Mh.Waziri Masha HAJUI idadi ya magereza Tanzania

La msingi siyo Waziri kufahamu idadi KAMILI, bali tunategemea angefahamu na kutoa ANGALAU rough estimate au approximation kwa mfano, "ninakisia idadi ya magereza nchi nzima ni zaidi ya elfu moja na mia tano" mfano. Kwa kushindwa kutoa ANGALAU makisio ya juu juu ni dalili kwamba hayuko serious and he's basically incompetent.

Vipi kama hakutaka kutoa an inexact figure? Na kuna estimation ngapi inambidi azijue? Ingebidi pia ajue estimation ya ajali za magari kila mwaka Tanzania? Wafungwa wanaotoroka? Wafungwa wanaofunga Ramadhan? Walio vegetarian? I mean where do you draw the line?

Ndiyo maana wizara kwa kuona kwamba kuna data muhimu nyingi ambazo si kila kiongozi au mtendaji yeyote anaweza kuwa nazo kichwani, ikaziweka mtandaoni. Sasa Clouds waliona ugumu gani kufanya google search kabla ya interview?

Au ndiyo mambo ya kuulizana maswali for the sake of kuulizana maswali? Bila tija?
 
Wewe si ni mzee wa preciseness wewe? Mimi siridhiki na hiyo "I don't have this info off the top of my head". Hiki siyo kitu kinachobadilika badilika kama idadi ya wahamiaji haramu kutoka Mexico. Hatujengi magereza mapya kila mwaka. Waziri mhusika anatakiwa kujua idadi yake period.

Masha katika hili yuko precise, hakuevade swali, amesema sijui jibu off the top of my head.That is precise to me. Ungeweza kusema hayuko precise kama angetoa a rough estimate, lakini hakutoa.

Wizara iko precise, imekupa breakdown ya magereza by wilaya.

Preciseness gani unayoitaka hapa?
 
Tukubali kwamba huyu mtu na mwingine wa aina hii hawafai.
Sasa hivi yuko Bungeni kuwasilisha bajeti ya Wizara. Anapotaja matumizi ya kawaida ya Wizara yake bila kujua idadi ya magereza, hiyo bajeti ameipanga vipi??? Ina maana hajui hata idadi ya wafungwa ambao anawapangia bajeti ya chakula na mavazi. Hajui idadi hiyo inashikiliwa ktk magereza mangapi. Nasema kwa sauti;

NONSENSE!!

Tusimtetee kwa sababu zisizoingia akilini na kujisahaulisha kazi ya waziri. Kwani kazi yake ni kusoma figures tu bila kujua chanzo chake ni nini!
 
Masha na Hando (wa Clouds) walikuwa wanajadili mambo mbalimbali yanayohusu Wizara ya Mambo ya ndani. Walikuwa wanajadili kitengo kimoja hadi kingine. Walipofika kwenye idara ya magereza Hando ali raise issue ya msongamano wa wafungwa/mahabusu katika magereza na basically kutaka kujua wizara/ waziri anafanya nini katika kutatua hilo tatizo.

Sasa ili kusema/kukubali kuwa kuna msongamano ni lazima ujue idadi ya wafungwa/mahabusu na pia capacity ya magereza. Kwa maoni yangu kama jambo hili waziri angekuwa kweli analishughulikia sioni ni kwa nini ashindwe kusema uwezo wa magereza yaliyopo ni upi na idadi ya wafungwa/mahabusu ni ipi. Kwa bahati nzuri alikuwa anakumbuka idadi ya wafungwa na mahabusu (ingawa alikiri sio actual figure) lakini ilipokuja idadi a magereza alishindwa kusema yapo mangapi au angalau angeweza kusema basi hayo magereza yanaweza kuaccomodate wafungwa/mahabusu wangapi (hata kama info hii ipo kwenye website!). Badala yake aliishia kusema aina za magereza zilizopo (max security, ya kilimo, ya wazi nk), jibu ambalo kimsingi lisingeweza kuonesha uwezo wa magereza yaliyopo.

Mimi nilitegemea baada ya kusema hakumbuki idadi kamili ya magereza angalau angesema yaliyopo yana uwezo wa kuchukua wafungwa/mahabusu wangapi ili kuweza kuonesha upungufu uliopo na then alieleze mikakati waliyonayo (say kupunguza mahabusu kwa kiasi fulani, kujenga/panua magereza yawe na uwezo fulani nk nk). Alisema anatembelea magereza mara kwa mara, sasa kama hilo ni kweli na yupo makini angalau angeweza kuonesha huo msongamano kwa kutolea mfano gereza mojawapo kwamba lina uwezo X lakini linapewa mahabusu/wafungwa Y and hence an overload of Z.
 
Mnataka hizo data ili iweje?

I strongly suspect hata hao Clouds walikuwa hawajui maswali ya kuuliza, mwishowe wanaanza kuuliza namba za magereza kama mbunge ambaye kakaa bungeni miaka mitano bila kuuliza swali lolote, sasa anajishtukia huu ni mwaka wa uchaguzi na wananchi jimboni mwake hawajawahi kumsikia akiuliza swali hata siku moja, kwa hiyo anaamua kuuliza swali la statistics tu, ili mradi na yeye aonekane ameuliza.

Kwa sababu kama una swali la msingi la follow up linaloanzia na starter question kama hii, halafu waziri anashindwa kujibu starter question, tungesikia waziri alivyovurunda zaidi kwenye maswala ambayo yangefuatia hili.

Lakini hapa ina sound kama waziri kaulizwa idadi ya magereza, akasema "I don't have that info off the top of my head" watu waka move on kwenye ushambenga mwingine wa kujitia wanafanya interview ya kisiasa.

Clouds FM nani afanye interview ya kisiasa in the first place ?
 
Mbona wagumu kutofautisha nini tofauti ya mtu kusema "I don't have this info off the top of my head" na "we don't have this info" ?

Yaani watu walivyomshupalia utadhani kasema Wizara haijui tuna magereza mangapi, kumbe data zipo na zimewekwa mpaka mtandaoni, na link tumetoa hapa.

Hivi mnafikiri hii decision making process inafanywa on the fly, off the top of people's heads?

This is exactly what Clouds FM intended, kuwa distract watu kutoka ku discuss serious issues kibao, waende ku focus kwenye trivialities za namba ya magereza. Na wabongo wamekubali line, hook and sinker.

At the end of the day Masha kafanya interview, kaulizwa softball questions, kashafanya distractions, watu wanaongelea trivia.

Akiulizwa anatamba I am in touch with the people and the press, I just did a live interview with a popular radio station and took some burning questions.

Huku watu hawaongelei strategy wala policy, wana focus kwenye trivia za accounting.

Nimecheka sana ninapo-imagine Waziri wa wizara ya mambo ya ndani hana makadirio ya askari police, idadi ya magereza, vituo vya police kichwani mwake.... anategemea computer. Hii ni sawa na mtu kutojua (visualize) urefu wa mita kumi ukoje. Mpaka uletewe mita upime. Kiranga watu hatutaki exact figure.... tunataka angalau makadirio ya karibu + or - something. Vinginevyo inaonyesha asivyowajibika na kazi yake...
 
Masha na Hando (wa Clouds) walikuwa wanajadili mambo mbalimbali yanayohusu Wizara ya Mambo ya ndani. Walikuwa wanajadili kitengo kimoja hadi kingine. Walipofika kwenye idara ya magereza Hando ali raise issue ya msongamano wa wafungwa/mahabusu katika magereza na basically kutaka kujua wizara/ waziri anafanya nini katika kutatua hilo tatizo.

Sasa ili kusema/kukubali kuwa kuna msongamano ni lazima ujue idadi ya wafungwa/mahabusu na pia capacity ya magereza. Kwa maoni yangu kama jambo hili waziri angekuwa kweli analishughulikia sioni ni kwa nini ashindwe kusema uwezo wa magereza yaliyopo ni upi na idadi ya wafungwa/mahabusu ni ipi. Kwa bahati nzuri alikuwa anakumbuka idadi ya wafungwa na mahabusu (ingawa alikiri sio actual figure) lakini ilipokuja idadi a magereza alishindwa kusema yapo mangapi au angalau angeweza kusema basi hayo magereza yanaweza kuaccomodate wafungwa/mahabusu wangapi (hata kama info hii ipo kwenye website!). Badala yake aliishia kusema aina za magereza zilizopo (max security, ya kilimo, ya wazi nk), jibu ambalo kimsingi lisingeweza kuonesha uwezo wa magereza yaliyopo.

Mimi nilitegemea baada ya kusema hakumbuki idadi kamili ya magereza angalau angesema yaliyopo yana uwezo wa kuchukua wafungwa/mahabusu wangapi ili kuweza kuonesha upungufu uliopo na then alieleze mikakati waliyonayo (say kupunguza mahabusu kwa kiasi fulani, kujenga/panua magereza yawe na uwezo fulani nk nk). Alisema anatembelea magereza mara kwa mara, sasa kama hilo ni kweli na yupo makini angalau angeweza kuonesha huo msongamano kwa kutolea mfano gereza mojawapo kwamba lina uwezo X lakini linapewa mahabusu/wafungwa Y and hence an overload of Z.

Angalau kidogo mazee unaweza kuliweka hili swala katika a policy/ strategic context.

Sio kubwata tu oo, Waziri hajui idadi ya magereza. Unaweza kujua idadi ya magereza usijue capacity ya magereza vile vile.Kwangu mimi swala la capacity ni swala la policy na waziri hatakiwi kutojua capacity ni ipi na tuna overload kiasi gani.This is a policy issue and not a mere numbering/ accounting issue.

Sasa ukiniambia Masha hajui magereza yako overloaded kwa kiwango gani nitaona kachemka. na usiniambie inabidi ujue idadi ya magereza ili ujue magereza yako overloaded kwa kiasi gani, si kweli.

Kama narrative yako ni kweli, mleta mada original kashindwa kuleta swala muhimu lililozungumzwa (la capacity) na kaleta trivia ya idadi ya magereza.

Kama kawaida yetu, maji marefu hatuyawezi, tunataka easy easy.
 
Sasa ukiniambia Masha hajui magereza yako overloaded kwa kiwango gani nitaona kachemka. na usiniambie inabidi ujue idadi ya magereza ili ujue magereza yako overloaded kwa kiasi gani, si kweli.

Katika mjadala huo wa msongamano hakuweza kusema magereza yako overloaded kwa kiasi gani. Hilo swali la idadi ya magrezea kimsingi lilikuwa linalenga kutaka kujua msongamano(overload) ni kiasi gani na wizara imejipanga vipi.
 
Katika mjadala huo wa msongamano hakuweza kusema magereza yako overloaded kwa kiasi gani. Hilo swali la idadi ya magrezea kimsingi lilikuwa linalenga kutaka kujua msongamano(overload) ni kiasi gani na wizara imejipanga vipi.

Sasa wewe ndiye unayeleta a strategic question, kwa sababu kama Waziri hajui hata prisoner/ capacity density tuna matatizo.

And this thread should have been about this question from the get go, kwamba Masha hajui msongamano wa wafungwa magerezani ukoje.

Si Masha hajui idadi ya magereza.Big difference.
 
Nimecheka sana ninapo-imagine Waziri wa wizara ya mambo ya ndani hana makadirio ya askari police, idadi ya magereza, vituo vya police kichwani mwake.... anategemea computer. Hii ni sawa na mtu kutojua (visualize) urefu wa mita kumi ukoje. Mpaka uletewe mita upime. Kiranga watu hatutaki exact figure.... tunataka angalau makadirio ya karibu + or - something. Vinginevyo inaonyesha asivyowajibika na kazi yake...

Sarungi alikuwa anafanya kazi hata majina ya wasaidizi wake ilikuwa inabidi akumbushwe kila siku, lakini alikuwa mtendaji mzuri tu.

Si lazima kuweka kila kitu kwenye kichwa wakati unaweza kukipata kirahisi.

Now kama Masha angekuwa nuclear physicist aliyegundua nuclear formulaes ambazo hazitakiwi kuandikwa popote, halafu anazisahau sahau, hapo ningeona kuna issue.

Hii thread ilivyokuwa framed kwamba Masha hajui idadi ya magereza iko totally misleading. It actually trivialize the issue of prison overload.
 
Sarungi alikuwa anafanya kazi hata majina ya wasaidizi wake ilikuwa inabidi akumbushwe kila siku, lakini alikuwa mtendaji mzuri tu.

Si lazima kuweka kila kitu kwenye kichwa wakati unaweza kukipata kirahisi.

Now kama Masha angekuwa nuclear physicist aliyegundua nuclear formulaes ambazo hazitakiwi kuandikwa popote, halafu anazisahau sahau, hapo ningeona kuna issue.

Hii thread ilivyokuwa framed kwamba Masha hajui idadi ya magereza iko totally misleading. It actually trivialize the issue of prison overload.

Hii sasa ni ugonjwa... na sitakubali lihalalishe hii issue ya Masha...
 
Alisema anatembelea magereza mara kwa mara, sasa kama hilo ni kweli na yupo makini angalau angeweza kuonesha huo msongamano kwa kutolea mfano gereza mojawapo kwamba lina uwezo X lakini linapewa mahabusu/wafungwa Y and hence an overload of Z.

Ona sasa...umesema alisema anatembelea magereza mara kwa mara...magereza gani hayo anayoyatembelea na asijue idadi yake....
 
Hii sasa ni ugonjwa... na sitakubali lihalalishe hii issue ya Masha...

Usikute jamaa alikuwa na early stages za Alzheimer's lol....

Kwa kifupi mimi huyu Masha sijaridhishwa na utendaje wake. Kwanza utendaji mzima wa serikali siridhishwi nao.
 
Hii sasa ni ugonjwa... na sitakubali lihalalishe hii issue ya Masha...

Robert McNamara alikuwa hard of hearing lakini alikuwa one of the best aides Kennedy had.

Swali ni, je upungufu wa mtendaji/ kiongozi uta affect vipi kazi yake?

Nyie mnaopiga kelele Masha akumbuke details zote si ajabu hata anniversaries za ndoa/ uchumba/ birthdays hamkumbuki, halafu mnataka damu za wenzenu.

In any case, a more important issue than the mere number of prisons has been identified.I would rather focus on this than the trivia of number of prisons like we are on some TV prize show for useless knowledge.
 
Masha katika hili yuko precise, hakuevade swali, amesema sijui jibu off the top of my head.That is precise to me. Ungeweza kusema hayuko precise kama angetoa a rough estimate, lakini hakutoa.

Wizara iko precise, imekupa breakdown ya magereza by wilaya.

Preciseness gani unayoitaka hapa?

"just below/above xxx", "not more than xx", "less than xxxx" ni bora maradufu kuliko NO NOTHING. Bila makadirio/makisio yoyote mtu huwezi kuwa na angalau idea ya idadi halisi - who knows, magereza yanaweza kuwa 10 au hata zaidi ya 100,000.
 
Nyie mnaopiga kelele Masha akumbuke details zote si ajabu hata anniversaries za ndoa/ uchumba/ birthdays hamkumbuki, halafu mnataka damu za wenzenu.

Inaleta picha mbaya unaposahau kwa mfano siku ya kuzaliwa ya mwanao. Kusahau kwako kunaweza kumfanya aone kama humjali. Utasahauje siku mwanao alipoingia duniani? Au utasahauje siku ambayo wewe na mwenzako mlifunga pingu za maisha?

In any case, a more important issue than the mere number of prisons has been identified.I would rather focus on this than the trivia of number of prisons like we are on some TV prize show for useless knowledge.

How can you thoroughly focus on whatever that important issue is if you don't have the number of prisons that you operate? That should be the first order of things to know.
 
"just below/above xxx", "not more than xx", "less than xxxx" ni bora maradufu kuliko NO NOTHING. Bila makadirio/makisio yoyote mtu huwezi kuwa na angalau idea ya idadi halisi - who knows, magereza yanaweza kuwa 10 au hata zaidi ya 100,000.

Halafu eti alisema anatembelea magereza mara kwa mara....lol
 
Usikute jamaa alikuwa na early stages za Alzheimer's lol....

Kwa kifupi mimi huyu Masha sijaridhishwa na utendaje wake. Kwanza utendaji mzima wa serikali siridhishwi nao.

Hata mimi hawaniridhishi, lakini let's talk strategy and policy, instead of the myopic smallmindedness of number cramming.
 
Back
Top Bottom