Watanzania
JF-Expert Member
- Jul 7, 2009
- 727
- 42
Mkuu hata kama ulikimbia hesabu unashindwa kusoma hata kilichoandikwa waziwazi na Mhadhiri. Sasa Mhadhiri huyu Dr. Bakari akikuita kwa mfano kuwa wewe ni kiazi atakuwa amekosea. Mhadhiri ametoa mahesabu ya kima cha chini kwa sababu ndizo hesabu alizotumia Kikwete kutoa hesabu ya trilioni 6.9 kwa wafanyakazi wote wa Serikali. Yeye kasema hapana hesabu hiyo ni uwongo siyo Trilioni 6.9 bali ni Trilioni 1.5. Soma hapa sehemu ya maandishi yake Mhadhiri alipokuwa ananukuu hotuba ya rais. Wewe maandishi haya hukuyaona?.Sikubaliani na Kokotozi gharama la huyu mhadhiri wetu. Hivi kweli msomi kama wewe tena kwenye faculty heshimika katika masuala haya unaweza kutoa maoni kama haya na takwimu hizo? Yaani wafanyakazi wote wa nchi hii wapewe kima cha chini cha mshahara!!!!! kweli kweli kweli!!!!!!! umenisikitisha sana, umenifadhaisha sana na umenidhalilisha sana katika hili naomba kumwandikia mkuu wa chuo namrudishia degree yangu niliyoipata kutoka faculty hiyo. Unapotoa ufafanuzi kama huo jiridhishe kwanza wewe kabla ya kuutoa katika jamii maana unajidhalilisha wewe, chuo chako pamoja na wahitimu tuliotoka hapo. Pole mheshimiwa rahisi kumbe unawajua wafanyakazi wako ndiyo maana unawafanya ma - toy
''Rais Kikwete, alitoa mfano kwamba Serikali ikitoa kiwango cha shilingi 315,000 (laki tatu na kumi tano elfu) za ki-Tanzania kwa kila mtumishi (mfanyakazi) itabidi iwalipe watumishi (wafanyakazi) zaidi ya 300,000 (laki tatu) wa sekta ya umma shilingi 6.9 trilioni (Mwananchi), shilingi 6.85 trilioni (Uhuru), na shilingi 6,852.93 bilioni (HabariLeo)''.