Mhariri wa Mwananchi, Theophil Makunga, naye kuburuzwa Mahakamani leo!

Wanabodi,

Baada ya Samson Mwigamba na Absolom Kibanda kuburuzwa mahakamani kwa uchochezi, leo ni zamu ya Mhariri Mtendaji wa Mwananchi Communications, Mzee Theophil Makunga, kuburuzwa mahakamani hapo, kuunganishwa na kesi hiyo.

Habari hizi ni kwa mujibu wa Mzee Theophil Makunga mwenyewe.
"Wahariri Wenzagu, baada ya Kibanda Mimi leo nilihojiwa na polisi kwa takriban saa kadhaa kuanzia saa 4.30 hadi saa saba na nusu kama acting MD wa Mwananchi ambao ni wachapaji (printer) wa magazeti ya Free Media Ltd. Baada ya kuandika maelezo yangu niliambiwa nirudi polisi kesho asubuhi saa tatu na kisha nitapelekwa mahakamani Kisutu kuunganishwa na akina Kibanda. Mimi nitashitakiwa kama mimi si kama Mwananchi Communications Ltd.
Makunga"


My Take.
Kwanza, Mzee Theophil Makunga, pole sana, sambamba na Kibanda na Mwigamba, tuko pamoja sana!

Wanabodi, nawaombeni concetration sasa iwe kwa chanzo cha haya yote na sio matokeo.
Kufikishwa mahakamani ni matokeo tuu, tena tusiwalaumu polisi, wao wanapokea maelekezo tuu, na watoaji maelekezo wanapo pa kuegemea.


Mzizi wa fitna yote hii ni Sheria ya Magazeti ya Mwaka 1976. Hii ni moja ya sheria 40 za ukandamizaji, zilizotajwa na Tume ya Nyalali. Kesi hizi ndio opportunity pekee ya kushinikiza hii sheria iwe scrapped of from the books of laws kabla ya katiba mpya Julai, 2014!


Nime attach hapa hiyo sheria ili tuu kuwajulisha, sheria ipo ila ilikuwa haitumiki, japo sasa matumizi yake ni kwa double standards. Ingetumika ipasavyo, magazeti kama Tanzania Daima, Mwananchi, Mwanahalisi na Raia Mwema, yangeshafungwa zamani!.

Swali dogo la kujiuliza, ni kuwa kama sheria hii siku zote ipo, na imekuwepo ila imekuwa haitumiki, why now?.

Jibu ni very simple, Serikali ya Tanzania inaogopa kilichotokea Misri, Libya na kwingineko, ambako vyombo vya dola, vimeitikia nguvu ya umma, hivyo kama ni kweli, askari wetu, wakiiukubali ushauri wa Mwigamba, na Wantanzania ambao tuna sifa ya utii wa Kikondoo, tukibadilika na kuvaa ujasiri kama wa wenzetu wa Misri, then inajua kitachofuatia!.

Ikulu Tamu Jamani msifanye masikhara!.

Angalizo:
Nawaombeni sana tunapochangia thead hii, tutangulize uzalendo kwa taifa letu Tanzania na viongozi wetu, tuchangie kwa heshima, adabu na nidhamu ya hali ya juu, ili tusiliponze jukwaa letu hili kuonekana na sisi ni 'wachochezi' tusije mponza bure
ndugu yetu, mwenzetu na kamanda wetu Max!.

Natanguliza Shukrani.

Pasco (wa jf).

Background

Kaka shukurani kwa taarifa hii....Wakati nikiungana nawe kuwatakia pole Kaka zangu Absalom Kibanda na Theophil Makunga kwa kuwa naamini kuwa mashtaka yao wameangukia katika wadhifa wao katika vyombo vyao kuliko uhusika wao wa moja kwa moja katika tuhuma za uchochezi kuna mambo yananiumiza kichwa na labda unaweza kunisaidia..

1. Hivi ukipitia ile makala ya Bwana Mwigamba unadhani kuwa alikuwa sawa na ni haki yake kabisa kuandika makala ile? Je nini mtazamo wako wa dhana ya uchochezi kuhusiana na makala ile, unadhani kuwa anaonewa ama dola linahaki na wajibu wa kumshitaki?

2. Kuhusiana na sheria hii ya Uchochezi unadhani kuwa haina umuhimu wake kwa dola na jamii kwa ujumla? Nini mtazamo wako wa kijumla na nini ushauri wako hasa ukitilia maanani muktadha wa uandishi wa makala kama hii husika na sakata hili?

3. Hivi ni kweli unadhani kuwa kesii hii dhidi ya makala hii ambayo imeandikwa na Samsom Mwigamba, ikahaririwa (kwa mujibu wa taratibu) na Absalom Kibanda na kuchapishwa (pia kwa mujibu wa taratibu) na Theophil Makunga ni kutokana tu na shinikizo la watu ama nyadhifa fulani nje ya mfumo wa kidola yaani Polisi na Mahakama ambao ni wajibu wao kushughulikia suala kama hili? Nini sababu zinazokupelekea kuamini kuwa ni shinikizo na sio mwamko - spirit ya utekelezaji wa makujukumu ndio sababu kuu ya mashitaka haya?

4. Ukitilia maanani kuwa Mwandishi wa makala hii inayoshutumiwa kwa uchochezi ni mwandishi wa habari lakini pia ni Kiongozi wa Chama cga Kisiasa (CHADEMA) chenye malengo na maslahi yake hasa wakati huo wa kuandikwa na kuchapishwa makala ambapo kwa upande wa dola kulikuwa na bado kunaweza kuwa na tafsriri ya kuwa nia ya kutumia njia zisizotambulika kikatiba kuondoa madarakani utawala unaotambulika kikatiba, hudhani kuwa ndugu yetu Mwigamba kwa kiasi alishindwa kutekeleza wajibu wake kama Mwandishi na alikosea kuandika na kusambaza makala ile?

NB: Najua kuwa kutokana na style ya ufanyaji kazi wa Kibanda yawezekana kabisa kuwa hakupata wasaa wa kuiona na kuihariri makala ile kwani kuna ushahidi wa wazi wa jitihada zake kubwa za kuzuia makala nyingi za aina hiyo kuchapishwa hapo kabla na hata wakati mwengine kumuweka katika hali ngumu na wenzake ambao wana mitazamo ya kihafidhina kama Mwigamba na Ngurumo, lakini ukweli unabaki kuwa kwa muda mrefu tumekuwa tukilalama kuwa tuna dola shaghalabaghala chini ya utawala legelege na hata kufikia kupigia debe UDIKTETA wa aina fulani tunayoamini kuwa utakuwa suluhu kwa changamoto,matatizo na madhila tunayokumbana nayo....tumekataa kusikia na wala kutambua buzara inayosema UDIKTETA HAUJUI KUCHAGUA MUHANGA....tujitahidi kukomaa na kuilinda demkorasia hii kiduchu lakini inayokuwa.....
 
umeandika msg kichochezi afu uka conclude kwa kututahadharisha tutoe comments zisizo na uchochezi.mbona kama upo kisengele nyuma flani ivi.unang'ata na kupuliza kama Ruhiza nini.
Ndugu yangu Inauma, japo sijui kwako inauma nini, ila nimezisoma shutuma zako kwa Mzee Mwanakijiji na sasa unazigeuzia kwangu.

Kusema ukweli nilipokusoma kule nikakutafsiri kama 'kichaa' tuu sio lazima mpaka uokote makopo!.

Mimi msimamo wangu unaeleweka wazi nasimama wapi na nasimamia nini. Ukweli uliposimama ndipo mimi ninaposimama nao. Sijikombi kombi wala sijipendekezi si kwa serikali dhalimu wala kwa wapinzani uchwala!. Nasimama tuu kama Pasco wa jf!.

Tatizo kubwa la mashabiki maandazi wa CCM na serikali yake wewe ukiwa ni mmoja wao, ni kujikomba komba na kujipendekeza hivyo serikali inapoboronga hamuweizi kuiambia ukweli.

Waliomzunguka JK wanamuogopa kumweleza ukweli kuwa this is a wrong move!. Hapa jf, hatumwogopi binadami yoyote, hata rais tunamheshimu kama rais na anapoboronga/serikali yake inapoboronga anaambiwa/inaambiwa!.

Kama unanidhania nami ni mmoja wa wanaojikomba komba kwa yeyote, you are very wrong tena hasira zinanipanda nafikiria kuvaa combat niingie uwanja wa mapambano kupigania haki!.

Maadam unaamini nimeanzisha thread ya uchochezi, haya kawaambie basi waliokutuma mje mtusombe na sisi wa jf mkatuunganishe kwenye ile kesi ya uchochezi!.
 
lakini ukweli unabaki kuwa kwa muda mrefu tumekuwa tukilalama kuwa tuna dola shaghalabaghala chini ya utawala legelege .....
Mkuu haya ni maneno yako? Najikuta nakuwa mzito kuamini? Vp kumetokea nini huko au utawala unaouzungumzia siyo wa JK?
 
Mapinduzi ya misri na tunisia yalifanikishwa sana kupitia internet nafikiri hakuna atakaweza kuzuia hilo na jf ina mchango wake katika hil0. Mungu ibariki tanzania
 
Kaka shukurani kwa taarifa hii....Wakati nikiungana nawe kuwatakia pole Kaka zangu Absalom Kibanda na Theophil Makunga kwa kuwa naamini kuwa mashtaka yao wameangukia katika wadhifa wao katika vyombo vyao kuliko uhusika wao wa moja kwa moja katika tuhuma za uchochezi kuna mambo yananiumiza kichwa na labda unaweza kunisaidia..

1. Hivi ukipitia ile makala ya Bwana Mwigamba unadhani kuwa alikuwa sawa na ni haki yake kabisa kuandika makala ile? Je nini mtazamo wako wa dhana ya uchochezi kuhusiana na makala ile, unadhani kuwa anaonewa ama dola linahaki na wajibu wa kumshitaki?

2. Kuhusiana na sheria hii ya Uchochezi unadhani kuwa haina umuhimu wake kwa dola na jamii kwa ujumla? Nini mtazamo wako wa kijumla na nini ushauri wako hasa ukitilia maanani muktadha wa uandishi wa makala kama hii husika na sakata hili?

3. Hivi ni kweli unadhani kuwa kesii hii dhidi ya makala hii ambayo imeandikwa na Samsom Mwigamba, ikahaririwa (kwa mujibu wa taratibu) na Absalom Kibanda na kuchapishwa (pia kwa mujibu wa taratibu) na Theophil Makunga ni kutokana tu na shinikizo la watu ama nyadhifa fulani nje ya mfumo wa kidola yaani Polisi na Mahakama ambao ni wajibu wao kushughulikia suala kama hili? Nini sababu zinazokupelekea kuamini kuwa ni shinikizo na sio mwamko - spirit ya utekelezaji wa makujukumu ndio sababu kuu ya mashitaka haya?

4. Ukitilia maanani kuwa Mwandishi wa makala hii inayoshutumiwa kwa uchochezi ni mwandishi wa habari lakini pia ni Kiongozi wa Chama cga Kisiasa (CHADEMA) chenye malengo na maslahi yake hasa wakati huo wa kuandikwa na kuchapishwa makala ambapo kwa upande wa dola kulikuwa na bado kunaweza kuwa na tafsriri ya kuwa nia ya kutumia njia zisizotambulika kikatiba kuondoa madarakani utawala unaotambulika kikatiba, hudhani kuwa ndugu yetu Mwigamba kwa kiasi alishindwa kutekeleza wajibu wake kama Mwandishi na alikosea kuandika na kusambaza makala ile?

NB: Najua kuwa kutokana na style ya ufanyaji kazi wa Kibanda yawezekana kabisa kuwa hakupata wasaa wa kuiona na kuihariri makala ile kwani kuna ushahidi wa wazi wa jitihada zake kubwa za kuzuia makala nyingi za aina hiyo kuchapishwa hapo kabla na hata wakati mwengine kumuweka katika hali ngumu na wenzake ambao wana mitazamo ya kihafidhina kama Mwigamba na Ngurumo, lakini ukweli unabaki kuwa kwa muda mrefu tumekuwa tukilalama kuwa tuna dola shaghalabaghala chini ya utawala legelege na hata kufikia kupigia debe UDIKTETA wa aina fulani tunayoamini kuwa utakuwa suluhu kwa changamoto,matatizo na madhila tunayokumbana nayo....tumekataa kusikia na wala kutambua buzara inayosema UDIKTETA HAUJUI KUCHAGUA MUHANGA....tujitahidi kukomaa na kuilinda demkorasia hii kiduchu lakini inayokuwa.....
Mkuu Omar Ilyas, kwanza nakushukuru kuaniuliza maswali hayo na hapo hapo kujijibu kwa mtazamo wako.

Naomba niwe very honest, mimi ni miongoni mwa waliopitia jeshi. Kanuni kuu kwa askari yoyote wa zamani ni utii kwa amri, baada ya utii ndipo unauliza maswali.

Kanuni kuu za jeshi la kisasa ni utii kwa amri halali sio utii kwa amri ili mradi ni amri.

Miongoni mwa masomo ya kijeshi, ni somo la mbinu za medani ambazo zinamtaka askari anapojikuta kwenye imposible angle, anapaswa kutumia his own initiative.

Majeshi yetu ni majeshi ya kizamani, makala ya Mwigamba ndio itayafanya yawe ya kisasa, ndio maana kule Arusha wamewafyatulia risasi za moto innocent victims and no one was booked!. Hakuna room ya kufanya mauaji ya kivile kwenye majeshi ya kisasa!.

Na mwisho nidhamu ya majeshi ni kufuata rank, na kitii amri za wakuu wako. Hiyo makala ya Mwigamba ingekuwa uchochezi kama Mwigamba yeye ni Field Marshal!.,
Mwigamba ni raia, sasa serikali inaogopa uchochezi gani kwa askari wake kutii amri ya raia Mwigamba, hivi ndivyo tulivyowafunza askari wetu?.

Omar kwa vile nakufahami fika na napajua unaposimamia, naamia inakijua fika serikali inachokifanya na pia unazijua sababu halisi ya kuyafanya inayoyafanya na sio hii scapegoat ya uchochezi.

Nchi hii ni yetu sote na mwaka 2015 ndio apex ya generation yetu kufanya mambo na baada ya hapo tutakuwa done!. Nawaomba wapiganaji wote na wewe ukiwemo tusiwaachie waifanya nchi hii watakavyo hata kama wengine wetu kwa sasa mko kivulini, baadae jua litatuwakia tena!.
 
Mkuu Omar Ilyas, kwanza nakushukuru kuaniuliza maswali hayo na hapo hapo kujijibu kwa mtazamo wako.

Naomba niwe very honest, mimi ni miongoni mwa waliopitia jeshi. Kanuni kuu kwa askari yoyote wa zamani ni utii kwa amri, baada ya utii ndipo unauliza maswali.

Kanuni kuu za jeshi la kisasa ni utii kwa amri halali sio utii kwa amri ili mradi ni amri.

Miongoni mwa masomo ya kijeshi, ni somo la mbinu za medani ambazo zinamtaka askari anapojikuta kwenye imposible angle, anapaswa kutumia his own initiative.

Majeshi yetu ni majeshi ya kizamani, makala ya Mwigamba ndio itayafanya yawe ya kisasa, ndio maana kule Arusha wamewafyatulia risasi za moto innocent victims and no one was booked!. Hakuna room ya kufanya mauaji ya kivile kwenye majeshi ya kisasa!.

Na mwisho nidhamu ya majeshi ni kufuata rank, na kitii amri za wakuu wako. Hiyo makala ya Mwigamba ingekuwa uchochezi kama Mwigamba yeye ni Field Marshal!.,
Mwigamba ni raia, sasa serikali inaogopa uchochezi gani kwa askari wake kutii amri ya raia Mwigamba, hivi ndivyo tulivyowafunza askari wetu?.

Omar kwa vile nakufahami fika na napajua unaposimamia, naamia inakijua fika serikali inachokifanya na pia unazijua sababu halisi ya kuyafanya inayoyafanya na sio hii scapegoat ya uchochezi.

Nchi hii ni yetu sote na mwaka 2015 ndio apex ya generation yetu kufanya mambo na baada ya hapo tutakuwa done!. Nawaomba wapiganaji wote na wewe ukiwemo tusiwaachie waifanya nchi hii watakavyo hata kama wengine wetu kwa sasa mko kivulini, baadae jua litatuwakia tena!.

Kaka kweli umewiva kisiasa..... lakini kwangu mimi nakataa kuamini kuwa kesi hii ni kwa ajili ya shinikizo hadi nitakapopata ushahidi lakini pia naamini kuwa makala ya Mwigamba ina element ya uchochezi kwa mtazamo wa wenye majukumu ya kulinda dola lakini zaidi naamini kuwa alipokuwa akiandika makala hiyo alijua wazi upende wa pili wa matokeo ya uandishi wake na hivyo kama mpambanaji alipaswa kuwa tayari na matokeo - repercussions kama hiz....ndio falsafa ya upambanaji inavyosema...

All in all naona kuwa hii ni hatua muhimu kupitia ili kwa pamoja tukomae kidemokrasia......

Tuwasiliane kaka...
 
Ndio maana Mwanakijiji akasema kuwa wahariri watusaidie kuichapa tena hiyo makala kwa sababu hakuna shaka kwamba demand yake inapanda kila siku...Ingekuwa ni muziki basi tungesema kuwa huo wimbo karibia utapiga hit katika chat za juu....

Ila nawaonea huruma...mwathirika wa ubakaji akitaka mambo yaishe bila kusambaa hukaa kimya...ila hawa jamaa wanafanya exponential increase ya wasomaji wa makala bila kujijua!!
Niliwahi kusema kuwa kwenye siasa kunahitajika ushauri wa kitaalamu katika nyanja zake zote (kuzungumza, kukemea, kutetea, kukamata na hata kufunga watu midomo) ili kuepuka advantage kwa opponent wurako kisiasa lakini hawa jamaa (magamba) huwa hawashauriki wanajiona wao nikila kitu na sasa wanaelekea ukingoni..
 
Mkuu haya ni maneno yako? Najikuta nakuwa mzito kuamini? Vp kumetokea nini huko au utawala unaouzungumzia siyo wa JK?

Yawezekana sikubaliani na mtazamo huo lakini kama unafuatilia ni style yangu ya kutojitoa katika fikira za kijumla......

Lakini zaidi kutobariki fikira hizo hakuna maana kuwa sikubaliani nazo moja kwa moja lakini ni style yangu pia kufocus katika nafasi chanya zinazojitokeza wakati wa changamoto kuliko kujigubika katika ubaya wake.....
 
Hii ni tosha kwa mapinduzi next election

"Pasipo na IMANI kuna Uovu, Pasipo na MISINGI kuna Ufedhuli, Pasipo na ITIKADI kuna Ujanjaujanja...Yote haya ni mazalia ya UFISADI" by
omarilyas
 
Kaka kweli umewiva kisiasa..... lakini kwangu mimi nakataa kuamini kuwa kesi hii ni kwa ajili ya shinikizo hadi nitakapopata ushahidi lakini pia naamini kuwa makala ya Mwigamba ina element ya uchochezi kwa mtazamo wa wenye majukumu ya kulinda dola lakini zaidi naamini kuwa alipokuwa akiandika makala hiyo alijua wazi upende wa pili wa matokeo ya uandishi wake na hivyo kama mpambanaji alipaswa kuwa tayari na matokeo - repercussions kama hiz....ndio falsafa ya upambanaji inavyosema...

All in all naona kuwa hii ni hatua muhimu kupitia ili kwa pamoja tukomae kidemokrasia......

Tuwasiliane kaka...

Thanks, pamoja sana!.
 
3. Hivi ni kweli unadhani kuwa kesii hii dhidi ya makala hii ambayo imeandikwa na Samsom Mwigamba, ikahaririwa (kwa mujibu wa taratibu) na Absalom Kibanda na kuchapishwa (pia kwa mujibu wa taratibu) na Theophil Makunga ni kutokana tu na shinikizo la watu ama nyadhifa fulani nje ya mfumo wa kidola yaani Polisi na Mahakama ambao ni wajibu wao kushughulikia suala kama hili? Nini sababu zinazokupelekea kuamini kuwa ni shinikizo na sio mwamko - spirit ya utekelezaji wa makujukumu ndio sababu kuu ya mashitaka haya?
Mkuu labda ungetusaidia kwa nini unaamini ni MWAMKO uliopelekea kufunguliwa kwa kesi hii???Je kwa upande wako hii sheria ya magazeti ya mwaka 1970 ni kandamizi au sio?Mimi kama mzalendo wa nchi yangu ninapenda kuona serikali inawajibika kwa wananchi wake kwa kuboresha miundombinu,huduma kwa umma kama elimu,afya nk pia kuwa accountable pale inapofanya makosa. Huo ni upande mmoja, upande wa pili ni kwa wananchi kufuata sheria ili kumaintain order in the society lakini kama wananchi wanaona kuna sheria ni kandamizi basi ni kuilalamikia ili iondolewe hata marekani hili linafanyika ili kutoa haki kwa wananchi.Sasa labda kwa mchango wangu na tafakari ya hayo unaona mambo yapo sawa???????
 
Pasco naona una uchungu kweli na hii issue. Pole sana. Pole pia kwa Mzee Makunga ambaye namfahamu vizuri sana.

Hivi mpaka sasa cha cha waandishi wa habari wametoa tamko lolote??? Kwa Bongo sitoshangaa kama watauchuna. Kama waandishi wa habari mtashindwa kutetea haki zenu wenyewe sidhani kama mwananchi wa kawaida itawasaidia. Wananchi wa kawaida huwa wanasaidia vyama vya siasa ambavyo sometimes vinawatumia bila wao kujua.

Kelele zitapigwa humu mtandaoni, kesho story mpya kila mtu atasahau. Wako wapi wale wanasheria na wanaharakati waliotaka kuitisha maandamano?? Wako wapi chama cha wafanyakazi (akina Mgaya) waliojifanya kuitisha mgomo?? Walimu (akina Mkoba) ambao wanadai kuitisha mgomo??

Kama kweli hiyo sheria ni ya ukandamizaji labda sasa ni wakati mwafaka wa kuipinga mahakamani!!
 
Pasco naona una uchungu kweli na hii issue. Pole sana. Pole pia kwa Mzee Makunga ambaye namfahamu vizuri sana.

Hivi mpaka sasa cha cha waandishi wa habari wametoa tamko lolote??? Kwa Bongo sitoshangaa kama watauchuna. Kama waandishi wa habari mtashindwa kutetea haki zenu wenyewe sidhani kama mwananchi wa kawaida itawasaidia. Wananchi wa kawaida huwa wanasaidia vyama vya siasa ambavyo sometimes vinawatumia bila wao kujua.

Kelele zitapigwa humu mtandaoni, kesho story mpya kila mtu atasahau. Wako wapi wale wanasheria na wanaharakati waliotaka kuitisha maandamano?? Wako wapi chama cha wafanyakazi (akina Mgaya) waliojifanya kuitisha mgomo?? Walimu (akina Mkoba) ambao wanadai kuitisha mgomo??

Kama kweli hiyo sheria ni ya ukandamizaji labda sasa ni wakati mwafaka wa kuipinga mahakamani!!
Mr. Zero, ni kweli hii issue imenigusa halafu tuna vyama mbalimbali vya waandishi wa habari zaidi ya 30!. Vyote ni kimya!. Jana kwenye TV nikawaona wahariri wameungana kumfariji Mkuu wa Jukwaa la Wahariri huku jukwaa hilo limenyamaza kimya!. Hizi njaa jamani mbaya!. Nilitegemea Jukwaa la Wahariri, MCT, MOAT, TAMWA, MISA etc kutoa tamko kali kulaani kitendo hicho lakini nothing so far. Hivi nikisema vyama vya waandishi wa habari vya Tanzania ni Vyama Utumbo Utumbo nitakuwa nimevionea?.
 
Mr. Zero, ni kweli hii issue imenigusa halafu tuna vyama mbalimbali vya waandishi wa habari zaidi ya 30!. Vyote ni kimya!. Jana kwenye TV nikawaona wahariri wameungana kumfariji Mkuu wa Jukwaa la Wahariri huku jukwaa hilo limenyamaza kimya!. Hizi njaa jamani mbaya!. Nilitegemea Jukwaa la Wahariri, MCT, MOAT, TAMWA, MISA etc kutoa tamko kali kulaani kitendo hicho lakini nothing so far. Hivi nikisema vyama vya waandishi wa habari vya Tanzania ni Vyama Utumbo Utumbo nitakuwa nimevionea?.

Mkuu pasco..
Nimepitia mabandiko yako kwa makini, ni kweli umeonyesha nia nzuri katika kuwaunga mkono Wahariri wetu...

Kingine jaribu kuwa makini kutokana na msimamo wako nanavyoujua, unaweza ukajitoa kumtetea Mhariri ambae ni wakala wa chama cha siasa mwisho wa siku ukawekwa kapu moja bila kufahamu...

Ni hayo tu mkuu wangu...
 
Kwa hali hii ipo sku hiyo sheria itaongeza na kipengele "...mwandishi, mchapishaji na MSOMAJI wa gazeti wote watashitakiwa..."
 
Pasco na omarilyas,


Nimefuatilia hoja zenu na naomba nitoe mchango wangu kuhusiana na kama polisi wanafanya kazi zao za kawaida katika hili suala au wanatelekeza amri ya wakubwa wao....

Banafsi naamini kwamba polisi wanatekeleza amri na siyo suala ambalo wao wenyewe wameliangalia kwa marefu na mapana na kuamua kulifuatilia bila pressure yoyote kutoka juu. Ushahidi wa hilo ni utendaji kazi wa kawaida wa polisi. Mara nyingi hawana muda au interest ya kufuatilia mambo yanayoigusa jamii kama rushwa za hovyo hovyo (petty corruption) na kesi za watu wa kawada.

Mtakuwa mmeona kwenye vyombo vya habari leo, kwamba kuna mwanafunzi wa CBE kapigwa risasi na driver wa kiongozi wa UVCCM lakini polisi hawajachukua hatua yoyote...Pia hata kesi kama ile ya mauaji ya jamaa wa Mahenge, walichukua hatua baada ya kubanwa.

Kwa historia yao, polisi wetu wanafanya kazi kwa pressure ya nje (ya wakubwa serikalini au wananchi kupitia media). Katika hili, nani kawaweka kwenye pressure??
 
Tunaokumbuka ya nyuma mwaka 2005, hawa wahariri walitumiwa na waliopo madarakani kuwachafua wasiasa wenzao waliokuwa kwenye mchakato wa kugombea kushika dola. Na kuna kiongozi mmoja alisema kuwa hao wanotafuta umaarufu kwenye media, hawatakubali kuona media hiyo hiyo kuonyesha mapungufu yao. Lazima watakuwa madikteta yametimia. Poleni wahariri, kwa misukosuko. Tunavuna tulichopanda.

SAFI SAANA, NIMEIPENDA HII- HANG WITH YOUR OWN ROPE.

Ni kweli Mh. Sumaye alisema hili na leo limeandikwa vizuri na Mwanahalisi
 
this is boring - I really mean it - it is BORING. Wapige tu marufuku watu kufikiria na waandishi wetu wajue kuwa huwezi kulala kitanda kimoja na wanasiasa bila kutunga mimba! Ukifika wakati wa kujifungua watu wasilalamikie maumivu!
 
Back
Top Bottom