Mheshimiwa John Mnyika Kazi unaiweza?

tpmazembe

JF-Expert Member
Jan 5, 2012
2,469
581
Kwanza nianze kwa kukupongeza kwa juhudi zako za kutatua matatizo yetu wana ubungo,ubungo ni sio jimbo dogo na pia lina matatizo mengi nianze na machache:

  • Wanafunzi wa udsm wanaolala watatu watatu una mbinu gani za kutatua tatizo hili na litaisha lini?
  • kumekuwa na tatizo la foleni kubwa sana hasa mitaa ya ubungo hili utalitatua lini?
  • ubungo hatuna hosipital ,wengine hawana uwezo wa kusafirisha watu amana au mwananyamala ,lini tutakuwa na hospital yetu ubungo?
  • wanafunzi wanaofukuzwa je kama ubunge wao na mtetezi wao umepanga kuchukua hatua gani?
  • kiingilio ubungo kwa shilingi 200 je hilo nalo utasaidiaje maana hapo walalahoi ndio wanaoteseka?
  • stendi ya ndogo ya daladala ubungo kumekuwa na vijana wacheza kamari na wezi mchana kweupe na watu wenyewe sio wageni kila siku wako hapohapo achana na wanaouza vipande vya sabuni na kujidai ni simu kwa hili una mkakati gani?
  • kumekuwa na tatizo la ajira kama mbunge ni mbinu gani utaokoa vijana wa jimbo lako na hili tatizo la ajira
Nadhani itapendeza kama ukiwa results oriented,yaani matokeo au majibiu ya matatizo yapatikane sio maneno matupu.
mfano:tatizo la hosp ijengwe iakamilike watu tuanze kupata tiba,stendi kiingilio walau kishuke kiwe sh 50,mabweni ya wanafunzi udsm yaongezwe n.k.
Nakutakia kazi njema, tunapenda kuona maendeleo sio maneno tu,iwepo tofauti kati ya kipindi akiwa mbunge anatoka ccm na sasa anatoka chadema.
 
kwa kifupi tu wewe utakuwa unamwonea huyu mbunge,kama unataka hayo yote mweleze kwanza mkulo au jk wampe bajeti mnyika ya hayo uliyoyabainisha.the duty of mnyika is to pressurelize the governments to do.mnyika as mnyika hawezi kujenga hospital as you wish,zaidi is for you to be a real great thinker
 
kwa kifupi tu wewe utakuwa unamwonea huyu mbunge,kama unataka hayo yote mweleze kwanza mkulo au jk wampe bajeti mnyika ya hayo uliyoyabainisha.the duty of mnyika is to pressurelize the governments to do.mnyika as mnyika hawezi kujenga hospital as you wish,zaidi is for you to be a real great thinker

Thankx alot
Yeah what we want is to the mbunge pressurelizing the gov, but so far we haven't see that. What we see from our mbunge is to be nationalize than Ubungolize. The pressure which he is puting on the gov the interest of whole nation is too big and if he try just one percent of that on Ubungo then we are better off.
Wake up brov.....Ubungo are the one who make you be where you are now so do not forget them.......
 
Thankx alot
Yeah what we want is to the mbunge pressurelizing the gov, but so far we haven't see that. What we see from our mbunge is to be nationalize than Ubungolize. The pressure which he is puting on the gov the interest of whole nation is too big and if he try just one percent of that on Ubungo then we are better off.
Wake up brov.....Ubungo are the one who make you be where you are now so do not forget them.......

Wewe ulitaka anachofanya mbunge Mnyika ukione kwenye ITV?? Kama ndivyo hivyo umepotea njia na kupotoka wewe pamoja na mleta mada.
MH.Mnyika ana page yake ya Facebook ambayo huweka updates ya kazi zote anazofanya na anazoendelea kufuatilia.

Mleta mada anatakiwa kutofautisha kati ya kazi za mbunge na kazi za mtendaji wa serikali.Mh.Mnyika kama mbunge anafanya kazi ya kuikumbusha serikali iweze tatua matatizo ya wananchi kama foleni na ya wanafunzi kupitia bungeni na kwenye baraza la madiwani.

Bahati mbaya sana wananchi huwa hawaoni kikao cha baraza la madiwani kwenye TV.
 
Thankx alot
Yeah what we want is to the mbunge pressurelizing the gov, but so far we haven't see that. What we see from our mbunge is to be nationalize than Ubungolize. The pressure which he is puting on the gov the interest of whole nation is too big and if he try just one percent of that on Ubungo then we are better off.
Wake up brov.....Ubungo are the one who make you be where you are now so do not forget them.......

Wewe ulitaka anachofanya mbunge Mnyika ukione kwenye ITV?? Kama ndivyo hivyo umepotea njia na kupotoka wewe pamoja na mleta mada.
MH.Mnyika ana page yake ya Facebook ambayo huweka updates ya kazi zote anazofanya na anazoendelea kufuatilia.

Mleta mada anatakiwa kutofautisha kati ya kazi za mbunge na kazi za mtendaji wa serikali.Mh.Mnyika kama mbunge anafanya kazi ya kuikumbusha serikali iweze tatua matatizo ya wananchi kama foleni na ya wanafunzi kupitia bungeni na kwenye baraza la madiwani.

Bahati mbaya sana wananchi huwa hawaoni kikao cha baraza la madiwani kwenye TV.
 
Wewe ulitaka anachofanya mbunge Mnyika ukione kwenye ITV?? Kama ndivyo hivyo umepotea njia na kupotoka wewe pamoja na mleta mada.
MH.Mnyika ana page yake ya Facebook ambayo huweka updates ya kazi zote anazofanya na anazoendelea kufuatilia.

Mleta mada anatakiwa kutofautisha kati ya kazi za mbunge na kazi za mtendaji wa serikali.Mh.Mnyika kama mbunge anafanya kazi ya kuikumbusha serikali iweze tatua matatizo ya wananchi kama foleni na ya wanafunzi kupitia bungeni na kwenye baraza la madiwani.

Bahati mbaya sana wananchi huwa hawaoni kikao cha baraza la madiwani kwenye TV.

Embu tuwe wakweli kidog jamani, kwanza mimi siyo mfuasi wa CCM, mimi ni mwanaChadema mkaazi wa Kigogo Luhanga kwanza nilimpigia kura yangu ndugu Mnyika, na kampeni pia kwa uwezo wangu niliokuwa nao.

Pili kwanini humu jamvini inaonekana kuikosoa Chadema au mbunge wa Chadema ni dhambi?
Wengine tunakosoa si kwa ubaya ndugu yangu ila ni kwa uzuri tu ili na wengine wajiunge...na mwishowe wachukue nchi. Embu jiulize juzi juzi tulipata kusikia mafanikio ya mbunge wa jimbo la Arusha mjini ndugu Lema, mbona yeye anaweza kujenga hospitali ya milioni 300? Kwanini wengine washindwe? Kama Mnyika atashindwa hayo atakuwa na tofauti gani na mbunge wa ccm aliyepita?

nawasilisha
J J Pikadili.
 
Maswali ya Raisi unataka ajibu Mbunge.


bunge wa ccm akiulizwa kitu anatakiwa ajibu yeye wa Chadema ajibu raisi.....tutafika kweli?
Kuna muda inatubidi tuwe wakweli na tuache mapenzi na tuzungumze ukweli kama mtu kasoea tunasema hata kama ni wa Chadema.
 
Sasa si wanaubungo walishapima vipaumbele vyake alivyojinadi na kuona ataweza....kuna jambo muhimu sana unapaswa ulifahamu(pamoja na watanzania wenye mtazamo kama wako). Mbunge si ATM au Father Christmass...yeye hajengi hospitali kama yeye bali anaisukuma serikali...anahoji mipango na migawanyo (bungeni, halmashauri nk) kisha hapo ndipo utekelezaji unakuwapo. Sasa; tangu aingie angalia hansard masuala mangapi amehoji serikali juu ya 1.foleni? 2.Huduma za afya? 3.Ajira 4.Sekta ya Elimu kisha ndipo uandike hoja kama hizo.

Tusizoee uvunjwaji wa majukumu kama Mbunge kumlipia ada mtoto au kutoa hela ya kula kwa kaya kadhaa tukadhani ndivyo inavyopaswa...Mbunge kujenga kwa hela zake zahanati....hilo si jukumu lake....ikiwa ni harambee ya wananchi wote na yeye akishiriki kama sehemu ya mwananchi vema.
 
Nadhani swali lisiwe kumhoji Mnyika kama anaiweza kazi, na badala yake kumtaka ashughulikie kero ulizozitaja kwa kadri ya uwezo wake. Vinginevyo angekuwa haiwezi kazi, asingekuwa na nafasi aliyonayo sasa bungeni, na kwenye chama chake cha Chadema. Pia ni umuhimu ukaelewa kwamba kazi ya ubunge sio rahisi kama wengi wanavyofikiri.
 
ipo haja ya kazi/majukumu ya mbunge/wabunge kuainishwa na wananchi tukazifahamu kiundani..vinginevyo tutabaki kuwalaumu kila siku kwa kutojua majukumu yao ndani na nje ya bunge
 
Back
Top Bottom