Mhe. Godbless Lema alichana Jeshi la Polisi

Lema sio tuu ni jembe, anaweza kuwa ni zaidi ya jembe, bali ni shoka kabisa au sime ya makali kuwili, asipodhibitiwa ndani ya chama chake, anaweza kuhamashisha maandamano ya wananchi wote, kuelekea Ikulu, kumng'oa rais halali, hivyo anaweza kutenda jinai ya uhaini kwa jina la siasa.
Sio siri, Lema ni hatari, hamungunyi maneno!.

We Pasco acha kutia aibu. Raisi halali gani ambaye hasimamii HAKI? Wewe huoni usambamba kati ya udhalimu wa CCM na ule wa Misri na Libya - ambapo hata kwa mfano serikali za Marekani na Uingereza zimekana kuwatambua Gaddafi na serikali yake, pale umma unapoamua? Hivyo serikali chini ya CCM imepoteza uhalali wa kutawala.
 
Hakuna cha u better wowote shyt is a shyt there is no better shyt.
<br />
<br />

Pumba za mchele na mahindi zote ni pumba, hakuna aliyenafuu wote ni vibaraka wa serikali ya magamba, kazi yao kutetea magamba tuu.

Mie nasubiri kinuke tuu niunge mapinduzi mtaani, yaani gharama za maisha zimepanda sanaa, life limekuwa ngumu mbaya afu mtu anatetea ujinga wa magamba
 
Hotuba nzuri ila kuna vitu vimekosekana kama kiongozi wa upinzani sijui amekifanya hicho kwa matashi yake mwenyewe au kusahau. Waliouwawa Arusha hawazidi zaidi ya waliouliwa Pemba. Arusha wameuwawa watu 5 wakati pemba inasemekana wamekufa zaidi ya watu 100 na unguja 12 kama sikosei hivyo basi anapopendekeza kuanzishwa kwa CORONER'S COURT TUNAOMBA ICHUNGUZE MAUAJI SI YA ARUSHA BALI PIA YA PEMBA NA UNGUJA KWANI WALE PIA NI WATANZANIA!!!!.

Mengineyo aliyozungumza Mh Lema ni sahihi kwani serikali pamoja na vyombo vya usalama vimelala na wananchi wamechoshwa. St. Augustine aliwahi kusema An unjust law is similar to the society of Lawlessness. Kwa maana ya kiswahili kukiwa hakuna haki katika sheria basi ni sawa tu na jamii isiyofuata sheria yeyote. Huo ni ukweli na wala si uchochezi kwasababu sheria zimewekwa ili kulinda haki na usawa nchini.

kama nakumbuka vizuri yale mauaji ya pemba na unguja yalihusu maandamano ya wafuasi wa CCF na leo CUF ni sehemu ya CCM huko huko pemba na unguja. Nina uhakika wameshayamaliza kimya kimya huko huko ikiwa ni pamoja na kumwingiza Maalim ofisini. Ili tuyazungumze maalim lazima aikane hiyo ofisi aliyopewa. jambo ambalo nina uhakika hawezi kulikubali.
 
Ukweli ni kwamba police wamejisahau mnoooooooooooooo kama police anayefahaa kuwa Kiongozi kwa kadri ya nyota begani nisijue kichwani, akiwa na nyota tatu xxx anakaa barabarani na vijana wake wanaomba RUSHWA ya elfu mbili tuwaeleweje makamanda hawaaaaaaaaaa!! Jamzani???? mnatuuumiza mapolice jamani!!! BADRIKA!!! MURA!!!!!
 
Nilitamani sana kuangalia bunge la leo ila waheshimiwa wameshachukua umeme wao, imebidi nije ofisini wamewasha generator lakini ndo hivo hakuna tv huku
 
Dah naibu spika kaamuru lema aruke paragraph moja...lema aligoma kukawa na majibishano kidogo, lema amwambia naibu spika hayupo kusoma ripoti kuitetea serikali so kasema hiyo paragraph iingie kwenye hansadi....<br /> <br /> Leo ngoja tuone mwisho wake.
<br /> <br / mwisho wa yote naibu spika kawatoa nje tundu lissu, mchungaji na G. Lema
 
Hii hotuba ya Mh Lema imegusa sana watanzania kwa vitu wanavyotendewa bila haki. Jamani vijana tusilale na kukubali kuburuzwa. Kama serikali inataka mwendo mdundo ibadilike na wananchi watapunguza hasira. Kweli serikali ikubali inafanya makosa na ifuatilia kwa karibu zaidi matendo ya hao polisi wao. Tutambue Mh Lema yupo karibu na wananchi na jinsi alivyorahisi kuongea na watu bila majivuna, watu hawatasita kumweleza shida zao. Na bado kuna mengi yapo huko uraiani wananchi wanavyofanyiwa unyama hayapo hapo kwenye hotuba.

VIVA!!!!!!!!VIVA.....BRAVO LEMA. Wapasulie ni zama za ukweli na uwazi.
 
Mimi kwa unjinga wangu nilio nao ninafikiri wanapopambana tembo wanakufa panzi na ndipo kunguru wanapata kula.Sasa hapa Acha Vyama vipambane na wenye nguvu waogope wakati mwingine wakijua watanzania japo wachache kwa sasa wana macho ya kuona kilicho haki na kisicho haki.Always RULLING PART WANAJIKINGA KWA NAMNA YEYOTE ILE HATA KAMA NI KOSA KUBWA SANA WAONEKANE WASAFI.lakini si kweli kabisa.Na
Nchi zooote Duniani siasa zake si za kirafiki kwa kukubali kila jambo.Sasa ukweli wa siasa za Tanzania unaonekana na ndipo tunajua nini tunachojifunza.Wabunge wetu hawana kazi nyingine zaidi ya siasa na na ndiyo maana wanakuwa na muda mwingi wa kupresent data za kweli ili wawe na uhakika hata kama ikitokea kesi ya kimahama wawe washindi.Tusiwadharau kwani hakuna hoja ya vita wanaitangaza.ni kuweka bayana mabaya yooote ya Serikali na ni wapi wanatenda maasi kwa Raia wake.MUNGU IBARIKI TANZANIA NA UKWELI UBAKIE UKWELI
 
Hahahaha magamba bwana, mda wa zidumu fikra sahihi za mwenyekiti umeshapitwa na wakati, nao ni uwazi na ukweli pasipo kumung'unya maneno.

Viva Lema mpaka kieleweke.
 
Hana jipya! anamwaga pumba tupu. Ni aibu kwa wapiga kura wake na kwa mji wa Arusha.

huyooooooooo, Aibu imewaja, Kawashika pabaya ee. Anataka tetea hao wapiga mabobu wenu, sasa tuone nao kama wanaakili, minadhani wakienda CCP huwa wanatolewa akili kiduchu, ivi inakuwaje umlinde na kumtetea mtu anayekuzulumu na kukunyanyasa, looo wanakatwa pesa kwaajili ya maandalizi ya mazishi yao wakati wangali hai? TOBA hii mupya.

KIGUMU CHA CHA MAPINDUZI, NI NGUMU FIKRA ZA MWENYEKITI WA CCM
 
Hana jipya! anamwaga pumba tupu. Ni aibu kwa wapiga kura wake na kwa mji wa Arusha.
<br />
<br />
Nina wasiwasi na uelewa wako mkuu! Kama umeiona hiyo hotuba ya mh Lema kwa mtizamo huo basi unaumwa na hujijui, omba ndg zako wakupeleke hospitali! Usiende mwenyewe.
 
Back
Top Bottom