Mh. Sitta kuendelea kukaa kwenye nyumba ya Spika Masaki ni halali?

Wakuu huyu 6 kwanza ndo mnafiki kuliko watu wote, na amevaa ngozi ya kondoo kumbe ni mbwa mwitu.sita amekuwa anaect kwamba ni mtetezi wa wanyonge kumbe ni mnafiki mno.sita c ndiye aliye jenga ofisi ya usipika kule urambo kwa mamilioni ya walipa kodi akiamini kwamba atakuwa spika wa maisha matokea yake ile ofisi c jui inafanya kazi gani kule urambo
 
Wakuu huyu 6 kwanza ndo mnafiki kuliko watu wote, na amevaa ngozi ya kondoo kumbe ni mbwa mwitu.sita amekuwa anaect kwamba ni mtetezi wa wanyonge kumbe ni mnafiki mno.sita c ndiye aliye jenga ofisi ya usipika kule urambo kwa mamilioni ya walipa kodi akiamini kwamba atakuwa spika wa maisha matokea yake ile ofisi c jui inafanya kazi gani kule urambo

Hivi wananchi wa Urambo wamfaidika vipi na jengo hilo? Wamapeta nafuu gani ya maisha baada ya Sitta kujenga ofisi ya Uspika? Title Deed ya hilo jengo inasemaje? Na Sitta mwenyewe anaweza sasa kuueleza umma wa Watanzani ni kwa nini aliona Urambo ndio sehemu stahiki (appropriate) kwa ofisi ya Urambo? What was it that made him reach that decision?
 
Wakuu huyu 6 kwanza ndo mnafiki kuliko watu wote, na amevaa ngozi ya kondoo kumbe ni mbwa mwitu.sita amekuwa anaect kwamba ni mtetezi wa wanyonge kumbe ni mnafiki mno.sita c ndiye aliye jenga ofisi ya usipika kule urambo kwa mamilioni ya walipa kodi akiamini kwamba atakuwa spika wa maisha matokea yake ile ofisi c jui inafanya kazi gani kule urambo
 
walimblackmail asiporopoka uaharo kwamba wapinzani ni wanafiki,watamlipua kwamba anaendelea kuishi kwenye nyumba ya spika wakati yeye sio spika,..niliwahi na nitaendelea kusema hilizee samwel sitta ni liroho kuliko lowassa,..anatamani everything alichokuwa nacho fisadi lowassa angepata yeye...akisimamishwa urais na ccm 2015,ukombozi utapatikana kirahisimon kuliko akisimamishwa lowassa..
 
Halafu hawa magamba wanashangilia kuondoka kwa RA, hivi hawaoni kuwa kwa majibu ya mzaha bungeni magamba yanazidi kuwa mengi na magumu. kama wanadhani ni enzi za zamani, basi wajue tunafuatilia haya yote na tunayarekodi, ikifika wakati wa uchaguzi tutawabana kwa majibu haya. nawasilisha
 
I THINK WE NEED TO THINK BEFORE WE DECIDE,NI NANI ALIWAINGIZA HAWA VIONGOZI MADARAKANI!???????? WANA JF TUPUNGUZE KULALAMA TUINGIE MTAANI TUWAELIMISHE RAIA NINI WAFANYE KUNAPOKUA NI KIPIND CHA UCHAGUZI.
SIO WANATUWEKEA VIONGOZI WANAOTAMKA WASICHOKISIMAMIA.
"NOW THIS IS NOT THE BEGINING,IT IS EVEN NOT THE END OF THE BEGINING, IT IS ACTUALY THE BEGINING OF THE END" Maneno ya Churchil
nayadedicate kwa wanaccm wote kuwa huu ndio mwisho wake
 
I THINK WE NEED TO THINK BEFORE WE DECIDE,NI NANI ALIWAINGIZA HAWA VIONGOZI MADARAKANI!???????? WANA JF TUPUNGUZE KULALAMA TUINGIE MTAANI TUWAELIMISHE RAIA NINI WAFANYE KUNAPOKUA NI KIPIND CHA UCHAGUZI.
SIO WANATUWEKEA VIONGOZI WANAOTAMKA WASICHOKISIMAMIA.
"NOW THIS IS NOT THE BEGINING,IT IS EVEN NOT THE END OF THE BEGINING, IT IS ACTUALY THE BEGINING OF THE END" Maneno ya Churchil
nayadedicate kwa wanaccm wote kuwa huu ndio mwisho wake

On the red: NEC!
 
Katika watu ambao siwaamini hata chembe ni huyu Samwel Sitta na Zitto Kabwe. ni rahisi kuzijuwa rangi za kinyonga kuliko rangi za watu hawa.
 
Hakuna nyumba ya Spika!

Mhe. Zitto ebu tuambie sisi wapiga kura wenu turidhike, inakuwaje huyo mzee Sitta akaendelea kukaa kwenye hiyo nyumba ambayo alipewa akiwa spika? sasa hivi si Spika tena, kwanini akae nyumba ya mtu binafsi na si ya serikali? Kumbuka tuna taarifa zake zote na jinsi alivyolazimisha nyumba hiyo apewe yeye. Akiwa bado Spika, nyumba aliyopewa ya serikali aliikataa kwa kisingizio kuwa hailingani na hadhi yake. Nyumba hiyo aliitafuta yeye binafsi, taarifa zinasema alibeba mkataba wa hiyo nyumba kwapani na kuitisha kikao cha Bodi ya Manunuzi ya Ofisi ya bunge na Wajumbe hawakuwa na option ila ni kumpitishia bwana mkubwa akale salama.

Nyumba hiyo kwanza ni ya mtu binafsi na kodi yake halali yasemekana ni U$ 3,000 kwa mwezi lakini yeye amekula dili na mwenye nyumba na kudai kuwa ni U$ 7,000 kwa mwezi ili wawe wakigawana fedha hiyo. Huo ni ujambazi wa wasasiasa!! Masaki kuna nyumba nzuri sana ambazo hazizidi hata U$ 5,000 kwa mwezi leo Sitta kwanini ang'ng'anie kukaa kwenye nyumba ya mtu binafsi kwa kodi ya US 7,000 kwa mwezi kama sio ufisadi? Ahame kwenye hiyo nyumba na apewe nyumba ya serikali!

Hoja nyingine hana ni kuhusu mafao ya hao wastaafu, kwani kuna aina ngapi za wastaafu? maana unaweza kustaafu kabisa shughuli za umma kama ilivyokuwa kwa maspika wengine kama marehemu Adam Sapi, alikaa nyumba ya serikali na kuhudumiwa na Bunge kwa kupewa usafiri, matibabu, maintanance ya gari na dereva hadi alipofariki. Mzee Msekwa naye alikaa nyumba ya serikali na alipoinunua aliendelea kupewa huduma ya usafiri, dereva, gari, matibabu. Sitta ni spika mstaafu lakini bado ni mtumishi wa umma kwa maana ya kuwa ni Waziri. Kwa nafasi yake ya uwaziri anapewa stahili zote na inabidi achague ahudumiwe na nani na si kuvuta Wizara ya Afrika mashariki na kuvuta Bunge, this is not good governance at all!! Yeye kama Waziri hata akienda nje ya nchi kwenye matibabu wizara yake ndio inawajibika na gharama zake kwa sababu bado yupo kwenye utumishi wa umma, why Bunge?

Ifike mahali viongozi wetu msituchanganye, mchague moja kuliko kujifanya watetezi wa wananchi wanyonge huku mkiwakamua jasho lao hadi tone la mwisho kulipia nyumba ya mtu mmoja zaidi ya milioni 12! huu ni mzaha kwa sisi watu wa kawaida! Sitta pia ana walinzi wawili wa usalama wa taifa anaofuatana nao kila mahali, gharama zinazidi kuongezeka bila sababu, kwenye ndege nao wanakatiwa tiketi daraja la kwanza na Business class, jamani tuoneeni huruma wenzenu. Ulinzi ndani ya nchi mnayoiita ya amani na utulivu wa kazi gani? Kwanini viongozi mnajiona miungu-watu? Mtu kama Sitta hana rekodi nzuri, ni mwizi, fisadi na mlafi ndio maana hata dhamira yake haimsuti kufuja fedha za walipa kodi masikini wa nchi hii ambao hata wengi wetu mlo wa siku moja ni tatizo kubwa!

Acheni kufuru!
 
Hakuna nyumba ya Spika!

Anaishi wapi sasa?au ndo zile za serikali zilizouzwa? sory mkuu!muda huu si nimekuona bungeni?unawezaje kuchangia huku JF muda huu! Unaiba muda wa mwajili wako ehe!
 
hivi kwa nini wabunge waliogombea majimbo wakapigwa chini hawaitwi wabunge wastaafu na kupewa haki zao?
sita alistaafu mwaka gani?
na uspika sheria inataka miaka mingapi?
je sita alishatimiza miaka hiyo?
je bunge lilikuwa linajua hilo?
je kwa mujibu wa sheria hiyo makinda amebakiza miaka mingapi?
je sheria za tanzania mtu mmoja npaka afariki anatakiwa kustaafu mara ngapi?
je akistaafu mara 5 labda serikali inawajibika kumpa nyumba tano?

magamba naombeni majibu tafadhali kabla sijaugeukia umma na kuwaamshia hasira.
 
Katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu aliulizwa ni lini Mh Sitta ataondoka kwenye nyumba ya Spika huko Masaki maana sio Spika tena. Kwa maelezo ya mbunge aliyeuliza swali ni kwamba serikali inatumia Tsh million 12 kila mwezi kwa nyumba ya huyu Spika. Lakini kama kawaida Mama Makinda alikurupuka na kujibu swali la serikali akisema kuwa hiyo ni stahiki ya Mh Sitta kama Spika mstaafu.Wana-JF, Sasa nitawahoji, ni sahihi kwa Mh Sitta kuendelea kuishi kwenye nyumba ya Spika hata kama sio Spika? Na kwa mantiki hiyo Marais wastaafu wanatakiwa waendelee kuishi IKULU maana wanastahili? Sera ya kuangalia maslahi ya viongozi wakuu wastaafu inasemaje?
Mimi mwenzenu bado nipo tofauti, kama suala ni nyuumba mbona kwa milioni 300 anaweza kujengewa nyuma ya hali ya juu sana badala ya hizo mil 12 kwa mwezi ambazo kwa mwaka ni mil 144 na miaka 5 ni milioni 720. Why unneccesary spending? hiyo nyumba ina thamani gani kama inalipwa mabilioni hayo yote kwa maisha yote ya spika?
 
We mwana magamba jiandae zamu yako yaja! Halafu wandugu tusiposhangaa 2015 labda JK ataendelea kukaa ikulu! Sita anjikomba kumbe naye magamba yamemkakamaa, anatakiwa ayabandue siyo kuvua tu!
 
Mimi mwenzenu bado nipo tofauti, kama suala ni nyuumba mbona kwa milioni 300 anaweza kujengewa nyuma ya hali ya juu sana badala ya hizo mil 12 kwa mwezi ambazo kwa mwaka ni mil 144 na miaka 5 ni milioni 720. Why unneccesary spending? hiyo nyumba ina thamani gani kama inalipwa mabilioni hayo yote kwa maisha yote ya spika?
Nadhani hili ndio swala la msingi hapa, kwanini mipesa yote hiyo kwa mwezi?
Issue ya yeye kuendelelea kuwepo pale kunaweza kutokana na taratibu zilizipo hata kama ni mapungufu, na nyumba ya spika sio sawa na ikulu
 
Ndugu yangu akikusikia Atakwambia wewe ni Mnafiki na Umetumwa na Mafisadi!
 
Mhe. Zitto ebu tuambie sisi wapiga kura wenu turidhike, inakuwaje huyo mzee Sitta akaendelea kukaa kwenye hiyo nyumba ambayo alipewa akiwa spika? sasa hivi si Spika tena, kwanini akae nyumba ya mtu binafsi na si ya serikali? Kumbuka tuna taarifa zake zote na jinsi alivyolazimisha nyumba hiyo apewe yeye. Akiwa bado Spika, nyumba aliyopewa ya serikali aliikataa kwa kisingizio kuwa hailingani na hadhi yake. Nyumba hiyo aliitafuta yeye binafsi, taarifa zinasema alibeba mkataba wa hiyo nyumba kwapani na kuitisha kikao cha Bodi ya Manunuzi ya Ofisi ya bunge na Wajumbe hawakuwa na option ila ni kumpitishia bwana mkubwa akale salama.

Nyumba hiyo kwanza ni ya mtu binafsi na kodi yake halali yasemekana ni U$ 3,000 kwa mwezi lakini yeye amekula dili na mwenye nyumba na kudai kuwa ni U$ 7,000 kwa mwezi ili wawe wakigawana fedha hiyo. Huo ni ujambazi wa wasasiasa!! Masaki kuna nyumba nzuri sana ambazo hazizidi hata U$ 5,000 kwa mwezi leo Sitta kwanini ang'ng'anie kukaa kwenye nyumba ya mtu binafsi kwa kodi ya US 7,000 kwa mwezi kama sio ufisadi? Ahame kwenye hiyo nyumba na apewe nyumba ya serikali!

Hoja nyingine hana ni kuhusu mafao ya hao wastaafu, kwani kuna aina ngapi za wastaafu? maana unaweza kustaafu kabisa shughuli za umma kama ilivyokuwa kwa maspika wengine kama marehemu Adam Sapi, alikaa nyumba ya serikali na kuhudumiwa na Bunge kwa kupewa usafiri, matibabu, maintanance ya gari na dereva hadi alipofariki. Mzee Msekwa naye alikaa nyumba ya serikali na alipoinunua aliendelea kupewa huduma ya usafiri, dereva, gari, matibabu. Sitta ni spika mstaafu lakini bado ni mtumishi wa umma kwa maana ya kuwa ni Waziri. Kwa nafasi yake ya uwaziri anapewa stahili zote na inabidi achague ahudumiwe na nani na si kuvuta Wizara ya Afrika mashariki na kuvuta Bunge, this is not good governance at all!! Yeye kama Waziri hata akienda nje ya nchi kwenye matibabu wizara yake ndio inawajibika na gharama zake kwa sababu bado yupo kwenye utumishi wa umma, why Bunge?

Ifike mahali viongozi wetu msituchanganye, mchague moja kuliko kujifanya watetezi wa wananchi wanyonge huku mkiwakamua jasho lao hadi tone la mwisho kulipia nyumba ya mtu mmoja zaidi ya milioni 12! huu ni mzaha kwa sisi watu wa kawaida! Sitta pia ana walinzi wawili wa usalama wa taifa anaofuatana nao kila mahali, gharama zinazidi kuongezeka bila sababu, kwenye ndege nao wanakatiwa tiketi daraja la kwanza na Business class, jamani tuoneeni huruma wenzenu. Ulinzi ndani ya nchi mnayoiita ya amani na utulivu wa kazi gani? Kwanini viongozi mnajiona miungu-watu? Mtu kama Sitta hana rekodi nzuri, ni mwizi, fisadi na mlafi ndio maana hata dhamira yake haimsuti kufuja fedha za walipa kodi masikini wa nchi hii ambao hata wengi wetu mlo wa siku moja ni tatizo kubwa!

Acheni kufuru!


Mawaziri wakuu wote waliostafuu wanaishi wapi? Makamu wa Rais waliostafuu wanaishi wapi? akuna kiongozi wajuu aliyewahi kunyangwa nyumba hapa Tanzania.

Nadhani kuna marupurupu ya spika mstaafu anayovuta kama Waziri Mkuu mstaafu ambayo house is included tuwe wapole jamani.

Makinda lazima atetee maana soon baada ya yeye kustafuu pia atafuta yake sasa serikali ikifuta ina maana itaanzia kwake una maana naye aje akose? Ahaa Makinda lazima atetee hadi mwisho.
 
Back
Top Bottom