Mhariri Mtanzania: Kwa siasa za shari, CHADEMA kinajifuta; marehemu alikuwa akiifanyia kazi CHADEMA

Kama watu watakumbuka vizuri kama kweli wana JF ni watu waliosoma vitabu huwezi msahau Yusph Halimoja, ni mwandishi mahili na wa siku nyingi na ndo mwandishi wa makala hii tunayojadili.

Kwenye makala hii sioni tatizo, mwenzetu kaleta mada ya kujadili ikiwa na observation zake, hebu kama watu huku ndani ni wasomi wenye uelewa wa mambo hebu jadili kipengele kimoja kimoja ukipinga au kuunga mkono hoja.
Ukisoma post nyingi hapa zilizokwisha za kupinga hapa zinakosa mashiko kwa sababu hatuna data za kutufanya tupinge hoja hii, mana wanasema ''kama huna data huna haki ya kuongea''
Tusipende kutumia insictinct kwenye hoja ambazo zinahitaji tuwe na majibu sahihi yaliyofanyiwa tafiti, majibu yanayokuja hapa ni dhahiri mwandishi yuko sahihi mana mifano tunaiona hapa, badala ya kujibu hoja wengine wanatukana, tena matusi mabaya, kwa nini tusiamini haya yanayozumzwa na mwandishi.

Wana jf tujifunze kujenga hoja na siyo kutumia matusi katika hoja

heri we uliyemsupporrt kihoja japo upofu wako wa kung'amua ndo'umepelekea hivyo.
Sasa tujiulize mi na wewe, kaanza na kushtumu CDM kuwa inaendeshwa kidikteta kua wasemacho dk.slaa na mh. Mbowe ndicho hicho hicho. Hivi inakuingia akilini. Inamaana viongozi na baadhi ya makada waliomo ktk ngazi za uongozi hawana ufahamu wa kutosha kama wako mpaka wamekubali hali hiyo? Na je hawa wenye kauli mbiu ya "ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI" unahisi hapa hamna udikteta, mpaka ujeuandike udikteta wa cdma? maana kauli mbiu tu yatoshakujulisha kilichopo ndani, kua afikiriacho na kunena mwenyekiti kibaki hivyo hivyo na kudumu.
2. Kadai kifo cha Marehemu Mwangosi chanzo ni CDM, hii hoja hata kisheria we mleta mada utaonekana Zuzu kama sio "kilaza". Inamaana CDM ndo'ilimpiga bomu/guruneti marehemu mpaka kupeleka kifo chake? Na je kama ni CDM, cdm ni nani? Na kwa nini husiwashauri polisi kutokana na ufahamu wako, wawafikishe mahakamani cdm wote na wamwanchie yule askari alipelekwa mahakamani?
3. Kadai marehemu alikua ni mwandishi wa cdm ndo'maana anahisi polisi walichukua fursa ya kutimiza wajibu wao. Hivi ni sheria ipi Tanzania\duniani inayoruhusu polisi kuzuia na ikiwezekana kuua mwandishi wa habari anapokua katika utendaji kazi yake, isipokua kama si mwandishi wa chadema?

Mwisho Mwenyezi Mungu katujalia vichwa kuhifadhia ubongo wenye akili na ufahamu na si vinginevyo.
 
nimegundua tatizo ni chuki uliyo nayo baina yako na Mbowe na Slaa kwa maslai binafsi
 
makala kama hizi ukisoma ni za kishabiki, ila mwandishi ajue ayo ni mawazo yake, hawezi kuwashika vijana kuchagua viongozi anaotaka. na mauaji yanayotokea ss, cdhani kama ni ya kwanza kwenye siasa za tanzania, angalia kipindi cha cuf, sasa wananchi wa sasa wanaelewa, ili vuguvugu la chadema haliepukiki, kwa mimi ambaye si mwanasiasa unajua kabisa wewe ni wa upande gani. Ila mpeni hongera mhariri kwa kufanya watoto wake wapate kula, maana posho nouma. Na nilishasema waandishi wa habari hawana umoja ila giza na nuru havikai pamoja, ipo siku mtaumbuka.
 
ningependa kujua kiwango cha elimu ya muhariri huyu kabla sijapoteza nguvu kuchangia.
 
hee!,eti yeye mwenyewe anajifanya kushangaa mbona viongozi wa CDM pamoja na mauaji yote hayo hawakamatwi,wakamatwe vp wakati wao hawajahamasisha hzo vurugu ila polisi wanazilazimisha hzo vurugu ili chadema kionekane ni chama cha vurugu,na kwa kujua hilo ndo maana wanaogopa kuwasimamisha kwa pilato kwani ushahidi utawabanaz,haiihitaji kuwa na shule saana kung'amua hili
 
Mtu anaye halalisha mauwaji ya Mwangosi kwa namna yoyote ile,huyo ndiye aliyetiwa mfukoni.Halafu jinsi asivyokuwa na akili,anatoa reference ya mwalimu ambaye hakutaka chama chake kichafuliwe,na kufananisha na Slaa na Mbowe,si afadhali chadema ina wawili wasiotaka uchafu ndani ya chama if thats the case?

Maana mwalimu Nyerere was an one man army,hakutaka uchafu wowote kwenye chama na wengine walidiriki pia kumwita dikteta!

Hata alipostaafu bado sauti yake ndani ya chama ilikuwa kubwa na ndiyo maana Lowassa na JK hawakuwa marais kwenye uhai wake.

Halafu eti huyu makala yake imetoka kwenye gazeti?Kweli Tanzania imekwisha!
Hapo kwenye gazeti ndipo kuna tatizo kubwa. Hivi hii gazeti haina ueledi? Huu upuuzi unatoka kwenye gazeti?
 
Hivi kuitumikia CDM ni kosa la jinai na adhabu yake ni kupigwa bomu?????????CDM si ni chama halali cha siasa ambacho mtu yeyote anaweza kujiunga na kukitumikia?hata JK alijiunga nacho kwa siri wakati ule upepo wa kuomba uteuze wa jina la mgombea!!!
 
Unajua mleta uzi unachanganya mambo kidogo.Katika uaongozi wowote ule usitegemee udikiteta ukose.Hata wewe kataika familia yako ni dikteta!Mbowe na Slaa nao ni madikteta!ni kwanini,ni kwa sababu hawataki kuendekeza ujinga,ujinga wa watu kama wewe wenye kutetea watenda maovu na mnaoshindwa kufuata maagizo halali ya chama.Kama udikiteta wao ungekunufaisha nina imani wangekuwa madikteta wazuri kwako!!
 
nngu007 Umesema ukweli wa mambo yalivyo, lakini sasa Tanzania ni nchi ya Siasa za majungu na kashfa ili watu wapate kula, nani atakuelewa ulichokiandika mkuu. Kitu kimoja naamini, "TUNGEJUA" ni neno ambalo watanzania watakuja kulisema endapo CHADEMA wataachiwa kuendesha siasa za shari, ni pale Nchi itakapoingia vitani kwani viongozi wengi wenye uchu wa madaraka na siyo uchu wa maendeleo hasa katika bara la Afrika huko ndiko walikofikisha nchi zao.
 
Last edited by a moderator:
Unataka nafasi ya Salva au unataka kutuaminisha nn hapa ww Mhariri? unataka kutuaminisha huu upuuzi wako je una reference gani kuthibitisha hizi Propaganda zako? umesema ulikua CDM ukiondoka na haujasema sababu zipi zilikuondoa sasa hauoni kua umeandika upuuzi?
 
Mhariri analalamika why Mboe na Slaa awataki kununuliwa na Magamba.Ndio popote pale Duniani kwenye wanamapinduzi wa kweli,watawala ufanya hila za kila namna kuwarubuni wapinzani kuwa vibaraka wao,CCM wanatamani Chadema iwe kibaraka wao kama vile. Walivyowafanyia wazanzibara na mwafaka kiini macho.Slaa na Mboe kazeni buti,Daima chadema isiwe na mamruki toka CCM kama walivyofanya kwa vyama vingine.Mtanzania ni la kada wa CCM,so atutegemei ata siku moja likemee ufisadi uliokubuu katika nchi hii
 
Unajua mleta uzi unachanganya mambo kidogo.Katika uaongozi wowote ule usitegemee udikiteta ukose.Hata wewe kataika familia yako ni dikteta!Mbowe na Slaa nao ni madikteta!ni kwanini,ni kwa sababu hawataki kuendekeza ujinga,ujinga wa watu kama wewe wenye kutetea watenda maovu na mnaoshindwa kufuata maagizo halali ya chama.Kama udikiteta wao ungekunufaisha nina imani wangekuwa madikteta wazuri kwako!!

Mkuu udikteta hata kwa viongozi wenzako ndani ya chama chako? Kukaidi amri ya Jeshi la Polisi siyo Udikteta, bali ni aina tu ya Propaganda ya kuwaamnisha wananchi kuwa wanaonewa, jambo ambalo siyo kweli. Wasiwasi wa mleta mada ni Udikteta ndani ya CDM yenyewe, endapo wakipewa ridhaa ya kuongoza nchi na kama tujuavyo dhana nzima ya uongozi na udikteta wao hakika nchi itapigana vita labda waamue kubadilika tangu sasa na mabadiliko hayo yaonekane kwa vitendo ndani ya CHAMA.
 
Unataka nafasi ya Salva au unataka kutuaminisha nn hapa ww Mhariri? unataka kutuaminisha huu upuuzi wako je una reference gani kuthibitisha hizi Propaganda zako? umesema ulikua CDM ukiondoka na haujasema sababu zipi zilikuondoa sasa hauoni kua umeandika upuuzi?
Kasema ukweli sana tu, ila najua ukweli unauma. Hakika sasa watanzania wengi wameanza kuona siasa chafu za CDM hazina nafasi tena.
 
Kabla sijachangia hapa,ningependa kujuwa kama hili gazeti lina wasomaji wa kutosha bongo,kama linao,nitachangia kuhusu mada iliyoko kwenye bandiko hili.

Kama sivyo,sitoweza kufanya hivyo,sababu ni kwamba hata mimi kuna magazeti nilikuwa siyasomi kwasababu ya mwelekeo wa kifisadi.Wenye kufahama tafadhali tujulishane.Natanguliza shukran.

Mkuu,gazeti hili ni mali ya fisadi Rostam Aziz na lina wasomaji kiduchu.
 
heri we uliyemsupporrt kihoja japo upofu wako wa kung'amua ndo'umepelekea hivyo.
Sasa tujiulize mi na wewe, kaanza na kushtumu CDM kuwa inaendeshwa kidikteta kua wasemacho dk.slaa na mh. Mbowe ndicho hicho hicho. Hivi inakuingia akilini. Inamaana viongozi na baadhi ya makada waliomo ktk ngazi za uongozi hawana ufahamu wa kutosha kama wako mpaka wamekubali hali hiyo? Na je hawa wenye kauli mbiu ya "ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI" unahisi hapa hamna udikteta, mpaka ujeuandike udikteta wa cdma? maana kauli mbiu tu yatoshakujulisha kilichopo ndani, kua afikiriacho na kunena mwenyekiti kibaki hivyo hivyo na kudumu.
2. Kadai kifo cha Marehemu Mwangosi chanzo ni CDM, hii hoja hata kisheria we mleta mada utaonekana Zuzu kama sio "kilaza". Inamaana CDM ndo'ilimpiga bomu/guruneti marehemu mpaka kupeleka kifo chake? Na je kama ni CDM, cdm ni nani? Na kwa nini husiwashauri polisi kutokana na ufahamu wako, wawafikishe mahakamani cdm wote na wamwanchie yule askari alipelekwa mahakamani?
3. Kadai marehemu alikua ni mwandishi wa cdm ndo'maana anahisi polisi walichukua fursa ya kutimiza wajibu wao. Hivi ni sheria ipi Tanzania\duniani inayoruhusu polisi kuzuia na ikiwezekana kuua mwandishi wa habari anapokua katika utendaji kazi yake, isipokua kama si mwandishi wa chadema?

Mwisho Mwenyezi Mungu katujalia vichwa kuhifadhia ubongo wenye akili na ufahamu na si vinginevyo.

Mimi nikishaona mnahusisha mada na Vifo walivyosababisha CHADEMA wenyewe najitoa kuchangia. Hapo Mwangosi ameingiaje, ulikosa cha kusema hapo? au ndo mnaendeleza propaganda zile zile za kujipatia umaarufu kupitia damu za watu?
 
huyu ni kama anajaribu kuleta mapinduzi katika uandishi wa habari..ni sawa na kubadilisha mkondo wa maji kuelekea mlimani..kwa sasa mabadiliko ni kama nature.. huwezi kuyazuia..hiyo style ya uandishi unayotumia ni ya kizamani sana..jifunze basi hata kwa wenzio ee..kama huwezi mbona kazi zipo nyingi..waachie wenye fani..
 
Umesema ukweli wa mambo yalivyo, lakini sasa Tanzania ni nchi ya Siasa za majungu na kashfa ili watu wapate kula, nani atakuelewa ulichokiandika mkuu. Kitu kimoja naamini, "TUNGEJUA" ni neno ambalo watanzania watakuja kulisema endapo CHADEMA wataachiwa kuendesha siasa za shari, ni pale Nchi itakapoingia vitani kwani viongozi wengi wenye uchu wa madaraka na siyo uchu wa maendeleo hasa katika bara la Afrika huko ndiko walikofikisha nchi zao.

Hata kitu hapo zaidi ya njaa tu,kesha pewa vijinsi hapo anajaribu kuuficha ukweli kwa njaa yake na yako lakini hamtofanikiwa kamwe.Kama angalikuwa mwandishi mwenye kujali taaluma yake, angelimshauri rais aunde tume huru ya kuchunguza vifo hivyo ili kila aliyehusika achukuliwe hatua kazi za kisheria.Zaidi ya hapo katumwa na njaa zake kuchafua ukweli nenda kamwambie shogawe hamtofanikiwa,na ipo siku ataongea ukweli ni nani alomtuma kuandika umbeya na kiasi alichompa.Ya nini joto?IUNDWE TUME HURU ZAIDI YA HAPO HAMNA KITU.
 
JUMAPILI, SEPTEMBA 16, 2012 08:05 NA YUSUF HALIMOJA, DAR ES SALAAM
HAPANA shaka wasomaji wa gazeti la Mtanzania Jumapili watakumbuka kwamba Jumapili iliyopita niliandika makala iliyosomeka "CHADEMA na ndoto ya nchi isiyotawalika.".....
Jukwaa la Wahariri litafakari hayo.



Makala haya yameandikwa na Kanjanja Mzoefu.


Hapa inaleta picha kwamba
marehemu alikuwa akiifanyia kazi Chadema. Na askari walimwona. Kwa hiyo askari mmojawao alipojaribu kumwokoa Mwangosi akisema kwamba anamjua kuwa ni mwandishi wa habari haikusaidia kitu. Polisi wengine walimwona kuwa ni mfuasi wa Chadema chama wanachopambana nacho.

kumbe ukiwa mfuasi wa chadema unakuwa kwenye mapambano ya uhasama na polisi? hapa muandishi anataka kufikisha maudhui gani kwa hadhira?


Ndiyo maana nchi yao ikaitwa "Kisiwa cha amani".

kwenye makaratasi


Tazama! Kule Iringa Slaa alimpigia simu Mkuu wa Jeshi la Polisi akisema

kumbe alipiga simu!! ndo maana ulifukuzwa Chadema, sisi hatutaki wazandiki wa kugeuzageuza maneno kama wewe.


 
Hivi kweli ndiye mhariri wa gazeti la Mtanzani kweli? Kama ni kweli hii siyo gazeti ni takataka tu.
 
Back
Top Bottom