Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,796
- 12,239
Ukiwa kama rais mstaafu na amiri jeshi wa majeshi ya ulinzi na usalama unatakiwa kuwa mshauri mkuu na mlezi wa viongozi wa kisiasa wa vyama vyote bila ubaguzi. Unatakiwa kuwa encyclopedia kwa mambo yote muhimu ya kitaifa.
Kuendelea kushiriki kwako katika harakati za kisiasa kunakuondolea sifa ya kuwa kiongozi mstaafu! Kuendelea kutoa matusi na kejeli kwa vyama vya upinzani kama ulivyofanya Igunga na Arumeru Mashariki kumekuondelea heshima kwa jamii! Kuendelea kuwashambulia kwa kejeli wanasiasa binafsi kunaonyesha jinsi usivyo na busara! Kuendelea kujisifu na kujigamba namna ulivyotumia vibaya ikulu kujinufaisha na kuwaita watanzania wote kuwa ni wavivu wa kufikiri ni utovu wa fadhili na heshima uliyopewa na watanzania.
Nakushauri kaa chini na ujirudi kwa kuwaomba radhi Watanzania! Watanzania wana mioyo ya imani watakusamehe!
Kuendelea kushiriki kwako katika harakati za kisiasa kunakuondolea sifa ya kuwa kiongozi mstaafu! Kuendelea kutoa matusi na kejeli kwa vyama vya upinzani kama ulivyofanya Igunga na Arumeru Mashariki kumekuondelea heshima kwa jamii! Kuendelea kuwashambulia kwa kejeli wanasiasa binafsi kunaonyesha jinsi usivyo na busara! Kuendelea kujisifu na kujigamba namna ulivyotumia vibaya ikulu kujinufaisha na kuwaita watanzania wote kuwa ni wavivu wa kufikiri ni utovu wa fadhili na heshima uliyopewa na watanzania.
Nakushauri kaa chini na ujirudi kwa kuwaomba radhi Watanzania! Watanzania wana mioyo ya imani watakusamehe!