Mh. Ana, Umshukuru Mungu kwa hizo vurugu na usizichukie ndizo 'zinakupaisha' mama. Kama bunge la sasa lisingekua na 'vurugu' hizi tunazoziona, basi mama bunge lako hili lisingekwa na mvuto kwa wanaolifuatilia. Wakati wa Samwel Sitta watu walilipenda bunge hilo kwa kuwa walau kulikua na fair treatment ya wabunge wa upinzani na wale wa chama tawala. Nina imani kwa vile unavyooendesha bunge hili na ikiwa wabunge wangekuwa wapole, wasiwe 'watovu wa nidhamu ' kwa kiti chako, basi wachache wa watazamaji wa vikao hivyo wangeendelea kutazama. Nionavyo mimi wengi wawatazamaji wanavutiwa na hivyo 'vituko' vinavyotokea kuliko mambo yanavyoendeshwa na ndiyo maana kuna uhakika wa audience, vinginevyo bunge lako hili lingekuwa na watazamaji wachache sana kuliko ilivyo sasa.