Mh Spika Makinda unatupeleka wapi?

Zipuwawa

JF-Expert Member
Nov 28, 2010
3,051
653
Mh Spika Toka Jana ameanzisha kamchezo ka ajabu mara baada ya maswali na majibu anajifanya anakazi nyingine na kumuita Mwenyekiti wa Bunge kusimamia Bunge. Ila Sasa hivi ameanzisha katabia ka kuzuia mijadala hasa ile ya Miongozo amabayo Wabunge huja nayo Mara baada ya maswali na majibu. Yafuatayo ndio yaliyofanywa toka jana.

Jana Baada ya Maswali na majibu akatoa matangazo mara baada ya kumaliza matangazo kabla ajakaa akaita Katibu hoja za kuwasilisha mezani. Wakati huo wabunge wakawa wamesimama kwa kuomba Muongozi bila kujali wabunge walikuwa na jambo gani Muhimu basi akasema nikishasema katibu basi hakuna Muongozi. hivyo akaktaaa katakata na na mara kumuita Mwanyekiti kwaajili ya kuendelea na shughuli za Bunge. Hii inaonesha wazi yeye amekuwa mtu wa kuendesha Bunge kama anavyotaka na kutoruhusu hoja yoyote kujadilia Je anatupeleka wapi?

Leo Katika Bunge amefanya kama jana mara baada ya matangazo akaita mwenyekiti huku wabunge wakiwa wamebaki wamesimama wakiomba muongozi na kusema anashughuli muhimu ofisini. Mara Mwenyekiti akakalia kiti na kusema waheshimiwa Wabunge nimewaona nitawapa nafasi baadae na kuruhusu wabunge kuendelea kuchangia hoja kwenye mjadala wa Wizara ya Uchukuzi.

Je kanuni hapa spika akiuki sheria kwa kuwaburuza wabunge? Je spika kama ana kazi za ofisi kuna haja gani kuja na kusimamia maswali tu na kuhakikisha hakuna hoja zinazoibuliwa? Je Anafikiri Watanzania hatuoni jinsi anavyoongoza Bunge? Tunajua anaongoza Bunge kibabe bila kujali maslai ya Taifa.

Nawasilisha Wanajamvi!
 
Pengine unaweza kujiuliza mara tisini hili swali usipate jibu
leo asbh nimemsikiliza mh david kafulila amenitoa machozi\
kwa kweli....kama ilivyokuwa kwa wengi kama sio watanzania kadhaa
kushangaa kumbe baadhi ya wabunge wanaoishabikia tanesco na huku nyuma
wakiihujumu kwenye muendelezo wa mgao wa umeme......ni mshangao huo huo
umenifanya leo kujiuliza je huyu spika anahusika na hivi vimgao vya mafisadi??

Samahani nauliza kwa nia njema sipepesi macho wala kuangalia pembeni na hili
ni kwaa ajili ya watanzania wote
--tuanze na skata la
-richmond...limeishia wapi??
---rada limeishia wapi???
---jairo kesi yake ya kitapeli imeishia wapi
badala ya kukaa chini na kujadili mambo yanaoyohusu umuhimu wa taifa kama migomo ya madk ,walimu ndio anakuwa wa kwanza kupinga kuongelewa bungen sasa huyu spika ni wani ni kama ayuko kwa ajili ya maslahi ya wananchi yuko kwa ajili ya nani kama si mafisadi???
Mh spika kama una muda kidogo onana na clouds wakupe speech ya david kafulila utajua kumbe huu uozo na wizi wa rushwa ndani ya bunge wwewe ndie mlezi mkubwa wa hawa mabwana na ndio maana kama mwananchi amabe nasikia tu nawiwa kuuliza jamii je hizi kesi za rushwa na uchafu wa bungeni ulioupata na unaoendelea kuupata ukaaukalia kimya je na wewe kama binadamu mwenye damu na hamu uhusiki kweli???

Mh kafulila amekiri kukaa kimya sakata hili kwa kusema yafuatayo
---kwanza alikuwa wa kwanza kukwambia kuna wabunge wanapokea rushwa kwenye kamati zao na akakupelekea ushahidi na mbaya katika moja ya wabunge aliokupelekea mmoja wa ccm amekamatwa na yuko na kesi mahakamani .....akauliza kama mh spika angechukua hatua toka kipindi kile sidhani huu uchafu ungeendelea kamati zingine lakini wazo lake la kukalia makaratasi chumbani haya ndio madhara yake saa sa wameanza kamati yqa mrema sasa kamati ya mh zitoo lakini pamoja na yote sipendi kupepepsa macho mh spika umekuwa ukibeba uchafu huu na kuuhifadhi kama kwamba baada ya kujadiliwa kuna kundi la watu wanakufwata na kukushikisha kidogo ili usiendelee na kuujadili uchafu huu wa bungeni

sasa basi kwa matokeo haya sishangai kuona hili la kina olesendeka na wenzake kutajwa na lissu sio jambo la kwanza na nawaambia watanzania kwa mh spika yule mamayetu kelele hizi zinaishia kwenye mlango wa chumba chake cha kuingia ndani akuna kitakachoendelea hata kidogo

2"double standard
mh kafulila ameshangazwa sana na kinachoendelea bungen na hiki ndicho hasa kimenifanya kumuuliza
bibie mama yetu spika haka kamgao na wewe unakaifadhi na kama ndio basi tukumbuke wanao wa jf hata kwa mchango tu wa kulipia vile vibili bili vidogo ili tuangalie tuakulindaje na wewe vijana wanapoamka kukushambulia ......

Mh kafulila amesema kuna issue ilitokea tanga akiwa kwenye kamati yake baadhi ya wabunge wakapewa million 20 wagawane ili wasipige kelele ...akasema unaweza ona mko 4 mnapewa million 20 ukiangalia kila mmoja anaondoka na 5 mill inakufikisha wapi huku wananchi wa korogwe na sehemu zingine wakiendelea kuteseka maisha yao yote ....akasema alipomplekea mh spika ushahidi akadai anaufwatilia ..mbaya alisimama kutaka kutaja majina ya wahalifu mh spika akamwomba awe mtulivu wafwate procedure....ambazo amesema leo hii tundu lissu kataja majina kaamb iwa ana kinga sasa anauliza kilichomfanya huyu mama spika makinda kumnyamazisha akae kimya asitaje na tundu lissu kuruhusiwa kutaja majina kuna kitu gani kati kati hapa???mh spika wee wewe unajua

lakini naamini kama mkristo ipo siku ama utasema ama atatokea mtu atasema kinachoendelea huko bungen kuficha uchafu wa kamati zako else basi mungu ataamua kuinuka na kusema sipendi lifike kwa mungu maana adhabu yake unaweza kuipata pasipokuiona kilichokupata

basi naomba kama mama yetu mlezi mzazi wetu spika wetu ili watu waendelee kuwa na majibu mema kwako embu vunja zile kamati zako chafu za kihuni zilizojaa wala rushwa na matapeli wasio na haya kama chura wa kihansi ili nasi tuwe na imani na wewe
 
She is incopentent, she was hard-pressed there for a reason so she is accomplishing her given tasks! Dont look at her, look on who are behind her. She is remotely controlled under the cover of kanuni. Shame on her!
 
kimeo hata sikumioja hakiwezi kusaidia.that mama ni kimeo kabisa,tena cha mchina.
 
Halafu jamani huyu mama ni ameshika dini kweli ni Mkarismatic mzuri sana hana watoto jamani si angetenda tu haki hata wakimdhuru ana hasara gani "i heit politiks"
 
Nilidhani ni mimi pekee ndio nimeona huu mchezo anaocheza Spika makinda tangu jana na leo karudia tena.

Huu mchezo ni mwendelezo wa ule mchezo wake wa awali kusema suala liko mahakamani, liko kwenye kamati,linashughurikiwa na kiti cha spika nk.

Siku za mwizi ni arobaini, siku si nyingi ataingia kwenye mtego tu na huo ndio utakuwa mwisho wake.
 
Ndiyo madhara haya ya kuchagua spika kwa kuangalia JINSIA badala ya UWEZO wa mtu.

Anne Makinda ana masilahi na kamati ya madini, Kumbuka aliye muweka hapo ni KING MAKER Rostam Aziz. Wote tunafahamu Rostam Aziz ni mdau mkubwa kwenye wizara ya Nishati na madini.

Hivyo Anne Makinda lazima afanye juu chini kumtetea boss wake aliyemuweka hapo. Mark my word hiyo kamati iliyoundwa ya kuchunguza rushwa za wabunge ni kiini macho. Itakaliwa kama vile report za kamati nyingine zilizotangulia.

Watanzania tunalo, mpaka siku tukayotia akili kichwani na kuachana na CCM!
 
Sijui Tulimtoa wapi Huyu mama

Zipuwawa,

Baada ya Yesu kusulubishwa msalabani akazikwa na kufufuka aliwatokea wanafunzi wale 11 na akaanza kuongea nao habari za kufa na kufufuka kwake bila ya wao kumjua. Yeye akajifanya hajui kinachoendelea na ndipo mwanafunzi mmoja akamwuliza hivi,''Je, wewe ni mgeni katika nchi hii, hata usijue habari hizi?"

Ninachotaka kusema hapa ni kwamba wewe siyo mgeni katika nchi yetu hii ya Wabongo.Habari za Mama Anne Makinda a.k.a Bi Mkora siyo ngeni. Kila mtu anajua kabisa Mama Makinda alipewa Uspika kwa mizengwe baada ya Mhe. Sitta kuondolewa kwenye kiti kwa mbinu chafu na haohao MAFISADI! Hii ilitokana na Sitta kuingilia mtandao wa Mafisadi kwenye issue ya Richmond hadi ikapelekea PM wa wakti huo Edward Lowassa kujiuzulu.

Jambo hili liliwaudhi sana MAFISADI na wakaweka mkakati wa kumng'oa Samweli Sitta kwa hali yoyote. Kumbuka kwamba Rostam Aziz alikuwa ndiye kinara wa Richmond baadaye Dowans na leo hii Symbion! Kwa hiyo MAFISADI walihakikisha kuwa baada ya Sitta wanaweka MTU WAO(ANNA MAKINDA) ambaye atasikiliza na kutetea MASLAHI yao NDANI NA NJE YA BUNGE na ndicho tunachokishuhudia kwa sasa kule Bungeni.

Kuanzia leo elewa kwamba Spika Anne Makinda amewekwa pale na MAFISADI ili ateteee maslahi yao. Hapa piga ua hakuna hoja yoyote ya kifisadi itakayopelekwa mezani kwake na ikapatiwa ufumbuzi wa kueleweka. Hata hili swala la Wabunge kutuhumiwa kula Rushwa toka makampuni ya mafuta yanayoimaliza TANESCO litapotezewa tu!!!Kama mtu anaweza kugundua hapa kinachofanyika ni danganya toto tu. Mfano mdogo ni pale Spika Makinda anapomtaka Mhe. Tundu Lissu ndiye awe shahidi wa kwanza kwenye tuhuma hii!!!????Kwanini awe Lissu kama siyo kutaka kupoteza lengo??Maana baadaye Kamati itakuja kudai kuwa ushahidi wa Tundu Lissu hauna ukweli wowote na ndiyo itakuwa mwisho wa kesi.

Hivi PCCB al-maarufu kama TAKUKURU wako wapi na wanafanya kazi gani???Hosea kama Mkurugenzi wao kajifungia ofisini akipulizwa na kiyoyozi full time huku akila mshahara wa bure!! PCCB walitakiwa waingie kazini kufuatilia na kuwahoji Wabunge watuhumiwa,Makampuni ya mafuta, Viongozi wa Wizara na wale wa TANESCO ili kujua ukweli wa jambo hili. Nje ya hapo naona hapa tunapotezeana muda tu hakuna ukweli utakaobainishwa hapa. Napenda kusema kuwa WATAENDEKEZA KULINDANA KAMA ILIVYO JADI YAO. Tusubiri! Ama kweli nchi hii imelaaniwa.
 
Halafu jamani huyu mama ni ameshika dini kweli ni Mkarismatic mzuri sana hana watoto jamani si angetenda tu haki hata wakimdhuru ana hasara gani "i heit politiks"

Si wote wasemao bwana bwana ndio wamchao bwana. Huyu mama ni mbwa mwitu aliyevaa ngozi ya kondoo. Anastahili kuzomewa kila anapopita mitaani
 
sasa hivi bunge halina ladha kabisa ni kama mboga bila chumvi. Kisa huyu mama spika anaroho mbaya sana hajali mambo ya msingi yanayolikabili taifa.!
 
sasa hivi bunge halina ladha kabisa ni kama mboga bila chumvi. Kisa huyu mama spika anaroho mbaya sana hajali mambo ya msingi yanayolikabili taifa.!

mh spika makinda amesema agombei tena ubunge .kwa hiyo anafanya ajali ana cha kupoteza .muhimu ni mafisadi ccm waendelee kuwapo wamlinde atakapo kuwa amestahafu
 
Kwenye katiba 84 (7)(d) inasema The speaker shall cease to be a speaker if that person is removed from the
office of Speaker by a resolution of the National Assembly supported by not less than two-thirds of all.


HIVI wabunge wanawezaje kukamilisha hili ili KUMWONDOA SPIKA katika kiti chake kisheria, mimi naona Hatutasonga mbele tusipokuwa wakali.
 
Kimsingi tukilemaa mwaka 2015 tutapata sipika, rahis,i jAji mkulu, mkurugenzi wa kula rushwa, mkuu wa majeshi ya kizamani ya ulinz,i NA mkuu wa mawaziri wa kiwango cha hatari kuliko hawa waja wa mwenyezi Mungu tulio nao leo!CHAMA LEGELEGE HUZAAA....................................LEGELEGEEEE!
 
Huyu ki UKWELI amewadhalilisha MAMA zetu, Dada zetu, Wake zetu, Shangazi zetu, na kibaya zaidi hata mabinti zetu kawadhalilisha pia
 
Back
Top Bottom