POLITIBURO
Member
- Apr 21, 2012
- 41
- 6
Ndg zangu wana JF na Wananchi wa Jimbo la Nkenge nawasalimu wote. Jimbo la Nkenge liko katika wilaya ya Missenyi, mkoa wa Kagera. Wilaya ya Missenyi ni changa na wananchi wa jimbo la Nkenge ni masikini hukikabilia na kipato duni, magonjwa ya mazao, maedeleo duni ya sekta ya elimu nk. Hali ya maendeleo iliyopo siyo zao la mbunge wa sasa au aliyepita! Kwa sasa mbunge wa Jimbo la Nkenge ni Asumpta Nshama Nshunju. Mhe huyu ni mbunge tangu uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 na aliupata ubunge baada ya DR Kamala kushindwa kuwajibika na kuwaletea maendeleo wana Nkenge pamoja na kushindwa kwa miaka 10 kutekeleza ahadi alizozitoa achilia mbali kuwatukana wapiga kura wake. Asumpta alitoa ahadi kedekede lakini kubwa zaidi ni kushirikiana na wananchi na kuwaletea maendeleo. Sasa ni wazi hakuna dalili ya utekelezaji wa lolote. Pia sisi wana Nkenge tunaamini maendeleo hayawezi kuja huku fedha na rasilimali za taifa zinaliwa na wachache ambao Mhe Asumpta haoneshi dalili au kuamka kupambana na mafisadi hao achilia mbali kushilikiana na wazalendo wanaoonekana kuchukizwa na ubadhilifu wa mali ya umma na matumizi mabaya ya madaraka yao. Mhe ameshindwa kuthubutu, amekosa hari ya kupambana wakati akiwa na silaha za kupambana na adui mafisadi. Kwa hilo sioni kama ana chembe ya jitihada za kuwaletea wananchi wa Nkenge maendeleo. Mimi naona ameamua mwenyewe kuuvua utu na uzalendo na amechagua kuwaunga mkono mafisadi. Kwa hiyo Mhe Asumpta ameamua kwa hiari yake kutokushirikiana na wapiga kura wake wanaishi kwenye umasikini uliotopea. Kwa kushindwa ama kusimamia au kushiriki kuunga mkono jambo hili la msingi ambalo siyo la kiitikadi naona ni usaliti kwa wana Nkenge na nchi yetu kwa ujumla. Mimi nawaomba wana Nkenge wote mlione hili, amkeni, jadilini hali inayoendelea jimboni. Kumbuka hizi sio zama za kusema heri enzi za fulani bali ni wakati muafaka wa kutafakari pamoja cha kufanya ili kunusuru jimbo letu na maendeleo. Naomba kutoa hoja!