Indume Yene
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 2,950
- 711
Wakuu nimekutana na habari hii hapa kutoka kwenye gazeti la Tanzania Daima kama ifuatavyo:-
JK: Wanyonge wakikosa haki hakuna utawala wa sheria
na Halfani Lihundi, Arusha
RAIS Jakaya Kikwete, amesema hakuna nchi itakayojigamba inatekeleza utawala wa sheria, wakati wanyonge walio wengi, wanakosa haki kutokana na hali ngumu ya kiuchumi inayowakabili.
Rais Kikwete alisema hayo jana alipokuwa akifungua mkutano wa siku mbili wa majaji wanawake kutoka nchi 11 za Kiafrika ulioanza mjini hapa kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).
Alisema upatikanaji wa haki umekuwa na gharama kubwa, hivyo kusababisha maskini kushindwa kumudu gharama hizo.
Aliwataka majaji hao kujadili changamoto hizo na kupendekeza njia zinazoweza kutumika kukabiliana na mapungufu hayo, ili kila raia aweze kufaidi matunda ya upatikanaji wa haki katika nchi zao.
Hili ni suala ambalo majaji, watendaji wa mahakama na watoa haki lazima walichukulie kama changamoto na kisha kutupa mapendekezo ya namna bora ya kurekebisha hali hiyo, alisemaRais Kikwete.
Rais Kikwete pia aliwataka majaji hao na mahakimu kuhakikisha utoaji wa haki unafanyika kwa njia ya haraka kutokana na matumanini waliyonayo wananchi wanapotafuta haki zao. Awali, Mwenyekiti wa Chama cha Majaji Wanawake Tanzania (TWJA), Jaji Eusebia Munuo, alisema mkutano huo wa kwanza kufanyika nchini, utazungumzia masuala ya haki za binadamu, haki za wanawake na watoto na unyanyasaji wa kijinsia pamoja na ukimwi na haki katika umiliki wa mali na biashara ya binadamu.
Nafikiri Mh. Rais alikuwa anazungumzia hali halisi barani Afrika Tanzania ikiwemo na ikiwa mwenyeji wa mkutano huo. Hakuna hasiyeelewa hali ngumu ya maisha inayowakabili watanzania kwa sasa. Maskini wameongezeka na waliokuwepo wameendelea kuwa maskini tena kwa kasi na ari mpya.
Leo mkuu wa nchi anapotoa kauli hii naamini alikuwa anakiri kuwa Tanzania hakuna utawala wa sheria kutokana na sababu ambazo ameweza kuzitambua kwa utambuzi wake. Kuna sababu zingine ambazo zinaweza kukuongoza kufikia conclusion kuwa Tanzania hakuna utawala wa sheria, mfano pale Bunge la JMT linapotoa miongozo kwa serikali na serikali inarudi kwa ngonjera bila kutekeleza miongozo hiyo huku zikifanywa mbinu za kumuondoa Spika wa Bunge kwa kuwa anaipelekesha serikali.
Lakini Mh. Rais kwa utambuzi wake kaona hilo kuwa kama wanyonge hawapati haki zao basi hakuna utawala wa sheria. Na ni kweli wanyonge wengi hapa Tanzania hawapati haki zao hata zile za msingi.
Mh. Rais nakushukuru kwa kutambua hili, sasa lililobaki ni nini kama hakuna utawala wa sheria???
1. Jilime memo wewe mwenyewe ni kwa nini husifukuzwe kazi kwa kushindwa kuwapa wanyonge haki zao.
2. Kwa nini husiadhibiwe kwa kuruhusu ufisadi kuendelea ndani ya serikali na chama chako.
3.
4.
5.
JK: Wanyonge wakikosa haki hakuna utawala wa sheria
na Halfani Lihundi, Arusha
RAIS Jakaya Kikwete, amesema hakuna nchi itakayojigamba inatekeleza utawala wa sheria, wakati wanyonge walio wengi, wanakosa haki kutokana na hali ngumu ya kiuchumi inayowakabili.
Rais Kikwete alisema hayo jana alipokuwa akifungua mkutano wa siku mbili wa majaji wanawake kutoka nchi 11 za Kiafrika ulioanza mjini hapa kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).
Alisema upatikanaji wa haki umekuwa na gharama kubwa, hivyo kusababisha maskini kushindwa kumudu gharama hizo.
Aliwataka majaji hao kujadili changamoto hizo na kupendekeza njia zinazoweza kutumika kukabiliana na mapungufu hayo, ili kila raia aweze kufaidi matunda ya upatikanaji wa haki katika nchi zao.
Hili ni suala ambalo majaji, watendaji wa mahakama na watoa haki lazima walichukulie kama changamoto na kisha kutupa mapendekezo ya namna bora ya kurekebisha hali hiyo, alisemaRais Kikwete.
Rais Kikwete pia aliwataka majaji hao na mahakimu kuhakikisha utoaji wa haki unafanyika kwa njia ya haraka kutokana na matumanini waliyonayo wananchi wanapotafuta haki zao. Awali, Mwenyekiti wa Chama cha Majaji Wanawake Tanzania (TWJA), Jaji Eusebia Munuo, alisema mkutano huo wa kwanza kufanyika nchini, utazungumzia masuala ya haki za binadamu, haki za wanawake na watoto na unyanyasaji wa kijinsia pamoja na ukimwi na haki katika umiliki wa mali na biashara ya binadamu.
Nafikiri Mh. Rais alikuwa anazungumzia hali halisi barani Afrika Tanzania ikiwemo na ikiwa mwenyeji wa mkutano huo. Hakuna hasiyeelewa hali ngumu ya maisha inayowakabili watanzania kwa sasa. Maskini wameongezeka na waliokuwepo wameendelea kuwa maskini tena kwa kasi na ari mpya.
Leo mkuu wa nchi anapotoa kauli hii naamini alikuwa anakiri kuwa Tanzania hakuna utawala wa sheria kutokana na sababu ambazo ameweza kuzitambua kwa utambuzi wake. Kuna sababu zingine ambazo zinaweza kukuongoza kufikia conclusion kuwa Tanzania hakuna utawala wa sheria, mfano pale Bunge la JMT linapotoa miongozo kwa serikali na serikali inarudi kwa ngonjera bila kutekeleza miongozo hiyo huku zikifanywa mbinu za kumuondoa Spika wa Bunge kwa kuwa anaipelekesha serikali.
Lakini Mh. Rais kwa utambuzi wake kaona hilo kuwa kama wanyonge hawapati haki zao basi hakuna utawala wa sheria. Na ni kweli wanyonge wengi hapa Tanzania hawapati haki zao hata zile za msingi.
Mh. Rais nakushukuru kwa kutambua hili, sasa lililobaki ni nini kama hakuna utawala wa sheria???
1. Jilime memo wewe mwenyewe ni kwa nini husifukuzwe kazi kwa kushindwa kuwapa wanyonge haki zao.
2. Kwa nini husiadhibiwe kwa kuruhusu ufisadi kuendelea ndani ya serikali na chama chako.
3.
4.
5.