Mwl.ngonyani
New Member
- Jun 26, 2011
- 4
- 0
Juzi asubuhi nikiwa nyumbani mke wangu alikuja nyumbani huku ameshika gazeti moja la kampuni maarufu kwa kuchapa magazeti ya udaku. Nilimwomba nilitazame(ingawa mimi sio msomaji wa magazeti ya aina hiyo).nilishangaa nilipokuta ukurasa mmoja watu wanatafuta wachumba huku wakiweka gazetini namba za simu za mikononi. Nilimuuliza mke wangu kuhusu hilo je ni sahihi? Hapo ulizuka mjadala wa muda kidogo kabla ya kuafikiana kuwa "hayo ni mambo ya utandawazi na ujana tu". Lakini jana alfajili niliamua kufanya utafiti niliandika kupitia mtandao huu kama natafuta mke ili nijionee huku nikiacha email adress niliyocreate jana hiyo hiyo. Huwezi amini nimekuta message 124. Duh!! Labla nikiri mapema kuwa sikumaliza kuzisoma, kabla ya mke wangu kunieleza kuwa tuwaulize wadau wanasemaje? Je mdau wa JF unaionaje hii!