pareto 8020
Member
- Mar 7, 2010
- 39
- 1
Wednesday, 21 April 2010 19:39
Felix Mwagara na Minael Msuya
HASARA ya Sh752.4 bilioni iliyopata serikali kutokana na misamaha ya kodi imewakera wasomi na wanasiasa ambao sasa wameitaka iifute misamaha yote ya kodi ambayo haina tija.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, walisema hali hiyo haivumiliki kuona nchi ikiendelea kupata hasara kiasi hicho wakati bado ni maskini.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana alimtaka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (Cag) na Mamlaka ya Mapato Tanzania (Tra) kuangalia vyanzo vingine vya kodi na kuifuta sheria ya misamaha ya kodi kwa kuwa haina tija wa taifa.
Dk Bana ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Sayansi ya Siasa na Uongozi cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alitoa kauli hiyo jana wakati akiwa anatoa maoni yake kuhusiana na serikali kupoteza Sh752.4 bilioni katika makusanyo yake ya kodi kutokana na kutoa misamaha mbalimbali ya kodi kwa watu binafsi, taasisi na wawekezaji wakubwa wa sekta ya madini.
Cag, Ludovick Utouh juzi mjini Dodoma aliwaeleza waandishi wa habari juu ya ripoti za ukaguzi wa serikali za mitaa, serikali kuu na ukaguzi wa mashirika ya umma.
Dk Bana alisema serikali inatakiwa itoze kodi shule za binafsi ambazo zinalipisha wanafunzi ada kubwa hali inayosababisha wamiliki wa shule hizo kupata faida zaidi ikiwa wanajipangia ada hizo kadiri wanavyopenda hali ambayo ni tofauti na shule za serikali ambazo zinajulikana.
Alisema baadhi ya shule inamlipisha mwanafunzi kwa ada ya mwaka mmoja tu zaidi ya milioni tatu wakati mwanafunzi wa PhD chuo kikuu anatoa milioni mbili inakaribia na nusu.
================================================================================
Wakati nakubaliana na hoja ya msingi juu ya serikali kupunguza misamaa ya kodi ili kuongeza pato lake, ninatofautiana na Mwalimu Bana katika hoja yake ya kuzitoza kodi shule zote (binafsi, serikali etc).
Misamaa ya kodi katika sekta ya elimu, ndio imevutia uwezekaji katika sekta hiyo ambayo kwa muda mrefu uwekezaji umekuwa ukifanywa na serikali na mashirika ya dini peke yake. Ukweli ni kwamba ilifika mahala mzigo ulikuwa mzito kwa serikali ndio maana milango ikafunguliwa watu binafsi wawekeze katika shule. Mwalimu Bana atakubaliana nami, taifa lisilowekeza katika elimu, mwisho wake si mzuri hata kidogo. Na uwekezaji katika elimu hauna mwisho ndio maana mpaka leo Marekani pamoja na maendeleo makubwa waliyopiga katika kila Nyanja, wanaongelea umuhimu wa kuwekeza zaidi katika elimu ya msingi na sekondari .leo hii wanahofu tatizo la viwango vya elimu, wana hofu upungufu wa waalimu wa sayansi na hesabu katika mashule ..sasa kama marekani inahofu sisi tusemeje.
Sisi bado tupo nyuma sana katika sekta ya elimu..actually tulishawahi kufika mbali, lakini sasa tumerudi nyuma in terms of education standards. Leo hii, tuna upungufu mkubwa wa waalimu, vifaa vya maabara na vitabu na fedha zilizopo hazitoshi. Last week tumesikia Mkuu wa Nchi akisema zinahitajika 1.3Billion USD, kwa ajili ya kuendeleza sekta ya elimu . Until that is figured out, attracting Private Capital katika sekta ya elimu bado ni muhimu sana katika kuendeleza sekta hii MAMA. Na tax incentive .ni mbinu moja wapo ya ku attract private investment katika sekta ya elimu. FAIDA yake tutaiona mbeleni zaidi ..
Hii hoja ya Mwalimu Bana ya kwamba fees za Private schools zipo juu sana ndio maana zinastahili kutozwa kodi kwa mtazamo wangu ni simplistic argument. Kufanya benchmark ya fees za private schools na public schools or universities ni makosa makubwa kama haujafanya student unit cost analysis. Ni lazima ku establish, what it takes to train a student ..hapo lazima uchukue costs zote..vitabu, vifaaa, mishahara, umeme, mafuta etc ndio ujue gharama halisi ya kumfundisha mwanafunzi
Kwa vyovyote vile zitafotautiana baina ya shule na shule kulingana na costs zao. Kama shule moja ikiamua kumujiri mwalimu aliyesoma vizuri mwenye credential kama za Mwalimu Bana Bachelor of Education (B. Ed.-First class Hons.), Master of Arts (M.A) (Political Science & Public Admin.) na Phd .kwa vyovyote gharama zake katika soko zitakuwa kubwa zaidi ya mwalimu aliyemaliza Form IV akapata crush-programme training ya miezi mitatu na kuingia darasani. Kwa msingi huo, utaona ulazima wa kuwepo tofauti ya fees katika ya shule moja na nyingine.
Isitoshe, kulinganisha fees za Private na Public schools ni kukosea sana .kwani hizi private zinajitegemea 100% kujiendesha hizi za public ..zipo subsidized. Hivi Mwalimu Bana anadhani gharama halisi ya kumfundisha Phd student ni 2.5 Million kweli? Leo hii pale Faculty kwake, serikali ikiacha kuwapa subsidy za kulipia mishahara, umeme na staff development programme .ataweza kuendesha Faculty kwa ada ya 2.5 Million kweli? Is that the real unit cost za ku train mwanafunzi?
Makosa ya aina hii ya Dk Bana hufanywa na watu wengi hasa policy makers kwa kutoa takwimu za juu juu bila kufanya in-depth analysis .ndio maana mtu anaweza kukutana na mfadhili akamuuliza ninahitaji kukusaidia ku trains wanafunzi wako 10, niambie gharama zake .mtu anakimbilia kutaja rate iliyo subsidized mwishowe anapewa pesa hizo, na zinamshinda kutrain watu hao kama alivyotakiwa kwasababu hakuzingatia gharama halisi.
Mimi nadhani cha kutilia mkazo ni STANDARDS shule zote, ziwe za public au Private lazima ziwe na viwango vya kuwawezesha kutoa elimu bora. Na ikibidi, kuna haja ya kuangalia upya utaratibu wa ku examine wanafunzi wetu mfumo wa sasa ume prove failure. Hivi hatuwezi ku harmonize standards zetu na nchi zote za East Africa, na wanafunzi wetu wakatainiwa kwa kutumia mtaala mmoja . Ninasema EAC kwasababu tunapokwenda huko mbeleni, products zetu ndio zitashindanishwa na wenzao wa Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi katika labour market na kwa mfumo ulipo sasa, sidhani kama vijana wetu wapo prepared kushindana na wenzao.
Aidha hizo Private Schools ziwe scrutinized kuhakikisha zinatoa elimu bora, na sio ubabaishaji, maana kama alivyokwishawahi kusema Mzee Mwinyi..unapofungua milango hewa iingie .hata inzi na mbu nao huingia .. Tu identify hao inzi na mbu, tuwatoe ndani ya mfumo.
Mwisho, my advice to Mwalimu Bana, akiwa msomi mahiri, tena kijana ajiwekee utaratibu wa kufanya research kabla ya kutoa matamko kwenye media....maana it seems yeye ni opinion leader katika media yetu...basi atutendee haki kwa kutoa matamko yaliyo balanced and well researched na sio kukurupuka kama wanasiasa na kutoa simplistic arguments based on insight with zero analysis. He can take a cue from Late Prof Chachage na waalimu wengine makini kama akina Prof Shivji.
Felix Mwagara na Minael Msuya
HASARA ya Sh752.4 bilioni iliyopata serikali kutokana na misamaha ya kodi imewakera wasomi na wanasiasa ambao sasa wameitaka iifute misamaha yote ya kodi ambayo haina tija.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, walisema hali hiyo haivumiliki kuona nchi ikiendelea kupata hasara kiasi hicho wakati bado ni maskini.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana alimtaka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (Cag) na Mamlaka ya Mapato Tanzania (Tra) kuangalia vyanzo vingine vya kodi na kuifuta sheria ya misamaha ya kodi kwa kuwa haina tija wa taifa.
Dk Bana ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Sayansi ya Siasa na Uongozi cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alitoa kauli hiyo jana wakati akiwa anatoa maoni yake kuhusiana na serikali kupoteza Sh752.4 bilioni katika makusanyo yake ya kodi kutokana na kutoa misamaha mbalimbali ya kodi kwa watu binafsi, taasisi na wawekezaji wakubwa wa sekta ya madini.
Cag, Ludovick Utouh juzi mjini Dodoma aliwaeleza waandishi wa habari juu ya ripoti za ukaguzi wa serikali za mitaa, serikali kuu na ukaguzi wa mashirika ya umma.
Dk Bana alisema serikali inatakiwa itoze kodi shule za binafsi ambazo zinalipisha wanafunzi ada kubwa hali inayosababisha wamiliki wa shule hizo kupata faida zaidi ikiwa wanajipangia ada hizo kadiri wanavyopenda hali ambayo ni tofauti na shule za serikali ambazo zinajulikana.
Alisema baadhi ya shule inamlipisha mwanafunzi kwa ada ya mwaka mmoja tu zaidi ya milioni tatu wakati mwanafunzi wa PhD chuo kikuu anatoa milioni mbili inakaribia na nusu.
================================================================================
Wakati nakubaliana na hoja ya msingi juu ya serikali kupunguza misamaa ya kodi ili kuongeza pato lake, ninatofautiana na Mwalimu Bana katika hoja yake ya kuzitoza kodi shule zote (binafsi, serikali etc).
Misamaa ya kodi katika sekta ya elimu, ndio imevutia uwezekaji katika sekta hiyo ambayo kwa muda mrefu uwekezaji umekuwa ukifanywa na serikali na mashirika ya dini peke yake. Ukweli ni kwamba ilifika mahala mzigo ulikuwa mzito kwa serikali ndio maana milango ikafunguliwa watu binafsi wawekeze katika shule. Mwalimu Bana atakubaliana nami, taifa lisilowekeza katika elimu, mwisho wake si mzuri hata kidogo. Na uwekezaji katika elimu hauna mwisho ndio maana mpaka leo Marekani pamoja na maendeleo makubwa waliyopiga katika kila Nyanja, wanaongelea umuhimu wa kuwekeza zaidi katika elimu ya msingi na sekondari .leo hii wanahofu tatizo la viwango vya elimu, wana hofu upungufu wa waalimu wa sayansi na hesabu katika mashule ..sasa kama marekani inahofu sisi tusemeje.
Sisi bado tupo nyuma sana katika sekta ya elimu..actually tulishawahi kufika mbali, lakini sasa tumerudi nyuma in terms of education standards. Leo hii, tuna upungufu mkubwa wa waalimu, vifaa vya maabara na vitabu na fedha zilizopo hazitoshi. Last week tumesikia Mkuu wa Nchi akisema zinahitajika 1.3Billion USD, kwa ajili ya kuendeleza sekta ya elimu . Until that is figured out, attracting Private Capital katika sekta ya elimu bado ni muhimu sana katika kuendeleza sekta hii MAMA. Na tax incentive .ni mbinu moja wapo ya ku attract private investment katika sekta ya elimu. FAIDA yake tutaiona mbeleni zaidi ..
Hii hoja ya Mwalimu Bana ya kwamba fees za Private schools zipo juu sana ndio maana zinastahili kutozwa kodi kwa mtazamo wangu ni simplistic argument. Kufanya benchmark ya fees za private schools na public schools or universities ni makosa makubwa kama haujafanya student unit cost analysis. Ni lazima ku establish, what it takes to train a student ..hapo lazima uchukue costs zote..vitabu, vifaaa, mishahara, umeme, mafuta etc ndio ujue gharama halisi ya kumfundisha mwanafunzi
Kwa vyovyote vile zitafotautiana baina ya shule na shule kulingana na costs zao. Kama shule moja ikiamua kumujiri mwalimu aliyesoma vizuri mwenye credential kama za Mwalimu Bana Bachelor of Education (B. Ed.-First class Hons.), Master of Arts (M.A) (Political Science & Public Admin.) na Phd .kwa vyovyote gharama zake katika soko zitakuwa kubwa zaidi ya mwalimu aliyemaliza Form IV akapata crush-programme training ya miezi mitatu na kuingia darasani. Kwa msingi huo, utaona ulazima wa kuwepo tofauti ya fees katika ya shule moja na nyingine.
Isitoshe, kulinganisha fees za Private na Public schools ni kukosea sana .kwani hizi private zinajitegemea 100% kujiendesha hizi za public ..zipo subsidized. Hivi Mwalimu Bana anadhani gharama halisi ya kumfundisha Phd student ni 2.5 Million kweli? Leo hii pale Faculty kwake, serikali ikiacha kuwapa subsidy za kulipia mishahara, umeme na staff development programme .ataweza kuendesha Faculty kwa ada ya 2.5 Million kweli? Is that the real unit cost za ku train mwanafunzi?
Makosa ya aina hii ya Dk Bana hufanywa na watu wengi hasa policy makers kwa kutoa takwimu za juu juu bila kufanya in-depth analysis .ndio maana mtu anaweza kukutana na mfadhili akamuuliza ninahitaji kukusaidia ku trains wanafunzi wako 10, niambie gharama zake .mtu anakimbilia kutaja rate iliyo subsidized mwishowe anapewa pesa hizo, na zinamshinda kutrain watu hao kama alivyotakiwa kwasababu hakuzingatia gharama halisi.
Mimi nadhani cha kutilia mkazo ni STANDARDS shule zote, ziwe za public au Private lazima ziwe na viwango vya kuwawezesha kutoa elimu bora. Na ikibidi, kuna haja ya kuangalia upya utaratibu wa ku examine wanafunzi wetu mfumo wa sasa ume prove failure. Hivi hatuwezi ku harmonize standards zetu na nchi zote za East Africa, na wanafunzi wetu wakatainiwa kwa kutumia mtaala mmoja . Ninasema EAC kwasababu tunapokwenda huko mbeleni, products zetu ndio zitashindanishwa na wenzao wa Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi katika labour market na kwa mfumo ulipo sasa, sidhani kama vijana wetu wapo prepared kushindana na wenzao.
Aidha hizo Private Schools ziwe scrutinized kuhakikisha zinatoa elimu bora, na sio ubabaishaji, maana kama alivyokwishawahi kusema Mzee Mwinyi..unapofungua milango hewa iingie .hata inzi na mbu nao huingia .. Tu identify hao inzi na mbu, tuwatoe ndani ya mfumo.
Mwisho, my advice to Mwalimu Bana, akiwa msomi mahiri, tena kijana ajiwekee utaratibu wa kufanya research kabla ya kutoa matamko kwenye media....maana it seems yeye ni opinion leader katika media yetu...basi atutendee haki kwa kutoa matamko yaliyo balanced and well researched na sio kukurupuka kama wanasiasa na kutoa simplistic arguments based on insight with zero analysis. He can take a cue from Late Prof Chachage na waalimu wengine makini kama akina Prof Shivji.