Sober
JF-Expert Member
- Jun 6, 2008
- 289
- 52
Mh. Mnyika siku zote nimekua namuona ni mbunge makini sana na anayejishughulisha kujua mambo.
Lakini kwa hili la kutaka sheria ipitiwe upya na kurudisha mafao ya kujitoa naona amepotoka sana. Nashawishika kuamini kuwa nayeye kwenye hili ameingia kwenye mkumbo wa kusaka cheap popularity kwenye mambo ya kitaalamu zaidi. Najua nitashambuliwa kwa mtizamo huu ila nieleze sababu za mtizamo huu wangu.
Kwanza, katika nchi zote za Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara, hakuna kitu kinaitwa mafao ya kujitoa kwa mfuko wowote wa pensheni. Hiki kituko kipo hapa Tanzania tu na chanzo chake ni wanasiasa wa aina za mh. Mnyika wanaokua tayari kuweka maisha ya maelfu ya wazee wa miaka ijayo kwenye maisha ya dhiki na hivyo kufa mapema baada ya kustaafu kwa ajili ya umaarufu wao(wanasiasa) wa mpito.
Pili, ukiondoa PPF na NSSF, Tanzania ina mifuko mingine pia, nayo ni LAPF, PSPF na ZSSF, huko kote hakuna hilo fao la kujitoa na halikuwahi kutolewa. Mtu ukiacha kazi hata baada ya miaka 15 ukapata kazi kwenye private sector, utatakiwa kurudi kwa ajili ya mafao yako pale tu umri wako utakapofika miaka 55 au 60.
Tatu hili jambo la kutumia "ujinga" wa watu(nikimaanisha kutojua sekta hii vizuri) ili kujitengezea umaarufu wa mpito ndio jambo ambalo kizazi hiki kilianza kuonekana kuchoshwa nacho, lakini Mh. Mnyika anaonekana kurudia kosa lilelile la kutumia "ujinga" wa watu kujinufaisha. Kumwambia mtu ajitoe at 46yrs ni kumhakikishia uzee usiokua na uhakika wa staha. Mheshmiwa hebu pita BRELLA wakupe data za biashara zinazofunguliwa kwa mwaka, halafuna baada ya miaka mitano asilimia ngapi ya hizo biashara bado zinakuwepo sokoni. Nakuhakikishia utaweza kuanguka kwa mshtuko! Kuna data inaongelea 67% ya biashara mpya zitapotea sokoni ndani ya miaka mitano. Hivyo kusema watu watajifungulia biashara ni wishful thinking ambazo kila mtu yupo entitled kuwa nazo, ila we need a reality check hapa. Huwezi kuwa mwajiriwa miaka nenda rudi halafu siku ukapewa bulungutu, bila kuwa na basic entrepreneurial skills ukategema kusurvive sokoni.
Nne, hii hadithi ya kupotosha ya Life Expectancy ya mtanzania ni miaka 53. Ni kweli Life expectancy ni miaka 53, ila ukokotaoji wake unapatikana kwa average ya vifo vyote nchini kwa mwaka. sasa kwa nchi kama yetu ambapo kuna vifo vingi sana vya watoto chini ya umri wa miaka mitano, si ajabu vikashusha life expectancy at birth. Lakini kama life expectancy ingetazamwa wakati wa umri wa kuanza kazi, say 20yrs, utakuta watanzania wengi wanafika miaka 65 na kuendelea... Hivyo si sahihi kusema watu wanakufa at 53 halafu mafao yatatolewa at 55yrs( hapa naona kuna gap kubwa mno ya uelewa wa hii concept).
Hivi mh. Mnyika anajua kuwa kwa kung'ang'ania kurudishwa kwa mafao ya kujitoa ni kuwaumiza wafanyakazi kuliko kama wangesubiri pensheni? Chukulia mfano, mtu aliyeanza kazi na miaka 25, akatumika kwa miaka 20. Atakuja kulipwa mafao ya kujitoa kwa kutizama kilichopo kwenye account yake kama kilivyo!!!... inawezekana kabisa huyu mtu kipato chake kilipanda sana ndani ya miaka mitano ya mwisho kutokana na experience, lakini kitakacholipwa ni kilichopo kwenye account yake kama kilivyo. Hapa utakuta kuna miaka ile 15 ya mishahara midogo akiwa bado junior officer ndio atakayojumlishiwa kama ilivyo na hii miaka mitano ya mishahara mikubwa. Wakati kama angekuwa ni wa kupokea pensheni angelipwa kufuatana na mishahara yake ya miaka ya mwisho kabla hajastaafu, ambayo mara nyingi ndiyo mikubwazaidi katika career ya mtu. Sijui mheshmiwa unalisemeaje hili...
Ukiwa kijana na nguvu zako, siku zote unaona kama kuwa mzee na kikongwe ni kitu cha mbali sana na kwamba unaweza kujipanga vizuri ili usizeeke kwa dhiki. Lakini ni muhimu tujiulize mh. Mnyika, kama ukiwa na nguvu na mshahara wako unachukuliwa asilimia 5% kwa ajili ya akiba ya uzeeni. Kwanini basi ushindwe kujipangilia maisha kwa hiyo asilimia 95% unayobakiwa nayo? Jamani tusipende cheap popularity, tuwawaingiza watanzania wenzetu kwenye dimbwi la dhiki wakati wa uzee, ambapo hata nguvu za kujishughulisha zimekwisha.
Hivyo ni vyema Mh. Ukakaa na wataalam wa kwenye hii mifuko, na hasa wataalamu wenye kufanya tathmini za mifuko ya pensheni na ujue kiundani nini hasa maana ya mifuko ya pensheni. Malengo na madhumuni yake. Ni vizuri na huwa nafarijika sana ninapoona mwanasiasa kijana akijishughulisha kutaka kujua mambo yanayokua ya kitaalam kwa kukaa na kujifunza kwa wataalam badala ya kuzunguka kusaka saini za wanasiasa wenzake ili kurudisha nyuma juhudi za muda mrefu za wataalam, wenye nia safi ya kuweka safety net kwa ajili ya wazee wa kitanzania na vizazi vyao.
Mimi nafkiri, badala ya kutaka kifungu cha mafao ya kujitoa kirudishwe na hivyo kujihakikishia kuona vurugu za wazee mitaani kama wale wa jumuiya ya afrika mashariki siku za usoni. Ni bora tukaacha sheria ibaki kama ilivyo(kwa maana ya kuzuia mafao ya kujitoa) ILA iongeze kifungu kitakachomtaka mwajiri awe na scheme ya kuchangia wafanyakazi ambayo ni over and above the basic pension scheme, ambayo mtu ataweza kuacess fedha zake pale atakapoacha kazi.
Bottom Line, pensheni ni muhimu muhimu sana... Kila siku ukienda kwenye fukwe za Zanzibar utakuta vizee vya kizungu vimejazana vinakula maisha. Na hii siyo rocket science. wenzetu waliona mbali, wakaamua kwa makusudi kufuta mafao ya kujitoa kama bado una nguvu zako. Ili unapozeeka uzeeke kwa heshma!
Niishie hapo, naomba tujadili bila matusi.
Lakini kwa hili la kutaka sheria ipitiwe upya na kurudisha mafao ya kujitoa naona amepotoka sana. Nashawishika kuamini kuwa nayeye kwenye hili ameingia kwenye mkumbo wa kusaka cheap popularity kwenye mambo ya kitaalamu zaidi. Najua nitashambuliwa kwa mtizamo huu ila nieleze sababu za mtizamo huu wangu.
Kwanza, katika nchi zote za Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara, hakuna kitu kinaitwa mafao ya kujitoa kwa mfuko wowote wa pensheni. Hiki kituko kipo hapa Tanzania tu na chanzo chake ni wanasiasa wa aina za mh. Mnyika wanaokua tayari kuweka maisha ya maelfu ya wazee wa miaka ijayo kwenye maisha ya dhiki na hivyo kufa mapema baada ya kustaafu kwa ajili ya umaarufu wao(wanasiasa) wa mpito.
Pili, ukiondoa PPF na NSSF, Tanzania ina mifuko mingine pia, nayo ni LAPF, PSPF na ZSSF, huko kote hakuna hilo fao la kujitoa na halikuwahi kutolewa. Mtu ukiacha kazi hata baada ya miaka 15 ukapata kazi kwenye private sector, utatakiwa kurudi kwa ajili ya mafao yako pale tu umri wako utakapofika miaka 55 au 60.
Tatu hili jambo la kutumia "ujinga" wa watu(nikimaanisha kutojua sekta hii vizuri) ili kujitengezea umaarufu wa mpito ndio jambo ambalo kizazi hiki kilianza kuonekana kuchoshwa nacho, lakini Mh. Mnyika anaonekana kurudia kosa lilelile la kutumia "ujinga" wa watu kujinufaisha. Kumwambia mtu ajitoe at 46yrs ni kumhakikishia uzee usiokua na uhakika wa staha. Mheshmiwa hebu pita BRELLA wakupe data za biashara zinazofunguliwa kwa mwaka, halafuna baada ya miaka mitano asilimia ngapi ya hizo biashara bado zinakuwepo sokoni. Nakuhakikishia utaweza kuanguka kwa mshtuko! Kuna data inaongelea 67% ya biashara mpya zitapotea sokoni ndani ya miaka mitano. Hivyo kusema watu watajifungulia biashara ni wishful thinking ambazo kila mtu yupo entitled kuwa nazo, ila we need a reality check hapa. Huwezi kuwa mwajiriwa miaka nenda rudi halafu siku ukapewa bulungutu, bila kuwa na basic entrepreneurial skills ukategema kusurvive sokoni.
Nne, hii hadithi ya kupotosha ya Life Expectancy ya mtanzania ni miaka 53. Ni kweli Life expectancy ni miaka 53, ila ukokotaoji wake unapatikana kwa average ya vifo vyote nchini kwa mwaka. sasa kwa nchi kama yetu ambapo kuna vifo vingi sana vya watoto chini ya umri wa miaka mitano, si ajabu vikashusha life expectancy at birth. Lakini kama life expectancy ingetazamwa wakati wa umri wa kuanza kazi, say 20yrs, utakuta watanzania wengi wanafika miaka 65 na kuendelea... Hivyo si sahihi kusema watu wanakufa at 53 halafu mafao yatatolewa at 55yrs( hapa naona kuna gap kubwa mno ya uelewa wa hii concept).
Hivi mh. Mnyika anajua kuwa kwa kung'ang'ania kurudishwa kwa mafao ya kujitoa ni kuwaumiza wafanyakazi kuliko kama wangesubiri pensheni? Chukulia mfano, mtu aliyeanza kazi na miaka 25, akatumika kwa miaka 20. Atakuja kulipwa mafao ya kujitoa kwa kutizama kilichopo kwenye account yake kama kilivyo!!!... inawezekana kabisa huyu mtu kipato chake kilipanda sana ndani ya miaka mitano ya mwisho kutokana na experience, lakini kitakacholipwa ni kilichopo kwenye account yake kama kilivyo. Hapa utakuta kuna miaka ile 15 ya mishahara midogo akiwa bado junior officer ndio atakayojumlishiwa kama ilivyo na hii miaka mitano ya mishahara mikubwa. Wakati kama angekuwa ni wa kupokea pensheni angelipwa kufuatana na mishahara yake ya miaka ya mwisho kabla hajastaafu, ambayo mara nyingi ndiyo mikubwazaidi katika career ya mtu. Sijui mheshmiwa unalisemeaje hili...
Ukiwa kijana na nguvu zako, siku zote unaona kama kuwa mzee na kikongwe ni kitu cha mbali sana na kwamba unaweza kujipanga vizuri ili usizeeke kwa dhiki. Lakini ni muhimu tujiulize mh. Mnyika, kama ukiwa na nguvu na mshahara wako unachukuliwa asilimia 5% kwa ajili ya akiba ya uzeeni. Kwanini basi ushindwe kujipangilia maisha kwa hiyo asilimia 95% unayobakiwa nayo? Jamani tusipende cheap popularity, tuwawaingiza watanzania wenzetu kwenye dimbwi la dhiki wakati wa uzee, ambapo hata nguvu za kujishughulisha zimekwisha.
Hivyo ni vyema Mh. Ukakaa na wataalam wa kwenye hii mifuko, na hasa wataalamu wenye kufanya tathmini za mifuko ya pensheni na ujue kiundani nini hasa maana ya mifuko ya pensheni. Malengo na madhumuni yake. Ni vizuri na huwa nafarijika sana ninapoona mwanasiasa kijana akijishughulisha kutaka kujua mambo yanayokua ya kitaalam kwa kukaa na kujifunza kwa wataalam badala ya kuzunguka kusaka saini za wanasiasa wenzake ili kurudisha nyuma juhudi za muda mrefu za wataalam, wenye nia safi ya kuweka safety net kwa ajili ya wazee wa kitanzania na vizazi vyao.
Mimi nafkiri, badala ya kutaka kifungu cha mafao ya kujitoa kirudishwe na hivyo kujihakikishia kuona vurugu za wazee mitaani kama wale wa jumuiya ya afrika mashariki siku za usoni. Ni bora tukaacha sheria ibaki kama ilivyo(kwa maana ya kuzuia mafao ya kujitoa) ILA iongeze kifungu kitakachomtaka mwajiri awe na scheme ya kuchangia wafanyakazi ambayo ni over and above the basic pension scheme, ambayo mtu ataweza kuacess fedha zake pale atakapoacha kazi.
Bottom Line, pensheni ni muhimu muhimu sana... Kila siku ukienda kwenye fukwe za Zanzibar utakuta vizee vya kizungu vimejazana vinakula maisha. Na hii siyo rocket science. wenzetu waliona mbali, wakaamua kwa makusudi kufuta mafao ya kujitoa kama bado una nguvu zako. Ili unapozeeka uzeeke kwa heshma!
Niishie hapo, naomba tujadili bila matusi.