MVUMBUZI
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 5,183
- 2,304
Mh. Lazaru Nyalandu(Naibu waziri) ametamka kuwa kuna watu CCM wanampiga kiasi cha kumwekea mitego mbalimbali ili kutimiza malengo yao ya kumchafua kisiasa. Maneno hayo aliyatoa wakati akikanusha shutuma zilizotengenezwa dhidi yake kwamba alitishia kwa bastola na kuvunja vizuizi vilivyokuwa vimewekwa barabara huko Singida katika jimbo lake. Nyalandu alisema hajawahi mtishia mtu kwa Bastola na hajafika jimboni kwake tangu February na kwamba yanayosemwa ni kwa lengo la kumchafua na wanaofanya hivyo ni CCM.
Amesema wamefikia hatua hata ya kumtega kwa kumchomekea wasichana ili akionekana tu yuko naye basi waseme wanachotaka kusema.
Kwa uchambuzi wangu inaonekana vijana walioko CCM wanaona mbali kuliko wazee wao na hii inaondoa status quo ya waasisi kiasi kwamba wazee wanaona vijana wanakosa adabu na kuaza kutumia mbinu chafu kuwanyamazisha.
CCM wako vijana ambao wameamua kutolalia godoro lenye chawa la CCM ya akina Kingunge na wameamua kuwa na mtazamo tofauti na hivyo kuonekana kuwa chukizo kwa wazee. Akina January Makamba, Filikunjombe, Lazaru Nyalandu, Selukamba na wengine wanaonekana kuwa na msimamo ambao utawakera sana CCM kiasi cha kutaka kuwapiga vita na kuzima nyota yao ya kisiasa.
Ninawashauri hawa vijana kuondoka na kujiunga na sisi tulioamua kuingia katika mapambano ya kidemokrasia kuikomboa nchi yetu. Milya amenza na wengine(Nyalandu, Januari Makamba, Filikunjombe, Selukamba) msipate kigugumizi karibuni tujenge upya taifa la kizalendo CCM iko kwenye steep downfall!!!!
Amesema wamefikia hatua hata ya kumtega kwa kumchomekea wasichana ili akionekana tu yuko naye basi waseme wanachotaka kusema.
Kwa uchambuzi wangu inaonekana vijana walioko CCM wanaona mbali kuliko wazee wao na hii inaondoa status quo ya waasisi kiasi kwamba wazee wanaona vijana wanakosa adabu na kuaza kutumia mbinu chafu kuwanyamazisha.
CCM wako vijana ambao wameamua kutolalia godoro lenye chawa la CCM ya akina Kingunge na wameamua kuwa na mtazamo tofauti na hivyo kuonekana kuwa chukizo kwa wazee. Akina January Makamba, Filikunjombe, Lazaru Nyalandu, Selukamba na wengine wanaonekana kuwa na msimamo ambao utawakera sana CCM kiasi cha kutaka kuwapiga vita na kuzima nyota yao ya kisiasa.
Ninawashauri hawa vijana kuondoka na kujiunga na sisi tulioamua kuingia katika mapambano ya kidemokrasia kuikomboa nchi yetu. Milya amenza na wengine(Nyalandu, Januari Makamba, Filikunjombe, Selukamba) msipate kigugumizi karibuni tujenge upya taifa la kizalendo CCM iko kwenye steep downfall!!!!