Mh Sitta, ondoka CCM watanzania tukuone shujaa wa kweli

Obvious hon.Sitta is a great hypocrite.He has emerged to criticise JK's government not just because he is a patriot but wants to show out his pains,for the two missing positions.I mean Prime Minister and Speaker.
 
Mimi nawashauri tumuunge mkono Sitta katika vita hii. Nawashangaa wale wanaompinga eti kisa yeye si chadema. Ni upumbavu uliotukuka kumpinga sitta katika vita hii.
Kuna wanoona eti serikali ya mkapa ilikuwa bora kwa kuwanyamazisha watu kama akina Sitta. Huo nao ni ujinga kwani kinakuwa ni kichaka cha wezi. Kipindi cha Jk wetu kicha kimefyekwa na sasa wezi tunawaona live.
 
Ngwendu ngwendu umeongea vizuri, tungekuwa na watu wenye mtazamo kama huu tungekuwa mbali, wewe unadhani sitta anapofunguka vile ni faida ya nani yako, yake au wote?kuna watu wanadhani vita hii ni ya sitta, no hii vita sio ya sitta ni sisi sote brother, huyu mzee amesaidia mambo mengi sana tangu akiwa speaker!sema watu hawaono na bado anapambana, tusiwe na ufinyu wa kuwaza, mungu katupa akili tupambanue mambo!!!!!!!!
 
Sitta anajijenga kwa kauli yake ili siku ya siku akituambia sasa nagombea Urais tusijiulize mara mbili kwa anatufaa au hatufai.... anasafisha njia ya kuelekea Ikulu
 
Huyu ndiye Siita aliyeongeza marupurupu, posho, kiinua mgongo na mishahara minono ya wabunge na kuwasahau watumishi wengi wa serikali ili tu kujijenga ndani ya mbunge lakini bado akaanguka....
 
Nakuunga mkono kwa makala hii ..Umechambua vyema kabisa kuhusu suala la Mh. Samwel Sitta
MH Sitta ni kiongozi aliyefanikiwa kupita kwenye nyazifa mbalimbali ndani ya serikali ikiwemo uspika pamoja na uwazir,ni kiongozi ambaye amekuwa akitoa kauli nyingi ambazo binafsi hazitoi taswira ya moja kwa moja kwamba kasimamia wapi,ni mtu ambaye amekuwa akiikosoa serikali ambayo yeye ni kiongozi,pengine anafanya hivyo kwa kuwa anajua serikali inayotuongoza kwa sasa ni dhaifu lkn siamini kama ingekua ni serikali ya mkapa angethubutu kuropoka hovyo kama anavyofanya,kama mh sitta ni kiongozi shupavu atoke ndani ya CCM ili atuaminishe watz kuwa ni mwanharakati wa kweli ambaye ana uchungu na nchi yake,aachie nyumba ya uspika ambayo ina gharimu serikali gharama kubwa,authibitishie umma pia hakuwahi kuwa mwanzalishi wa CCJ,kwa kuwa ameonyesha dhahiri kutofautiana na serikali ambayo na yeye ni sehemu ya serikali basi hana sababu ya kuendelea kuwa ndani ya CCM tofauti na hapo ni mnafiki ambaye anapaswa kupingwa kwa kila jambo aache kuwaongopea watz,ni huyuhuyu Sitta alisimama bungeni na kusema posho za wabunge ziongezwe huku akijua kuwa wabunge wamekuwa ndo wanaonufaika kwa sasa na kusahau kuwa wafanyakazi ambao ndo nguvu kazi ya nchi yetu wanalipwa ujira mdogo,pengine alifanya hivi ikiwa ni namna ya kujipigia kampeni ya kurudi kwenye nafasi ya uspika ingawa pia CCM ilimtosa,kwa mtizamo awe jasiri ahamie upinzani au CCJ ili watz tuamini haya anayoyasema na pia ili awe huru zaidi kuzungumza.....

Naomba kutoa hoja
 
Sikiliza maneno ya sitta eti kati ya siku ambazo hatapata kuzisahau ni kujiuzulu kwa Lowassa eti hakutegemea ni unafiki wa hali ya juu wakati ripoti ya Mwakyembe ilisema apime uzito na kuchukua hatua kisha akapima na kujizulu ......mzee huyu vipi?
 
Sitta anatafuta kuungwa mkono, amejaribu kuunda CCJ kashindwa karudi tena CCM akatolewa usipika.... hivi ni kwa nini hawamfukuzi uwaziri
 
kwake Sitta katika suala la maslahi ana kauli mbiu yake kama ya kilimo kwanza yeye anasema mbunge kwanza wengine mtafuata baadaye
 
wabunge wako chini ya sitta, wafanyakazi wa serikali wapo chini ya hawa ghasia, hivi nyie mbona uwezo wenu wa kuchambua mambo ni mdogo!?sitta afanye nini au hamuelewi serikali inaendeshwa vp???na humu mmefata nini/?huku ni great thinkers jamani ehee!!!!!!!!!!!
 
sasa wewe mbu sugu kwahiyo riport ya mwakyembe kusema apime ndo basi sitta kajua kuwa anajiuzulu??we kapime malaria!mnapostpost mambo ya jabu humu!!!!!!!!
 
Ameisha pima maji akagundua hakuna wa kumfukuza kwenye utawala huu dhaifu vinginevyo ingekula kwake staili hii anayoifanya anajua mwenyewe alikoitoa yakupingana na maamuzi ya baraza la mawaziri,acha tusubiri kitakacho tokea pengine jk ataibuka toka usingizini.
 
Back
Top Bottom