Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Wakati sakata la posho mbili au zaidi kwa kazi moja likiendelea kuchukua sura mpya kila siku huku "mpambanaji" Ole Sendeka akitishia kumharibi Mh Rais Kikwete kwa kuanika mabaya ya serikali endapo kama hataacha suala la posho mbili kwa kazi moja Waziri Mkuu alidai wakati anafungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwamba fedha kinachopata chuo hicho ni kidogo sana, TSh 2bn/-, ambazo amedai ni posho ya vigogo wawili au watatu tena kwa kikao cha ovyo ovyo tu! Jamani suala la posho za vikao liangaliwe, kumbe sio dogo kama wengine walivyodai! Yaani TSh 2bn/- kwa posho ya vigogo wawili watatu? Hivi Serikali hutumia TSh ngapi hasa kwa vikao? Hili itabidi liwekwe wazi kwa kweli!
Bajeti ya OUT kama posho ya vigogo wawili - Pinda
Na Salim Said
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesikitishwa na kiwango kidogo cha bajeti inayotengwa na serikali kwa ajili ya Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT), akisema kiwango hicho ni sawa na posho za vigogo wawili wa serikali, tena kwenye vikao vya ovyo.
Waziri Mkuu alisema hayo jana wakati akiwahutubia wanafunzi wa jumuiya ya OUT katika mkutano mkuu wa mwaka wa chuo hicho kwenye majengo ya ofisi zake zilizo Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Pinda alisema alikuwa mmoja wa watendaji walioshiriki kupitisha bajeti ya mwaka 2009/10, na kwamba kiasi kilichopitishwa kilikuwa Sh2 bilioni kwa ajili ya shughuli za OUT.
"Nimemuuliza Profesa Tolly Mbwette bajeti ya mwaka huu ameniambia ni Sh2 bilioni, lakini fedha hii si chochote kwa shughuli zinazoendeshwa chuoni hapa mimi nilikuwa sijawahi kufika na kujionea shughuli za hapa," alisema Pinda.
"Shilingi bilioni 2 ni sawa na posho za wakubwa wawili au watatu tu serikalini tena katika vikao vya ovyo ovyo tu."
Alisema licha ya kuwa karibu na OUT kutokana na marafiki zake ambao wengi ni wadau wakuu wa chuo hicho, alikuwa hajui kinachoendelea chuoni hapo.
Miongoni mwa watu wa karibu na waziri mkuu ambao ni wadau wa chuo hicho ni mke wa wake, Tunu Pinda ambaye ni mwanafunzi, mkuu wa OUT, Samuel Malecela (mbunge), mwenyekiti wa baraza la chuo hicho, Profesa Samuel Wangwe na mama Anne Kilango (mbunge).
"Nitaishauri serikali kuongeza bajeti ya chuo ili kuhakikisha kwamba inapata fedha nzuri za kukifanya kiwe miongoni mwa vyuo vikubwa duniani. Pia nitawashawishi wadau mbalimbali kuchangia... kwa kweli kazi zinazofanyika ni kubwa," alisema Pinda.
Panda alifafanua kuwa kumekuwa na mtazamo potofu juu ya elimu masafa na huria (DLO) kwamba si elimu nzuri na inafananishwa na elimu isiyo rasmi.
Chuo kikuu huria ambacho kina matawi yake karibu mikoa yote nchini Tanzania kinatoa elimu kwa njia huria na ya masafa ili kuwawezesha hata watu waliomo kazini kupata fursa ya kusoma.
"Ni wajibu wetu serikali, nyinyi na wadau wote wa elimu nchini kuhakikisha kwamba tunaielimisha jamii kuhusu ubora wa elimu ya DLO ili jamii iondokane na mtazamo huo potofu," alisema Pinda.
"Msikate tamaa wala kuvunjika moyo OUT ni chuo kikubwa nchini tena kizuri na kinachotoa elimu bora, jitahidini na mimi nitazidi kuwashawishi watu mbalimbali kusoma hapa."
Akijibu swali kuhusu suala la jinsia katika vikao vya maamuzi, Pinda alisema suala hilo linafanyiwa kazi na serikali na kwamba mategemeo yake katika serikali na bunge lijalo uwakilishi wa wanawake utaongezeka hadi kufikia kati ya asilimia 40 na 47.
"Kwa sasa bungeni wanawake ni asilimia 30 na katika baraza la Mawaziri robo ni wanawake, lakini mategemeo yangu ni kwamba serikali na bunge lijalo uwakilishi wa wanawake utaongezeka hadi kufikia asilimia 47 kwa sababu huenda wabunge wengi wanaume wakaanguka," alisema Pinda.
(Source: www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=15660).
Bajeti ya OUT kama posho ya vigogo wawili - Pinda
Na Salim Said
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesikitishwa na kiwango kidogo cha bajeti inayotengwa na serikali kwa ajili ya Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT), akisema kiwango hicho ni sawa na posho za vigogo wawili wa serikali, tena kwenye vikao vya ovyo.
Waziri Mkuu alisema hayo jana wakati akiwahutubia wanafunzi wa jumuiya ya OUT katika mkutano mkuu wa mwaka wa chuo hicho kwenye majengo ya ofisi zake zilizo Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Pinda alisema alikuwa mmoja wa watendaji walioshiriki kupitisha bajeti ya mwaka 2009/10, na kwamba kiasi kilichopitishwa kilikuwa Sh2 bilioni kwa ajili ya shughuli za OUT.
"Nimemuuliza Profesa Tolly Mbwette bajeti ya mwaka huu ameniambia ni Sh2 bilioni, lakini fedha hii si chochote kwa shughuli zinazoendeshwa chuoni hapa mimi nilikuwa sijawahi kufika na kujionea shughuli za hapa," alisema Pinda.
"Shilingi bilioni 2 ni sawa na posho za wakubwa wawili au watatu tu serikalini tena katika vikao vya ovyo ovyo tu."
Alisema licha ya kuwa karibu na OUT kutokana na marafiki zake ambao wengi ni wadau wakuu wa chuo hicho, alikuwa hajui kinachoendelea chuoni hapo.
Miongoni mwa watu wa karibu na waziri mkuu ambao ni wadau wa chuo hicho ni mke wa wake, Tunu Pinda ambaye ni mwanafunzi, mkuu wa OUT, Samuel Malecela (mbunge), mwenyekiti wa baraza la chuo hicho, Profesa Samuel Wangwe na mama Anne Kilango (mbunge).
"Nitaishauri serikali kuongeza bajeti ya chuo ili kuhakikisha kwamba inapata fedha nzuri za kukifanya kiwe miongoni mwa vyuo vikubwa duniani. Pia nitawashawishi wadau mbalimbali kuchangia... kwa kweli kazi zinazofanyika ni kubwa," alisema Pinda.
Panda alifafanua kuwa kumekuwa na mtazamo potofu juu ya elimu masafa na huria (DLO) kwamba si elimu nzuri na inafananishwa na elimu isiyo rasmi.
Chuo kikuu huria ambacho kina matawi yake karibu mikoa yote nchini Tanzania kinatoa elimu kwa njia huria na ya masafa ili kuwawezesha hata watu waliomo kazini kupata fursa ya kusoma.
"Ni wajibu wetu serikali, nyinyi na wadau wote wa elimu nchini kuhakikisha kwamba tunaielimisha jamii kuhusu ubora wa elimu ya DLO ili jamii iondokane na mtazamo huo potofu," alisema Pinda.
"Msikate tamaa wala kuvunjika moyo OUT ni chuo kikubwa nchini tena kizuri na kinachotoa elimu bora, jitahidini na mimi nitazidi kuwashawishi watu mbalimbali kusoma hapa."
Akijibu swali kuhusu suala la jinsia katika vikao vya maamuzi, Pinda alisema suala hilo linafanyiwa kazi na serikali na kwamba mategemeo yake katika serikali na bunge lijalo uwakilishi wa wanawake utaongezeka hadi kufikia kati ya asilimia 40 na 47.
"Kwa sasa bungeni wanawake ni asilimia 30 na katika baraza la Mawaziri robo ni wanawake, lakini mategemeo yangu ni kwamba serikali na bunge lijalo uwakilishi wa wanawake utaongezeka hadi kufikia asilimia 47 kwa sababu huenda wabunge wengi wanaume wakaanguka," alisema Pinda.
(Source: www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=15660).