Mhakama nchini Iraq yamhukumu adhabu ya kifo Mkamu wa Rais wa nchi hiyo.

Gumzo

JF-Expert Member
Jan 2, 2012
211
7
Mahakama nchini Iraq imepitisha hukumu ya kifo kwa makamu wa rais, Tariq al-Hashemi, baada ya kumkuta na hatia kwa kuongoza makundi ya kuuwa watu, yaliyowalenga Washia na askari wa usalama.
Makamo wa rais, wa madhehebu ya Sunni, hakuweko mahakamani wakati wa hukumu hiyo kwani alishaikimbia Iraq awali mwaka huu, akiwa sasa anaishi Uturuki.
Kesi hiyo imezusha msukosuko wa kisiasa katika serikali ya Iraq, iliyogawa madaraka kati ya Wa-Sunni, wa-Shia na WaKurd.
Bwana al-Hashemi amemshutumu Waziri Mkuu Nuri al-Maliki ambaye ni M-Shia, kuwa anawasaka wapinzani wake wa kisiasa wa madhehebu ya Sunni, lakini serikali inasisitiza kuwa kesi hiyo inafuata misingi ya sheria tu.
Hukumu hii ya mahakama imekuja huku watu wasiopungua 45 wakiwa wameuawa katika mfululizo wa mashambulizi 24 nchini Iraq. Siku ya Jumapili mashambulizi kadhaa yalishuhudiwa katika maeneo ya Tuz Khurmatu, Baquba, Basra na Samarra.
Wanajeshi 11 waliuawa kaskazini mwa Baghdad, huku katika mji wa Amara watu 14 wakiuawa na wengine 60 kujeruhiwa katika mashambulio mawili ya mabomu ya kutegwa katika gari.

CHANZO:GUMZO LA JIJI
 
Back
Top Bottom