rais kikwete ametahadharisha vitendo vya rushwa vinavyoendelea ndani ya chaguzi za ccm kwamba vitaibomoa ccm ambayo tayari imeshaanza kupoteza imani kwa wanachama wake na makada wake ambapo tayari wameshaanza kukihama chama hicho kwa kasi
vilevile rais ameuthibitishia umma kwamba ccm kwa sasa ni kiwanda cha kuzalisha wala rushwa na mafisadi kwa ujumla hivyo basi ni watu wasiokuwa wazalendo na ni hatari kwa maendeleo ya taifa letu.
akuli hyo ya mh.rais ni sawa na kuithibitishia chadema ushindi kwa sababu watanzania wametokea kuiamini chadema kuwa ni tumaini jipya katika ukombozi wa mustakabali wa maisha ya watanzania hasa vijana ambao wengi wao wameshakata tamaa kutokana na utawala dhalimu wa ccm unaowanyonya.
MY TAKE
Ndugu zangu watanzania wote tumeshudia ccm inavyoendesha chaguzi zake za ndani kwa rushwa (kununua viongozi) ni lazima tujue ya kwamba mtu anatoa pesa kwa kutegemea kuja kuirudisha siku akiingia madarakani kwa sababu hiyo basi
kwa vyote viongozi wa aina hiyo lazima wapore rasilimali za nchi yetu ili kurejesha fedha zao walizohonga ili kuupata uongozi
naomba tushirikiane kwa pomoja kuiangamiza ccm kwa sababu kwa sasa chama hicho ni janga la taifa.
we dont have to discover how to reach the next generation they will discover that themselves. CCM ni washindi tu we ngoja uone 2015 we si umeona maandalizi!