ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Wakati akiwahutubia wazee wa ccm wa mkoa wa dar es salaam kuhusu mgogoro kati ya serikali na tucta ni dhairi kabisa mhe. Rias alionekana ni mtu mwenye jabza, asiyejua utawala bora na aliyolewa madaraka.
Akisema kuwa yeye ategemei ushindi katika uchaguzi mkuu toka kwa wafanyakazi na kuwaponda wafanyakazi mhe. Rais hata kama hakushauriwa vizuri, kama kingozi wa watu na aliyekuwa madarakani (katika nyazifa mbalimabli nyeti) alipaswa kufikiri sana kabla ya kukurupuka, kuitisha kikao na kuanza kuropoka mbele ya wanachama wenzake wa CCM (sio watanzania wote) kauli zisizoendana na dhamana aliyonayo kama Rais wa watanzania (bila kujali matabaka, dini, rang, kabila na mlengo wa kisiasa).
Kwa kauli yake ya kuonyesha hajali kabisa wafanyakazi na madai yao hayatekelezeki, Rais amejitia doa na asijue yafuatayo ambayo yanaweza kumwangusha:
Akisema kuwa yeye ategemei ushindi katika uchaguzi mkuu toka kwa wafanyakazi na kuwaponda wafanyakazi mhe. Rais hata kama hakushauriwa vizuri, kama kingozi wa watu na aliyekuwa madarakani (katika nyazifa mbalimabli nyeti) alipaswa kufikiri sana kabla ya kukurupuka, kuitisha kikao na kuanza kuropoka mbele ya wanachama wenzake wa CCM (sio watanzania wote) kauli zisizoendana na dhamana aliyonayo kama Rais wa watanzania (bila kujali matabaka, dini, rang, kabila na mlengo wa kisiasa).
Kwa kauli yake ya kuonyesha hajali kabisa wafanyakazi na madai yao hayatekelezeki, Rais amejitia doa na asijue yafuatayo ambayo yanaweza kumwangusha:
- kwa kukataa kura za wafanyakazi mbele ya wana CCM wenzake, ameonyesha wazi kuwa anauhakika wa kusshinda kwa mbinu zozote zile na kuwa wafanyakazi wa nchi hii hawana ulazima wowote wa kuwepo katika orodha ya wapiga kura wa CCM (ubaguzi wa hadhira).
- akae akijua kuwa wale wazee aliokuwa wakimpigia makofi siku ile kwa mbwembwe wao ni wazazi wa hao wafanyakazi na kuwa wafanyakazi wanaweza kuwashawishi ndugu na jamaa zao wote ambao wanategemea misadaa na huduma zao kutompa kura kabisa yeye na wagombea wote wa ccm ili kumwonyesha tu kuwa wafanyakazi hawafanyiwi mchezo!
- ajue kuwa kwa kauli ile ya kukataa hadharani kura za wafanyakazi alionyesha kuwa yeye ni mbinafsi na asie fikiria kuwepo kwa wanasiasa wenzake ndani ta CCM ambao wanahitaji hizo kura ili ziwape ushindi katika ngazi mablimbali za uongozi kuanzia tawi mpaka taifa. Hivyo, kamwe wasingethubutu kuwabeza wafanyakazi.
- ameonyesha unafiki kwa kuwa yeye ndie aliekuwa akihubiri kila siku kuwa cheo ni dhamana kuwataka wafanyakazi wa umma kuheshimu wateja kupitia mikataba ya huduma kwa wateja (CLIENT SERVICE CHATER) huko Serikali ambayo inawataka watumishi wa umma yeye akiwa mmoja wapo kutotumia lugha za dharau, kuwasikiliza na kuwajali wateja. Tulitegemea yeye kama kiongozi mkuu wateja wake ni watanzania wote ikiwemo wafanyakazi, hivyo alipaswa awasikilize kwanza baada ya Waziri husika (Kapuya) kushindwa na sio kukurupuka na kwenda kuanika hadharani misimamo yake binafsi ambayo kimsingi ilionyesha ni jisni gani Serikali yake isivyo na subira pia na inavyoichuka maamuzi kwa kukurupuka na kinyume na kanuni za utawala bora ambao anadai Serikali inaufuata.
- Akiwa mwenye dhamana ya nchi, hakupaswa kutamka kuwa yeye ndo "mwajiri Mkuu" na kusahau kuwa watanzania ndio waliomwajiri yeye na kuwa hali bora ya maisha yake na viongozi wengine wa chama na Serikali ilipaswa iendane kipoato halisi cha mtanzania na hivyo busara si kusimamai kwenye kadamnasi na kuelezea jambo ambalo angeweza kulitatua ndani ya vyombo vya Serikali yake.
- ameonyesha jinsi gani ambavyo Mawaziri wake kama Msomi Prof Kapuya wasivyokuwa na uwezo wa kushughulikia masuala yahusuyo Wizara zao mpaka yeye mwenyewe ainigilie kati jambo ambalo ni dharau kwa hao mawaziri wake.
- akae akijua kuwa hao wafanyakazi ndio waliomsaidia ushindi wa uchaguzi uliopita na ndio wanaomfanya ajivunie mafanikio ya serikali yake.
- ajue kuwa kuvuja kwa siri za serikali pengine kunatokana na viongozi wa serikali yake kutosikiliza matatizo ya wafanyakazi.
- ajue kuwa kuendelea kuwepo kwa ufisadi wa wazi na ule wa siri siri ni kutoka na wafanyakazi kutolipwa vizuri na atahri zake ni kujenga tabaka la watumishi wa umma wasio waadilifu.
- ajue kuwa amewapa kiburi maafisa wa usalama kuhusiana na jinsi ya kukabilina na matatizo yanayohusu migomo ya wananchi iwe wafanyakazi, wanafunzi na wengine kwa kauli yake ya kurejea kauli ya hatua ambazo serikali ilichukua dhidi ya mgomo wa kilombero na ambao kimsingi wawez kutokuwa na sura linganifu na hii inayotoke sasa.