Mh. JK hatimaye akiri

Indume Yene

Platinum Member
Mar 17, 2008
2,950
711
Wakuu nimekutana na habari hii hapa kutoka kwenye gazeti la Tanzania Daima kama ifuatavyo:-


JK: Wanyonge wakikosa haki hakuna utawala wa sheria


na Halfani Lihundi, Arusha


RAIS Jakaya Kikwete, amesema hakuna nchi itakayojigamba inatekeleza utawala wa sheria, wakati wanyonge walio wengi, wanakosa haki kutokana na hali ngumu ya kiuchumi inayowakabili.
Rais Kikwete alisema hayo jana alipokuwa akifungua mkutano wa siku mbili wa majaji wanawake kutoka nchi 11 za Kiafrika ulioanza mjini hapa kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).
Alisema upatikanaji wa haki umekuwa na gharama kubwa, hivyo kusababisha maskini kushindwa kumudu gharama hizo.
Aliwataka majaji hao kujadili changamoto hizo na kupendekeza njia zinazoweza kutumika kukabiliana na mapungufu hayo, ili kila raia aweze kufaidi matunda ya upatikanaji wa haki katika nchi zao.
‘‘Hili ni suala ambalo majaji, watendaji wa mahakama na watoa haki lazima walichukulie kama changamoto na kisha kutupa mapendekezo ya namna bora ya kurekebisha hali hiyo,” alisemaRais Kikwete.
Rais Kikwete pia aliwataka majaji hao na mahakimu kuhakikisha utoaji wa haki unafanyika kwa njia ya haraka kutokana na matumanini waliyonayo wananchi wanapotafuta haki zao. Awali, Mwenyekiti wa Chama cha Majaji Wanawake Tanzania (TWJA), Jaji Eusebia Munuo, alisema mkutano huo wa kwanza kufanyika nchini, utazungumzia masuala ya haki za binadamu, haki za wanawake na watoto na unyanyasaji wa kijinsia pamoja na ukimwi na haki katika umiliki wa mali na biashara ya binadamu.

Nafikiri Mh. Rais alikuwa anazungumzia hali halisi barani Afrika Tanzania ikiwemo na ikiwa mwenyeji wa mkutano huo. Hakuna hasiyeelewa hali ngumu ya maisha inayowakabili watanzania kwa sasa. Maskini wameongezeka na waliokuwepo wameendelea kuwa maskini tena kwa kasi na ari mpya.

Leo mkuu wa nchi anapotoa kauli hii naamini alikuwa anakiri kuwa Tanzania hakuna utawala wa sheria kutokana na sababu ambazo ameweza kuzitambua kwa utambuzi wake. Kuna sababu zingine ambazo zinaweza kukuongoza kufikia conclusion kuwa Tanzania hakuna utawala wa sheria, mfano pale Bunge la JMT linapotoa miongozo kwa serikali na serikali inarudi kwa ngonjera bila kutekeleza miongozo hiyo huku zikifanywa mbinu za kumuondoa Spika wa Bunge kwa kuwa anaipelekesha serikali.

Lakini Mh. Rais kwa utambuzi wake kaona hilo kuwa kama wanyonge hawapati haki zao basi hakuna utawala wa sheria. Na ni kweli wanyonge wengi hapa Tanzania hawapati haki zao hata zile za msingi.

Mh. Rais nakushukuru kwa kutambua hili, sasa lililobaki ni nini kama hakuna utawala wa sheria???
1. Jilime memo wewe mwenyewe ni kwa nini husifukuzwe kazi kwa kushindwa kuwapa wanyonge haki zao.

2. Kwa nini husiadhibiwe kwa kuruhusu ufisadi kuendelea ndani ya serikali na chama chako.
3.
4.
5.
 
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425


clip_image002.jpg

PRESIDENT'S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewataka mahakimu Barani Afrika kulinda heshima yao kwa kutoa hukumu za haki, zenye kutimiza hisia za watu na na kuwaridhisha kuwa ni kweli haki inatendeka.

Rais Kikwete pia amesema kuwa uhuru wa majaji siyo haki binafsi ama heshima ya jaji, bali ni uhuru huo ni kwa ajili ya kulinda utawala wa sheria na kulinda wale ambao wanatafuta na wanatarajia kupata haki kutoka kwa majaji hao.

Aidha, Rais Kikwete amezitaka Mahakama kuangalia jinsi ya kupunguza gharama kubwa za kutafuta haki, ili haki hiyo ya msingi kwa binadamu iweze kupatikana kwa gharama nafuu kwa watu masikini zaidi katika jamii.

Vile vile, Rais Kikwete amezitaka Mahakama hizo kuhakikisha kuwa haki na hukumu zinatolewa kwa haraka bila uchelewesho ama bila haki yenyewe kuonekana imevurugwa.

Rais Kikwete ametoa ujumbe huo mzito kwa mahakama, mahakimu na majaji wa Afrika leo, Agosti 27, 2009, wakati alipofungua Mkutano wa Chama cha Kimataifa cha Majaji Wanawake, Tawi la Afrika, kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) mjini Arusha.

Mkutano huo wa siku mbili unahudhuriwa na majaji wanawake kutoka nchi 11 ambazo ni pamoja na wenyeji Tanzania, Kenya, Uganda, Cameroun, Afrika Kusini, Zambia, Zimbabwe na Marekani na mada kuu ya mkutano huo ni "Upatikanaji wa Haki za Kisheria na Nafasi Sawa kwa Wote." Ni mara ya kwanza mkutano huo huo unafanyika katika nchi yoyote ya Afrika Mashariki.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Rais Kikwete amewaambia majaji hao: "Kwa sababu nyinyi ni maofisa makini wa mahakama, ni lazima kwa vyovyote vile muelewe hisia za watu, mahitaji na matarajio yao wakati wanapoletwa mahakamani. Ni lazima mfungue milango ya mahakama kwao."

Ameongeza: "Ni lazima muwatumikie kwa dhati, ni lazima kulinda heshima yenu siyo kwa kupitia kwenye madaraka makubwa ya nafasi zenu, bali kwa kutoa hukumu ambazo zinathibitika kuwa ni za haki."

Kuhusu uhuru wa majaji, Rais Kikwete amesema: "Hata hivyo ni muhimu uhuru wa mahakama usije kueleweka ama kukubalika kuwa ni uhuru wa kuruhusu majaji na mahakimu kuendesha shughuli zao bila kufuata taratibu zilizowekwa na bila kufuata sheria. Ni lazima tukumbuke kuwa uhuru wa mahakama upo kwa faida na manufaa ya jamii yote."

Akizungumzia gharama za mahakama na watu kutafuta na kupata haki, Rais amefafanua: "Katika karibu nchi zetu zote, haki bado inabakia kuwa jambo ghali sana, na matokeo yake ni kwamba wengi wa watu wetu wanashindwa kumudu gharama za kuendesha kesi zao. Na lazima ikumbukwe kuwa haki hii ya mahakama ni moja ya haki za msingi za binadamu."

Ameongeza: "Bila watu kupata haki hii, ni vigumu wakaweza kufurahia haki zao nyingine za msingi. Kwa hakika, kama wale watu fukara hawawezi kupata haki kwa ukamilifu na vile vile kufurahia haki zao za msingi, hakuna Serikali yoyote inaweza kudai kuwa inao mfumo wa sheria unaofanya kazi vizuri."

Juu ya umuhimu wa kuharakishwa kwa kesi na kutolewa kwa hukumu na haki, Rais amewaambia majaji hao: "Napenda kuziasa sana mahakama zetu katika Afrika kuhakikisha kuwa zinatoa hukumu haraka na kwa namna ambako kesi hazionekani kuvurugwa. Kwa sababu ni dhahiri kabisa kuwa watu wengi wanazitumaini mahakama kuweza kupata haki. Wanatumaini haki ya mahakama zetu kwa sababu na wanayo haki ya kupata haki bora kutoka kwenu."

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

27 Agosti, 2009
 
SPEECH BY PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, HIS EXCELLENCY JAKAYA MRISHO KIKWETE, AT THE OPENING OF THE INTERNATIONAL ASSOCIATION OF WOMEN JUDGES AFRICA REGION CONFERENCE, ARUSHA TANZANIA AUGUST 27, 2009.

Honorable Augustino Ramadhani, Chief Justice of
the United Republic of Tanzania,
Hon. Hamid Mahamud, Justice of Zanzibar
Honorable Eusebia Munuo, Vice President of International Association of Women Judges and Vice Chairperson of Tanzania Women Judges Association;
Honorable Judge Leslie Alden, President of the International Association Women Judges;
Honorable Justice and Judges of different jurisdictions in Africa Countries,
Distinguished Delegates, Invited Guests, Ladies and Gentlemen,
Introduction
It is an honour and a privilege for me to be invited to address this very distinguished audience comprising of learned and esteemed jurists of our region. I wish to thank the Chief Justice of Tanzania, Judge Augustino Ramadhani and Vice President of the International Association of Women Judges who is also the Chairperson of Tanzania Women Judges Association, Madam Judge Eusebia Munuo for the invitation.
Cognizant of the important contribution being made by the Tanzania Women Judges Association in promoting unity within the African judiciaries, ensuring adherence to the rule of law and good governance and advancing the cause of human rights, I could not hesitated to accept your invitation.
Honourable Chief Justice, Distinguished Delegates, Ladies and Gentlemen;
Allow me to take this opportunity to extend a very warm welcome to Tanzania to Honorable Justices, Judges and distinguished delegates from within the African region and beyond. Karibuni sana, Tanzania. I wish you an enjoyable stay in Arusha and I hope you will find time, before you depart, to visit some of the scenic places and tourist sites in the vicinity of Arusha. These include world reknown game parks such as the Ngorongoro Crater and the Serengeti National Park as well as the Manyara National Park, Tarangire National Park and the Arusha National Park to mention just few. There is, also Mount Kilimanjaro and the Snake Park at Meserani Monduli.

Contribution of Tanzania Women Judges Association
Honorable Chief Justice, Ladies and Gentlemen;
I am pleased to know that this conference is one of the activities being undertaken by the International Association of Women Judges. There is no doubt that the gathering of Honorable Women Judges from African countries is an important occasion which deserves our attention and interest. I believe this is a good opportunity and forum for Women Judges to discuss several issues of interest including current developments in various branches of the law in our region. The conference is a positive move for forging closer judicial ties among our countries. I wish therefore, to commend the International Association of Women Judges and Tanzania Women Judges Association as well as the judiciary of Tanzania for the decision to organize this conference.
I am aware of the outstanding performance of Tanzania Women Judges Association in providing judicial and human rights education to judicial officers and to the members of the public with the aim of enhancing accessibility to courts and elimination of discrimination against women.
The activities of women Judges have contributed remarkably in the implementation of some national policies and programmes as well. One such example is the National Poverty Reduction Strategy where our esteemed women Judges have helped the government in addressing some of the challenges particularly those related to ensuring adherence to the rule of law and ethics, addressing human rights issues and domestic violence including sexual abuse and mainstreaming gender issues in planning and budgeting at all levels. The other is the Legal Sector Reform Programme where women Judges have played an important role with regard to speeding up of court cases; improving the quality of court decisions; increasing the pace of reviewing outdated laws and capacity building at all levels across the legal sector institutions.
.
The Theme
Honourable Chief Justice, Ladies and Gentlemen;
The theme for this conference: "Access to Justice" is very opportune and relevant in contemporary Africa. There are still many people in our region who do not enjoy some of their rights enshrined in their national constitutions. They cannot have access to justice due to ignorance and lack of adequate financial resources because they are poor. In almost all countries, justice remains an expensive affair as a result, many of our people cannot afford litigation costs. It should be noted that access to justice is one of the most basic human rights. Without access to justice, the enjoyment of many other fundamental rights may not be assumed. Indeed, if poor people cannot fully access justice and enjoy basic rights, no government can claim to have a well functioning system of the rule of law. This is a challenge for which views of this distinguished gathering of women judges may guide us to a better way out.
People's Expectations From the Courts
Honorable Chief Justice, Distinguished Delegates, Ladies and Gentlemen;
I strongly urge our judiciaries in Africa to ensure that delivery of justice is fast and untainted. For it is only too obvious that our people look up to the courts of law for justice. They count on the fairness of our courts. They deserve the best of justice you are required to deliver to them. Judges and magistrates are important public officials, whose authority touches every corner of the society. They are held in high esteem by the people because their role in society is special well recognized, respected and appreciated.
Judges and magistrates resolve disputes between people, interpret and apply the law of the land. In doing this, they, therefore define peoples' rights and responsibilities, determine the distinction of vast amounts of public and private resources and correct erroneous actions of public officials in the other branches of the government. Generally people generally, have belief in the righteousness and fairness of the judicial decisions.
Judges and Magistrates must reciprocate this trust and confidence of the society by demonstrating a great sense of responsibility and integrity. It is imperative that not only must judges be independent and courageous, but they must, also, maintain high standards of continued learning. These important attributes give people confidence and assurance that they will be judged justly in the courts of law and that they will enjoy adequate protection under the law.
In serving the people, judges must not lose sight of the fact that courts interpret laws, which to a layman, they are a body of complex and incomprehensible enactments. As judges, therefore you must not, be overly technical nor should you mystify the proceedings under the guise of the independence of the judiciary. Being serious judicial officers, you should, indeed, understand people's feelings and concerns when they come before the courts. You must make courts accessible to them. You must serve them with great dedication; you must protect your integrity not by the high office you hold, but by delivering judgements that accord to a sense of justice.




Independence of the Judiciary
Honouable Chief Justice, Honourable Judges, Ladies and Gentlemen;
It is the duty of the governments to guarantee and ensure the independence of the judiciary which is the prerequisite of the rule of law, constitutionalism and a fundamental guarantee of fair trial. It is exemplified and outlined in the United Nation's basic principles and clarified in several other regional instruments and Conventions that, "judges are charged with the ultimate decision over life, freedoms, rights and duties and property of citizens."
The independence of judges is not a prerogative or privilege in their own interests, but in the interest of the rule of law and those seeking and expecting justice. The independence of the judiciary must exist in relation to society generally and in relation to the particular parties to any dispute in which judges and magistrates have to adjudicate and determine impartially, without fear or favor.
Through judicial independence, the courts should ensure that the administration and the legislature are held to account for their actions, and to ensure that the duly enacted laws are enforced, and that they comply with any relevant constitution or statutory provisions. I personally take pride that the Constitution of the United Republic of Tanzania, in its Article 107B, guarantees the independence of the judiciary. I am sure that the constitutions of the other jurisdictions represented here have similar provisions for the guarantee of the independence of their respective judiciaries.
However, judicial independence should not be interpreted or taken to authorize judges and magistrates to operate without laid down guidelines and laws. It should be remembered that independence of the judiciary exists for the interest of the society at large. It is important to emphasize here that the conduct of judges on their professional activities is, understandably, seen by members of the public as essential to the credibility of the courts. It is through independence of the judiciary that the state seeks to ensure that the judiciary functions impartially and with integrity.

The Importance of Judicial Education and Training
Honorable Chief Justice, Delegates, Ladies and Gentlemen,
There can be no argument that an independent judiciary is a critical element of a democratic society. It is a fact which, however, calls upon judicial officers to be in possession of the requisite intellectual and moral strength to discharge their duties with competence and fairness. All these can be acquired only through judicial education and training. There is increasing realization of the fact that judicial competence requires more than just knowledge of the law. Our judges and magistrates, must, by necessity develop skills which will enable them to effectively serve the society, and apply the law with due dispatch and accuracy. Continued judicial education and training, as well as interaction among judges, particularly of various jurisdictions, like the Honourable Judges who are meeting here, contribute a great deal to the improvement of judicial skills and competence.
Professional training is important and is common in other fields. It is heart warming indeed, that this is now also becoming common with judges and magistrates. The importance of training arises from the need to cope with the changing trends in science, arts, ideas, habits and many other aspects. Regular judicial training must, by all means, be encouraged, so as to equip judges and magistrates with the most current developments in the world, not only in judicial matters but also on issues of other disciplines. Allow me to quote an old adage, but with modification to it, to illustrate this point. "Judges and Magistrates should be the jacks of all trades and masters of most of them, if not all".



Issues to be Discussed by the Conference
Honorable Chief Justice, Distinguished Delegates, Ladies and Gentlemen;
I have been made to understand that this conference will receive and discuss presentations by resource luminaries on various topics and issues. It is my expectation that the conference will find answers and solutions to the problems associated with discrimination, violence against women, HIV AIDS, property rights to women and children, judicial ethics, trafficking in persons together with technology and cyber crimes. I hope also you will find time to look at the problems of drug abuse and drug trafficking which are increasingly becoming a big menace to our societies on the continent.
Our respective governments in the region will be interested to hear your views on the subjects and receive your conclusions and recommendations at the end of your conference. I hope this conference will be a gateway not only towards a better understanding of the concept of access to justice but also to commitment to ensuring access to justice in your jurisdictions improves accordingly.

Conclusion
Honourable Chief Justice, Judges, Ladies and Gentlemen;
Let me conclude by, once again, expressing my very sincere appreciation, to Hon. Judge Leslie Alden, President of the International Association of Women Judges for deciding to organize this conference for women judges in our region. I do so on behalf of the government and the people of the United Republic of Tanzania and my own behalf. I am also grateful to the organizers, for affording Tanzania and Arusha in particular the honour to play host to this important and historic conference. I wish to commend the Tanzania Women Judges Association for accepting to host this important conference and for a job very well done. You have organised this conference with finesse and high levels of excellence. We thank you for making us proud.
Allow me also to thank on behalf of the organizers all those who have in many ways contributed to the success of this conference.
Honourable Chief Justice, Honourable Judges, Ladies and Gentlemen;
This conference would not have been held, if participants would not have been able to find time, within their normally busy schedules of work, to come and attend. I extend very sincere appreciation to all delegates for your kind decision to participate in this important conference. This is a clear testimony of your commitment to your organisation and the promotion of access to justice, judicial training, and indeed, general cooperation in Africa.


Honorable Chief Justice, Distinguished Delegates, ladies and Gentlemen,
Having said all this, it is now my singular honour and pleasure to declare this Africa Regional Conference on Access to Justice of the International Association of Women Judges officially opened. I wish you very fruitful deliberations over the next two days.

I thank you for your kind attention!
Asanteni Sana.
 
Hii ingeanza wakati wa kesi ya Marehemu Ditopile, ikaja kwenye kesi ya Zombe na kwenye kesi za EPA ingekuwa nzuri sana. Sijui mheshimiwa ana maana gani, kuzungumzia haki wakati katika kipindi chake usimamiaji wa haki ni tofauti kabisa na anayoyasema.
 
The problem with President Kikwete is that he is too much of a "Mswahili" (i.e. a person of double standards and coward at the same time). There are so many examples (e.g. during his first inaugural Paliamentary speech he said that his government will not be in partneship with corrupt individuals. But when it came to the time of appointing ministers and other senior officials in his government, he appointed corrupt ministers and heads of directorates/departments despite mass outcry). For example there is a politician with a $1m account in a foreign bank who walks with his/her nose high in Tanzania of Kikwete without being asked to account for the money. Forex regulations are quite clear in this regard but who will bell the cat? May be it is a political accident Mr President!
 
Si ndo maana watu wanamwita "Msanii". Maneno mazuri lakini utekekelezaji wake ni sifuri. Kwa mwendo huu sijui kizazi kijacho tunawarithisha nini.
 
Anayoyasema ni tofauti kabisa na anayoyatenda. Sina imani naye hata kidogo, 2010 yeye na CCM hawatapata kura yangu.
 
Uchaguzi 2010 - "Kama mnampenda Mpeni chai, lakini sio NCHI" (J.K. Nyerere)
 
waswahili wanasema "maneno matamu humtoa nyoka pangoni".sasa haya maneno ya jk ni kutaka wananchi wakampigie kura tu mwakani hakuna lolote cha maana ni mambo ya politics.
 
Anayoyasema ni tofauti kabisa na anayoyatenda. Sina imani naye hata kidogo, 2010 yeye na CCM hawatapata kura yangu.

Kuna kitu wengi naona tunakioverlook hapa kwamba HIZI HOTUBA ANAANDIKIWA NA WATU AMBAO NDIO KAZI YAO HIYO. Lakini pia ukimwalika rais kwenye shughuli yako unatakiwa umwandalie na cha kusema. So anachofanya ni kuimba mashairi yaliyoandikwa kama akapela kinachokosekana ni vyombo kuwa bongo flavor na si zaidi ya hapo.

Next time muwe makini jamani kwenye headings zingine hazisemi kilichopo kwenye habari yenyewe sioni kukiri hapo jamani kwenye porojo za hotuba.
 
The problem with President Kikwete is that he is too much of a "Mswahili" (i.e. a person of double standards and coward at the same time). There are so many examples (e.g. during his first inaugural Paliamentary speech he said that his government will not be in partneship with corrupt individuals. But when it came to the time of appointing ministers and other senior officials in his government, he appointed corrupt ministers and heads of directorates/departments despite mass outcry). For example there is a politician with a $1m account in a foreign bank who walks with his/her nose high in Tanzania of Kikwete without being asked to account for the money. Forex regulations are quite clear in this regard but who will bell the cat? May be it is a political accident Mr President!

Is this your definition of "Mswahili".

However, the guys does not do what is says!! That is our Prez!!!!!!!
 
Kwa kuwa kikao hicho kinajumuisha majaji wengine kutoka nchi zingine za Africa anataka kuonekama kwamba hapa nyumbani kwake hayo anayotoa kama challenge ya kikao yanatekelezeka ili Kujipatatia SIFA maana huko nje wanamfagilia kweli!! wakati nyumbani kunateketea
 
huyu jamaa ukimsikiliza utadhani ni bonge la mtekelezaji ile yote siasa hakuna mabadiliko

mambo mangapi yanafanyika bila haki amekaa kimya
hii ndio tanzania zaidi ya tu ijuvyo siasa kila kona mpaka kwenye mambo ya ukweli
 
RAIS Jakaya Kikwete amewataka mahakimu Afrika kulinda heshima yao kwa kutoa hukumu za haki, zenye kuridhisha hisia za watu kuwa ni kweli haki inatendeka. Pia amesema uhuru wa majaji si haki binafsi au heshima ya jaji, bali uhuru huo ni kwa ajili ya kulinda utawala wa sheria na kuwalinda wanaotafuta na wanaotarajia kupata haki kutoka kwa majaji.

Aidha, Rais Kikwete amezitaka mahakama kuangalia jinsi ya kupunguza gharama za kutafuta haki, ili iweze kupatikana kwa gharama nafuu kwa watu masikini zaidi katika jamii. Amezitaka mahakama hizo kuhakikisha kuwa haki na hukumu zinatolewa kwa haraka bila uchelewesho wala haki yenyewe kuonekana imevurugwa.

Rais Kikwete alitoa ujumbe huo kwa mahakimu na majaji wa Afrika alipofungua Mkutano wa Chama cha Kimataifa cha Majaji Wanawake, Tawi la Afrika, kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) mjini hapa jana.

Mkutano huo wa siku mbili unahudhuriwa na majaji wanawake kutoka nchi 11 za Tanzania, Kenya, Uganda, Cameroon, Afrika Kusini, Zambia, Zimbabwe na Marekani na mada kuu ya mkutano huo ni “Upatikanaji wa Haki za Kisheria na Nafasi Sawa kwa Wote.”

Rais aliwaambia majaji hao: “Kwa sababu ninyi ni maofisa makini wa mahakama, ni lazima kwa vyovyote vile muelewe hisia za watu, mahitaji na matarajio yao wakati wanapoletwa mahakamani. Ni lazima mfungue milango ya mahakama kwao.”

Aliongeza: “Ni lazima muwatumikie kwa dhati, ni lazima kulinda heshima yenu si kwa kupitia kwenye madaraka makubwa ya nafasi zenu, bali kwa kutoa hukumu ambazo zinathibitika kuwa za haki.”

Kuhusu uhuru wa majaji, alisema: “Hata hivyo ni muhimu uhuru wa mahakama usije kueleweka au kukubalika kuwa ni wa kuruhusu majaji na mahakimu kuendesha shughuli zao bila kufuata taratibu wala sheria. Ni lazima tukumbuke kuwa uhuru wa mahakama upo kwa faida na manufaa ya jamii yote.”

Akizungumzia gharama za mahakama na watu kutafuta na kupata haki, Rais alifafanua: “Katika karibu nchi zetu zote, haki bado inabakia kuwa jambo ghali sana na matokeo yake ni kwamba wengi wa watu wetu wanashindwa kumudu gharama za kuendesha kesi zao.

Na lazima ikumbukwe kuwa haki hii ya mahakama ni moja ya haki za msingi za binadamu. “Bila watu kupata haki hii, ni vigumu wakaweza kufurahia haki zao nyingine za msingi.

Kwa hakika, kama watu fukara hawawezi kupata haki kwa ukamilifu na kufurahia haki hizo, hakuna Serikali inayoweza kudai kuwa ina mfumo wa sheria unaofanya kazi vizuri.”

Juu ya umuhimu wa kuharakishwa kwa kesi na kutolewa kwa hukumu na haki, Rais aliwaambia majaji na mahakimu kuhakikisha mahakama zinatoa hukumu haraka na kwa namna ambayo kesi hazionekani kuvurugwa
http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=3399
 
Wakuu nimekutana na habari hii hapa kutoka kwenye gazeti la Tanzania Daima kama ifuatavyo:-


JK: Wanyonge wakikosa haki hakuna utawala wa sheria


na Halfani Lihundi, Arusha


RAIS Jakaya Kikwete, amesema hakuna nchi itakayojigamba inatekeleza utawala wa sheria, wakati wanyonge walio wengi, wanakosa haki kutokana na hali ngumu ya kiuchumi inayowakabili.
Rais Kikwete alisema hayo jana alipokuwa akifungua mkutano wa siku mbili wa majaji wanawake kutoka nchi 11 za Kiafrika ulioanza mjini hapa kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).
Alisema upatikanaji wa haki umekuwa na gharama kubwa, hivyo kusababisha maskini kushindwa kumudu gharama hizo.
Aliwataka majaji hao kujadili changamoto hizo na kupendekeza njia zinazoweza kutumika kukabiliana na mapungufu hayo, ili kila raia aweze kufaidi matunda ya upatikanaji wa haki katika nchi zao.
‘‘Hili ni suala ambalo majaji, watendaji wa mahakama na watoa haki lazima walichukulie kama changamoto na kisha kutupa mapendekezo ya namna bora ya kurekebisha hali hiyo,” alisemaRais Kikwete.
Rais Kikwete pia aliwataka majaji hao na mahakimu kuhakikisha utoaji wa haki unafanyika kwa njia ya haraka kutokana na matumanini waliyonayo wananchi wanapotafuta haki zao. Awali, Mwenyekiti wa Chama cha Majaji Wanawake Tanzania (TWJA), Jaji Eusebia Munuo, alisema mkutano huo wa kwanza kufanyika nchini, utazungumzia masuala ya haki za binadamu, haki za wanawake na watoto na unyanyasaji wa kijinsia pamoja na ukimwi na haki katika umiliki wa mali na biashara ya binadamu.

Nafikiri Mh. Rais alikuwa anazungumzia hali halisi barani Afrika Tanzania ikiwemo na ikiwa mwenyeji wa mkutano huo. Hakuna hasiyeelewa hali ngumu ya maisha inayowakabili watanzania kwa sasa. Maskini wameongezeka na waliokuwepo wameendelea kuwa maskini tena kwa kasi na ari mpya.

Leo mkuu wa nchi anapotoa kauli hii naamini alikuwa anakiri kuwa Tanzania hakuna utawala wa sheria kutokana na sababu ambazo ameweza kuzitambua kwa utambuzi wake. Kuna sababu zingine ambazo zinaweza kukuongoza kufikia conclusion kuwa Tanzania hakuna utawala wa sheria, mfano pale Bunge la JMT linapotoa miongozo kwa serikali na serikali inarudi kwa ngonjera bila kutekeleza miongozo hiyo huku zikifanywa mbinu za kumuondoa Spika wa Bunge kwa kuwa anaipelekesha serikali.

Lakini Mh. Rais kwa utambuzi wake kaona hilo kuwa kama wanyonge hawapati haki zao basi hakuna utawala wa sheria. Na ni kweli wanyonge wengi hapa Tanzania hawapati haki zao hata zile za msingi.

Mh. Rais nakushukuru kwa kutambua hili, sasa lililobaki ni nini kama hakuna utawala wa sheria???
1. Jilime memo wewe mwenyewe ni kwa nini husifukuzwe kazi kwa kushindwa kuwapa wanyonge haki zao.

2. Kwa nini husiadhibiwe kwa kuruhusu ufisadi kuendelea ndani ya serikali na chama chako.
3.
4.
5.

:) what can I say ...
 
Huwa anajitahidi sana anapokuwa kwenye hizi za akina Mama. Tena wanapenda sana kumwalika. Hivi kwanini hamtumi makamu wake kwenye hivi vitu vidogo vodogo namna hii?
 
Back
Top Bottom