Mh Rais Hakuvunja KATIBA yupo sahihi kwa katiba ya nchi yetu

engmtolera

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
5,150
1,437
baada kujiridhisha mwenyewe kwa kusoma katiba ya jamuhuri wa muungano wa tanzania,nimeona kuwa Mh Rais hakuvunja katiba ya nchi yetu kama baadhi ya watu wanavyo dai

mnaweza pia kujionea wenyewe hapa chini,kwani nimeweka vifungu vinavyomruhusu raisi kumteua waziri pasi ya kuvunja katiba ya nchi

katiba inasema:-
54.-(1) Kutakuwa na Baraza la Mawaziri ambalo wajumbe wake watakuwa ni Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Rais waZanzibar na Mawaziri wote.


(2) Rais atahudhuria mikutano ya Baraza la Mawaziri na ndiye atkayeongoza mikutano hiyo. Na endapo Rais hayupo basi
mikutano itaongozwa na Makamu wa Rais na kama wote wawili Rais na Makamu wa Rais hawapo Waziri Mkuu ndiye ataongoza
Mikutano hiyo.


(3) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara ya 37(1) ya Katiba hii, Baraza la Mawaziri litakuwa ndicho chombo kikuu cha
kumshauri Rais juu ya mambo yote yanayohusika na utekelezaji wa madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii, na litamsaidia na kumshauri Rais juu ya jambo lolote litakalowasilishwa kwenye Baraza hilo kwa mujibu wa maagizo maalum au maagizo ya jumla yatakayotolewa na Rais.


(4) Mwanasheria Mkuu wa Serikali atahudhuria mikutano yote ya Baraza la Mawaziri na atakuwa na haki zote za mjumbe wa
mikutano hiyo isipokuwa hatakuwa na haki ya kupiga kura katika mikutano hiyo.


(5) Suala kama ushauri wowote, na ni ushauri gani, ulitolewa na Baraza la Mawaziri kwa Rais, halitachunguzwa katika
mahakama yoyote.


55.-(1) Mawaziri wote ambao ni wajumbe wa Baraza la Mawaziri kwa mujibu wa ibara ya 54 watateuliwa na Rais baada
ya kushauriana na Waziri Mkuu.


(4) Mawaziri na Naibu Mawaziri wote watateuliwa kutoka miongoni mwa Wabunge.


56. Waziri au Naibu Waziri hatashika madaraka yake ila mpaka awe ameapa kwanza mbele ya Rais kiapo cha uaminifu na pia kiapo kingine chochote kinachohusika na utendaji wa kazi yake kitakachowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.


68. Kila Mbunge atatakiwa kuapishwa katika Bunge kiapo cha uaminifu kabla hajaanza kushiriki katika shughuli za Bunge; lakini Mbunge aweza kushiriki katika uchaguzi wa Spika hata kabla
hajaapishwa.


KWA MANENO MENGINE mawaziri na manaibu waziri walioteuliwa na bado hawa pata kiapo cha uaminifu bungeni,hatafanya kazi za kibunge ama kujibu hoja za wabunge bungeni mpaka pale atakapo pata kiapo cha uaminifu ndani ya bunge.

lakini ataendelea kufanya kazi za serikali kama waziri baada ya kuapishwa na Mh raisi kama inavyojielekeza hapo juu

nawasilisha(tusome na tuelewe tusikurupuke)
 
Wiki tatu kabla ya kikao cha bajeti Waziri atatakiwa Kukutana na Kamati husika ya bunge kulingana na wizara anayoiongoza (Hapo ni shughuli za kibunge) ili kamati husika ya bunge waipitie bajeti yake na kutoa mapendekezo na maboresho kwa bajeti husika... sasa atakutana nao vipi wakati bado hajaapishwa?????? Kwa hiyo huo utata wa kikatiba, kikanuni tupatie majibu!
 
Wiki tatu kabla ya kikao cha bajeti Waziri atatakiwa Kukutana na Kamati husika ya bunge kulingana na wizara anayoiongoza (Hapo ni shughuli za kibunge) ili kamati husika ya bunge waipitie bajeti yake na kutoa mapendekezo na maboresho kwa bajeti husika... sasa atakutana nao vipi wakati bado hajaapishwa?????? Kwa hiyo huo utata wa kikatiba, kikanuni tupatie majibu!

kaka
hapo atafanya kazi kama waziri nje ya bunge si ndani ya bunge,kitakacho mzuia yeye ni kuto kujibu hoja zozote zile ndani ya bunge kabla ya kula kiapo cha uaminifu
 
Mawaziri au naibu mawaziri watatokana na wabunge na sio 'wabunge wataule'. Now, mbunge ni nani na mbunge-mteule ni nani?

Pili, huwezi kuwa mbunge (i.e mbunge mteule kula kiapo) siku hiyo hiyo na ukawasilisha hoja yako kwa Spika (swali/majibu) siku hiyo hiyo. Kama sikosei unatakiwa walau kuwepo na siku 14 tangu ulipokula kiopo ndipo hoja yako ipokelewe. Kwa maana hiyo waziri wa nishati na madini, na manaibu wawili wa wizara ya afya hawawezi kupeleka majibu ya maswali watakayoulizwa na wabunge kwa sasa kwa ajili ya bunge la mwezi June hadi pale watakapokula kiapo!

NB: Kumbuka maswali mengi hupelekwa bungeni kitambo kabla ya vikao vya bunge kuanza.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
mko bize kudili na teknicality ndogondogo, za kijinga I must say, ilhali mambo ya msingi yenye tija kwa mvuja jasho yanapuuzwa.

yakupasa kusoma maandishi na kuyaelewa sio upelekwe kama ling'ombe,nilidhani umesoma hapo juu na labda ungekuja na dukuduku kama hili hapa((5) Suala kama ushauri wowote, na ni ushauri gani, ulitolewa na Baraza la Mawaziri kwa Rais, halitachunguzwa katika mahakama yoyote.)

nilidhani ungejiuliza kwanini tusihoji mahakamani ama kuchunguza ushauri wowote ule,maana waweza kuwa ulikuwa ni ushauri wa kuuza nchi kwa nini usichunguzwe ktk mahakama yoyote ile? hata hilo wewe huwezi kuliona mkuu

maana hii ni kwa faida ya wote si kwa engmtolera peke yake

soma katiba,ielewe na mwisho wa siku ujekutoa maoni yako,usije kuja piga kelele siku za usoni
 
68. Kila Mbunge atatakiwa kuapishwa katika Bunge kiapo cha
uaminifu kabla hajaanza kushiriki katika shughuli
za Bunge
; lakini Mbunge aweza kushiriki katika uchaguzi wa Spika hata kabla hajaapishwa.
Hapo kwenye red kunanitatiza, aweza kushirika uchaguzi wa spika, does it mean anaweza kuwa na waziri?
 
mko bize kudili na teknicality ndogondogo, za kijinga I must say, ilhali mambo ya msingi yenye tija kwa mvuja jasho yanapuuzwa.

Nyie ndio mnaingia mikataba ya ajabu ajabu kwa uvivu, attention to details is super important.
 
kaka
hapo atafanya kazi kama waziri nje ya bunge si ndani ya bunge,kitakacho mzuia yeye ni kuto kujibu hoja zozote zile ndani ya bunge kabla ya kula kiapo cha uaminifu

nakubaliana na anayesema hizi technicality, huenda siyo za muhimu kihivyo lakini swali la nje na ndani ya bunge halina mantiki zote ni shule za bunge siyo lazima zifanywe mjengoni
 
Mawaziri au naibu mawaziri watatokana na wabunge na sio 'wabunge wataule'. Now, mbunge ni nani na mbunge-mteule ni nani?

Pili, huwezi kuwa mbunge (i.e mbunge mteule kula kiapo) siku hiyo hiyo na ukawasilisha hoja yako kwa Spika (swali/majibu) siku hiyo hiyo. Kama sikosei unatakiwa walau kuwepo na siku 14 tangu ulipokula kiopo ndipo hoja yako ipokelewe. Kwa maana hiyo waziri wa nishati na madini, na manaibu wawili wa wizara ya afya hawawezi kupeleka majibu ya maswali watakayoulizwa na wabunge kwa sasa kwa ajili ya bunge la mwezi June hadi pale watakapokula kiapo!

NB: Kumbuka maswali mengi hupelekwa bungeni kitambo kabla ya vikao vya bunge kuanza.

66.-(1) Bila ya kuathiri masharti mengine ya ibara hii, kutakuwa na aina zifuatazo za Wabunge, yaani-

(e) Wabunge wasiozidi kumi walioteuliwa na Rais kutoka miongoni mwa watu wenye sifa kwa mujibu wa ibara ya 67, isipokuwa sifa iliyotajwa katika ibara ya 67(1)(b).


(3) Kwa madhumuni ya utekelezaji wa madaraka yake Bunge laweza-


(a) kumuuliza Waziri yeyoyote swali lo lote kuhusu mambo ya umma katika Jamhuri ya Muungano ambayo yako katika wajibu wake;

kwanza utambue kuwa mawaziri wanaruksa ya kuingia bungeni,ikimaanisha kuwa wakiwa ndani ya bunge kabla ya kula kiapo cha bunge ndani ya bunge,wanaruhusiwa kufanya kazi za kiwaziri ndani ya bunge,moja ya kazi hiyo ni kujibu MASWALI YA WABUNGE kama mawaziri waliokula kiapo cha utii kwa MH RAISI.
 
Nashindwa kukuelewa mkuu! Hapo juu 56 umetaja kiapo cha uaminifu kwa Rais lakini pia unasema na kiapo kingine kilichowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge. Hapa mimi ningesema hicho kingine ni kile cha ubunge. Kwa maana hiyo walipaswa kwanza kuapishwa bungeni kabla ya kiapo cha Rais. Katiba imekiukwa jamani tuache porojo. Utatenganishaje kazi za kibunge na uwaziri? Kama kichwa cha NAZI alikuwa na haraka si angemshauri supika kuitisha Bunge la dharura?! Hapo hapo tungemshughulikia na Pinda!
 
yakupasa kusoma maandishi na kuyaelewa sio upelekwe kama ling'ombe,nilidhani umesoma hapo juu na labda ungekuja na dukuduku kama hili hapa((5) Suala kama ushauri wowote, na ni ushauri gani, ulitolewa na Baraza la Mawaziri kwa Rais, halitachunguzwa katikamahakama yoyote.)

nilidhani ungejiuliza kwanini tusihoji mahakamani ama kuchunguza ushauri wowote ule,maana waweza kuwa ulikuwa ni ushauri wa kuuza nchi kwa nini usichunguzwe ktk mahakama yoyote ile? hata hilo wewe huwezi kuliona mkuu

maana hii ni kwa faida ya wote si kwa engmtolera peke yake

soma katiba,ielewe na mwisho wa siku ujekutoa maoni yako,usije kuja piga kelele siku za usoni

Maoni anakusanya Warioba ndg. injinia wa UDOM.

Ila sio mbaya kujikip bize nyuma ya kakompyuta kako..kama Ustaadh al Hajj Mwinyi angesema 'RUKSA'!
 
Nyie ndio mnaingia mikataba ya ajabu ajabu kwa uvivu, attention to details is super important.
Mikataba inaingiaje hapa? hakuna details hapa, it is about teknicalities za kuwasimika wasaidizi wa mfalume, ni zoezi ambalo tumelizoea tangia uhuru, in way or another litafanyika (whether katiba inavunjwa au la) na as usual at the end of the sunny darisalama's day, hakutakuwa na tija and nobody will remember, as always.
 
Hapo kwenye red kunanitatiza, aweza kushirika uchaguzi wa spika, does it mean anaweza kuwa na waziri?

maanake ni rahisi kuwa wabunge wanamchagua Spika ili wabunge wote waape kiapo cha uaminifu kwake. Kwa kuwa kabla ya uchaguzi bunge huvunjwa na kunakuwa hakuna spika. So wakitoka kwenye majimbo baada ya kuchaguliwa wabunge hufanya uchaguzi wa spika.
 
Mkuu engmtolera sogea mbele kidogo kwenye ibara ya 69 utusaidie zaidi.

69.-(1) Kila Mbunge atatakiwa, kabla ya kumalizika siku thelathini tangu aapishwe kushika madaraka yake kama Mbunge
kuwasilisha kwa Spika nakala mbili za tamko rasmi kwamba hajapoteza sifa za uchaguzi kwa mujibu wa masharti ya aya ya (d) ya ibara ndogo ya (2) ya ibara ya 67.


(2) Tamko rasmi linalotakiwa kuwasilishwa kwa Spika kwa mujibu wa masharti ya ibara hii litatolewa kwa kutumia fomu
maalum itakayowekwa kwa mujibu wa Sheria iliyotungwa na Bunge.


(3) Spika atawasilisha kwa Kamishna wa Maadili nakala moja ya kila tamko rasmi lililowasilishwa kwake kwa mujibu wa masharti ya ibara hii.


kimbunga

hii ipo wazi,wale wabunge walioteuliwa na mh raisi bado ni wabunge,na wataendelea kufanya kazi za kiuwaziri nje na ndani ya bunge,kitakacho kuja kutokea ni pale bunge linapotaka kutunga sheria mbalimbali kama bado watakuwa hawajala kiapo cha bunge ndani ya bunge hawatashiriki kutunga sheria hzo lakini hilo haliwazuii wao kutokufanya kazi za serikali
ila hawatafanya kazi za kuisimamia serikali kwa kuuliza maswali ndani ya bunge.

na baada ya kula kiapo cha bunge basi atatekeleza Tamko rasmi la Wabunge kuhusu maadili ya viongozi Sheria ya 1995 Na.12 ib.11
 
Maoni anakusanya Warioba ndg. injinia wa UDOM.

Ila sio mbaya kujikip bize nyuma ya kakompyuta kako..kama Ustaadh al Hajj Mwinyi angesema 'RUKSA'!

anakusanya maoni kutoka kwa nani? si mtu kama wewe mvivu wa kusoma ndiye utakayetakiwa kuyatoa maoni hayo? hamchelewi kuja kulalama kuwa hatukufikiwa na sikuwa na muda wa kusoma katiba,

timiza wajibu wako wakati ndio huu
 
hao hawaja apa so sio wabunge kamili bado ni wabunge wateule
kaka
hapo atafanya kazi kama waziri nje ya bunge si ndani ya bunge,kitakacho mzuia yeye ni kuto kujibu hoja zozote zile ndani ya bunge kabla ya kula kiapo cha uaminifu
 
Mkuu engmtolera tatizo langu lipo hapo kwenye kushika madaraka ya ubunge. Nikaelewa kuwa ili uwe na madaraka ya ubunge lazima uapishwe na ili uwe waziri lazima uwe mbunge. Kwa hiyo ubunge ni madaraka ambayo yanashikwa baada ya kuapa. The law of transitivity inasemaje hapo?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom