotengenezwa na kuwafanya wananchi wajikute wapo barabarani bila hata ya kuitwa au kuhimizwa kufanya hivyo.....ni rahsi sana, ni kama uji kwa mwenye mapengo.....Mtakapoona hayo yanatokea mjue yametimia.

Mkuu sijakuelewa do you mean CCM are instigating their own downfall...???

Mimi sidhani kama wanapenda hali hii itokee ila sababu wamezoea kula na 10% nyingi hii imeshakuwa kama tabia hadi wamesahau jinsi ya kufanya kazi vizuri sitashangaa kama hazina hakuna pesa kabisa na Tanesco haina hata chembe ya pesa..., yaani serikali hii imefilisika sababu ya tabia yao mbovu ya matumizi ya ajabu..., na mbaya zaidi hata hii hali ikikaa sawa bado tutailipia kwa bei za umeme kuongezeka maradufu..
 
Mkuu sijakuelewa do you mean CCM are instigating their own downfall...???

Mimi sidhani kama wanapenda hali hii itokee ila sababu wamezoea kula na 10% nyingi hii imeshakuwa kama tabia hadi wamesahau jinsi ya kufanya kazi vizuri sitashangaa kama hazina hakuna pesa kabisa na Tanesco haina hata chembe ya pesa..., yaani serikali hii imefilisika sababu ya tabia yao mbovu ya matumizi ya ajabu..., na mbaya zaidi hata hii hali ikikaa sawa bado tutailipia kwa bei za umeme kuongezeka maradufu..

VOR ukweli ni huo kwamba je hizi dharura zina pesa
Kuna pesa za kufinance hizi hatua za dharura wanazosema
Na je hiyo plan C inafanywa na nani na nani atakayeianzisha na ionekane kuwa haina madhara
 
VOR ukweli ni huo kwamba je hizi dharura zina pesa
Kuna pesa za kufinance hizi hatua za dharura wanazosema
Na je hiyo plan C inafanywa na nani na nani atakayeianzisha na ionekane kuwa haina madhara

Naam mkuu ndio maana nikashauri kama tatizo ni hakuna mafuta na baadhi ya mitambo imezimwa.., basi inabidi hata tufahamu gharama ya kuendeshea mitambo hio kwa siku hata moja tu..!! na sisi wanajamiii na wananchi tuchangishe na kuendesha hio mitambo kwa siku moja kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeonyesha njia ya kufanya ambapo serikali itaona aibu na hata waheshimiwa wetu itabidi waone aibu kwa kula maposho wakati wananchi tunakopa ili tu, tupate mwanga hata wa siku moja
 
Mkuu sijakuelewa do you mean CCM are instigating their own downfall...???

Mimi sidhani kama wanapenda hali hii itokee ila sababu wamezoea kula na 10% nyingi hii imeshakuwa kama tabia hadi wamesahau jinsi ya kufanya kazi vizuri sitashangaa kama hazina hakuna pesa kabisa na Tanesco haina hata chembe ya pesa..., yaani serikali hii imefilisika sababu ya tabia yao mbovu ya matumizi ya ajabu..., na mbaya zaidi hata hii hali ikikaa sawa bado tutailipia kwa bei za umeme kuongezeka maradufu..

Mkuu jibu ni NDIYO ila unknowingly kwa sababu ndani ya CCM hatuna uwezo wa kuji-evaluate, tuna tabia ya kuishi kwa mazoea tu, yaani kama ilivyokuwa jana tunaamini ndivyi itakavyokuwa leo...
Watu wanakula mpaka wanajisahau, wakiambiwa wanaruka lakini evidence is all over their fingers, wamekumbatia mali na vyeo hawaamini kama katika watanzania zaidi ya milioni 40, wanaweza wakatokea viongozi mahiri au familia mahiri zaidi ya zile zilizozoeleka, kwa wenye maono wachache walioamini kunaweza kukatokea vichwa katoka nje ya uzio wao, wakaamua kuviua mapema vichwa hivyo kwa kuvipelekea shule za kata, shule zisizo na waalimu vitabu, vitendea kazi wala mazingira yenye kuwavutia waalimu na wanafunzi.
Amini maneno yangu pamoja na udogo wake penya akiona hana pa kutokea huamua kupambana, watanzania si panya wala si wadogo, ila wanaaminishwa wajione kuwa ni wadogo, na muda umefika baada ya kupita katika tanuri hilo lijalo watu wakipewa dhamana ya kuiongoza jamii hii watakuwa wanajiuliza mara mbilmbili kama waikubali ama lah.....na ikitoke wameteleza kiuwajibikaji, haraka sana watachukua hatua stahiki ili kutuliza au kusafisha hali ya hewa, tuombe tuwe kati ya watu wakaofanikiwa kuiona Tanzania mpya.....Note my words.......
 
Kinacho tughalimu ni Katiba inayo tukandamiza kuongozwa na Rais hata kama kaiba kura kwenda Ikulu. Kiongozi wa nchi mda wote anautumia kujenga chama alichokizoofisha mwenyewe, atakumbuka saa ngapi suala la umeme na impact yake kwenye uchumi?
 
Back
Top Bottom