Dr. Kikwete wakati anahutubia mkutano wa wawekezaji huko Kenya nilimsikia anazungumza Kiingereza chetu kile cha kuunga unga, alipopewa nafasi balozi wa Kenya nchini Tanzania yeye akaongea Kiswahili. Binafsi nimekuwa nashangaa inakuwaje viongozi wetu hawataki kukitukuza kiswahili? Nakumbuka wakati mmoja Mkapa kwenye mkutano wa AU alitoa hotuba kwa kiingereza (ingawa Mkapa kiingereza chake ni kile cha kwa Malkia hasa), lakini alipohutubia Joakimu Chisano akaongea kiswahili fasaha mkutano huohuo.
Wazo langu:
Kiingereza ni muhimu lakini Kiswahili nacho kina nafasi yake, hata kama tumeshindwa kuuza vizuri rasilimali kama madini na mbuga za wanyama, bado viongozi wetu wangelitilia umuhimu suala la lugha ya kiswahili bado tungeweza kuuza hiyo huduma kwa wale wanaoihitaji. Siwezi kushangaa kwa wale mlioko huko majuu kuwa walimu wa kiswahili huko ni kutoka Kenya au Ghana. Kama mkuu wa nchi bado fikra zimefungwa na ukoloni je anatuongoza anatupeleka wapi?
Wazo langu:
Kiingereza ni muhimu lakini Kiswahili nacho kina nafasi yake, hata kama tumeshindwa kuuza vizuri rasilimali kama madini na mbuga za wanyama, bado viongozi wetu wangelitilia umuhimu suala la lugha ya kiswahili bado tungeweza kuuza hiyo huduma kwa wale wanaoihitaji. Siwezi kushangaa kwa wale mlioko huko majuu kuwa walimu wa kiswahili huko ni kutoka Kenya au Ghana. Kama mkuu wa nchi bado fikra zimefungwa na ukoloni je anatuongoza anatupeleka wapi?