Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Niko kwenye mahusiano na mdada wa miaka 28, uhusiano wetu sasa una takribani miezi 9. Kimsingi tumekuwa sawa kwa muda wote lakini kuna kitu kimoja ambacho kwangu kinanishangaza kuhusu huyu mpenzi wangu. Kila ninapotaka kufanya nae mapenzi muda ambao kwa kweli hata akili nimeshai-tune kula mzigo utasikia anakwambia " ah! subiri kwanza mi nilikwambia nataka simu mbona hujaninunulia?" au mi nina shida ya hela nataka kununua kitu fulani mbona hujanipa?...Hii hali kwa kweli siipendi kabisa na hunipotezea kabisa stimu. Mwanzoni nilidhani huenda ndio alivyokuwa kabla sijakuwa naye na nikajaribu kumueleza vizuri tu kuwa kila kitu kina muda wake ili ajirekebishe. Tukiwa kwenye love basi wote tuwe hapo hayo mambo mengine nayo yana muda wake....ataelewa kwa muda lakini baada ya wiki hiyo kitu inajirudia sijui tatizo nini???