Mwanaukweli
JF-Expert Member
- May 18, 2007
- 4,786
- 1,710
Siku ya Alhamisi tarehe 23/7/2009, Mbunge wa Singida Kusini Mh. Mohamed Misanga (CCM) aliahidi kuwasilisha hoja binafsi ya kuundwa tume huru ya Bunge kuchunguza Baraza la Mitihani na Katibu wake mtendaji. Mara moja ilionekana hata katika wabunge kuna kutofautiana katika azma yake hiyo.
Iwapo kweli Mh. Missanga anakerwa na utendaji mbaya, basi hatua yake ni ya kizalendo na inalenga kuboresha utendaji wa Taasisi hiyo nyeti. Lakini nahoji mambo kadhaa.
Kwanza nafahamu kuwa mmoja wa Maafisa waliohamishwa ni Mkwe wa Mh. Missanga, yaani ni mume wa binti yake. Hapa napata mashaka kama kweli Mh. Missanga anatumia nafasi hii kwa kutetea ndugu yake binafsi katika wadhifa wake kama mbunge au kweli anakerwa na utendaji mbaya.
Hivi Mh. Missanga kuhamishwa kutoka sehemu moja ya kazi kwenda nyingine ni jambo la ajabu??? Au kwa kuwa na mkwe yumo? Na je Dr. Ndalichako hana bodi inayosimamia kazi yake? Na anatoa maamuzi bila kushirikisha bodi?
Binafsi namfahamu Dr. Ndalichako tangu akiwa Lecturer UDSM (mwalimu wangu). Ana sifa zote za kuliongoza vema Baraza la Mitihani, na mpaka sasa anafanya vizuri. Mh. Missanga ukiweza kumhusisha yeye binafsi na ufisadi wa aina yoyote, utakuwa umeleta hoja inayoweza kutushawishi na sisi.
Nashawishika kusema kuwa kuna hujuma zinafanyika dhidi yake na watu ambao wanamchukia au kwa kuwa walihamishwa au kwa kuwa wanakwamishwa katika azma ya kufanikiwa bila jasho kwa kufutiwa mitihani, shule kufungiwa n.k. Because she is very strict and tough and does not buy in to any corrupt temptations. Prove me otherwise if you have evidence plz.
Wateja wa mitihani ivujayo si watu wanyonge, ni wenye pesa na wenye madaraka makubwa. Hawa wanaweza kutengeneza mazingira ya kumwondoa mtu yeyote aliye kikwazo katika kutimiza malengo yao, mtindo unaotumiwa na genge la MAFIA la ITALIA. Nashawishika kuwa Mh. Missanga umo mbioni katika kutimiza azma hiyo. All the best.
Wabunge na wengine kuweni macho na hoja ambazo zinaletwa kwa sababu za chuki binafsi.
Ni vema kujadili issues, na si kupersonalize issues.
Iwapo kweli Mh. Missanga anakerwa na utendaji mbaya, basi hatua yake ni ya kizalendo na inalenga kuboresha utendaji wa Taasisi hiyo nyeti. Lakini nahoji mambo kadhaa.
Kwanza nafahamu kuwa mmoja wa Maafisa waliohamishwa ni Mkwe wa Mh. Missanga, yaani ni mume wa binti yake. Hapa napata mashaka kama kweli Mh. Missanga anatumia nafasi hii kwa kutetea ndugu yake binafsi katika wadhifa wake kama mbunge au kweli anakerwa na utendaji mbaya.
Hivi Mh. Missanga kuhamishwa kutoka sehemu moja ya kazi kwenda nyingine ni jambo la ajabu??? Au kwa kuwa na mkwe yumo? Na je Dr. Ndalichako hana bodi inayosimamia kazi yake? Na anatoa maamuzi bila kushirikisha bodi?
Binafsi namfahamu Dr. Ndalichako tangu akiwa Lecturer UDSM (mwalimu wangu). Ana sifa zote za kuliongoza vema Baraza la Mitihani, na mpaka sasa anafanya vizuri. Mh. Missanga ukiweza kumhusisha yeye binafsi na ufisadi wa aina yoyote, utakuwa umeleta hoja inayoweza kutushawishi na sisi.
Nashawishika kusema kuwa kuna hujuma zinafanyika dhidi yake na watu ambao wanamchukia au kwa kuwa walihamishwa au kwa kuwa wanakwamishwa katika azma ya kufanikiwa bila jasho kwa kufutiwa mitihani, shule kufungiwa n.k. Because she is very strict and tough and does not buy in to any corrupt temptations. Prove me otherwise if you have evidence plz.
Wateja wa mitihani ivujayo si watu wanyonge, ni wenye pesa na wenye madaraka makubwa. Hawa wanaweza kutengeneza mazingira ya kumwondoa mtu yeyote aliye kikwazo katika kutimiza malengo yao, mtindo unaotumiwa na genge la MAFIA la ITALIA. Nashawishika kuwa Mh. Missanga umo mbioni katika kutimiza azma hiyo. All the best.
Wabunge na wengine kuweni macho na hoja ambazo zinaletwa kwa sababu za chuki binafsi.
Ni vema kujadili issues, na si kupersonalize issues.
Last edited: