Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Leo asubuhi nilikuwa nikisikiliza BBC na katika moja ya taarifa zilizonishangaza ni kuwa nchini botswana kuna sheria inayomkataza mume au mke kumfatilia mwenza wake pindi mmoja wao anapoamua kutoka na mwanamke au mwanaume mwingine. Kwamba kama mwanaume atamkuta mkewe yuko bar au klabu anajivinjari na njemba mwingine ni kosa kwa mume kumfata huyo mke na kuhoji kinachoendelea pale hali hii pia ni kwa wanawake. mama akimkuta mzee yuko bar na sholi mwingine haruhusiwi kabisa kuwaghasi. Na katazo hili linakuwa pale inapotokea kama mume au mke huyo hawakutoka pamoja kwenda mahali pale. Pia ni kosa mume au mke anapokuwa amesafiri kikazi nje ya nyumbani kwake zaidi ya wiki 3 kurudi nyumbani kwake bila ya kutoa taarifa kwa mume au mke kwa simu kuwa unarudi nyumbani kutoka hiyo safari yako ya kikazi....Sasa kali zaidi ni kuwa inapotokea mume au mke amerudi kutoka safari ya kikazi bila kutoa taarifa utakachokuta nyumbani kwako unatakiwa kuwa kimya. Kwa maana kuwa kama mzee ndio unarudi kutoka safari kimya kimya ukikuta mama ameingiza njemba nyingine nyumbani kwako wewe unatakiwa kuwaheshimu na kutowafanyia fujo........Hii ingekuwa hapa bongo nina imani watu wangekatana shingo mchana kweupe hata kama ndio sheria.....:twitch::twitch::A S-eek::A S-eek: