CHAKA CHUWA
Member
- May 26, 2011
- 69
- 10
Wana JF;
Jana tarehe 8/05/12 majira ya saa sita mchana nilikuwa pale chini kwenye jengo la Wizara ya Uchukuzi ilikuwa ni siku ambayo Viongozi waliokuwepo wakiongoza Wizara hizo walikuja kukabidhiana Ofisi na waheshimiwa walioteuliwa kuongoza Wizara hiyo.Nikiwa pale chini ghafla alitelemka Mhe. Mfutakamba kwenye gari na kuelekea kwenye lango kuu la kuingia Wizarani hapo ghafla mhe.Nundu nae alikuwa ameshamaliza zoezi lake la kukabidhi na anatoka kueleka kwenye gari lake tayari kwa kuondoka. Kitu ambacho kimenisukama kuandika thread hii ni hao Viongozi tenawalikuwa mawaziri wa Wizara moja kupishana kama watu ambao hawajuani hata hawajawahi kuonana kabisa katika Dunia hii. Najua katika siasa kuna mambo mengi ya kukwazana hasa katika suala zima la maslahi lakini tayari unga umeshamwagika kuendeleza chuki baina yao sioni kama ni jambo la heri.
Naleta kwenu wana JF ili tuwashauri hao waliotoswa wasiendeleze chuki kati yao najua hata mhe.Chami na Nyalandu mambo ni yale yale tuwape moyo.
MWANA JF
Jana tarehe 8/05/12 majira ya saa sita mchana nilikuwa pale chini kwenye jengo la Wizara ya Uchukuzi ilikuwa ni siku ambayo Viongozi waliokuwepo wakiongoza Wizara hizo walikuja kukabidhiana Ofisi na waheshimiwa walioteuliwa kuongoza Wizara hiyo.Nikiwa pale chini ghafla alitelemka Mhe. Mfutakamba kwenye gari na kuelekea kwenye lango kuu la kuingia Wizarani hapo ghafla mhe.Nundu nae alikuwa ameshamaliza zoezi lake la kukabidhi na anatoka kueleka kwenye gari lake tayari kwa kuondoka. Kitu ambacho kimenisukama kuandika thread hii ni hao Viongozi tenawalikuwa mawaziri wa Wizara moja kupishana kama watu ambao hawajuani hata hawajawahi kuonana kabisa katika Dunia hii. Najua katika siasa kuna mambo mengi ya kukwazana hasa katika suala zima la maslahi lakini tayari unga umeshamwagika kuendeleza chuki baina yao sioni kama ni jambo la heri.
Naleta kwenu wana JF ili tuwashauri hao waliotoswa wasiendeleze chuki kati yao najua hata mhe.Chami na Nyalandu mambo ni yale yale tuwape moyo.
MWANA JF