Mh. Mnyika kwa hili umepotoka!...

Nikusahihishe tu, kuchangia kwa miezi 180 ndio kigezo cha kupata pensheni na siyo kwamba ukishachangia miezi 180 unaweza kuchukua pensheni yako. Miaka ya pensheni inabaki ilele ile 55 voluntary na 60 compulsury!

Pili, unategemea hela za withdrawal ndio ukaanzishie mradi?? Huu ni kama wendawazimu

Hapo juu angalia sana.
Mimi naona huo 'wendawazimu' ni kwa serikali kushindwa kukusanya kodi kwa ajili ya matumizi yake, na badala yake kukimbilia kuchulua pesa kwenye mifuko ya pension.
Mimi nimeshachukua 'withdrawal' yangu mwaka jana, na sasa nimeanzisha mradi unaoniletea mapato ya kutosha tu. Nimejiajiri. Niambie kama kufanikiwa kujiajiri ni 'wendawazimu', au serikali kuogopa kukusanya kodi kwenye makampuni ya madini ndio 'wendawazimu' ???
Humu JF kuna watu wa ajabu sana.
 
mkuu usibadilishe hilo neno,ni sahihi na limekaa vema,usiwaendekeze umetoa hoja za msingi zimewaingia na wamekosa hoja wanajaribu kutaka kukosoa kitu ambacho sio hoja msingi.Wao ndio watumia wanaoongoza kwa lugha mbaya na chafu.Na hao jamaa zao wa cdm wanawaona kama malaika wasiokosea,kiasi unapoweka mapungufu yao huwa huweleweki.Wengi ni watoto na wamelelewa kwa kukaririshwa,hawajafunzwa kushindanishwa hoja mbadala
Sijui mwenzangu unalielewaje neno KUPOTOKA!

Lakini kwa vile hapa sio mashindano ya semantics, naomba upendekeze neno ambalo litakufurahisha wewe pamoja na wengine waliolichukulia negatively hilo neno.

Nami nitarekebisha title ya uzi huu.
 
Mh. Mnyika siku zote nimekua namuona ni mbunge makini sana na anayejishughulisha kujua mambo.

Lakini kwa hili la kutaka sheria ipitiwe upya na kurudisha mafao ya kujitoa naona amepotoka sana. Nashawishika kuamini kuwa nayeye kwenye hili ameingia kwenye mkumbo wa kusaka cheap popularity kwenye mambo ya kitaalamu zaidi. Najua nitashambuliwa kwa mtizamo huu ila nieleze sababu za mtizamo huu wangu.

Kwanza, katika nchi zote za Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara, hakuna kitu kinaitwa mafao ya kujitoa kwa mfuko wowote wa pensheni. Hiki kituko kipo hapa Tanzania tu na chanzo chake ni wanasiasa wa aina za mh. Mnyika wanaokua tayari kuweka maisha ya maelfu ya wazee wa miaka ijayo kwenye maisha ya dhiki na hivyo kufa mapema baada ya kustaafu kwa ajili ya umaarufu wao(wanasiasa) wa mpito......

Huku ndo tunakuita kufikiri ndani ya box...kufikiri kitu kilichopo hakiwezi kuundwa tofauti na kilivyoundwa au kilivyofikiriwa awali...kwa maneno mengine kufikiri kwa namna yako mkuu tunakuita conventional/traditional thinking...me naungana na mnyika na muunga mkono amewachagiza wanaofikiri ndani ya box kufikiri tofauti..kumbukeni hizi conventional theories za social security siyo biblia wala Quran kiasi cha practice kutobadilika..

Angalia na uchambue reasoning ya mheshimiwa mnyika siyo kuteteea traditional thinking, toa mapendekezo ya kuboresha thinking ya mnyika na siyo kutetea a conservative approach to doing business..namna yetu ya kufikiri ndo imeifanya sehemu hii ya dunia yaan Afrika kusini mwa jangwa la sahara kuendelea kuwa masikini licha ya utajiri wote tulionao....

Rejea zama za kuhurisha uchumi..afrika tulipoletewa proposal za kuhurisha chumi zetu na benki ya dunia na IMF(structural adjustment proposals) sisi tulichukuwa kama zilivyo yani tukazizoa kama dodoki na kuanza kuzitekeleza matokeo yake wote ni mashaidi.umaskini kuongezeka, ufisadi kuongezeka, kuuza kama siyo kugawa mashirika yetu ya umma, siasa za maji taka na zinazolinda mifumo ya wezi na mafisadi, kuongezeka kwa matabaka ya maskini na matajiri nk..

Wenzetu Asia na hasa kusini mashariki mwa Asia na Latini America walichukua zile proposal wakazichambua wakatekeleza yanayowafaa yasiyofaa wakaachana nayo hata pale benki ya dunia na IMF walipoonekana kuwashinikiza walisimamia kile walichoamini kina manufaa kwa nchi zao na kinarandana na mazingira ya nchi zao kwa wakati huo...leo hii sisi wa ndani ya boxi viongozi wetu wanaenda kutega mabakuri kuomba misaada katika nchi hizi hizi ..kumbuka baadhi ya nchi hizi zilikuwa maskini kama sisi na nyingine maskini zaidi yetu lakn leo wanaishi kwenye dunia tofauti.

Kwa taarifa yako nyingi ya nchi hizi hazina rasmali asili kama tulizonazo sisi huku ambazo nazo tumeanza kuzigawa bure...fuatilia historia za nchi kama China, Korea ya kusini, malaysia , singapore, india, philipines, thailand, brazil nk....toka nje ya box ichagize dunia badala ya dunia na maandiko ya enzi ya Adam smith kuendelea kukuchagiza wewe...dunia inaenda kwa kasi mwenzetu unaonekana umesimama unasubiri wenzio tutengeneze historia alafu wewe uandike tu.

Tafadhali shiriki nasi kutengeneza historia badala ya kusubiri kuandika..bila kuchallenge conventional wisdom tutauza hadi wajukuu zetu...kumbukeni sisi siyo kizazi cha mwisho hapa duniani kiasi cha kufanya yanayotuhusu sisi tu.we are responsible for the future generation too..nakuachia tafakuri moja tu as food of thought..."HEBU FIKIRIA MABABU ZETU WANGEFIKIRIA KUPANDA NYANYA TU KWA AJILI YA MATUMBO YAO JE HII MITI TUNAYOIONA IKIPENDENZESHA MAZINGIRA YETU INGEKUWEPO??..Alipata kusema mzee mmoja
 
Nadhani ile post humu kwamba mifuko inakaribia kufilisika ina ukweli. Kwanini mlione hili sasa wakati hii mifuko iko tangu enzi. Ina maana mlipoanzisha fao la kujitoa hamkuona taabu za uzeeni ndo mnaziona leo? Siku hizi ajira hasa binafsi hazitabiriki mtu anaweza fanya kazi miaka miwili mitatu wanakutema then unaniambia nisubiri uzeeni? Miduko hii inafilisika na wala siyo huruma kwe wazee wala nini.
chichiem walichotaka ma billion wakati wa kampeni ya 2010. kwani mmesahau wara hii au hamjuyajua haya?
 
Mnyika ange raise hii concern yake wakati hii sheria ikipitishwa. Nashangaa hakufanya hivyo. Sijui anataka ijadiliwe tena upya kwa mantiki ipi.

Naye pia tumweke kwenye hilo kundi la BENDERA FUATA UPEPO!!

lwani we hujui kuwa wale wa ndiyooo ndo hushinda mara zote?
 
Nadhani ieleweke wazi leo tunao wazee wangapi ambao kwa kuchukua mafao yao wanapata shida?

Nadhani pia wapo watu kwa sababu zao wamekuwa wakiaacha pesa zao katika mfuko akiwa na matumaini ya siku moja atafikia muda na sifa za kupokea mafao. Mh Mnyika ungeza kasi ya kukusanya maoni mtu aweze amua mwenyewe ama achukue au aache pesa zake mfukoni.

Hapa hoja ni uhuru wa ama kuchukua au kuaacha, kimsingi hiki kitendo cha lazima hatukitaki kabisa
 
Nimeacha kazi nikiwa na miaka 30 sina cha kufanya... Embu nisaidieni nitaishije hapo katikati mpaka nifike hiyo miaka 55 ya kuanza kupata hiyo pension? Hapa ukweli wa kwamba serikali imebadilisha mfumo sio kwa nia nzuri kama anavyojaribu kutoaminisha mtoa hoja upo wazi. Serikali inatumia hela hizo kwa kufanyia shughuli zingine. Wanachotaka hapa ni kukwepa usumbufu wa kuja kupungua hela endapo serikali itaendelea kuchota na wanamafao wataendelea kuchukua mafao yao. kwa hesabu za haraka itafika mahali mifuko itakuwa haina pesa. Hii mifuko ingekuwa na nia njema ingetoa elimu kwa umma kwanza badala ya kuvizia wananchi na kukimbilia kutunga sheria.
 
Nashukuru kwa majibu yako though hujajibu maeneo yote niliyopenda watanzania wapate majibu kwa mashaka ya fedha zao katika mashirika ya pendion.

Sheria hii unasema imejadiliwa April 2012 kwa nini haiku fanyiwa enough advocacy kwa wadau kabla ya kupelekwa bungeni kujadiliwa na kupitishwa? Vyama huru vya wafanyakazi vimekanusha kushirikishwa on behalf of employees. Lakini napata mashaka ya maelezo yako ktk hili, umesema pia kuwa katika sheria ya pension hapakuwepo clause ya withdrwal, je ipi ilijadiliwa April 12?

Act no 8 ya pension schemes iliyoiokoa PPF baada ya privatization ya parastotal organizations, sheria hii ilitangazwa sana na PPF kws sababu ilikuwa inawapa uhai wa kuishi wakati NSSF wakiipinga sababu ilikuwa inawanyima wanachama, kwa sababu walitegemea watumishi kutoka katika mashirika ya umma kuhamisha michango yao kwenda NSSF. Tunachojiuliza mbona hii haikufanyika kuelimisha wanachama mapema?

Katika mkutano wa mwaka 2006/2007 uliofanyika Golden Tulip organized by World Bank na ILO kutaka kutaka kuyaunganisha mashirika ya pension Tanzania baada ya kuwa utitiri wa mifuko yenye calculation tofauti, idea ya wafadhiri ktk mpango huu ni kutaka kuboresha pension system Tanzania, je hii imefikia wapi au imehujumiwa na mafisadi wansofadika na uwepo wa utitiri wa mifuko unaosababisha pension kuwa duni?

Katika majibu yako on investment policy esp on long term, the matching concept, ni sahihi, lakini je hizo fedha za wanachama mnazokopesha serikali za hazirudi kwa mujibu wa maelezo yako, je loan policy kwa govt inasemaje? Mnakopesha out of the policy or within the policy? Kama kuna loan policy je si wanakuwa na collateral ln the loan ambayo we can recover our money on default?
On the same, how do we project ufisadi and misuse of funds, is it part of our plans?
Nafurahi sana kuona watu kama wewe ambao kweli mnafahamu kilichopo na kinachoendelea kwenye mifuko ya pensheni.

Masuala mengine nashindwa kukupa majibu yake hapa directly cuz natumia mobile.
Labda niongelee machache, suala la kuunganishwa mifuko lilishadaliwa na serikali pamoja na wadau wakuu wa hii mifuko wakaona iendelee kuwepo mingi ili ushindani uwepo ambapo utababisha wanachama wapate huduma nzuri.

Investment policy za hii mifuko zimetoa muongozo ni kiasi gani kiwekezwe kwenye miradi ya serikani. Na ukiangalia muongozo mpya wa uwekezaji uliotolewa na SSRA hili suala limeelezwa vizuri sana. Na kunampango wa kuwa na Fund managers na custodians ambao watahusika na masuala ya investments za mifuko na itabidi wacomply na SSRA investment policy. Kwa hilo la uwekezaji lisikutie shaka kabisa.

Kumbuka pia nia na madhumuni ya hii mifuko siyo kumaximize returns, haiendeshwi kibiashara. Kusaidia kwenye miradi ya kijamii kama wanavyofanya NSSF ni moja ya majukumu yao though ndio wanapata challenge ya faida kidogo/hasara kwenye uwekezaji wa aina hiyo.

Madeni mengi ambayo serikali imeshindwa kuilipa hii ni mifuko ni ile ya michango ya nyuma ya wafanyakazi wake waliostaafu na kulipwa na hii mifuko, ambapo serikali ilikuwa haijapeleka michango yao. Serikali inajitahidi kuyalipa ila ulipaji wake ni wa kusua sua sana.

Kwa suala la collateral, kumbuka serikali kwenye kuikopesha huwa tunasema ni risk free loans. Huitaji kuidai serikali collateral yoyote as guarantee ya kulipwa ni 100%. Kitakachotokea ni kucheleweshewa tu marejesho yako lakini uhakika wa kulipwa upo.

Mwisho, mkuu kuwa na imani na mifiko yako na waliopewa dhamana kuiongoza. Kumbuka kuwa hesabu za mifuko zinaandaliwa kwa kucomply IFRS na zinaguliwa na external auditors, kamati za bunge na CAG pia. Kungekuwa na ufisadi wowote lazima ungeonekana. Chamuhimu ni wewe mwanachama kuwapa support, wakikuambia withdraw inaharibu mipango yao, wewe usipingane nao cuz wanakuandalia mambo mazuri baadaye.
 
Nawashanga sana wanaouliza Mnyika alikuwa wapi siku hiyo sheria ikipitishwa. Nani asiyejua kuwa bunge la tz hoja hupita kwa wingi wa wabunge na siyo uzito wa hoja. Pia hata kama alikuwepo hakuona kosa akaliona baadae asihoji?
 
Kwa upande wako sishangai sababu hoja ameileta 'MNYIKA' ingekuwa imetolewa na mtu kutoka ule upande mwingine ungeshawishika kuipima hoja,lakini kwa sababu hoja imeletwa na flani basi!
Nikuulize,
Wewe hii sheria wakati inapitishwa bungeni uliiona? Waweza kunitajia kifungu kilichoipitisha hii sheria?

Kukusaidia tu, Sheria inapotungwa kunaweza kukawa na "supporting regulations" ambazo si lazima zipite bungeni, ndio uhuni uliofanyika hapa!!

So hata kama Mnyika (usisahau na wabunge wako wa Magamba pia) walikuwepo, basi serikali iliwapiga "chenga ya mwili"
Mkuu mmeshaambiwa kuwa hamna sheria ya mfuko wowote inayoongelea hilo fao la withdrawal. SSRA walichofanya ni kama reglator ni kulipiga stop tu!

Mnyika kakosea kuingilia kitu asichokifahamu kwa ajili ya kujipatia umaarufu wa kisiasa. Asione wengine waliokaa kimya kuwa ni wajinga.
 
wewe ndiye uliyepotoka! ungetuambia wastaafu wa watz ambao wamenufaika na mifuko! usitoe mifano na wazungu wenzetu wako smart siyo sisi " mchwa kila kona" ushawahi kusikia waziri mkuu na mfanya biashara(manji) walifanya nini! wewe ndiye unayetafuta cheap popularity jf
 
Acha kujitoa ufahamu kwa ajili ya kutetea mafisadi na matumbo yenu,report ya CAG imesema live hii mifuko ipo mbioni kufilisika na fedha za wanachama kupotea,mbona unapotosha umma? Wewe ndio CAG?
Elewa mantiki ya CAG kuliongelea hili na siyo kukurupuka tu. Alichokiongelea ni mifuko inaweza kufilisika kama serikali haitalipa deni inayodaiwa na hii mifuko. Kumbuka guarantee ya mikopo ya serikali ni 100% kulipwa, so kwa hili wanachama hawatakiwi kuwa na wasiwasi wowote
 
Mkuu mimi nitajadili hayo niliyoweka red.
Mkuu upo nchi gani? nakuuliza hivyo kwa sababu pengine hujui au labda unapotosha kwa makusudi kabisa.
Mfanyakazi hukatwa 10% ya mshahara wake na mwajiri wake hukatwa 10% ya huo mshahara ukipiga mahesabu jumla ya mchango wa mwajiriwa(jumlisha na ule anotoa mwajiri) ni 20% ya mshara wake wa kila mwezi na sio 5% kama ulivyosema.
Pili hiyo michango mwajiriwa ambayo anakuja kuchukua(fao la kujitoa) ni malimbikizo ya kipindi chote alichokuwa akifanya kazi so unavyojaribu kulinganisha malimbikizo na mshahara wa mwezi mmoja kunakuwa hakuna uwiano wowote.

pili ningependa kukuelimisha jambo moja.
Pensheni ni kitu tofauti kabisa na fao lakujitoa.
Kwa Serikali makini hutoa pensheni kwa wazee bila hata kujali kama (huyo mzee) katika ujana alaiajiriwa au la.
Pension inatakiwa iwe ni grant kwa mwananchi mzee.
Fao la kujitoa ni pesa za mwajiriwa ambazo alikuwa akizihifadhi ili zimsaidie kuendesha maisha yake pindi ambapo hatokuwa na ajira tena.(iwe ni kwa kuacha, kufukuzwa kazi au kutokuwa na nguvu za kufanya kazi tena)

aksante sana kwa kumuelimisha huu ndugu yetu nafikiri kuna vitu alikuwa anavichanganya
 
Lakini huenda kuna agenda ya siri ambayo imeingizwa au inaingizwa toka 2004 ilijadiliwa kwa mara ya kwanza Bungeni na wadau wako tayari kuitetea au wadau wengine wapo tayari kuipinga.Mifuko ya hifadhi ya jamii ipo tangu na tangu na uchangiaji wake ni tofauti kati ya mfuko na mfuko,wengine 5 asilimia na wengine 10 asilimia.Kwa hiyo wachangiaji wote wapo sawa ikizingatiwa ni wanachama wa mfuko gani.
Jambo la msingi tuelewe kuna wenzetu toka sekta isiyo rasmi katika ajira hasa watumishi wa Migodi(Mfano Geita na kwingineko).Wao huchangia katika moja ya mifuko na hawana guarantee ya kufanya kazi hadi miaka 55 au 60.Sasa mtu huyu akijitoa,akifukuzwa,akiacha aau kufa kabla ya muda wake wa 55 au 60,hapa ndipo palipo na utata wa kupata maslahi yake/mwajiri wake kabla ya umri tajwa.Kwa hili ndipo Mh.Mnyika anaposimamia ili ikiwezekana sheria ibadirishwe(Nilivyoelewa mimi).
Lakini kuna uwezekano wa mifuko hii ya jamii imefilisika au itafilisika muda si mrefu na ndio chanzo cha kuongeza umri wa kustaafu kutoka 40 hiari au 45 lazima kwa Askari polisi hadi 50 kwa askari asiye na cheo yaani private,na 55 hadi 60 kwa afisa ili kufidia/kupunguza tatizo.Ingawa masharti ya penshen ni kutunzwa hadi kifo.Sasa mtu akistaafu 60 yrs ni ngumu kuishi miaka 20 zaidi.Kwanza unakuta amefanya kazi kwa miaka karibu 40 mfururizo na kubadiri hali ya utumishi hadi maisha ya kijijini vya Tanzania ni rahisi kufa kwa BP,STROKE,Kisukari au maradhi yatokanayo na umri na kuacha mafao yake.Ambapo mkataba utasimama kuwa mdau ameshafariki.
Halafu utaratibu wa kujitoa ulikuwepo toka zamani,sasa ukiona watu wanapiga makelele basi ujue kuna tatizo,suala sheria yetu ni tofauti na nchi za saddc haituhusu.sheria ni ya watanzania kwa manufaa ya watanzania bila kujali wengine wanasheria gani.Mimi kwa mtazamo wangu Mh.Mnyika yuko sawa ila amekosea namna ya kuwasilisha hoja kwa kuanza na sahini za kubadirisha mswada kabla ya kuonana wataalamu.
 
Mkuu mmeshaambiwa kuwa hamna sheria ya mfuko wowote inayoongelea hilo fao la withdrawal. SSRA walichofanya ni kama reglator ni kulipiga stop tu!

Mnyika kakosea kuingilia kitu asichokifahamu kwa ajili ya kujipatia umaarufu wa kisiasa. Asione wengine waliokaa kimya kuwa ni wajinga.

hivi hii tabia ya kusema mh.flani anatafuta umaarufu imetoka wapi?mbunge anafanya kazi yake ya kuwawakilisha wananchi kwa kuwasemea pale bungeni sasa akisema utasikiwa watu wanasema anatafuta umaarufu huyo akikaa kimya utasikia mbinge tuliyomchagua ni bubu anasubiri kupiga makofi sasa which is which? Mi nafikiri si vizuri kutumia kauli hii hata kama kakosea.wabunge wanaotafuta umaarufu hawana hoja siku zote ni kama nchemba,lusinde na komba wao kuropoka tu na kuomba muongozo usio na tija ilimradi aonekane yupo bungeni
 
Mh. Mnyika siku zote nimekua namuona ni mbunge makini sana na anayejishughulisha kujua mambo.

Lakini kwa hili la kutaka sheria ipitiwe upya na kurudisha mafao ya kujitoa naona amepotoka sana. Nashawishika kuamini kuwa nayeye kwenye hili ameingia kwenye mkumbo wa kusaka cheap popularity kwenye mambo ya kitaalamu zaidi. Najua nitashambuliwa kwa mtizamo huu ila nieleze sababu za mtizamo huu wangu.

Kwanza, katika nchi zote za Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara, hakuna kitu kinaitwa mafao ya kujitoa kwa mfuko wowote wa pensheni. Hiki kituko kipo hapa Tanzania tu na chanzo chake ni wanasiasa wa aina za mh. Mnyika wanaokua tayari kuweka maisha ya maelfu ya wazee wa miaka ijayo kwenye maisha ya dhiki na hivyo kufa mapema baada ya kustaafu kwa ajili ya umaarufu wao(wanasiasa) wa mpito.

Pili, ukiondoa PPF na NSSF, Tanzania ina mifuko mingine pia, nayo ni LAPF, PSPF na ZSSF, huko kote hakuna hilo fao la kujitoa na halikuwahi kutolewa. Mtu ukiacha kazi hata baada ya miaka 15 ukapata kazi kwenye private sector, utatakiwa kurudi kwa ajili ya mafao yako pale tu umri wako utakapofika miaka 55 au 60.

Tatu hili jambo la kutumia "ujinga" wa watu(nikimaanisha kutojua sekta hii vizuri) ili kujitengezea umaarufu wa mpito ndio jambo ambalo kizazi hiki kilianza kuonekana kuchoshwa nacho, lakini Mh. Mnyika anaonekana kurudia kosa lilelile la kutumia "ujinga" wa watu kujinufaisha. Kumwambia mtu ajitoe at 46yrs ni kumhakikishia uzee usiokua na uhakika wa staha. Mheshmiwa hebu pita BRELLA wakupe data za biashara zinazofunguliwa kwa mwaka, halafuna baada ya miaka mitano asilimia ngapi ya hizo biashara bado zinakuwepo sokoni. Nakuhakikishia utaweza kuanguka kwa mshtuko! Kuna data inaongelea 67% ya biashara mpya zitapotea sokoni ndani ya miaka mitano. Hivyo kusema watu watajifungulia biashara ni wishful thinking ambazo kila mtu yupo entitled kuwa nazo, ila we need a reality check hapa. Huwezi kuwa mwajiriwa miaka nenda rudi halafu siku ukapewa bulungutu, bila kuwa na basic entrepreneurial skills ukategema kusurvive sokoni.

Nne, hii hadithi ya kupotosha ya Life Expectancy ya mtanzania ni miaka 53. Ni kweli Life expectancy ni miaka 53, ila ukokotaoji wake unapatikana kwa average ya vifo vyote nchini kwa mwaka. sasa kwa nchi kama yetu ambapo kuna vifo vingi sana vya watoto chini ya umri wa miaka mitano, si ajabu vikashusha life expectancy at birth. Lakini kama life expectancy ingetazamwa wakati wa umri wa kuanza kazi, say 20yrs, utakuta watanzania wengi wanafika miaka 65 na kuendelea... Hivyo si sahihi kusema watu wanakufa at 53 halafu mafao yatatolewa at 55yrs( hapa naona kuna gap kubwa mno ya uelewa wa hii concept).

Hivi mh. Mnyika anajua kuwa kwa kung'ang'ania kurudishwa kwa mafao ya kujitoa ni kuwaumiza wafanyakazi kuliko kama wangesubiri pensheni? Chukulia mfano, mtu aliyeanza kazi na miaka 25, akatumika kwa miaka 20. Atakuja kulipwa mafao ya kujitoa kwa kutizama kilichopo kwenye account yake kama kilivyo!!!... inawezekana kabisa huyu mtu kipato chake kilipanda sana ndani ya miaka mitano ya mwisho kutokana na experience, lakini kitakacholipwa ni kilichopo kwenye account yake kama kilivyo. Hapa utakuta kuna miaka ile 15 ya mishahara midogo akiwa bado junior officer ndio atakayojumlishiwa kama ilivyo na hii miaka mitano ya mishahara mikubwa. Wakati kama angekuwa ni wa kupokea pensheni angelipwa kufuatana na mishahara yake ya miaka ya mwisho kabla hajastaafu, ambayo mara nyingi ndiyo mikubwazaidi katika career ya mtu. Sijui mheshmiwa unalisemeaje hili...

Ukiwa kijana na nguvu zako, siku zote unaona kama kuwa mzee na kikongwe ni kitu cha mbali sana na kwamba unaweza kujipanga vizuri ili usizeeke kwa dhiki. Lakini ni muhimu tujiulize mh. Mnyika, kama ukiwa na nguvu na mshahara wako unachukuliwa asilimia 5% kwa ajili ya akiba ya uzeeni. Kwanini basi ushindwe kujipangilia maisha kwa hiyo asilimia 95% unayobakiwa nayo? Jamani tusipende cheap popularity, tuwawaingiza watanzania wenzetu kwenye dimbwi la dhiki wakati wa uzee, ambapo hata nguvu za kujishughulisha zimekwisha.

Hivyo ni vyema Mh. Ukakaa na wataalam wa kwenye hii mifuko, na hasa wataalamu wenye kufanya tathmini za mifuko ya pensheni na ujue kiundani nini hasa maana ya mifuko ya pensheni. Malengo na madhumuni yake. Ni vizuri na huwa nafarijika sana ninapoona mwanasiasa kijana akijishughulisha kutaka kujua mambo yanayokua ya kitaalam kwa kukaa na kujifunza kwa wataalam badala ya kuzunguka kusaka saini za wanasiasa wenzake ili kurudisha nyuma juhudi za muda mrefu za wataalam, wenye nia safi ya kuweka safety net kwa ajili ya wazee wa kitanzania na vizazi vyao.

Mimi nafkiri, badala ya kutaka kifungu cha mafao ya kujitoa kirudishwe na hivyo kujihakikishia kuona vurugu za wazee mitaani kama wale wa jumuiya ya afrika mashariki siku za usoni. Ni bora tukaacha sheria ibaki kama ilivyo(kwa maana ya kuzuia mafao ya kujitoa) ILA iongeze kifungu kitakachomtaka mwajiri awe na scheme ya kuchangia wafanyakazi ambayo ni over and above the basic pension scheme, ambayo mtu ataweza kuacess fedha zake pale atakapoacha kazi.

Bottom Line, pensheni ni muhimu muhimu sana... Kila siku ukienda kwenye fukwe za Zanzibar utakuta vizee vya kizungu vimejazana vinakula maisha. Na hii siyo rocket science. wenzetu waliona mbali, wakaamua kwa makusudi kufuta mafao ya kujitoa kama bado una nguvu zako. Ili unapozeeka uzeeke kwa heshma!

Niishie hapo, naomba tujadili bila matusi.

You are not yet sober...have some soup and plenty of water..see you when you are done
 
At least we're informed of what is happening behind the scene(NSSF,PPF and others),please wanachama hatuhitaji issue za kudanganywa,tunajua fedha zetu zinatumiwa na akina nani...tuacheni na fedha zetu,we know exactly malengo ya SSRA tuacheni! kama kuna watu mna uelewa mzuri mbona hamkuelimisha watu mapema,wazee wetu wakistaafu huwa wananyanyaswa kuzipata pension zao utadhani wanaomba kukopeshwa! Ifike mahali tuseme basi yatosha,let our future be at our own hands,tena hatutaki mifano ya ajabu ya huko nchi za wenzetu,kwani kuna factors nyingi tunatofautiana,Say no to propaganda and mob psychology!
 
Mkuu nakupongeza kwa kuchambua kitaalam, huu ndo ukweli, sema siku hizi kupinga kila kitu imekuwa ndo style yetu.

Ni mazoea tu, watu akibadilisha walichokizoea hata kama ni kwa faida yao watakuwa wagumu tu.

Hawa kina Mnyika wanakurupuka tu, si unakumbuka hata ile ya nauli ya feri wao ni kupinga tu bora wapate attention ya watu.
 
Kuna wachangiaji wanasema Mnyika alishindwa kuzuia mswada usiwe sheria kwa sababu wabunge wa wapinzani ni wachache. Swali, je sasa hivi anavyopeleka hoja bungeni wabunge wa upinzani wameshakuwa wengi kuliko wa CCM?
 
Mnyika anawakililisha mawazo yake na pia ya kundi kubwa la wafanyakazi wa mshahara wa kima cha chini na ambao hawana hakika ya ajira za kudumu. Hivi mnawafikiria wale wanaofanya kazi ya manamba kwa wahindi?
Mfano, I was working with certain institution ya wahindi kwa contract ya miaka 2, na nilikuwa nachangia NSSF, baada ya mwaka 1, nimepata kazi kwa govt, nachangia LAPF. sasa is it fair kuniambia nisubiri mpaka miaka 30 ijayo nikachukue 4M NSSF? waangalie sera zao. ni kweli mpo wataalam, lakin sisi wengine sio majuha wa kushindwa kufanya simple analysis. Ni wizi huo, mbona hamgusii maelelezo ya CAG kuhusiana na afya ya hiyo mifuko? Na kwanini hilo fao litolewe sasa na si enzi za Mkapa au Mwinyi. Ninyi wataalam hamkuwepo?
 
Back
Top Bottom