Mhe. Magufuli kwa hili hatupo pamoja

babu M

JF-Expert Member
Mar 4, 2010
5,221
3,167
Magufuli amekuwa ni kati ya mawaziri wachache ambao utendaji wao umekuwa ni wakuridhisha.Wiki hii tumeona amefanikiwa kuliokolea taifa zaidi ya billion 5 kutoka kwenye malipo hewa. Wakati akiwa anafichua ufisadi huo alielezea pia kuhusu ulipaji wa fidia, ambapo kuna sehemu niliona amepotoka . Nina mnukuu “Kama nyumba yako imeingia nusu ndani ya eneo la barabara, itabomolewa hiyo nusu na wewe utalipwa kulingana na ulivyobomolewa, hatuwezi kulipa gharama ya nyumba nzima wakati umebomolewa nusu”

Kwanza haya ni makosa ambayo yameanywa na serikali kwa tamaa za watu wachache kukiuka taratibu zilizopo ili kujinufaisha wao wenyewe.Watu kama awa matokeo ya udhalimu wao awatakaa wayaone na labda wanaishi happy life Mbezi beach.

Waliouziwa viwanja nusu kiko kwenye eneo la barabara ni binadamu kama sisi, na sio mashine uneyoweza kuiprogramu ifanye jinsi unavyotaka,.Ni watu ambao wamekuwa wanaanya kazi kwa bidii na wakafanikiwa kutimiza ndoto zao za muda mrefu.

Sasa leo unakuja kuwaambia nitakulipa fidia nusu ya aka kabafu,sebule,jiko na chumba cha watoto .SIO HAKI KABISA. Kwa nini isiwe f idia ya nyumba nzima na pesa za usumbufu ili start from the scratch na kuishi life ambayo walikuwa wameipangilia toka mwanzo.

Mbona wasijifunze kwenye swala la Radar tulilipa £28m lakini tukalipwa fidia ya £30m na radar tunabaki nayo.
 
basi mshitaki hizo city council waliowapa land! kwani huo uwezo hamna?
 
Huu mji una ramani tangu wakati wa mkoroni, so wanaposema hifadhi ya barabara ni kwa wale tu ambao wamejenga majumba na kuyatanua mpk maeneo ambayo ni restricted kwa ajiri ya barabara. Ndo maana wamesema kuna mtaa nadhani Yombo huko, wao watalipwa in full kwa sababu barabara imewakuta na wao hawakuifuata. Nadhani hiyo ndo idea ya Magufuri.
 
binafsi, huyu mzee simkubali kabisa. Ana kiherehere tu,na mtu wa kupenda sifa machoni kwa watu huku akiwakandamiza walio chini yake...pia ni just another fisadi. Muda ukifika atakapotaka kwenda ikulu tutayaweka bayana wananchi wamjue.

inashangaza kuona makosa na gharama ya ama wizara husika,ama halmashauri ama manispaa husika wanabebeshwa wananchi walalahoi pekee; kwani hao waliotoa vibali wako wapi? kwanini na wao wasiwajibishwe? mnaogopana eeh

kwasababu mtu unakuta ana file lililopita kwa viongozi husika wote, kalipa kodi zote..eti ghafla barabara inapita chumbani kwake?! Jamani..au kwakuwa yeye ndio analala hapo, na nyie mnalala huko mnapolala
 
Mwacheni afanye kazi. wewe unajenga barabarani unategemea nini?
 
Magufuli amekuwa ni kati ya mawaziri wachache ambao utendaji wao umekuwa ni wakuridhisha.Wiki hii tumeona amefanikiwa kuliokolea taifa zaidi ya billion 5 kutoka kwenye malipo hewa. Wakati akiwa anafichua ufisadi huo alielezea pia kuhusu ulipaji wa fidia, ambapo kuna sehemu niliona amepotoka . Nina mnukuu “Kama nyumba yako imeingia nusu ndani ya eneo la barabara, itabomolewa hiyo nusu na wewe utalipwa kulingana na ulivyobomolewa, hatuwezi kulipa gharama ya nyumba nzima wakati umebomolewa nusu”

Kwanza haya ni makosa ambayo yameanywa na serikali kwa tamaa za watu wachache kukiuka taratibu zilizopo ili kujinufaisha wao wenyewe.Watu kama awa matokeo ya udhalimu wao awatakaa wayaone na labda wanaishi happy life Mbezi beach.

Waliouziwa viwanja nusu kiko kwenye eneo la barabara ni binadamu kama sisi, na sio mashine uneyoweza kuiprogramu ifanye jinsi unavyotaka,.Ni watu ambao wamekuwa wanaanya kazi kwa bidii na wakafanikiwa kutimiza ndoto zao za muda mrefu.

Sasa leo unakuja kuwaambia nitakulipa fidia nusu ya aka kabafu,sebule,jiko na chumba cha watoto .SIO HAKI KABISA. Kwa nini isiwe f idia ya nyumba nzima na pesa za usumbufu ili start from the scratch na kuishi life ambayo walikuwa wameipangilia toka mwanzo.

Mbona wasijifunze kwenye swala la Radar tulilipa £28m lakini tukalipwa fidia ya £30m na radar tunabaki nayo.

Alichosema ni magufuli ni sawa kabisa. Kama hukubaliani ni wewe na si wananchi wote.

Wengi ya watu waliojenga barabarani wamejenga maduka, bar, fremu na masuala mengine yahusuyo biashara na walifanya hivyo wakijua fika kuwa ipo siku watabomolewa. Sioni sababu ya kulalamika, tena hata kulipa hiyo nusu amefanya fea lakini hawakustahili malipo kabisa.

Nitoe mfano mmoja: pembezoni mwa barabara ya morogoro kushoto na kulia yaliwekwa mabango makubwa (enzi magufuli akiwa waziri wa ujenzi) yanayoonesha mipaka ya barabara tena yalikuwa yanaeleza kuwa hairuhusiwi kufanya shughuli yoyote katika eneo hilo la hifadhi ya barabara ikiwemo kujenga. Badala yake watu waliendelea kujenga huku mabango hayo nayo yakiendelea kuwapa onyo; walijifanya hawayaoni au walitegemea nini?
 
wacha utanuzi ufanyike sio kila mahali duka,grocery,salon,bar na vibanda vya chips...bila utawala wa sheria jiji lote litakuwa vichochoro
 
binafsi, huyu mzee simkubali kabisa. Ana kiherehere tu,na mtu wa kupenda sifa machoni kwa watu huku akiwakandamiza walio chini yake...pia ni just another fisadi. Muda ukifika atakapotaka kwenda ikulu tutayaweka bayana wananchi wamjue.

inashangaza kuona makosa na gharama ya ama wizara husika,ama halmashauri ama manispaa husika wanabebeshwa wananchi walalahoi pekee; kwani hao waliotoa vibali wako wapi? kwanini na wao wasiwajibishwe? mnaogopana eeh

kwasababu mtu unakuta ana file lililopita kwa viongozi husika wote, kalipa kodi zote..eti ghafla barabara inapita chumbani kwake?! Jamani..au kwakuwa yeye ndio analala hapo, na nyie mnalala huko mnapolala

Anti- Hebu weka simile kidogo. Hivi unajua maana ya mwanasiasa? Unasema kiherehere. Siasa ni kuonekana machoni mwa watu ukitenda mema. Ni yupi anayekufaa wewe? Nani Kawambwa, anayepwaya kila aendako?

Usahihi hautokani na sahihi ulizopata kukupa nafasi ya kujenga bali pia ni kwa kiasi gani wewe binafsi ulitafuta uhalali wa hiyo nafasi. Ni jukumu lako wewe muhusika kutumia ufahamu wako kuona kama hiyo ni nafasi halali. Nafasi haiwezi kuwa halali kwa sababu ya sahihi ya rais tu! lakini,

Kumbuka kuna watu wanatafuta nafasi hizo kwa kuwa-influence watendaji ili wapate sahihi hizo. Ikifika kwa magufuli, imekula kwako. Si ulimuona huyo jamaa aliyetaka kumushitaki Tibaijuka, yuko wapi? unalikumbuka lile ghorofa lililopigwa nyundo kule karibu na Golden tulip?
 
binafsi, huyu mzee simkubali kabisa. Ana kiherehere tu,na mtu wa kupenda sifa machoni kwa watu huku akiwakandamiza walio chini yake...pia ni just another fisadi. Muda ukifika atakapotaka kwenda ikulu tutayaweka bayana wananchi wamjue.

inashangaza kuona makosa na gharama ya ama wizara husika,ama halmashauri ama manispaa husika wanabebeshwa wananchi walalahoi pekee; kwani hao waliotoa vibali wako wapi? kwanini na wao wasiwajibishwe? mnaogopana eeh

kwasababu mtu unakuta ana file lililopita kwa viongozi husika wote, kalipa kodi zote..eti ghafla barabara inapita chumbani kwake?! Jamani..au kwakuwa yeye ndio analala hapo, na nyie mnalala huko mnapolala

un,mkubali nani? Asante kawambwa? Acha uzandiki..
 
Huyo Magufuli ana huruma sana, ilitakiwa aliyevamia eneo la barabara awajibike kulipia gharama za kuvunjiwa!
 
Kwanza hata kama wanakulipa hiyo nusu wamekuhurumia sana ulipaswa uvunje mwenyewe harafu ulipe gharama za usumbufu. Watu wanapimiwa viwanja halali halafu wenyewe wanatanua mpaka barabarani hebu tuache unafiki bwana! Hamjaona mijini watu wanavyojiongezea viwanja kwenda ndani ya hifadhi ya barabara? Kama hilo atalifanya mimi namfagilia na aendelee hivyo hivyo! Watu hatuna adabu na nchi yetu bwana!!

Lazima watu tuheshimu sheria zilizopo! Tena hata hiyo fidia ya nusu amewahurumia sana mlitakiwa kutopata kitu hapo maana mmeingilia barabara. Magufuli tunakuomba uchape kazi!!
 
..kama mtu amevunja sheria na kujenga barabarani basi jengo lake linapaswa kuvunjwa bila fidia, na mara nyingine inawezekana mvamizi huyo alipishwa faini kwa makosa yake.

..ninachoomba kuuliza huu utaratibu wa kulipa nusu au robo ya gharama za jengo lililovunjwa upo KISHERIA au Magufuli anataka kuanzisha utaratibu wake mwenyewe?

..ubabe wa Magufuli ulisababisha serikali kulipa faini ya shilingi bilioni 15 kwa mmiliki aliyevunjiwa kituo cha mafuta kule Mwanza.

..naona JK ameona mapungufu ya Magufuli kwenye kufuata sheria hivyo akamteua Dr.Mwakyembe, mzamifu ktk masuala ya sheria, kuwa naibu waziri wa ujenzi.
 
Magufuli amekuwa ni kati ya mawaziri wachache ambao utendaji wao umekuwa ni wakuridhisha.Wiki hii tumeona amefanikiwa kuliokolea taifa zaidi ya billion 5 kutoka kwenye malipo hewa. Wakati akiwa anafichua ufisadi huo alielezea pia kuhusu ulipaji wa fidia, ambapo kuna sehemu niliona amepotoka . Nina mnukuu "Kama nyumba yako imeingia nusu ndani ya eneo la barabara, itabomolewa hiyo nusu na wewe utalipwa kulingana na ulivyobomolewa, hatuwezi kulipa gharama ya nyumba nzima wakati umebomolewa nusu"

Kwanza haya ni makosa ambayo yameanywa na serikali kwa tamaa za watu wachache kukiuka taratibu zilizopo ili kujinufaisha wao wenyewe.Watu kama awa matokeo ya udhalimu wao awatakaa wayaone na labda wanaishi happy life Mbezi beach.

Waliouziwa viwanja nusu kiko kwenye eneo la barabara ni binadamu kama sisi, na sio mashine uneyoweza kuiprogramu ifanye jinsi unavyotaka,.Ni watu ambao wamekuwa wanaanya kazi kwa bidii na wakafanikiwa kutimiza ndoto zao za muda mrefu.

Sasa leo unakuja kuwaambia nitakulipa fidia nusu ya aka kabafu,sebule,jiko na chumba cha watoto .SIO HAKI KABISA. Kwa nini isiwe f idia ya nyumba nzima na pesa za usumbufu ili start from the scratch na kuishi life ambayo walikuwa wameipangilia toka mwanzo.

Mbona wasijifunze kwenye swala la Radar tulilipa £28m lakini tukalipwa fidia ya £30m na radar tunabaki nayo.


Kama kiwanja kipo barabarani kweli ni haki kilipwe?

Kama nyumba ipo kwenye eneo la barabara nionavyo mie si halali kulipwa kwa sababu watu wengi watakuwa wanajenga kwenye barabara.

Magufuli anatimiza matakwa ya sheria, kama anatenda kinyume cha sheria basi watu wana haki ya kwenda mahakamani na fidia zitalipwa!


 
Big up magufuli pia eti utakuta mtu kaweka ukuta ina maana hapo ndio mwisho wa kiwanja chake, ajabu nje ya ukuta anajenga bustani na kuweka minguzo hadi barabarani. wananchi tuwe wastaarabu kama unataka bustani kwa nini usiweke ndani ya fensi yako?

Nampongeza sana huyu magufulu
 
Magufuli amekuwa ni kati ya mawaziri wachache ambao utendaji wao umekuwa ni wakuridhisha.Wiki hii tumeona amefanikiwa kuliokolea taifa zaidi ya billion 5 kutoka kwenye malipo hewa. Wakati akiwa anafichua ufisadi huo alielezea pia kuhusu ulipaji wa fidia, ambapo kuna sehemu niliona amepotoka . Nina mnukuu Kama nyumba yako imeingia nusu ndani ya eneo la barabara, itabomolewa hiyo nusu na wewe utalipwa kulingana na ulivyobomolewa, hatuwezi kulipa gharama ya nyumba nzima wakati umebomolewa nusu

Kwanza haya ni makosa ambayo yameanywa na serikali kwa tamaa za watu wachache kukiuka taratibu zilizopo ili kujinufaisha wao wenyewe.Watu kama awa matokeo ya udhalimu wao awatakaa wayaone na labda wanaishi happy life Mbezi beach.

Waliouziwa viwanja nusu kiko kwenye eneo la barabara ni binadamu kama sisi, na sio mashine uneyoweza kuiprogramu ifanye jinsi unavyotaka,.Ni watu ambao wamekuwa wanaanya kazi kwa bidii na wakafanikiwa kutimiza ndoto zao za muda mrefu.

Sasa leo unakuja kuwaambia nitakulipa fidia nusu ya aka kabafu,sebule,jiko na chumba cha watoto .SIO HAKI KABISA. Kwa nini isiwe f idia ya nyumba nzima na pesa za usumbufu ili start from the scratch na kuishi life ambayo walikuwa wameipangilia toka mwanzo.

Mbona wasijifunze kwenye swala la Radar tulilipa £28m lakini tukalipwa fidia ya £30m na radar tunabaki nayo.

Sheria inasemaje? Magufuli yupo makini sana na suala la sheria. Jiridhishe kwanza ndipo upinge.
 
Tatizo ya hizi hela za kupata kwa deal. Watu wanajenga bila kufuata sheria ilmradi wana pesa. Sasa akiingia kiongozi anayefuata sheria ndo wanaanza kuhaha. Mimi kwa upande wangu nadhani inabidi watanzania tubadilike. Tufuate sheria maana hizi sheria hata kama hazitumiki zipo kwenye vitabu. Akitokea mtu wa kuzitumia wengi tutaumia.

Mi naimagine mtu kama yule jamaa wa Landmark Hotel pale Ubungo....kajenga barabarani kabisa..kisa..he has money....sasa akikutana na watu design ya akina Magufuri ndo wanaanza kulalamika. Hata kununua viwanja..utakuta watu wananunua viwanja well aware kabisa kwamba kuna barabara inapita/au itapita. To be honest..mimi nikiwa kiongozi nitaanza kudeal na wananchi wazembe kama hao. Harafu kibaya wanasingizia wataala wa jiji/manispaa..well..I wont buy it... Kwa nini udanganywe? Unless umejiridhisha kabisa otherwise..hivi viwanja vya deal tuviepuke..vina matatizo.

Hapana bwana watanzania tumezidi. Tufuate sheria. siyo kujenga tuu..simply because one has money!
 
Pamoja na kwamba mipango miji walistahili kupangilia viwanja vizuri tokea awali walijisahau ktk hili kutokana na sababu wanazozijua wao...lakini nijuavyo wanaotakiwa kufidiwa ni wale nyumba zao zimeingia kwenye hifadhi ya barababara kwa upimaji uliofanyika baada ya watu hao kujenga na si wale walioingilia hifadhi ya barabara wakati upimaji ulikwishafanyika!
 
bravo bravo Maguful kaz unayoifanya tunaiona utekelezaj wa sheria hauna msamaha wala kuoneana huruma si unajua huruma huzaa dhambi?
hii itakuwa fundisho kw wahuni wengne wote, wakaambiane bila kufchana wajue kwamba hiyo wizara ya ujenz ameingia mtu wa kaz.
 
Mwacheni afanye kazi. wewe unajenga barabarani unategemea nini?

Serikali ipo kusaidia watu wake, kama hawakuwazuia kujenga huo ni uzembe wa serikali na ni vema wakalipwa pesa ya jengo zima. Watu wengine hawana uwezo wa kujenga tena, sasa wakibomoliewa nyumba wataishi wapi - ama watapewa mahema kwa muda na kujengewa nyumba baadaye kama wanaokumbwa na Mafuriko.

Hiyo ya kulipwa kipande cha nyumba vema iwe ni kwa wale tu waliowahi andikiwa barua za kusitisha kujenga lakini wakakaidi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom