Majuzi waziri mkuu Mh. Mizengo Kayanza Peter Pinda aliwaasa makatibu muhtasi wa serikali na mashirika ya umma kutotoa siri za ofisi zao. Mimi kwa nguvu zote napingana na wito huo wa Mh. Pinda kwa sababu madhambi mengi ya ufisadi tumeyajua kwa msaada wa hawa makatibu muhtasi pamoja na wadau wengine wa maendeleo na wapinga ufisadi.
Baadhi ya nyaraka muhimu ambazo zimewezesha kuibuliwa kwa kashfa/skandali mbali mbali za wizi wa mali ya umma ziliweza kupatikana kwa msaada wa hawa watu. Sasa mimi najiuliza Mh Pinda badala ahimize kila mfanya kazi kwa nafasi yake popote alipo ajitahidi kutoa taarifa zozote za uhujumu uchumi na rushwa inayofanywa na wakubwa kwa kutumia ofisi zao, yeye anakemea watu kutotoa taarifa je hizi nyimbo za kupambana na rushwa hapa nchini zina maana yoyote?
Binafsi natoa wito kwa makatibu muhtasi wote Tanzania kutoijali kauli ya Pinda na kujitahidi kuanika uozo wowote unaotokea ktk ofisi zao.
Baadhi ya nyaraka muhimu ambazo zimewezesha kuibuliwa kwa kashfa/skandali mbali mbali za wizi wa mali ya umma ziliweza kupatikana kwa msaada wa hawa watu. Sasa mimi najiuliza Mh Pinda badala ahimize kila mfanya kazi kwa nafasi yake popote alipo ajitahidi kutoa taarifa zozote za uhujumu uchumi na rushwa inayofanywa na wakubwa kwa kutumia ofisi zao, yeye anakemea watu kutotoa taarifa je hizi nyimbo za kupambana na rushwa hapa nchini zina maana yoyote?
Binafsi natoa wito kwa makatibu muhtasi wote Tanzania kutoijali kauli ya Pinda na kujitahidi kuanika uozo wowote unaotokea ktk ofisi zao.